Klabu ya Toto African ya Mwanza
inatarajiwa kufanya uchaguzi wa kujaza nafasi zilizo wazi katika kamati yake ya
utendaji ifikapo tarehe 11 Oktoba 2015. Katika barua yake kwa Katibu Mkuu wa
Toto African, Katibu Mkuu wa TFF ameuagiza uongozi wa Toto African kuwasiliana
na Kamati yao ya Uchaguzi ili tangazo la uchaguzi litolewe si chini ya siku
sitini (60) kabla ya tarehe ya kufanyika uchaguzi.
Kwa muda mrefu kumekuwa na mvutano
katika klabu ya Toto na suala kubwa likiwa ni kuhusu ujazaji wa nafasi zilizo
wazi. Awali TFF ilipokea maombi ya wanachama na wadau wa Toto African wakitaka
ufanyike uchaguzi ili kumaliza mvutano ndani ya klabu.
TFF ilishauri uchaguzi huo kusubiri
klabu kukamilisha mchakato wa usajili.
Vilevile TFF imewataka wadau wote wa
klabu hiyo kongwe ya mjini Mwanza kuheshimu uongozi uliopo madarakani kwani
ndio unaotambulika na ndio utaendelea kuiongoza Toto African katika kipindi cha
kuelekea uchaguzi uchaguzi.
IMETOLEWA
NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
--
Best Regards,
Baraka Kizuguto
MEDIA & COMMUNICATION OFFICER
Tanzania Football Federation - TFF
T: +255 22-2861815 I F: +255 22-2861815 I C: +255 713 455970
E: b.kizuguto@tff.or.tz, I W: www.tff.or.tz
A:I P.O.BOX 1574 Karume Memorial Stadium /Shaurimoyo/Uhuru Street I Dar es salaam I Tanzania