Na Oscar Assenga,TANGA.
HABARI NA MATUKIO MBALIMBALI
Na Oscar Assenga,TANGA.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda amesifu ubunifu unaofanywa na Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organization (TOIO) ya kubuni vifaa mbalimbali vya umeme ikiwemo Baiskeli na Pikipiki huku akihaidi kuunga mkono juhudi hizo.
Profesa Mkenda aliyasema hayo wakati alipoitembelea Taasisi hiyo wakati wa ziara yake ya kutembelea Mradi wa pikipiki za umeme,baiskeli ambazo zinazoziunda wenye shule ya Sekondari Tanga Ufundi.
Akiwa katika eneo hilo Waziri Profesa Mkenda alizitaka taasisi zinazojihusisha na teknolojia na ubunifu kuwasaidia wabunifu nchini kuweza kuzalisha bidhaa zenye ubora.
Alisema kwamba kupitia ubunifu ambao unafanywa na taasisi kama TOIO wanaweza kuona namna ya kupata bajeti ambayo wanaitumia kuweza kuitumia kwa ajili ya kununua hivi vitu ili kuwaunga mkono watanzania ambao wanabuni vitu mbalimbali vyenye manufaa.
“Kupitia bajeti hiyo tutaitumia kununua hivi vitu vinavyotengenezwa hapa kitu kimoja tutangeneza mfumo wa kuvifabrikate kwa scale ya haraka”Alisema
Waziri Mkenda alisema kwamba vipaumbele vyao kwa bajeti iliyopo ya serikali ni kuona namna ya kuwasaidia wabunifu hao kununua hivi vitu tayari na serikali itanunua.
Awali akizungumza Mwakilishi wa Botna Foundation Dkt Hassan Mshinda alisema wao walipata ufadhii wa kujenga ujuzi huo sio kwa wanafunzi tu bali na jamii ya nje.
Alisema wanachofikiria ile integration kwenye mafunzo kama hayo ni fursa nyengine nzuri wanaweza kuona namna ya kupatna pamoja
Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organization (TOIO) Shaukatali Hussein alisema wamekuwa wakitoa ujuzi jinsi ya kutengeneza na kurekebisha vifaa mbalimbali ikiwemo pikipiki za umeme na baiskeli nia ikiwa na ya kuwa mjasiriamali anaweza kutengeneza pia
Kamati ya Ujenzi ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo |
Waziri wa Elimu Sayansi na Teklonojia Profesa Adolf Mkenda |
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Elimu, Mafunzo ya Ufundi Stadi Veta Anthon Mzee Kasore |
Na Mashaka Mhando Tanga
SERIKALI imesema inaendelea na ujenzi wa vyuo 65 vya ufundi stadi Veta utakaohharimu kiasi cha shilingi bilioni 54 katika Mikoa na Wilaya hapa nchini, ikiwa ni mkakati wa kuhakikisha inatoa elimu ya Amali itakayokidhi matakwa ya mabadiliko ya sera ya elimu.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teklonojia Profesa Adolf Mkenda alisema hayo jana alipotembelea chuo cha ufundi stadi Veta Jijini Tanga ili kujionea namna kinavyotoa mafunzo ya Ufundi Stadi lakini pia kuhakikisha wanatoa huduma zinazostahiki kwa jamii.
Waziri Mkenda amesema kuwa kati ya vyuo 65 vinavyojengwa Nchini, Vyuo 64 ni za Wilaya na Chuo Kimoja cha Mkoa ambapo hadi sasa tayari imetoa kiasi cha shilingi bilioni 37 huku matumaini yakiwa makubwa katika kila maeneo yanayojengwa vyuo hivyo ambavyo ni mkakati wa serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.
"Tukiwa bungeni swali kubwa ambalo limekuwa likiulizwa mara nyingi kuliko maswali mengine yote katika wizara ya elimu sayansi na teknolojia ni kuhusu veta kila mmoja anauliza ni lini veta itajengwa kwake watu wanamatarajio makubwa sana kwenye veta kwa maana hiyo sisi tuna kazi ya kuhakikisha tunakidhi matarajio yao kwa kutoa elimu ya amali ambayo ni bora na ambayo itakidhi matakwa ya vijana, "alisema Waziri Mkenda.
Prof Mkenda amesema zipo namna mbili za kuendelea kuwapima wahitimu wa Mafunzo ya Ufundi Stadi Veta ambapo moja ya njia ni kuangalia wahitimu wanafanya wapi kazi mara baada ya kuhitimu mafunzo yao na kuwahoji waliowaajiri namna walivyoridhika na utendaji kazi wao.
Pia Waziri Profesa Mkenda aliwaagiza viongozi wa Veta kuhakikisha wanaandaa bajeti na kuiwasilisha wizarani itakayoomba fedha kwa ajili ya kununulia zana bora zinazokidhi teklonojia ya sasa katika karakana za Ufundi wa magari ili vyuo hivyo vya Veta viweze kuingia sokoni kutengeneza magari ya serikali, mashirika na watu binafsi.
Mkurugenzi wa Veta kanda ya Kaskazini Monica Mbele, alisema wamepokea maagizo hayo ambayo pindi wakipata nyenzo na zana bora za kisasa wataweza kuwa na utayari wa kutengeneza magari lakini pia kuongeza walimu wenye ujuzi wa teklonojia ya kisasa.
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi VETA Antony Mzee Kasore alisema watahakikisha wanakwenda kutekeleza maagizo ya Waziri ya utoaji wa mafunzo bora na kuhakikisha wanatoa mafunzo yanayohitajika na yanayozingatia ubora unahitajika.
"Kama tulivyosikia kuna vyuo vinavyojengwa 65 katika wilaya mbalimbali na Mkoa na chenyewe pia tunakwenda kusimamia kama maelekezo aliyotoa ya kuhakikisha tunasimamia ujenzi huo uweze kufanyika tukiamini tutakuwa tumekwenda kutekeleza yale yote yaliyoanishwa, "alisema
Mwisho.
SERIKALI kwa kushirikiana na Project Inspire ipo kwenye mchakato wa kujenga kituo kikubwa cha Sayansi na teknolojia Mkoani Dodoma.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teklonojia Profesa Adolf Mkenda alisema jana kwamba kituo hicho kitatumiwa na viongozi wengine wa serikali kama mfano utakaosaidia vituo vya aina hiyo kujengwa maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha wanafunzi kusoma na kupenda masomo ya sayansi.
Profesa Mkenda ametoa kauli hiyo wakati alipotembelea kituo cha sayansi cha Stem Park kilichopo jijini Tanga, na kwamba mpango huo utasaidia kumaliza tatizo la wanafunzi kutopenda masomo ya sayansi wanapokuwa shuleni.
Waziri Mkenda alisema kituo hicho kitajengwa mjini Dodoma kitakuwa kama kituo cha mfano ambacho wabunge na viongozi wengine wa serikali watakitembelea ili kuona umuhimu wa kuwa na vituo vya aina hiyo kwenye maeneo yao.
"Dodoma ni katikati ya nchi yetu halafu pale wabunge, mawaziri wenzangu na watu mbalimbali wakuu wa mikoa nitapenda watembelee waone nini kinaweza kufanyika vituo hivi vinapaswa kujengwa kila mkoa najua haitafikia wanafunzi wote vitu vyote hivi ni matumda ambayo yanapatikana kirahisi, "alisema Waziri Mkenda.
"Kwahiyo mimi mwenyewe nitasapoti kwanza tutafute eneo jijini Dodoma litupe eneo na majengo waje pale na tusiwatoze hata thumni kwasababu wenyewe hawawatozi wanafunzi wanaokuja kufanya mafunzo hapa hawalipishwi chochote,"alisisitiza Prof Mkenda.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Project inspire Lwidiko Edward alisema kituo hicho kinawatengeneza wanafunzi kwenye masomo ya sayansi kwa kutumia mbinu mbalimbali ikiwemo kujifunza kwa miradi na kuandaa mazingira yanayotoa hamasa ya kusoma.
Mkurugenzi mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech) Amos Nungu alisema kituo hicho kitasaidia kujenga mapenzi ya watoto kupenda masomo ya sayansi tokea wakiwa katika umri mdogo.
Mpango wa ujenzi wa vituo hivyo unakuja wakati kukiwa na ari ndogo ya wanafunzi wanaopenda masomo ya sayansi ambao wengi wamekuwa wakikimbilia masomo ya sanaa kutokana na mazingira duni ya kujifunza masomo hayo.
Mwisho.