MKUU WA WILAYA YA MOSHI ,NOVATUS MAKUNGA AAJIONEA ATHARI YA MAFURIKO .

April 27, 2016
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga akizungumza jambo na wataalamu alioongozana nao katika uwanja mdogo wa ndege wa Moshi kwa ajili ya kuruka na ndege ndo ya Shirika la Hifadhi za taifa (TANAPA) kwa ajili ya kujionea hali ya mafuriko.
Mkuu wa wilaya akiwa katika uwanja wa ndege wa Moshi kwa ajili ya maandalizi ya kwenda kujionea hali ya mafuriko katika maeneo mbalimbali.
Mtaalamau anayeshughulikia Majanga kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Canon Masanja (wa tatu toka kulia) akimuelekeza jambo rubani muda mfupi kabla ya ndege kuruka.
Mkuu wa wilaya ya Moshi akiteta jambo na Kaimu meneja wa uwanja mdogo wa ndege wa Moshi ,Fredrick Kimaro muda mfupi kabla ya kwenda kutizama eneo lililo athirika kwa mafuriko.
Maeneo mbalimbali ,zikiwemo nyumba zikiwa zimezingirwa na maji katika vijiji vya Miwaleni huku mashamba yakiwa yameharbika vibaya.
Mioundo mbinu ya barabara pia imeathirika vibaya.
Maashamba yamejaa maji ,
Maeneo mengine barabara hazipitiki hali inayochangia wananchi wanaoishi katika maeneo hayo kushindwa kupata huduma za kibinadamu.
Eneo la Mabogini pia liliathirika na mafuriko ingawa yalikuwa ni ya muda mfupi.
Sehemu ya mji wa Moshi unavyoonekana kwa juu.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

SERIKALI YAZUIA UINGIZAJI HOLELA WA MCHELE

April 27, 2016


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameviagiza vyombo vya dola viimarishe ulinzi kwenye mipaka ya nchi na hasa katika mwambao wa Bahari ya Hindi ili kuzuia uingizwaji holela wa mchele wa magendo kutoka nje ya nchi.
Ametoa agizo hilo leo mchana (Jumatano, Aprili 27, 2016) wakati akijibu hoja za wabunge na kuhitimisha hoja ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2016/2017 bungeni mjini Dodoma.
“Napenda kuviagiza vyombo vya dola viendelee kuimarisha ulinzi wa mipaka yetu hasa katika mwambao wa Bahari ya Hindi ili kuzuia uingizwaji holela wa mchele wa magendo kutoka nje ya nchi. Endapo patatokea upungufu wa mchele nchini, Serikali itaangalia uwezekano wa kuruhusu kuagiza mchele kutoka nje,” amesema.
Waziri Mkuu amesema katika kipindi cha miaka sita iliyopita, kumekuwa na ongezeko la asilimia 14 katika uzalishaji wa mpunga hapa nchini na hivyo kufanya kiwango cha uzalishaji kiwe ni kikubwa kuliko mahitaji.
“Takwimu za uzalishaji mpunga zinaonesha kuwepo ongezeko katika kipindi cha miaka sita iliyopita ambacho kiliongezeka kutoka tani 1,699,825 mwaka 2009/2010 hadi kufikia tani 1,936,909 mwaka 2014/2015 sawa na ongezeko la asilimia 14. Katika kipindi chote hicho, kiwango cha uzalishaji wa mpunga kimekuwa kikubwa kuliko mahitaji,” amesema.
“Kutokana na mwenendo huo mzuri wa uzalishaji wa mpunga hapa nchini, Serikali ilisitisha kutoa vibali vya kuagiza mchele kutoka nje ya nchi tangu Machi, 2013. Hatua hii itasaidia wakulima wetu kupata soko la uhakika na bei nzuri, jambo ambalo linawaongezea kipato na pia kuwahamasisha kuongeza uzalishaji zaidi,” amesema.
Akizungumzia kuhusu deni la sh. bilioni 134 ambalo Serikali inadaiwa na Bohari ya Dawa nchini (MSD), Waziri Mkuu alisema Serikali imeanza kulishughulikia deni hilo kwa kumwelekeza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ahakiki deni hilo. “Mpaka sasa CAG amehakiki madai ya jumla ya shilingi bilioni 67 na kazi ya uhakiki inaendelea.”
Akifafanua kuhusu vigezo vilivyutumika kugawanya majimbo mapya ya uchaguzi, Waziri Mkuu alisema mwaka 2015, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilipokea maombi 77 ya kuanzishwa majimbo mapya, ambapo Halmashauri 37 ziliwasilisha maombi ya kugawa majimbo ya uchaguzi na maombi 40 yalitoka katika majimbo yaliyokuwepo yakiomba kugawanywa. Kati ya maombi yaliyowasilishwa, maombi 35 tu ndiyo yalikidhi vigezo na yalistahili kugawanywa.
“Kutokana na ongezeko la Halmashauri mpya ambazo kisheria ni majimbo ya uchaguzi, ongezeko la idadi ya wabunge wanawake wa viti maalum na uwezo wa ukumbi wa Bunge; Tume iliamua kutumia vigezo vitatu tu ili kupata idadi ya majimbo yanayoweza kugawanywa. Vigezo hivyo ni: Wastani wa idadi ya watu (Population Quota), mipaka ya kiutawala na uwezo wa ukumbi wa Bunge,” alisema.
Waziri Mkuu alisema chini ya mchakato huo, Tume ilianzisha majimbo mapya 25  ambapo majimbo 19 yalitokana na ongezeko la Halmashauri mpya; na majimbo sita yalitokana na kigezo cha wastani wa idadi ya watu.
Hata hivyo, Waziri Mkuu alibainisha kwamba kwa sasa Serikali haina mpango wa kuongeza maeneo mapya ya utawala zikiwemo wilaya na mikoa mipya kwa sababu bado inaendelea kujengea uwezo wa rasilmali watu na vitendea kazi katika maeneo mapya ya utawala yaliyopo hivi sasa.
Bunge limepitisha bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2016/2017.

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO SAID MECKY SADICK AFANYA KIKAO NA WATUMISHI WILAYA YA HAI.

April 27, 2016

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Said Mecky Sadicky akizungumza na watumishi,wakuu wa idara za Halmashauri na Wenyeviti wa vijiji na vitongoji katika wilaya ya Hai wakati wa kikao cha utamburisho kilichoafnyika katika ukumbi wa KKKT Bomang'ombe.
Baadhi ya viongozi wa Taasisi mbalimbali katika wilaya ya Hai wakiwa katika kikao hicho.
Mkuu wa Wilaya ya Hai ,Gelasius Byakanwa akizungumza katika kikao hicho.
Baadhi ya watumishi na viongozi mbalimbali wa Dini wakiwa katika kikao hicho.
Mkurugenzi wa Halmshauri ya wilaya ya Hai,Said Mderu akijibu hoja mbalimbali zilizoibuliwa katika kikao hicho.
Baadhi ya Wenyeviti wa vitobgoji na vijiji,
Baadhi ya Wenyeviti wa vitongoji na vijiji wakiuliza maswali wakati wa kikao hicho.
Viongozi wa dini pia waliwasilisha hoja zao kwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadick

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini
Programu ya Fursa Kwa Watoto yazinduliwa Dar, lengo kuboresha elimu ya awali

Programu ya Fursa Kwa Watoto yazinduliwa Dar, lengo kuboresha elimu ya awali

April 27, 2016

_MG_9991
Na Rabi Hume
Kwa kutambua umuhimu wa elimu kwa watoto ambao ndiyo watakuja kuwa viongozi wa baadae nchini, programu mpya inayofahamika kama Fursa Kwa Watoto imezinduliwa leo ikiwa na malengo ya kuboresha elimu kwa watoto wanaoanza elimu ya awali ili kuwafanya kuwa na uwezo pindi wanapoanza elimu ya shule ya msingi.
Akizungumzia programu hiyo, Mratibu wa Elimu ya Awali kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo, Clarence Mwinuka amesema kuwa kabla ya kuletwa kwa programu hiyo kulikuwa na matatizo ambayo yakikabili elimu ya awali hivyo kuwafanya wanafunzi wanaomaliza elimu hiyo kutokuwa na uwezo wa kutosha kuanza elimu ya msingi.
Amesema kupitia programu hiyo ambayo kwa kuanzia itafanyika Mwanza na Moshi ambapo itafanyika kwa miaka miwili na baada ya hapo watawachunguza watoto hao kama watakuwa wamekuwa na uwezo wa kutosha kwa ajili ya kujiunga na elimu ya msingi.
“Kila mtoto anatakiwa kuanzia elimu ya awali na kupitia programu hii walimu watapewa mafunzo, vifaa vitatolewa na kuwatengenezea mazingira mazuri ya kuwapa motisha alafu baada ya programu kumalizika tutaona matokeo yakoje,” amesema Mwinuka.
DSC_0902
Mratibu wa Elimu ya Awali kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo, Clarence Mwinuka akizungumzia hali ya elimu ya awali ilivyo nchini na mafanikio yanayoweza kupatikana kutokana na programu hiyo. (Picha zote na Rabi Hume wa MoDewjiBlog)
Nae Mtendaji Mkuu wa Dubai Cares ambao dhiyo wadhamini wa programu hiyo, Tariq Al Gurg amesema wameamua kudhamini programu hiyo nchini ili kusaidia kukuza elimu nchini.
Amesema Falme za Kiarabu imekuwa nchi ambayo inashirikiana na Tanzania katika mambo mbalimbali na hivyo wanaamini programu hiyo itakuwa na matokeo mazuri na kuwafanya wanafunzi wanaoingia kuanza elimu ya msingi kuwa na uwezo wa kutosha.
“Tumesaidia programu hii ili kuboresha elimu ya Tanzania ambayo itafanyika mpaka 2018, tuna tumaini itafanikiwa,” amesema Gurg.
DSC_0822
Mtendaji Mkuu wa Dubai Cares, Tariq Al Gurg akizungummzia udhamini wao kwa programu hiyo na matarajio yao. Kushoto ni Meneja Programu wa Dubai Cares, Saeed Alissmaily.
Kwa upande wa Mkurugenzi wa Shirika la Crossfire nchini ambayo inahusika maendeleo ya elimu kwa watoto, Graig Ferla amesema ni jambo zuri kuwekeza katika elimu ya watoto kwa ajili ya matokeo mazuri ya baadae kwa kuanzia darasani hadi katika maisha ya kawaida.
DSC_0862
Mkurugenzi wa Shirika la Crossfire nchini, Graig Ferla akizungumzia jinsi programu hivyo inaweza kufanikiwa nchini na umuhimu wa kuwekeza katika elimu kwa kuanza na elimu ya awali. Kulia ni Meneja Programu wa Dubai Cares, Saeed Alissmaily na Mtendaji Mkuu wa Dubai Cares, Tariq Al Gurg
DSC_0878
Mkuu wa Elimu kutoka Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), Cecilia Baldeh akizungumzia umuhimu wa kuwa na mipango wa kuboresha elimu nchini hasa kutokana na kuwa na waziri ambaye yupo tayari kuona hilo likifanyika. Kushoto ni Mratibu wa Elimu ya Awali kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo, Clarence Mwinuka na Mtendaji Mkuu wa Dubai Cares, Tariq Al Gurg.
_MG_9991
Uzinduzi wa programu ya Fursa Kwa Watoto ukifanyika.
DSC_0899
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka Tanzania na Falme za Kiarabu (UAE) waliohudhuria mkutano wa uzinduzi wa programu hiyo.
CCM ZANZIBAR YATOA MSAADA WA VIFAA VYA SH. MIL.5 KWA WAHANGA WA MAFURIKO NA KIPINDUPINDU ZANZIBAR

CCM ZANZIBAR YATOA MSAADA WA VIFAA VYA SH. MIL.5 KWA WAHANGA WA MAFURIKO NA KIPINDUPINDU ZANZIBAR

April 27, 2016

zan1 
Katibu wa kamati maalum ya NEC, idara ya itikadi na uenezi CCM Zanzibar Bi, Waride Bakar Jabu akimkabidhi misaada Katibu mkuu wa ofisi ya makamo wa pili wa rais, Joseph Abdallah Meza huko kwa ajili ya kuwasaidia wahanga wa mafuriko waliopo kambi ya mwanakwere “C” Unguja.Katibu wa kamati maalum ya NEC, idara ya itikadi na uenezi CCM Zanzibar Bi, Waride Bakar Jabu akimkabidhi misaada Katibu mkuu wa ofisi ya makamo wa pili wa rais, Joseph Abdallah Meza huko kwa ajili ya kuwasaidia wahanga wa mafuriko waliopo kambi ya mwanakwere “C” Unguja.
zan2 
Katibu wa kamati maalum ya NEC, idara ya itikadi na uenezi CCM Zanzibar Bi, Waride Bakar Jabu akikagua wahanga wa mafuriko katika kambi ya mwanakwere zanzibar. 
zan3 
Kambi ya kipindupindu iliyopo chumbuni zanzibar.
…………………………………………………………………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.
CHAMA chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimewataka wananchi kuendelea kufuata kanuni na taratibu zinazotolewa na  wataalamu wa kiafya ili kujikinga na maambukizi ya maradhi ya kipindupindu yaliyopo nchini.
Wito huo umetolewa na Katibu wa Kamati Maalum NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar,   Waride Bakar Jabu katika ziara ya kuwatembelea na kuwafariji wagonjwa wa  Kipindupindu wa kambi iliyopo Chumbuni Zanzibar, alisema endapo wananchi watafuata kanuni za kiafya itasaidia kutoweka  ugonjwa huo kwa haraka.
Waride alisema CCM itaendelea kutoa misaada ya hali na mali kwa wagonjwa wa kipindupindu ili kusaidia serikali huduma za uendeshaji kwa wagonjwa hao.
“ Tunawaomba wananchi waendelee kuweka mazingira yao katika hali ya usafi sambamba na kutumia maji salama, vyoo kuwa visafi na wagonjwa wenye dalili za maradhi hayo kupelekwa haraka katika kambi za kipindupindu.
Pia CCM inawapa pole wananchi wote waliopata maradhi ya kipindupindu na kuwasihi waendelee kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu cha matibabu yao.”, alisema Bi, Waride na kuzisihi taasisi zingine za serikali na binafsi kutoa misaada kwa wagonjwa hao kwani maradhi ya Kipindupindu hayana itikadi za kisiasa bali yanawapata wananchi wote.
Aliwashauri wanawake nchini ambao ni walezi wa watoto na mama wa nyumbani kuacha tabia ya kutupa ovyo pempasi za kuwafungia watoto kwani nazo ni miongoni mwa vitu vinavyopelekea kuenea kwa maradhi ya kipindupindu nchini.
“ Wanawake tukumbuke kuwa kila janga lolote sisi pamoja na watoto  ndiyo waathirika wa mwanzo hivyo  lazima tuwe makini katika kuweka mazingira yetu katika hali ya usafi pia tusitupe pempasi ovyo bali tuziweke katika sehemu zinazostahiki.” Alisisitiza Waride.
Naye Daktari dhamana wa Wilaya ya Magharibi Unguja ambaye pia ni Mkuu wa Kambi ya Kipindupindu Chumbuni Zanzibar, Ramadhan Mickdad Suleiman ameshukru msaada uliotolewa na CCM na kuahidi kuutumia kwa malengo yaliyokusudiwa.
Akitoa takwimu za hali ya maambukizo ya ugonjwa huo kwa sasa, Mickdad alisema ya hali ya maambukizo kwa sasa imepungua kutoka wagonjwa 40 kwa siku hadi 21 wanaolazwa katika kambi hiyo.
Alisema hali hiyo imetokana na utekelezaji wa  agizo la Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein alipowaagiza wananchi wanaofanya biashara za vyakula na vinywaji kuacha kuuza kwa muda ili kudhibiti kupunguza kasi ya maambukizi ya kipindupindu.
Alifafanua kuwa mpaka sasa kambi hiyo tayari imeshapokea wagonjwa 2026 waliopatiwa matibabu na kupona na wakaondoka na kati ya hao wamefariki wagonjwa 43 mpaka sasa.
“ Tunaishauri jamii kudumisha usafi wa vyoo na kula vyakula na maji vilivyokuwa salama kwani ugonjwa huu unaambukizwa kwa kasi katika maji ya kunywa yenye bakteria wa kipindupindu ama kumgusa maiti yaliyekufa kwa ugonjwa  au kugusana na mtu aliyeambukizwa kipindupindu.”, alisema Bi, Micjdad.
Aliwaomba wananchi wenye uwezo pamoja taasisi binafsi na serikali kutoa misaada kujitokeza kutoa misaada mbali mbali  ya kuwasaidia wagonjwa wa maradhi hayo waliopo katika kambi hiyo.
Mapema Waride alitembelea  na kuwafariji Wahanga wa mafuriko waliopo katika kambi ya  Shule ya Mwanakwerekwe “ C”  Unguja, aliwapa pole kwa matatizo yaliyowafika na kuwaomba waendelee kuwa wavumilivu katika kambi hili huku serikali ikiendelea kutafuta mbinu za kuwasaidia ili wapate makaazi katika sehemu salama.
Alitoa wito kwa wananchi wanaoishi katika sehemu za mabonde na sinazojaa maji wakati wa msimu wa mvua za maska kuhama haraka kabla hawajapata athari za kukumbwa na mafuriko hayo.
Kwa upande wake Katibu mkuu wa Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar, Joseph Abdallah Meza alitoa shukrani kwa uongozi wa CCM kwa msaada wao wa kuisaidia kambi hiyo yenye wananchi zaidi 400.
Alisema serikali bado inaendelea kuwahudumia wananchi hao ambao wamepata maafa ya mafuriko na kupoteza makaazi yao hivyo bado panahitajika misaada mbali mbali ya maji na vyakula pamoja na huduma za kibinadamu.
Misaada iliyotolewa na CCM katika ziara hiyo ina thamani zaidi ya shilingi milioni tano (5)  kwa upande wa kambi ya kipindupindu Chumbuni ni pamoja na Maji ya kunywa, Dawa za Chroline, Sabuni za kufulia na kuogea, viatu vya mvua, dawa ya choo na mashine za kufukizia dawa Sprayers.
Vingine vilivyotolewa  katika kambi ya wahanga wa mafuriko iliyopo Mwanakwere “C” ni pamoja na Pempasi za watoto, maji ya kunywa, sabuni za kuogea na kufulia, sabuni za chooni na madaftari ya wanafunzi.
MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA UONGOZI WA BARAZA LA TAWLA NA UONGOZI WA SKAUT LEOMAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA UONGOZI WA BARAZA LA TAWLA NA UONGOZI WA SKAUT LEO

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA UONGOZI WA BARAZA LA TAWLA NA UONGOZI WA SKAUT LEOMAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA UONGOZI WA BARAZA LA TAWLA NA UONGOZI WA SKAUT LEO

April 27, 2016

mak1 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na uongozi wa Baraza la Wanachama waChama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) wakati Uongozi huo ulipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es salaam leo April 27,2016  kwa lengo la kumpongeza na pamoja na kumuelezea malengo na mikakati ya kiutendaji ya Chama hicho.
mak2 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Baadhi ya Wawakilishi na Wanachama wa Chama cha SKAUT Nchini wakati ujumbe wa wawakilishi hao ulipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es salaam leo April 27,2016 kwa ajili ya kumuelezea Makamu wa Rais shuhuli zao za kiutendaji hasa katika kutoa mafunzo mbalimbali kwa Mtoto wa kike.
mak3 
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Wanachama wa SKAUT Nchini.Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Wanachama wa SKAUT Nchini.
mak4 

Makamu wa Rais Mhe. Samia akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Baraza la TAWLA
mak6 
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiungumza na Katibu Mkuu Kiongozi Baolozi Peter Kijazi Baada ya kuapishwa kwa Makatibu wa Mikoa leo April 27,2016 Ikulu Dar es salaam. (Picha na OMR)

USAID WAZINDUA MRADI WA UIMARISHAJI MIFUMO YA SEKTA ZA UMMA MKOANI MTWARA LEO

April 27, 2016


MKUU wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendegu akitoa hutuba yake wakati wa uzinduzi wa Uzinduzi wa kimkoa wa Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma, unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID).
 Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Fatma Ally akizungumza wakati wa Uzinduzi wa kimkoa wa Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma, unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID).
 Abdul Kitula ambaye ni mtaalam wa fedha wa mradi wa PS3 akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mradi huo wakati wa uzinduzi hii leo mjini Mtwara.
Mwakilishi wa USAID, Laura Kikuli alikuwepo na kutoa salamu zake katika uzinduzi huo a,mbao ulishirikisha watendaji wa Halamashauri zote za Mkoa wa Mtwara.
 Baadhi ya viongozi wa meza kuu wakifuatilia hotuba za ufunguzi
 Washiriki mbalimbali ambao ni watendaji kutoka Halmashauri za Mkoa wa Mtwara wakifuatilia mada katika uzinduzi huo.
 Mkurugenzi Msaidizi Rasilimali watu kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Miriam Mmbaga akisema neno.
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendegu pamoja na wakuu wa Wilaya za Mkoa huo wakifuatilia mawasilisho kutoka kwa maafisa Mradi wa PS3.
 Afisa Rasilimali watu wa  mradi wa PS3, Godfrey Nyombi akitoa mada.
**************
Uzinduzi wa kimkoa wa Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma, unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID), umefanyika mjini Mtwara  siku ya Jumatano na Alhamisi, Aprili 27-28, 2016.

Mradi huo ujulikanao kwa Kiingereza kama Public Sector Systems Strengthening (PS3) ni wa miaka mitano, na utafanya kazi na Serikali Kuu pamoja na Halmashauri 97 katika mikoa 13 ya Tanzania bara. 
PS3 inalenga kuunda ushirikiano na Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kuimarisha mifumo ya sekta za umma yakiwemo masuala ya utawala bora, rasilimali watu, fedha, utoaji wa taarifa, na tafiti tendaji.  Ushirkiano huu wa PS3 katika ngazi ya Serikali kuu na  Halmashauri, una nia ya kukuza utoaji, ubora, na matumizi ya huduma za umma, hususan kwa jamii ambazo hazijanufaika vya kutosha.

Katika uzinduzi huo, mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana, na uzinduzi ulihudhuriwa pia na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Dodoma ambaye amehamishiwa mkoa wa Songwe, Chiku Galawa.  Watu takribani 180 walihudhuria.  Washiriki wa uzinduzi huo walikuwa ni: Katibu Tawala wa Mkoa (RAS), Wakuu wa Wilaya za Dodoma, Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wajumbe wa Sekretarieti ya Mkoa, na Wajumbe  wa Timu ya Mejenimenti kutoka kwenye Halmashauri. 

Mkoa wa Dodoma una Halmashauri  nane, ambazo ni Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, na Halmashauri ya Mji wa Kondoa.

PS3 ni mradi wa miaka mitano ambao umeandaliwa na USAID kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania, na unafadhiliwa na USAID.  Unatekelezwa na mashirika saba yakiwepo ya kitaifa na kimataifa, ambayo ni:  Abt Associates Inc., kama mtekelezaji mkuu, na watekelezaji wasaidizi ambao ni Taasisi ya Benjamin Mkapa (BMF), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo cha Mafunzi ya Serikali za Mitaa Hombolo (LGTI), Taasisi ya Ushauri Tanzania (TMA), Broad Branch Institute, Intra Health International, na Urban Institute. 

Mikoa 13 ya Tanzania Bara ambako mradi utatekelezwa ni: Iringa, Dodoma, Kagera, Kigoma, Lindi, Mara, Mbeya, Morogoro, Mtwara, Mwanza, Njombe, Rukwa, na Shinyanga.

PS3 itaimarisha mifumo katika ngazi ya Taifa, Mkoa na Halmashauri. Mradi utahakikisha mifumo iliyopo katika ngazi ya Halmashauri inaimarishwa kupitia kitita cha afua zilizoundwa kwa ajili ya kuongeza ufanisi wa utoaji huduma kwa wananchi wa Tanzania.  Mafanikio yanayotarajiwa ni pamoja na:

·   Utawala Bora na Ushirikishwaji wa Raia: Uimarishaji wa utawala katika ngazi ya kitaifa na ya Mamlaka za Serikali za Mitaa, ili kuweza kutumia rasilimali kwa uwazi, kuwezesha ushiriki wa wananchi katika kupanga, kufuatilia, na kutoa matokeo katika kila sekta.

·   Rasilimali Watu: Kuongezeka kwa usawa katika mgawanyo wa rasilimali watu kwa ajili ya utoaji wa huduma bora kwenye maeneo yenye uhitaji zaidi.  Kuimarisha mfumo wa ajira pamoja na kudumu kwa watumishi katika ajira serikalini.

·   Fedha: Ongezeko la pato la ndani kwa ajili ya huduma za umma, kuongeza ufanisi  katika matumizi ya fedha za umma, na pia kuongeza uwiano kati ya kiasi cha fedha kilichotumika na mali iliyonunuliwa.

·   Mifumo ya Mawasiliano: Kuimarisha mifumo ya utoaji taarifa iliyopo nchini, pamoja na matumizi ya takwimu kwa wadau.

Utafiti Tendaji: Tafiti Tendaji muhimu zitakazosaidia mradi kujua changamoto na mikakati ya kuzishughulikia changamoto hizo. Tafiti hizi zitasaidia kugundua fursa zilizopo na kuzitumia kuweza kupata matokeo yanayotarajiwa.  Pia tafiti hizo zitasaidia kuboresha maamuzi serikalini.        
 Mtaalam wa Mawasiliano na Takwimu wa Mradi wa PS3, Desideri Wengaa akitoa mada juu ya mawasiliano na utoaji takwimu sahihi.
 Washiriki wakifuatilia kwa makini.
 Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendegu akisisitiza jambo
Wakuu wa Wilaya wakifuatilia mada
 
 Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendegu akimpa mkono wa shukrani Afisa wa Mradi wa PS3, Abdul Kitula baada ya uzinduzi. Kushoto ni Mwakilishi wa USAID, Laura Kikuli.
 
 Wakuu wa Wilaya wakijadiliana jambo

Picha mbalimbali za makundi tofauti zilipigwa baada ya uzinduzi huo.