YANGA,URA HAKUNA MBABE

July 21, 2013
Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam.

TIMU ya Yanga leo imeshindwa kutamba  mbele ya Wanganda baada ya kulazimisha sare ya goli 2-2,katika mchezo wa kirafiki ulifanyika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mchezo huo ulikuwa wa kusisimua kutokana na timu zote kuonyesha kandanda safi na la kuvutia lililowafanya mashabiki kushangili kila wakati huku Simba wakionekana kuwashangilia URA.

Katika mchezo huo timu zote zilishambuliana kwa zamu huku URA,wakionekana kuutawala mchezo katika kipindi cha kwanza.

Dakika ya 9,Yanga walipata faulo nje kidogo ya 18,baada ya Jerison Tegete kufanyiwa madhambi na kipa wa URA,lakini faulo hiyo haikuzaa matunda.

Katika dakika ya 14 Tegete tena aliunganisha mpira kwa kuachia kiki kali baada ya kupata krosi kutoka kwa Saidi Bahanuzilakini lilipaa juu.

Timu ya URA,ilifanya shambulizi la ngumu mnamo dakika ya 27,baada y mshambuliaji wa timu hiyo Ngawe Emanuel kuachia mkwaju mkali ambao kipa wa Yanga Deogratus Munis 'dida',kudaka shuti hilo ndani ya eneo la hatari.

URA,waliliandama kama nyuki lango  la Yanga ambapo katika dakika ya 42,Lutimba Yoyo aliiandikia timu yake goli la kwanza baada ya kuwatoka walinzi wa Yanga na kuachia mkwaju mkali ulimshinda mlinda mlango wa Yanga na kuukwamisha nyavuni.

Kipindi cha pili timu zilianza mchezo kwa kasi kila moja ikitaka kupata ushindi kutokana na maelekezo waliyopata kutoka kwa makocha wao.

Matunda  ya mapunziko yalionekana kuwa mazuri kwa URA,ambapo walifanikiwa kushinda goli la pili kupitiakwa mshambuliaji wake aliyefunga goli la kwanza Lutimba Yoyo baada y kupiga faulo na kujaa kimiani huku ikimuacha Dida asijue la kufanya.

Baada ya kuona mambo magumu Yanga walifanya mabadiliko walimtoa Saidi Bahanuzi na nafasi yake ikachukuliwa na Abdalah Mguli.

Mabadiliko hayo yalizaa matunda katika dakika ya 58,Abdalah Mguli aliwainua mashabiki wa Yanga baada ya kufunga goli la kwanza.

Yanga walizi kucharukua wakiliandama lango la URA kama nyuki ambapo dakika ya 66,Didier Kavumbagu anaisawazishia Yanga baada ya kupata krosi safi na kuunganichwa kwa kichwa kutoka kwa Juma Abdul.

Yanga waliendelea kutandaza soka la uhakika huku URA ,wakionekana  wamechoka ambapo dakika za lala salama waliandika goli la tatu kupitia kwa Jerison Tegete lakini muamuzi wa mchezo huo Kenedy mapunda alipiga filimbi ya kuotea na mpaka mwisho wa mchezo magoli 2-2.

Kikosi Yanga:

Deogratus Munis,Juma Abdul,Oscal Joshua,Ibrahimu Job Rajabu Zahir,Salum Terela,Said Bahanuzi/ Haruna Niyonzima,Hamisi Thabit/Bakari Masood,Didier Kavumbagu,Jerison Tegete,Shabani Kondo/Abdalah Mguli.
Tanga Beach Resort Winner for BID Internation Quality Summit Award in New york 2013

Tanga Beach Resort Winner for BID Internation Quality Summit Award in New york 2013

July 21, 2013
http://imarpress.com/mag_content/award/13-ny/cabecera.jpg
Award Winners at the 2013 Business Initiative Directions (B.I.D.) Convention in New York, from left to right: Édgar Samaniego Rojas, Chancellor of Universidad Central del Ecuador; Thomas Cooney, Director of Luna-National Food Industries Company Ltd; Alexey Abrameytsev, Chairman of the Board of RusslavBank; Jose E. Prieto, President and CEO of B.I.D.; Metin Recepoglu, General Manager of Delta Group; and Laura Collada, Managing Partner of Dumont Bergman Bider.
Leaders Joined Under BID Quality Achievement
Tanga Beach Resort from Tanzania, winner of the BID International Quality Summit Award in New York 2013
New York played host to this year's BID International Quality Summit Convention, where professionals and business representatives from around the world gathered in recognition of achievements and recent successes. In particular, the convention celebrated quality in business and operations. Award winners demonstrated commitment to the criteria of the QC100 TQM Model, which ensures customer satisfaction and cost efficiency at every level of activity.
Among this year's winners, Joseph Chome Ngonyo of Tanga Beach Resort, from Tanzania, proudly accepted the International Quality Summit Award in the Gold Category at the BID Quality Convention in New York. The company has made huge strides this year as a leader not only for its sector, but also in Tanzania. The Award came as an ideal way to celebrate yet another successful year of operations well underway.
Business Initiative Directions selected New York, considered the world's most important city economically and culturally, as it is the reference point for international businesses. With a population of over 8 million inhabitants within an area of 1,214 square kilometers, it is distinguished among other cosmopolitan cities as the location of the United Nations and with its stock market as the center of the global economy. It is also a cultural and entertainment center with a wealth of monuments of great historical value: the Statue of Liberty, Rockefeller Center, the Empire State Building, its museums, most notably the Museum of Modern Art (MOMA), the center of theatrical productions (Broadway) and the location of the world's most visited media enclave- Times Square, all of which have made it the perfect city to present the B.I.D. International Quality Awards.
http://imarpress.com/mag_content/award/13-ny/TangaBeachResort.jpg
Tanga Beach Resort won the International Quality Summit Award in the Gold category in New York in the presence of leaders and representatives from 52 countries at the International Quality Summit Convention. The prestigious award, representing the height of quality and innovation in a field, is presented by BID President and CEO, Jose E. Prieto. From left to right: Jose E. Prieto, President and CEO of B.I.D, Joseph Chome Ngonyo, General Manager of Tanga Beach Resort, Craig Miller, President of the QC100 and Norman Ingle, President of the Quality Mix.
Joseph Chome Ngonyo stood before the international community gathered, sharing the company's achievements as well as its future ambitions and goals. Defiant in the face of current difficulties in the global economy, Tanga Beach Resort strives to excel in quality each day, creating a competitive advantage in its industry. For this reason, Tanga Beach Resort was named a winner of the 2013 BID International Quality Summit Award in New York; a trophy which BID presents to those companies and organizations from around the world that best adhere to excellence and innovation in their practices, putting quality first at all levels of organization.
Leaders awarded through the BID community clearly demonstrate creativity and leadership in their respective sectors. This year, such winners included Luna-National Foof Industries Company, from Saudi Arabia. A top exporter of dairy and canned food items to over 60 countries, the National Food Industries Company factory has made it the largest integrated food industry in the Middle East. Cutting edge modern facilities, its own can-making facility and tetra pack line make it a comprehensive food industry.
Innovation expert, was also awarded in New York, WIR Group Indonesia. With a presence in London, Europe, and throughout Asia, WIR Group of Companies is rapidly expanding and has become an expert in branding in the innovation, technology, and entertainment sectors. Its prestigious clientele includes names like Sky, McDonald's, and Ronald McDonald's House Charities.
Likewise receiving the honor was Universidad Central del Ecuador. Founded in 1826, UCE is both the largest and oldest University in Ecuador with a student body of 50,000. Its main campus is in Northern Quito with locations in different cities as well as the Galapagos Islands, offering a full range of academics.
Original Birth Limited, from Egypt. A leader in luxury hospitality Original Birth has pioneered innovation in its field through conceptualizing, creating and managing boutique hotels, restaurants, events and hospitality consulting. Original Birth is part of Tatanaki Group, an international conglomerate comprised of a vast range of companies from oil drilling to construction, which operate in Europe, Asia, the Middle East and Africa.
Batumi Oil Terminal, from Georgia. An expert in transshipment services for oil products from Kazakhstan, Azerbaijan, Turkmenistan, Georgia, as well as other countries located on the shore of the Black Sea, Batumi Oil Terminal, along with the Batumi Sea Port, is a key player for both Georgia and Kazakhstan, providing a strategic alternative export route for Kazakh crude.
The companies honored in New York were recognized not only for their entrepreneurial achievements, but also for their dedication to continuous improvement and innovation, key concepts of the QC100 Total Quality Management Model. Seeking to increase customer satisfaction and optimize efficiency, the model promotes an organizational culture of engagement and a proactive approach to improving processes.
Each of the winning companies in New York this year has proven the success of the QC100 TQM Model, and serves as a fantastic example for other companies in today's rapidly changing business environment. By making customer satisfaction the highest measure of quality, BID award winners set the benchmark in their sectors and contribute to the social and economic development of their countries, paving the way for world-changing initiatives. A key example can be seen through Tanga Beach Resort, whose spirit of innovation and positive growth has overcome and indeed thrived in the current global economic climate.
The enduring commitment to Quality, one of the core requirements for receiving a BID Award, can be witnessed through the distinguished companies previously honored with a BID Quality Award. Companies which already share BID's corporate seal are present in more than 170 countries and include world-renowned names on the Fortune 500 list such as: Wal-Mart Stores (1) Indian Oil Corporation Limited (83); ArcelorMittal (70); and Alcoa Helmet (439).
Other previous BID winners worthy of mention include Turner Construction (USA); Haki (Sweden); Ansaldo Energy (Italy); Zepter (Austria); RAO-Unified Energy Systems (Russia); Als & Cachou-TBWA (France); Tata Group (India); Plamex-Plantronics (USA); Korea Electric Power (264); Beijing COFCO Plaza Development (393); Dogus Holding A.S. (Tukey); Franklin Electric (USA and Mexico); QMS International from the United Kingdom, FSUE VO "Safety" (Russia); and Viking Line (Finland).

“CHIPUNGAHELO aipigia saluti Kokoliko Digner”

July 21, 2013


(Mkurugenzi wa Kampuni ya Kokoliko Disgner, Aisha Kisoki “Mama Sophia akiwa bize ofisni kwake hivi karibuni)

Na Mwandishi Wetu, Tanga.

RAIS wa Miss Utalii nchini, Gidion Chipungahelo amesema kampuni ya Kokoliko Disgner ndio kampuni pekee waliyoamua kuipa kibali cha kuwavalisha washiriki wa Miss Utalii hapa nchini na nje ya nchi lengo likiwa ni kutambua mchango wao kwenye tasnia hiyo.

Akizungumza jana, Chipungahelo alisema licha ya kuwavalisha na kuwabuni mavazi washiriki wa miss Utalii hapa nchini lakini watawatangaza kitaifa na kimataifa kwenye mashindano ya Tourist Model of the world itakayofanyika mwezi septemba mwaka huu nchini Japan kwa kuwa nao.

Chipungahelo alisema suala lengine ambalo kampuni hiyo itakalolifanya ni kuondoka nao hapa nchini kwenda kushuhudia shindano la Miss Utalii Dunia ambalo litafanyika Equatorial Guinner desemba 10 mwaka huu.

 “Mchango wa kampuni hiyo ni mkubwa sana hasa kwenye suala zima la ubinunifu wa mavazi hivyo hii itakuwa fuksa adimu kwao kuwaonyesha mavazi yao na mitindo mbalimbali kwenye nchi hizo “Alisema Chipungahelo.

Alisema safari nyegine ya tatu ambao watakuwa nao ni kwenye shindano la Miss tournament Umoja wa Mataifa ambalo litafanyika Florida nchini Marekani na kueleza watashirikiana na kampuni ya Sophia production ,kokoliko kwa ajili ya kwenda kuwatangaza  kama wabunifu wa mavazi wa kitanzania.

Aliongeza kwa kuishukuru Kokoliko disgner kwa kushirikiana na kampuni ya Sophia Production kwa kubuni na kutengeneza mavazi yaliyopelekea kuchangia warembo walioshiriki mashindano hayo kutoka hapa nchini kufanya vizuri.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya Kokoliko Disgner, Aisha Kisoki “Mama Sophia”alisema kampuni hiyo itaendelea kuwabunia mavazi washiriki hapa nchini lengo likiwa ni kutangaza asili ya watanzania.

Mwisho.

WABUKINI KUCHEZESHA STAR, UGANDA

July 21, 2013
Na Boniface Wambura,Dar es Salaam.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Madagascar kuchezesha mechi kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Uganda (The Cranes) itakayochezwa Jumamosi (Julai 27 mwaka huu) Uwanja wa Mandela ulioko Namboole nje kidogo ya Jiji la Kampala.


Waamuzi wataongozwa na Kanoso Abdoul Ohabee wakati mwamuzi msaidizi namba moja ni Andirvoavonjy Pierre Jean Eric. Mwamuzi msaidizi namba mbili ni Jinoro Velomanana Ferdinand huku Andriamiharisoa Hubert Marie Bruno akiwa mwamuzi wa mezani (fourth official).


Kamishna wa mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya mwisho kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) ni Ismail Kamal kutoka Ethiopia.


Mechi hiyo namba 38 itachezwa kuanzia saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki. Taifa Stars ilipoteza mechi ya kwanza iliyochezwa Julai 13 mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa bao 1-0.


Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iko kambini jijini Mwanza ikijiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itacheza Fainali za CHAN mwakani nchini Afrika Kusini.