AZAM FC WAFUNGA 'SOFA ZA HATARI' CHAMAZI, KOMBE LA SHIRIKISHO PALE PALE MWAKANI

December 19, 2013

Imewekwa Desemba 19 saa 2:23

Mafundi wakiendelea na zoezi la uwekaji wa viti vya kisasa katika majukwaa ya Uwanja wa Azam Complex, uliopo Chamazi, Dar es Salaam. Klabu ya Azam inataka kuutumia Uwanja huo kwa michuano ya Afrika pia mwakani na inapambana na muda kuhakikisha uboreshaji unakamilika mapema ili mechi zake za Kombe la Shirikisho icheze hapo mwakani.
Siti za kulala

SASA KESI ZA MAPENZI HADI KWA MADOGO: MWANAFUNZI WA KIKE WA KIDATO CHA TATU ACHOMWA KISU TUMBONI NA MWANAFUNZI MWENZAKE WA KIKE KWA WIVU WA MAPENZI‏

December 19, 2013
Na Walter Mguluchuma .Mpanda Katavi
Mwanafunzi  wa kidato cha  tatu  katika shule ya Sekondari ya  Istiqama  iliyoko mjini Mpanda  Mkoa wa Katavi  (17) jinalake limehifadhiwa  amejeruhiwa  kwa kuchomwa  na kisu mara mbili tumboni  na mwanafunzi mwenzake wa kike  (15)   wa kidato cha tatu wa shule hiyo  kwa kisa cha kugombea mwanaume.
Kwa mujibu wa Kamanda wa  Polisi wa Mkoa wa Katavi Kamishina Dhahiri Kidavashari  alisema tukio hilo  la mwanafunzi huyo kuchomwa kisu  tumboni mara mbili lilitokea hapo  Desemba 14 mwaka huu majira ya saa kumi na mbili  na nusu jioni katika eneo la mtaa wa Kashaulili  mjini hapa 

TASWIRA ZA KIJIJI CHA QUNU ALIKOZIKWA MZEE NELSO MANDELA JUMAPILI DESEMBA 15, 201

December 19, 2013
IMEWEKWA DESEMBA 19 SAA 01;21MCHANA
 Daraja la waendao kwa miguu likipita juu ya barabara mpya ya lami inayojengwa kuelekea kijijini Qunu.
Siku ya mazishi barabara ya kuelekea Qunu ilifungwa na ni magari yaliyokuwa na kibali tu ndiyo yaliyoruhusiwa kupita
Ulinzi ulikuwa mkali kila sehemu kijijini Qunu
Wageni wakiwa katika geti kuu la nyumba ya Mzee Mandela hapo Qunu

MAANDALIZI YA MWILI WA ALIYEKUWA KATIBU WA CCM MKOA WA IRINGA YAENDELEA MORTUARY YA HOSPITALI YA RUFAA MKOA WA IRINGA

December 19, 2013
 Mzee Teming'ombe akilia  kwa  uchungu  kufuatia  kifo  cha kijana wake aliyekuwa katibu  wa CCM mkoa wa  Iringa Emanuel Mteming'ombe aliyerafiki usiku wa   kuamkia  leo  katika Hospital ya Rufaa ya  mkoa wa Iringa alikolazwa kwa  zaidi ya siku mbili
 waombolezaji wakiwa  ktk hospital ya rufaa ya mkoa wa Iringa katika maandalizi  ya mwili  wa aliyekuwa katibu wa CCM mkoa wa Iringa  hivi  sasa
 Waombolezaji  wakishusha jeneza  la kuuweka mwili wa katibu wa CCM mkoa wa Iringa

BREAKING NEWS.. KATIBU WA CCM MKOA WA IRINGA AFARIKI DUNIA

December 19, 2013


Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa Bw. Emanuel Mteming'ombe. Bw. Mteming'ombe
KATIBU  wa  chama cha mapinduzi  (CCM) mkoa  wa  Iringa Bw Emanuel Mteming'ombe amefariki  dunia katika hospital  ya  mkoa  wa  Iringa.
Katibu   huyo  alikuwa amelazwa  katika Hospital  ya  mkoa  wa  Iringa kwa  zaidi  ya siku moja akisumbuliwa  kwa ugonjwa athima na  leo amefariki  dunia.
Mwenyekiti  wa  CCM  mkoa wa  Iringa Jesca Msambatavangu  amethibitisha   juu ya taarifa  hiyo  na  kuwa  taratibu  za mazishi  zinafanywa .
Habari  zaidi  juu ya taarifa  hii  utaendelea  kuzipata  endelea  kutembelea  mtandao  huu

WATU WANNE WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA TUHUMA ZA UJAMBAZI MOSHI.

December 19, 2013
 Afisa wa polisi katika ofisi ya kamanda wa polisi akipanga vitu mbalimbali walivyokutwa navyo watu
hao wanaotuhimiwa kuwa majambazi.
Laptop mbili pia zilikuwa ni miongoni mwa vitu walivyokutwa navyo.
 Vifaa mbalimbali vya kubomolea.
 Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro Koka Moita akionesha Vocha za mitandao mbalimbali walizokutwa nazo watu hao.
 Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro Koka Moita akionesha bunduki aina ya Shotgun waliyokutwa nao watu hao.

****************
IMEWEKWA DESEMBA 19 SAA 12:33 MCHANA.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Moshi 
 JESHI la polisi mkoani Kilimanaro, limewatia mbaroni watu 4 kwa tuhuma za kushiriki katika matukio mbali mbali ya uhalifu na unyangaji wakutumia silaha yaliyotokea mkoani hapa.
Kaimu kamanda wa jeshi hilo, Koka Moita, alisema jeshi hilo lilifanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa hao baada ya kukamata gari lenye namba za usajili T564 AUW aina ya Grand Mark 2 wenye rangi ya siliva, katika maeneo ya Kiusa Manispaa ya Moshi ambalo limesadikika kushiriki kwenye matukio hayo. 
 Alisema dereva wa gari hilo ambaye alifahamika kwa jina la Nicksoni Elias Urio (28) mkaazi wa Majengo Moshi alitoa ushirikiano mkubwa ambao ulipelekea kuwakamata watu 3 ambao wamesadikika kuwa majambazi walioshiriki katika baadhi ya mtukio mkoani hapa. 
 “ Baada ya kuwatia mbaroni watumiwa hao, operatini kali ilifanyika yakuwapekuwa na kubaini vitu mbali mbali ikiwemo ikiwemo bumbuki aina ya shotgun ikiwa imekatwa mtutu na kitako cha bunduki hiyo hivyo hatukupata namba zake”alisema na kuendelea kuwa “laptop, 2 aina ya dell na hp, Plate namba 3 na funguo za magari, simu 8 za mkononi , vocha za simu za mitandao yote , ambaye thamani yake haijatulikana, pamoja na vifaa mbali mbali vya kuvunjia”alisema Moita. Moita alisema Vocha za simu bado hazijajulikana thamani yake, na uchunguzi unaendelea marautakapokamilisha watuhumiwa watafikshwamahakamani. 
 Aidha Kamanda Moita aliwataka wananch kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kufichua matukio mbali mbali ya uhalifu yanayojitokeza mkoani hapa.  Kwa Hisani ya Michuzi Blog

MWENYEKITI CCM WILAYA YA TANGA AHAMASISHA MICHEZO KWA VIJANA.

December 19, 2013

 Na Oscar Assenga, Tanga.
MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Tanga (CCM)Kassim Mbuguni amesema endapo vijana watajituma na kuithamini michezo itaweza kuwa mkombozi wao wa baadae pamoja na jamii zao kwa ujumla.