RAIS WA CAF AWASILI TANZANIA
michezoRais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Dkt. Patrice Motsepe, amewasili rasmi nchini Tanzania asubuhi ya leo kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa Kamati Tendaji ya Shirikisho hilo.
Mutsepe amepokelewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere International Airport, Terminal 1, jijini Dar es Salaam.
Dkt. Motsepe ataongoza mkutano huo unaotarajiwa kufanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam, The Kilimanjaro.
Mkutano huo unatarajiwa kukutanisha viongozi mbalimbali wa soka barani Afrika kwa ajili ya kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya mpira wa miguu.
Kuwa mwenyeji wa mkutano huo ni ishara ya nafasi ya Tanzania katika ramani ya soka barani Afrika, hususan katika kipindi hiki cha maandalizi ya mashindano ya AFCON 2027.
AKWILAPO ATEMBELEA ENEO UNAPOJENGWA UWANJA WA AFCON ARUSHA
michezo
§ Atoa siku kumi na tano wasiokamilisha malipo ya viwanja vinavyozunguka uwanja kukamilishaAsisitiza waliomilikishwa viwanja kufanya maendelezo
Na Munir Shemweta, WANMM ARUSHA
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Akwilapo tarehe 11 Februari 2026 ametembeleo eneo unapojengwa uwanja wa kisasa wa mpira kwa ajili Mashindano ya Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON 2027) mkoani Arusha.
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetekeleza Mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi katika eneo lililopo pembezoni unapojengwa Uwanja wa mpira wa Afcon katika kata ya Olmoti Jiji la Arusha, mkoani Arusha.
Hata hivyo, pamoja na viwanja kuuzwa kwa ajili ya matumizi mbalimbali lakini kuna baadhi ya waliochukua viwanja kushindwa kukamilisha malipo ndani ya muda huku baadhi waliomilikishwa wakishindwa kuendeleza maeneo yao.
Akiwa katika eneo la uwanja huo, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo alijionea maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo ambapo alipongeza jitihada zinazofanyika za kuhakikisha uwanja huo unakamilika kwa wakati na hatimaye kutumika katika mashindano hayo makubwa ya Afrika.
Akigeukia wananchi waliochukua viwanja na kushindwa kukamilisha malipo kwa wakati, Mhe Akwilapo amewataka kuhakikisha wanafanya malipo ndani ya siku kumi na tano kuanzia tarehe 12 Februari 2026.
"Kuna wananchi walioomba viwanja katika maeneo yanayozunguka uwanja wa AFCON 2027 na kushindwa kukamilisha malipo ya viwanja hivyo, wanatakiwa kulipa ndani ya siku kumi na tano na baada ya hapo tutawanyang'anya na kuwapatia wengine". Amesema Akwilapo
Aidha, amesisitiza wananchi wenye hati milki za ardhi katika eneo linalozunguka uwanja huo kuhakikisha wanafanya maendelezo kwenye maeneo yao huku akiweka bayana kuwa, kama kuna mtu anayedhani hawawezi kufanya maendelezo katika muda wa kuelekea Mashindano ya AFCON 2027 basi airejeshe hati ili kupatiwa wale wanaoweza kufanya maendelezo.
Ujenzi wa mradi wa uwanja wa AFCON Arusha kwa sasa umefikia asilimia 74 na unatarajiwa kukamilika Julai, 2026.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa uwanja wa mpira unaotarajiwa kutumika katika mashindano ya mataifa ya afrika (AFCON 2027) jijini Arusha jana

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo (Kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Bi. Lucy Kabyemera wakipata maelezo ya mradi wa viwanja vinavyozunguka uwanja wa AFCON Arusha jana alipofanya ziara katika eneo hilo.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo (wa tatu kulia) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Bi. Lucy Kabyemera (kushoto) wakielekea katika uwanja wa AFCON wakati wa ziara ya siku moja katika maeneo ya uwanja huo jana. (PICHA NA WIZARA YA ARDHI)
AMBONI ADVENTURE RUN, FURSA YA KUTANGAZA MAPANGO YA AMBONI TANGA
michezoNa Kassim Nyaki, Amboni Tanga.
Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro imeshiriki na kudhamini mbio za AmbonI Adventure run zilizofanyika leo tarehe 31 Januari 2026 jijini Tanga kwa lengo la kutangaza vivutio vya utalii hususan mapango ya Amboni yanayosimamiwa na Mamlaka yah ifadhi ya Ngorongoro
Mbio hizo za umbali wa kimomita 6, 10 na 20 ambazo zimehudhuriwa na wakimbiaji zaidi ya 500 kutoka maeneo mbalimbali nchini zimeanzia katika viwanja vya Shule ya Sekondari Galanos hadi Mapango ya amboni ambapo washiriki wa mbio hizo wamepata fursa ya kufanya utalii wa ndani katika mapango hayo.
Kaimu meneja uhusiano wa Ngorongoro Hamis Dambaya ambaye ameshiriki mbio hizo kwa kukimbia kilomita 10 ameeleza kuwa Ngorongoro imeamua kuungana na wadau mbalimbali kuendelea kutangaza vivutio vilivyoko katika mapango ya Amboni ili yaendelee kujulikana kitaifa na kimataifa na kuvutia wageni wengi kutembelea na kuona vivutio vinavyopatikana katika mapango hayo na kupataa taarifa mbalimbali ikiwemo historia ya wapigania uhuru.
Msimamizi wa Mapango ya Amboni Afisa Uhifadhi Daraja la kwanza Ramadhan Rashid ameeleza kuwa baadhi ya vivutio vinavyopatikana katika Mapango ya Amboni ni pamoja na maumbo ya asili ya kijiolojia, vivutio vilivyochongwa na maji kama meli, mlima Kilimanjaro, kanisa, msikiti, shughuli za kimila na mataambiko, ndege ndani ya mapango, pango la jinsia, Pango la fatuma ambalo watu hulitumia kuomba mchumba wa kuoa, mimea ya aina mbalimbali, mto pamoja na mazingira asilia yanayopaambwa naa upepo mwanana wa bahari ya hindi.
Mkuugenzi wa Kale Amboni Caves Sophia Mulamula ameeleza kuwa Mbio za Amboni Adventure Run ambazo zimefanyika kwa msimu wa tatu na kuhudhuriwa na wakimbiaji takriban 500 zinatendelea kuboreshwa ili kuvutia wakimbiaji wengi zaidi mwaka ujao 2027
“Tumefanya tathmini kwa miaka hii miwili tumeona mbio hizi zinavutia watu wengi, tunaamini mwakani tunaboresha vitu vingi zaidi ili tupate wakimbiaji wengi kwa lengo la kutangaza vivutio vya utalii, kutangaza nchi yetu lakini kuendelea kuhamasisha utalii wa michezo” alilisitiza Mulamula.
WANAFUNZI 500 JIJINI TANGA WASHIRIKI BONANZA LA MICHEZO LA MICHEZO PLUS .
michezoNa Oscar Assenga, TANGA
BONANZA la Michezo maarufu kama Michezo Plus limekuwa na mvuto wa aina yake huku likifanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Tanga Ufundi kwa kushirkisha wanafunzi zaidi ya 500.
Wanafunzi hao kutoka shule 50 Jijini Tanga ambao walishiriki katika Michezo ya Mpira wa Miguu,Pete na Wavu huku wakionyesha vipaji vya hali ya juu hatua iliyoshangiliwa na wadau wa michezo ambao walijitokeza kushuhudia bonanza hilo
Akizungumza baada ya kumalizika kwa Bonanza hilo Afisa Michezo wa Jiji la Tanga na Mratibu wa Michezo Plus katika mradi unaotekelezwa na Jiji hilo ukifadhiliwa nan a Botnar Foundation chini ya Programu ya Tanga Yetu Lucy Michael alisema kwamba waliliandaamaalumu kwa ajili ya kujenga mahusiano na kuwajenga kiakili.
Alisema kwamba bonanza hilo litakuwa linafanyika kila mwaka mara mbili ambapo hilo limeanza kwa kufungua mwaka na kukaribisha wanafunzi na watafanya bonanza la vijana.
Awali akizungumza Mratibu wa Bonanza hilo Haji Milao alisema kwamba nia na madhumuni yake ni kuwaweka watoto sawa kwa ajili ya michezo ya Umistashumta mwaka huu 2026 ikiwemo kutengeneza afya za watoto ili waweze kuwa sawa na watoto wakiwa vizuri kwenye michezo hata darasani watakuwa vizuri.
Naye kwa upande wake Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Makorora Zuhuru Ally alisema michezo hiyo ina faida kubwa sana kwao kutokana na kwamba inawafanya wakutana na wenzao na kubadilisha mawazo jambo ambalo linawapa fursa.
MCC RAJAB AWAKABIDHI AFRICAN SPORTS BASI JIPYA, AHAIDI KUENDELEA KUISAPOTI IREJEE LIGI KUU
michezo
Na Oscar Assenga,TANGA


Alisema timu hiyo imekuwa ikisuasua kupanda daraja kwa muda mrefu kutokana na changamoto mbali mbali ikiwemo basi la kuwasafirisha wachezaji pamoja na benchi la ufundi hivyo uwepo wa basi hilo utasaidia kuwawezesha kuondokana nazo

Aliyasema hayo Januari 24 mwaka huu katika hafla ya kuukabidhi uongozi wa timu hiyo gari Jipya aina ya TATA lililogarimu takribani shilingi Milioni 170, katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Klabu hiyo barabara 12 Jijini Tanga .

Rajabu ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa (MCC) alisema kwamba kurudi kwa timu hiyo kongwe hapa nchini ambayo ilianzishwa mwaka 1936 kutarejesha heshima ya Mkoa wa Tanga kutokana na kwamba bila African Spots hakuna Coastal Union inayochangiwa na utani wa jadi timu hizo kama ilivyokuwa Simba na Yanga za Jijini Dar es Salaam.

Mbali ya kununua basi na kukabidhi, Mwenyekiti ameahidi kusaidia timu hiyo na kuiinua hadi kufikia kucheza ligi kuu ambapo ataipambania na kujenga Jengo la Ofisi la Gorofa tatu ikiwa ni pamoja na kununua gari kubwa zaidi wakati gari iliyokabidhiwa kubaki kuwa ya kuwapeleka wachezaji mazoezini.

Sambamba na kukabidhi gari hilo mwenyekiti huyo pia alitoa kiasi cha shilingi Milioni 30 na kukabidhi kwa uongozi wa timu ya Coastal Union kwa ajili ya kutatua changamoto kadhaa zinazowakabili.


Awali akizungumza katika Halfa hiyo Rais wa TFF Walles Karia aliwasihi wanachama kushirikiana na vionhozi ili kufanya maamuzi pamoja na kujitokeza uwanjani pindi timu zitakapokuwq zancheza kwani ndio jambo sahihi la kuvuta wawekezaji.

Lakini pia aliwasihi viwanja vya michezo vilivyopo Myanjani Technically Center, "kile kituo kipo na kinafanya vizuri sana lakini kinanufaisha vijana walioko nje ya Tanga, niwasiji kwamba mpeleke vijana pale ili timu zetu zipate wachezaji bora" alisema Karia.

Katika hafla hiyo alikuwepo Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma (Mwana FA) ambaye alisisitiza suala la wanachama kushirikiana na vionhozi wa timu hiyo na kuchangia kipato kwenye timu matokeo yataonekana.

"Kama tutakuwa na timu mbili (2) zinazoenda ligi kuu, hata uchumi wa Tanga utaimarika kupitia michezo, tuchangie timu kwa kwenda uwanjani na hata kununua jezi, kwa kufanya hivyo kutaimarisha timu zetu na wachezaji kuwa na ari uwanjani" alisema.
Katika kuinua timu hizo Naibu Waziri Mwana FA alitoa kiasi cha shilingi Milioni 10 ambapo kila timu imekabidhiwa kwa vionhozi wa timu zote mbili kiasi cha shilingi Milioni 5.

Rais Karia amewahakikishia Watanzania kwamba timu ya African Spots ikismama imara kama awali na Coastal Union ndiyo timu pekee ambazo zina uwezo wa kusimamishana na Simba na Yanga na siyo timu nyingine.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi, Dk. Batilda Buriani aliwataka vionhozi wa timu za mipira na wanamichezo wote kutumia fursa ambazo zipo mkoani humo katika kuimarisha timu na kuleta manufaa katika Mkoa.
"Mradi wa Bomba la mafuta nao una fursa katika michezo, kule Uganda wamesaidia kujenga uwanja wa mpira, na hata timu yetu ya Coastal Union imeshapeleka maombi yake tunasubiri utekelezaji mwengine uendelee" alisema
WAZIRI MAKONDA AKABIDHI BARUA YA RAIS DKT. SAMIA KWA RAIS WA CAF
michezo
.jpeg)

.jpeg)
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Paul Christian Makonda amekutana na Rais wa Shirikisho la Kandanda Barani Afrika (CAF) Dkt. Patrice Motsepe Jijini Rabat, Morocco na kukabidhi barua kutoka kwa Rais Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Pamoja na kukabidhi barua hiyo Mheshimiwa Makonda aliyeongozana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa amemhakikishia Dkt. Motsepe kuwa Rais Samia yupo tayari wakati wote kushirikiana na CAF katika utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo ya kandanda ikiwemo mashindano mbalimbali.
Amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika maandalizi ya kuwa wenyeji wa AFCON 2027 sambamba na Kenya na Uganda na kwamba imedhamiria kuonesha tofauti kubwa na mashindano yaliyopita.
Aidha, Makonda amemuomba Dkt. Motsepe kuiangalia Tanzania kimkakati ili mipango inayowekwa na Serikali ipate mafanikio makubwa yanayotarajiwa.
Kwa upande wake Dkt. Motsepe amemshukuru Rais Samia kwa kumuandikia barua na salamu zake za upendo na ushirikiano kwa CAF na amemhakikishia kuwa CAF ipo tayari kufanya kazi bega kwa bega na Tanzania ili kufikia maendeleo makubwa katika kandanda.
Motsepe ameelezea kufurahishwa na jitihada kubwa zilizofanywa na Rais Samia na Serikali anayoiongoza katika maendeleo ya mpira ikiwemo ujenzi wa miundombinu, kufanya mashindano ya CHAN 2024 kwa mafanikio makubwa na maandalizi mazuri yanayoendelea kuelekea AFCON 2027.
Amesema CAF itatuma timu ya wataalamu kwenda Tanzania kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali katika kukamilisha maandalizi makubwa ya AFCON 2027 ambayo yanatarajiwa kushirikisha nchi 28 badala ya 24.
Motsepe ameahidi kuja Tanzania hivi karibuni kujionea maandalizi mbalimbali ya AFCON 2027 na kukutana na viongozi kwa mazungumzo.
.jpeg)
MAGAMBA FOREST WALKATHON AND ADVENTURE SEASON III KUFANYIKA DESEMBA 17 HADI 20 MWAKA HUU
michezo
Na Oscar Assenga, LUSHOTO.
MATEMBEZI Maalumu ndani ya Hifadhi ya Misitu ya Mazingira Asilia Magamba (Magamba Forest Walkathon and Andventure Season 111) yenye lengo la kutangaza na kuhamasisha utalii zinatarajiwa kufanyika Desemba 17 -20 katika mji wa Lushoto mkoani Tanga huku maandalizi yakielezwa kukamilika kwa asilimia 85.
Akizungumza na Mtandao huo Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Misitu ya Mazingira Asilia Magamba, Christoganus Vyokuta amesema kwamba kuelekea mbio hizo wadau mbalimbali wa uhifadhi na utalii watapata fursa ya kujitangaza na kuonesha huduma na bidhaa zao mjini Lushoto.
Alisema kilele cha mbio hizo kitafanyika Desemba 20 ambapo washiriki watashiriki katika matembezi maalumu ndani ya Hifadhi ya Misitu ya Magamba ikiwa ni sehemu ya kutangaza pia vivutio vya utalii vilivyopo ndani ya hifadhi ya Mazingira Asilia ya Magamba wilayani humo
Mhifadhi huyo alisema pia lengo jingine la mbio hizo za Magamba Forest Walkathon and Adventure Season III ni kuunga mkono juhudi za Serikali katika uhifadhi wa mazingira na kukuza utalii ikolojia ikiwemo kuhamasisha Watanzania kutembelea vivutio vya asili vilivyopo nchini.
Mhifadhi huyo amewataka wananchi na wadau wa sekta ya utalii kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mbio hizo huku akisisitiza kuwa ushiriki wao ni muhimu katika kulinda rasilimali za asili na kuhakikisha uhifadhi endelevu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

TIMU YA MPIRA WA WAVU (VOLLEYBALL) YA WANAUME YA REA YAANZA KWA KISHINDO MASHINDANO YA SHIMMUTA
michezo
TIMU ya mpira wa wavu ya wanaume ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza mashindano ya Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMMUTA) kwa kishindo baada ya kuibuka na ushindi mkubwa dhidi ya timu ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea (TFRA).
Katika mchezo uliochezwa leo Novemba 27, 2025 katika viwanja vya Bwalo Mkoani Morogoro, wachezaji wa timu ya REA walionyesha kiwango cha juu cha mchezo na kasi iliyowaduwaza wapinzani wao, na hivyo kuweza kuwagaragaza TFRA kwa ushindi wa seti 2 kwa 1.
Ushindi huu wa mwanzo unatoa motisha kubwa kwa timu ya REA kuelekea michezo mingine, huku wakiwa na matumaini ya kutwaa ubingwa katika mashindano hayo yanayoendelea mkoani Morogoro.
Kocha wa timu hiyo alieleza kuridhishwa na juhudi za wachezaji wake na kuahidi kuendelea kuweka mikakati imara ili kuhakikisha REA inasalia kileleni mwa kundi hilo gumu.
Timu hiyo ambayo imeshiriki mashindano hayo kwa mara ya kwanza imeonekana kuwavutia mashabiki wengi waliokuwa katika viwanja hivyo.

BARRICK BULYANHULU YAENDELEA KUDUMISHA UHUSIANO MZURI NA JAMII KUPITIA JUKWAA LA MICHEZO
michezo
Mchezo kati ya timu ya Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na Sixers ukiendelea










