RAIS MAGUFULI AZINDUA UWANJA WA NDEGEVITA WA KAMBI YA NGERENGERE, MOROGORO

RAIS MAGUFULI AZINDUA UWANJA WA NDEGEVITA WA KAMBI YA NGERENGERE, MOROGORO

March 06, 2017

01
Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt John Pombe Magufuli akijiandaa kufyatua risasi ya bastola kuashiria matumizi rasmi ya Uwanja wa kisasa wa ndegevita wa Ngerengere mkoani Morogoro leo Machi 6, 2017
02
Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt John Pombe Magufuli na Balozi wa China nchini Dkt wakifunua kitambaa kuashiria uzinduzi  rasmi ya Uwanja wa kisasa wa ndegevita wa Ngerengere mkoani Morogoro leo Machi 6, 2017
03
Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt John Pombe Magufuli akihutubia wakati wa  uzinduzi  rasmi ya Uwanja wa kisasa wa ndegevita wa  Ngerengere mkoani Morogoro leo Machi 6, 2017.
04
Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt John Pombe Magufuli na Balozi wa China nchini Dkt katika picha ya pamoja na viiongozi mbalimbali baada ya uzinduzi  rasmi ya Uwanja wa kisasa wa ndegevita wa  Ngerengere mkoani Morogoro leo Machi 6, 2017.
PICHA NA IKULU

KATIBU TAWALA IRINGA JOSEPH CHITINKA CHEZENI MPIRA ACHENI KUKAA VIJIWENI

March 06, 2017
Katibu tawala wilaya ya Iringa Joseph Chitinka akiwasalimia wachezaji wa timu ya Waandishi wa habari mkoa wa Iringa (IMFC) kabla ya mchezo kati yao dhidi ya timu ya kijiji cha Mangalali uliochezwa katika uwanja wa kalenga kwenye mashindano ya Mbuzi Cup. Katibu tawala wilaya ya Iringa Joseph Chitinka akiwa katika picha ya pamoja na  wachezaji wa timu ya Waandishi wa habari mkoa wa Iringa (IMFC) kabla ya mchezo kati yao dhidi ya timu ya kijiji cha Mangalali uliochezwa katika uwanja wa kalenga kwenye mashindano ya Mbuzi Cup.
 Katibu tawala wilaya ya Iringa Joseph Chitinka akiwa katika picha ya pamoja na  wachezaji wa timu ya kijiji cha Mangalali kabla ya mchezo kati yao dhidi ya timu ya Waandishi wa habari mkoa wa Iringa (IMFC) uliochezwa katika uwanja wa kalenga kwenye mashindano ya Mbuzi Cup.
Na Fredy Mgunda,Iringa.

MASHINDANO ya kombe Mbuzi Cup yatafikia tamati tarehe 30 mwezi wa tatu kwa kuzikutanisha timu za Mkwawa Rangers na Waandishi wa habari mkoa wa Iringa na fainal hiyo itachezwa katika kijiji cha Kalenga kata ya Kalenga wilayani Iringa mkoani Iringa ikiwa lengo la kuinua vipaji wa wachezaji kata hiyo.

Akishudia mchezo wa nusu fainal kati ya timu ya Waandishi wa habari mkoa wa Iringa (IMFC) na timu ya kijiji cha Mangalali uliochezwa katika uwanja wa kalenga katibu tawala wilaya ya Iringa Joseph Chitinka ambaye alikuwa mgeni rasmi alisema ni wakati mzuri kwa sasa kuyageukia mashindano ya mchangani kwani yamesheheni vipaji vingi vitakavyosaidia kuendeleza mpira wa Tanzania wakati ambapo taifa likiendelea kupata matokeo yasiyoridhishwa kwenye soka kwa sasa,

"Mashindano haya ni muhimu sana kwa wakati huu kwani yatasaidia kuinua vipaji vya vijana wetu na kuweza kupata timu bora ya taifa hivyo nidhamu ni muhimu wakati wa michezo hiyo" alisema Chitinka

Aidha Chitinka aliongeza kwa kusema kuwa mpira wa miguu umekuwa na faida kwa wachezaji kwani wanaweza kujitengezea vyanzo vya ajira kama mbwana samatta na wachezaji wengine walipwa vizuri saizi hapa nchini hata nje ya nchi.

 “Mwaka huu tumekuja na wataalamu wanachagua vipaji maalumu kwaajili ya kujiunga na timu mbalimbali na lengo likiwa ni kuhakikisha vipaji vyote vinaonekana na vinafika mbali kwa kuwa sasa mpira ni ajira si mnamuana mchezaji Mbwana Samatta”.alisema Chitinka
  
Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano hayo Obeid Msigwa aliwataka washiriki wa mashindano hayo kujituma ili ipatikane timu ya bora ambayo itakuwa ikiwakilisha katika mashindano ya mbalimbali.

“Soka imewapa ajira mamilioni ya wachezaji na viongozi ulimwenguni na wameweza kuishi maisha ya kifahari kutokana na mishahara wanayopata”, alisema Msigwa

Kwa upande wake mlezi wa mashindano hayo kamanda wa vijana wa chama cha mapinduzi (ccm) wilaya Iringa Jackson Kiswaga alisema ataendelea kwaunganisha vijana kupitia michezo na kusaidia kukuza mpira wa wilaya ya Iringa.

“Ilani ya chama cha mapinduzi inatutaka mwenyeviti kote nchini kuhakikisha michezo inafanyika mara kwa mara na kuleta tija kwa taifa ili tuondokane kuwa kuwa vichwa vya wendawazimu”alisema Kiswaga.

Mashindano ya Mbuzi Cup ni miongoni mwa mashindano yanayolenga kuibua vipaji vya vijana vijijini ili kuwawezesha kupata nafasi ya kucheza katika vilabu vikubwa nchini.

MAZISHI YA MAREHEMU MTONGORI MANG'ACHE YAFANYIKA TARIME MKOANI MARA.

March 06, 2017
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Tarime, Mchungaji Canon Yohana Chacha (katikati), akiongoza ibada ya mazishi ya Anna Mtongori Mang'ache hii leo katika Mtaa wa Kenyamanyori, halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara.

Wengine ni Mchungaji wa Kanisa la Angilikana Parishi ya Kenyamanyori Tarime, Wyclif Chereme (kulia) pamoja na Mchungaji wa Kanisa Anglikana Parishi ya Kemange Tarime, Charles Mwita (kushoto).

Marehemu Anna Mtongori Mang'ache aliyezaliwa mwaka 1931 Kenyamanyori Tarime, alifariki dunia alihamisi iliyopita Machi 02,2017 katika Hospitali ya Rufaa Bugando Jijini Mwanza.

Familia ya Mang'ache inawashukuru Madaktari wote wakiwemo wa Hospitali ya Winani Tarime, CF na Bugando Jijini Mwanza, jeshi la polisi, viongozi wa dini, ndugu, jamaa na marafiki kwa ushirikiano wao wa dhati katika kumuuguza marehemu Anna Mtori Mang'ache na hata katika kufanikisha mazishi yake. Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe, Amina!

ULAJI WA VYAKULA NA KUTOFANYA MAZOEZI WACHANGIA ONGEZEKO LA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZWA NCHINI

March 06, 2017
 mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqqaro akichukuliwa vipimo  mara baada ya kuzindua wiki ya wanawake duniani ambayo kwa mkoa wa Arusha imeathimishwa katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid
 Muuandaaji ya wiki ya wanawake duniani kwa mkoa wa Arusha Phidesia Mwakitalima wa kwanza kulia  akishuhudua jinsi mkuu wa wilaya ya Arusha akiwa anachukuliwa vipimo vya afya yake




Mgeni Rasmi Mkuu wa wilaya ya Arusha Mh Gabriel Fabian Daqarro akiwa anaingia uwanjani tayari kwa  uzinduzi  Rasmi zoezi la kupima Moyo, Cancer, Kisukari, Macho, Magonjwa Sugu ya mfumo wa hewa Bure yanayofanyika Arusha katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid  yaliyoandaliwa na Phide Entertainment kushirikiana na wafadhili mbalimbali ambapo kilele chake ni siku ya wanawake duniani tar 8/3/2017

Habari picha na Woinde Shizza,Arusha
Tatizo la baadhi ya watanzania kula vyakula bila mpangilio na kutofanya mazoezi ili kulinda afya zao limechangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la magonjwa ya kisukari ,kansa,na shinikizo la damu.

Hayo yalisemwa na mtaalamu wa magonjwa ya yasiyoambukizwa kutoka hospitali ya mkoa wa Arusha,Mt meru,Dk Beatrice Ngogi wakati wa zoezi la upimaji wa afya bure lililofanyika jana katika uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid jijini hapa.

Akihojiwa na waandishi wa habari mtaalamu huyo alisema asilimia kubwa ya kundi la watu walioathirika na magonjwa yasiyoambukizwa ni kati ya umri wa miaka 45-60 na kudai kuwa  mtindo wa maisha ya watu umechangia kwa kiasi kikubwa  ongezeko la magonjwa hayo.

“mtindo wa maisha umekuwa ni tatizo kubwa kwetu ndio maana tunawasihi watanzania tufanye mazoezi  na kuzingatia mlo wenye utaratibu”alisema mtaalamu huyo

Hatahivyo,mtaalamu wa magonjwa ya kisukari katika hospitali ya rufaa ya KCMC mkoani kilimanajro,DK Valeria Matei alisema kwamba  katika siku za karibuni watoto wadogo wanazaliwa wakiwa na ugonjwa wa kisukari mbali na wazee ambao ilikuwa imezoeleka.


Alisema kwamba elimu ya afya ni muhimu sana itolewe katika jamii ya watanzania kwa kuwa wengi wanakumbwa na ugonjwa huo bila kujijua na wakishajitambua ugonjwa huo unakuwa umeshawathiri kwa kiasi kikubwa.

Doroth Kuziwa, ambaye ni mwathirika wa ugonjwa wa kisukari alisema ya kwamba alikuwa kubaini kuathirika na ugonjwa huo kwa muda mrefu huku akisisitiza kwamba vyakula vya wagonjwa wengi wa kisukari vimekuwa ghali hali ambayo inawafanya washindwe kumudu gharama hizo.

Hatahivyo,Hiza Omary ambaye ni mgonjwa wa macho alisema kwamba aliacha kazi ya udereva kutokana na kusumbuliwa na matatizo ya macho huku akisema kwamba vyombo vya habari vina jukumu kubwa la kuhabarisha umma kuhusu elimu ya afya katika jamii.

Mkurugenzi wa kampuni ya Phide Entertainment,Phidesia Mwakitalima alisema kwamba kampuni yake imeingia mkataba na hospitali za KCMC  na Mt Meru kwa lengo la kufadhili  zoezi la upimaji wa afya bure kwa wakazi wa mkoa  wa Arusha  katika kuelekea siku ya wanawake duniani.

Alisema kwamba zoezi hilo litahitimishwa siku ya kilele cha siku ya mwanamke duniani  huku akisisitiza kundi la wanawake kuzingatia mfumo wa ulaji wa vyakula mbalimbali ili kuepuka magonjwa yasiyoambukizwa.

 mmoja wa madaktari wanaotoa huduma akiwa anachukuwa damu salama kutoka kwa mwananchi ambaye amejitolea kuchangia damu
 mmoja wa daktari akimpongeza mamaa mara baada ya kupimwa na kukutwa anaugongwa wa presha
Dokta kutoka katika hospiotali ya kcmc akitoa elimu kwa wamama waliouthuria kupata huduma ya kupimwa bure
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mh Gabriel Fabian Daqarro Akisaini Daftari la Wageni la Phide Entertainment baada ya Uzinduzi wa Zoezi la kupima buree wananchi Moyo, Cancer, Kisukari, Macho na Magonjwa sugu ya mfumo wa Hewa .. Pamoja na changizo la Damu kwa ajili ya Ward za Wazazi Mkoani Arusha

Mshindi wa Tigo Reach for Change kutangazwa March 9

March 06, 2017
Washiriki Wa Tigo Reach  For Change Waliofanikiwa Kuingia Katika Mchujo Wa Mwisho Wakiwasilisha Wazo Lao Ubunifu Mbele Ya Majaji Mapema Wiki Hii Katika Ofisi Za Makao Makuu Ya  Tigo ,Kijitonyama Jijini Dar Es Salaam.
Majaji wa Tigo Reach for Change wakimsikliza kwa makini mmoja wa washiriki aliyefanikiwa kuingia katika mchujo 

Na Mwandishi Wetu

  Mashindano ya mwaka huu  ya Waleta mabadiliko ya kidijitali wa Tigo yamefikia katika hatua ya juu  ya kuchagua washindani watano  kufuatia mchakato wa mapitio ambao ulijumuisha waombaji 358. Shindano hili hufanyika kila mwaka na liko wazi  kwa waombaji kutoka  nchi nzima  limejielekeza katika  kuibua vijana mahiri  walio na ubunifu wa miradi ya kidijitali inayoboresha maisha ya watu, hususani watoto kwa kutumia programu za kidijitali.

  Vijana watano wanaoingia katika hatua ya fainali  hupata nafasi ya kuhudhuria warsha  ya maendeleo ya maudhui ya siku mbili pamoja na kuwasilisha miradi yao wakisubiri uthibitisho wa mwisho  kutoka kwa jopo la wataalamu wa ndani na nje katika ujasiriamali na stadi za  kidijitali.

  Waleta mabadiliko  wa Kidijitali wa Tigo ni wazo  la Kampuni ya Tigo kwa kushirikiana na asasi isiyo ya kiserikali ya Reach-for- Change ikiwa ni programu ya ushauri na  kuunga mkono  ambayo inawapa washindi fursa ya kuanzisha ujasiriamali endelevu katika maeneo ya elimu,  ujumuishwaji wa kidijitali na shughuli za ujasiriamali.

  Meneja wa Huduma za kijamii wa Tigo, Halima Okash alisema kuwa  washindi wawili wa kwanza  watapata  fedha taslimu dola 20,000 (takribani shilingi milioni 44,000,000) kuwezesha utekelezaji wa maudhui yao.


  “Miradi hii ina matokeo makubwa kijamii, inatoa masuluhisho halisi  kwa matatizo  yanayoikabili jamii  na yana umuhimu katika  kuboresha moja kwa moja maisha na hususani maisha ya watoto,” alisema Okash, akibainisha kuwa kampuni hiyo ya simu  tayari imeshawasaidia  wajasirimali kijamii tisa kupitia mkakati wa waleta mabadiliko wa Tigo (Tigo Digital Changemakers).

 Huu ni mwaka wa sita  ambapo Tigo na Reach-for-Change wanaendesha shindano la kutafuta  wajasiriamali kijamii.
  Mshindi wa mwaka huu  atatangazwa Machi 9.

WABUNGE WATATU WAPAMBA KONGAMANO LA MUZIKI JIJINI DAR ES SALAAM

March 06, 2017
 Mbunge na Katibu Mkuu  Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT), Amina Nassoro Makulagi (kulia), akizungumza katika Kongamano la Siku moja la wadau wa muziki nchini lililoandaliwa na Tanzania Music Foundation (TMF) na kufanyika Ukumbi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kutoka kushoto ni Mtaalamu wa Sheria kutoka Jeshi la Polisi Dk. Mkaguzi wa Polisi Ezekiel Kyogo  na Rais wa TMF, Dk.Donald Kissanga.
 Mbunge, Halima Bulembo, akizungumza kwenye kongamano hilo.
 Mbunge, Kiteto Zawadi Koshuma akichangia jambo kwenye kongamano hilo.
 Rais wa TMF, Dk.Donald Kissanga, akizungumza katika kongamano hilo, Kutoka kulia ni mtoa mada, Dk. Baraka Kanyabuhinya kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Rais wa Chama cha Muziki wa Rhumba Tanzania (Chamruta), Dk.Salim Mwinyi na Mtaalamu wa Sheria kutoka Jeshi la Polisi Dk. Mkaguzi wa Polisi Ezekiel Kyogo.
 Mwezeshaji katika kongamano hilo, Dk.Baraka Kanyabuhinya kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), akizungumza.
 Rais wa Chama cha Muziki wa Rhumba Tanzania (Chamruta), Dk.Salim Mwinyi akizungumza.
 Mchungaji Simon Mkologo kutoka nchini Malawi akichangia jambo kwenye kongamano hilo.
 Mtaalamu wa Sheria kutoka Jeshi la Polisi Dk. Mkaguzi wa Polisi Ezekiel Kyogo akizungumza machache katika kongamano hilo.
Katibu Mwenezi wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania, Stella Joel akiongoza kongamano hilo.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Benki ya Equity Tanzania LTD, Janety Zoya (kushoto), akizungumzia kazi mbalimbali zinazofanywa na benki hiyo na masuala ya kifedha. Kulia ni Meneja wa Benki hiyo Tawi la Mwenge, Godfrey Kiama.
Wanamuziki wakiwa kwenye kongamano hilo.
Kongamano likiendelea.
Wasanii ndani ya ukumbi.
Wanamuziki wakiwa katika kongamano.
Muonekano wa ukumbi huo.


Hapa ni mserebuko kitambaa cheupe juu.
Mwanamuzi  mkongwe na muimbaji wa nyimbo za injili Dk. Makassy alikuwepo kwenye kongamano hilo.
Mwanamuziki, Kikumbi Mwanza Mpango (King Kiki), naye alikuwepo kwenye kongamano hilo.

Na Dotto Mwaibale

SERIKALI imeombwa kuangalia kwa karibu mapungufu ya adhabu ya makosa ya wizi wa kazi za wasanii ili kuweza kusaidia kukua kwa pato la taifa linalopotea kutokana na wizi huo.


Hayo yamesemwa na Mtaalamu wa Sheria kutoka Jeshi la Polisi Dk. Mkaguzi wa Polisi Ezekiel Kyogo katika kongamano la siku moja lililowakutanisha wadau wa muziki wakiwemo wa muziki wa  injili lililofanyika Ukumbi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Kijitonyama Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.


Alisema kongamano hilo lina lengo la kuwajengea  uelewa wasanii wa muziki  juu ya kazi zao, hususani changamoto na suluhu za kazi za Sanaa nchini.


Kyogo alisema kazi za Sanaa ni mali lakini  zimekosa ulinzi pamoja na jitihada zilizopo bado nguvu zaidi inahitajika kama vile kuangalia Sheria ya haki miliki ya mwaka 1966 na 1999.


Alisema jitihada zaidi zinatakiwa kwa ajili ya  kuongeza nguvu ili tufike mahali ambapo wasanii wataweza kunufaika na kazi zao ili na wao waweze kulipa kodi na serikali kupata mapato yake.


Kyogo alishauri sheria ya makosa ya wizi wa kazi za wasanii ibadilishwe  iwe katika makosa ya jinai na isimamiwe na jeshi la polisi kama inavyosimamia makosa mengine tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo kazi hiyo inafanywa na wasanii wenyewe na kukosa nguvu ya ufatiliaji wahalifu.


Aliongeza kuwa wasanii wamekosa ubunifu na watu wamekata tamaa na kujiingiza katika wimbi la dawa za kulevya lakini wakipatiwa elimu na kujengewa mazingira mazuri ya uuzaji wa kazi za sanaa waifanyayo itawasaidia na kutoingia katika tamaa ya kupata fedha kwa njia zisizostahili. 


Alisema kuwepo kwa  mapungufu ya adhabu haipunguzi uhalifu kwani wasimamizi wa sheria wanatakiwa kuwa na uwezo zaidi katika  sheria hizo ili kusaidia kutokomeza wizi wa kazi za wasanii.


“Lazima kuwe na sheria ya makosa ya wizi za kazi za wasanii kwani itasaidia kupunguza wizi na itaongeza kipato na ajira, kwa kuwa muziki ni mali ya jamii na ni afya na tiba”, alisema Kyogo.


Rais wa Tanzania Music Foundation (TMF) Dk. Donald Kassanga aliongeza kuwa lengo kubwa la kongamano hilo ni kuhakikisha serikali inatengeneza mazingira bora  katika tasnia nzima ya muziki jambo litakalosaidia kuongeza pato la taifa.


“Watu  wamekuwa wakiiba kazi za wasanii na kama TMF tunalaaani na kuomba serikali kupitia vyombo vya dola kuziba mianya hiyo" alisema Dk. Kissanga.


Katika hatua nyingine alisema TMF inaungana na Serikali katika mapambano ya dawa za kulevya nchini kwani waathiri ni pamoja na wanamuziki na wasanii kwa ujumla.


Mwimbaji wa nyimbo za injili, Faraja Ntaboba, alisema kuwa wasanii wamekuwa wakiibiwa sana kazi zao wakati wanatumia nguvu kubwa kwa kuziandaa.



"Tuna amini endapo Serikali ikisimamia vizuri kwa kushirikiana na  TMF  wataweza kulipa kodi sawa sawa na kuendesha kazi  vizuri" alisema Ntaboba.






“MPINA: AMTAKA MKANDARASI WA UJENZI WA UKUTA WA MTO PANGANI KUUKAMILISHA KWA WAKATI”

March 06, 2017

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina akisisitiza jambo wakati akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella mara baada ya kutua mkoani Tanga kwa ajili ya ziara ya kutembelea ukuta wa mto Pangani kuona namna ulivyo ambao ujenzi wake unatarajiwa kukamilika kwa kipindi cha miezi 10

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina wa pili kulia akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kushoto mara baada ya kuwasili mkoani hapa kwa ajili ya ziara ya siku moja kutembelea ujenzi wa Mto Pangani kulia ni Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Tanga,Monica Kinala

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina kulia akilakiwa na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso mara baada ya kuwasili wilayani Pangani kwa ajili ya ziara ya siku moja kukagua ujenzi wa mto Pangani kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa.

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina akiwa na mwenyeji wake Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso wakiingia kwenye ofisi ya Mkuu wa wilaya Pangani Zainabu Issa anayewaongoza mbele wakati alipowasili kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina wa pili kushoto aliyevaa shati la njano akimsikiliza kwa umakini Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso wakati alipofanya ziara ya siku moja kutembelea wilaya hiyo kuangalia ukuta wa mto Pangani

 Mkuu wa wilaya ya Pangani,Zainabu Issa akitoa taarifa za Mradi wa Ujenzi wa Ukuta wa Mto Pangani kwa
NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina kulia ambaye alifanya ziara ya kutembelea ukuta wa Mto Pangani ambao ujenzi wake unatarajiwa kuanza wakati wowote

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina akizungumza na watumishi wa Halamshauri ya wilaya ya Pangani leo mara baada ya kufanya ziara ya siku moja kukagua ukuta wa Mto Pangani kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso na kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa
 Afisa Misitu wa wilaya ya Pangani,Twahiru Mkongo akielezea jambo kwa
NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina wakati wa ziara yake wilayani humo
 Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Cletus Shengena akieleza jambo kwa
NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina


NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina wa tatu kutoka kushoto akiteta jambo na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso wakati wa ziara yake wilayani humo
 Mhandisi wa Mradi kutoka Kampuni ya Dezo Civil Contractor,Daudi Abdallah  akimueleza jambo
NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina akisisitiza jambo kwa
Mhandisi wa Mradi kutoka Kampuni ya Dezo Civil Contractor,Daudi Abdallah  kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso
 Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Cletus Shengena akisisitiza jambo kwa
NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina kushoto namna mradi huo unavyotekelezwa

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina kulia akimsikiliza kwa umakini Afisa Mazingira ofisi ya Makamu wa Rais,Cletus Shengena alipokuwa akimueleza jambo

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina akitoka kukagua eneo ambalo kutaanza ujenzi wa ukuta wa mto Pangani wakati wa ziara yake

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina kushoto akimsikiliza kwa umakini
Mhandisi wa Mradi kutoka Kampuni ya Dezo Civil Contractor,Daudi Abdallah wakati wa ziara yake wilayani Pangani leo
NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina kushoto akimsikiliza kwa umakini Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) wakati alipofanya ziara ya kutembelea ukuta wa Mto Pangani.

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina amemuagiza Mkandarasi anayetekeleza mradi wa ujenzi wa ukuta wa Mto Pangani kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa kipindi cha miezi kumi ili kuweza kuuepusha mji huo kutoweka kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi.
Mpina aliyema hayo jana wakati alipofanya ziara ya kutembelea ukuta wa mto Pangani ambao unatarajiwa kuanza ujenzi wake kutokana na uliokuwepo zamani kuliwa na maji kutokana na mabadiliko hayo.
Alisema kuwa mradi huo ambao utagharimu kiasi cha sh.bilioni 2.4 wenye urefu wa mita 950 ambapo ujenzi huo tayari umekwisha kuanza tokea February mwaka huu na unatarajiwa kukamilika Novemba mwaka huu.
Naibu Waziri huyo aliwataka wakandarasi hao kutekeleza ujenzi huo kwa umakini mkubwa ili thamani halisi ya fedha zinazotumika ziweze kuonekana na kuweza kuwasaidia wananchi wa mji huo wa Pangani.
“Huu mradi ni mkubwa na tumezoea kuona asilimia kubwa ya miradi kama hii inatekelezwa chini ya kiwango lakini niwaambie kuwa hatumvulimia mtu yoyote atakayoonekana kukwanisha juhudi hizi”Alisema.
Awali akizungumza katika ziara hiyo, Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso alimuomba Naibu Waziri Mpina kulitupia macho pia eneo la Pangadeco ambalo limeathiri kwa kiasi kikubwa na hatarishi kwa maisha ya wananchi.
Alisema hatari hiyo inatokana kina cha bahari kuongezeka na kusababisha eneo la makazi ya wananchi kupungua siku hadi siku na kupelekea hofu kwa jamii ya watanzania wanaoishi pembezoni mwa bahari hiyo.
“Mh Naibu Waziri awali kulikuwa na tathimini ya eneo la Pangani Kaskazini lenye urefu wa mita 950 lakini wakati suala hilo linafanyika miaka ya nyuma ikiwa eneo la Pangadeco limesahaulika na ndipo kwenye athari kubwa zaidi hivyo tunakuomba Mh uliangalie hili”Alisema.
 Sambamba na hayo lakini pia Mbunge huyo alimuomba Naibu Waziri huyo wakati utekelezaji wa mradi huo vijana wa wilaya ya Pangani waweze kunufaika na ajira ambayo ndio sera ya serikali.
“Mh Naibu Waziri tunakuomba mradi huu uwe na manufaa kwa wananchi wa wilaya ya Pangani hasa vijana waweze kupata ajira kwenye mradi huo na kuwakwamua na ugumu wa maisha “Alisema.
Naye, Mhandisi wa Kampuni ya Dezo Civil Contractor inayotekeleza mradi huo, Mhandisi Joseph mhina alisema tayari wamekwisha kupata kibali kutoka Halmashauri ya wilaya ya Pangani hivyo wanatajia kukamilisha mradi huo kama ilivyopangwa “Alisema.
Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya ya Pangani, Zainabu Issa aliiomba serikali iwekeze nguvu kwenye mji huo ambao upo chini ya usawa wa bahari na hivyo kuathiriwa na mabadiliko ya tabia ya nchi kila wakati.