WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII,PROF,JUMANNE MAGHEMBE AZINDUA BODI MPYA YA TANAPA

January 05, 2017
Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof,Jumanne Maghembe akitoa hotuba yake wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) iliyofanyika katika ukumbi wa Mahakama ya Afrika jijini Arusha.
Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof ,Jumanne Maghembe .
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Mkuu wa Majeshi Mstaafu ,Jenerali George Waitara akifuatilia hotuba ya uzinduzi wa Bodi hiyo iliyotolewa na Waziri wa Maliasili na Utalii ,Prof,Jumanne Maghembe.
Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe akimkabidhi vitendea kazi Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi ambaye pia ni mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Tanapa .
Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe akimkabidhi vitendea kazi Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Tanapa Dkt Chanasa Mpelumbe Ngeleja.
Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe akimkabidhi vitendea kazi Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Tanapa Prof Wineaster Anderson
Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe akimkabidhi vitendea kazi Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Tanapa Prof,Alexander Songorwa.
Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe akikabidhi vitendea kazi Devota Mdachi mjumbe wa bodi ya Wadhamini wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) .
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Mkuu wa Majeshi Mstaafu ,Jenerali George Waitara akitoa salam zake wakati wa uzinduzi wa Bodi hiyo uliofanika katika ukumbi wa Mhakama ya Afrika jijini Arusha.
Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe akifurahia jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini iliyomaliza muda wake Modestus Lilungulu walpkutana katika hafla fupi ya uzinduzi wa bodi mpya .
Mkurugenzi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi ambaye pia ni mjumbe wa Bodi hiyo akifanya utamburisho wa wajumbe wa bodi ya Wadhamini wa shirika hilo.
Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA,Prof,Wineaster Anderson ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Taasisi ya Maliasili na Utalii endelevu Afrika (NARESTi Africa) akitamburishwa kwa wafanyakazi wa Shirika hilo.
  Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA, Dkt Lucy Lugwisa kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira akitamburishwa kwa wafanyakazi wa Shirika hilo.
  Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA,Prof,Alexander Songorwa ambaye pia ni Mkurugenzi wa Wanyamapori kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii akitamburishwa kwa wafanyakazi wa shirika hilo.
  Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA,Kamishna Marijani Nsato ambaye pia ni Mkuu wa Operesheni na Mafunzo Makao Makuu ya jeshi la Polisi akitamburishwa kwa wafanyakazi wa shirika hilo.
  Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA,Dkt Chanasa Mpalumbe Ngeleja ambaye pia ni Daktari Mkuu wa Mifugo ,Wizara ya Kilimo ,Mifugo na Uvuvi akitamburishwa kwa wafanyakazi wa shirika hilo.
  Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA,George Fumbuka ambaye pia ni Mtendaji Mkuu na Mwenyekiti wa Kampuni ya Core Securities akitamburishwa kwa wafanyakazi wa shirika hilo.
Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA,Devota  Mdachi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii nchini akitamburishwa kwa wafanyakazi wa Shirika hilo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) iliyomaliza muda wake ,Modestus Lilungulu akitoa salam zake wakati wa uzinduzi rasmi wa Bodi mpya ya Wadhamini ya TANAPA.
Baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) wakifuatilia uzinduzi huo uliofanyika katika ukumbi wa Mahakama ya Afrika jijini Arusha.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA),Mkuu wa Majeshi Mstaafu,Jenerali George Waitara (kushoto) akizungumza jambo na Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof ,Jumanne Maghembe mara baada ya kuzinduliwa kwa Bodi hiyo.katikati ni Mkurugenzi wa TANAPA,Allan Kijazi.
 Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) muda mfupi baada ya bodi hiyo kuzinduliwa.
 Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) wakiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi wa idara mbalimbali katika shirika hilo.
Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) wakiwa katika picha ya pamoja na mameneja katika shirika hilo. 

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kasazini.
KIKAO KAZI NGAZI YA MAKATIBU WAKUU CHAFANYIKA ZANZIBAR KUJADILI CHANGAMOTO ZA MUUNGANO

KIKAO KAZI NGAZI YA MAKATIBU WAKUU CHAFANYIKA ZANZIBAR KUJADILI CHANGAMOTO ZA MUUNGANO

January 05, 2017

lul1
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais – Zanzibar Bw. Joseph Meza (wa kwanza kulia) akiongoza kikao kazi cha Makatibu Wakuu kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katikati ni Mwenyekiti Mwenza Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Prof. Faustin Kamuzora. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Muungano kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Dar es Salaam Bw. Baraka Rajab. Kikao kazi hicho kimefanyika leo tarehe 05/01/2017 katika Ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar na kwa pamoja wamejadili changamoto za Muungano.
lul2
Baadhi ya Makatibu Wakuu kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia kikao kazi kilichojadili changamoto za Muungano. Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
lul3
Baadhi ya Makatibu Wakuu kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia kikao kazi kilichojadili changamoto za Muungano. Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
lul4
Bw. Shomari Omar Shomari Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji, Bi. Fatma Gharib Bilal Katibu Mkuu Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto na Bi. Khadija Bakari Juma Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya amali kwa pamoja wakifuatilia kikao kazi kilichojadili changamoto za Muungano na namna bora ya kuzipatia ufumbuzi.
lul5
Mwenyekiti na Mwenyekiti Mwenza Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais – Zanzibar Bw. Joseph Meza (wa pili kulia) na Prof. Faustin Kamuzora (wa tatu kutoka kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Makatibu Wakuu kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mara baada ya kumalizika kwa kikao kazi.
lul6
Pichani ni Mwenyekiti na Mwenyekiti Mwenza Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais – Zanzibar Bw. Joseph Meza (wa pili kulia) na Prof. Faustin Kamuzora (wa tatu kutoka kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Sekretarieti iliyoratibu kikao hicho ikiwa na wajumbe kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

MO DEWJI FOUNDATION YATOA MSAADA WA VITANDA, MAGODORO NA MASHUKA KATIKA HOSPITALI YA SEKOU TOURE

January 05, 2017
Katika kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano ya kuboresha hudumza za afya kwa mama na mtoto, Taasisi ya MO Dewji imetoa msaada wa vitanda 20, magodoro 20 na mashuka 100 kwa Hospitali ya SekouToure iliyopo mkoani Mwanza. Akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada huo, Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez amesema msaada huo ni sehemu ya malengo ya taasisi hiyo ya kuhakikisha inasaidia sehemu zenye uhitaji katika sekta ya afya, elimu na ustawi wa jamii. Amesema msaada huo unalenga kusaidia kupunguza vifo vya wanawake na watoto kwani kwa sasa idadi ni kubwa hivyo msaada huo utawezesha mkoa wa Mwanza kuongeza kasi ya mapambano ili kumaliza kabisa vifo vya wanawake na watoto. 
Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez akizungumza kuhusu juhudi ambazo zinafanywa na taasisi hiyo kwa ajili ya kusaidia jamii na malengo ya kutoa msaada katika Hospitali ya Sekou Toure.

"Tunafahamu kwamba asilimia 32 ya vifo vya watoto chini ya miaka mitano vinatokea katika siku 28 za mwanzo lakini pia tunaelezwa kuwa kila mwaka cha wanawake 8,000 hufariki dunia wakati wa ujauzito na wakati wa kujifungua kwa sababu ambazo zinaweza kuzuilika na sisi kitu cha kwanza tunachotaka ni kusaidia mapambano ya kupunguza vifo vya watoto na wanawake," amesema Barbara. Nae mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella ameitaja Taasisi ya MO Dewji kuwa mfano wa kuigwa kwa msaada ambao wameutoa kwa hospitali ya mkoa huo na kuwaomba kuendelea kuwasaidia pindi wanapohitaji msaada zaidi.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akizungumzia mipango ya Serikali kuboresha huduma za afya lakini pia kuishukuru Taasisi ya MO Dewji kwa msaada ambao wamewapatia.

"Ukimpa mama afya bora, umesaidia jamii nzima, jambo lililofanywa na Taasisi ya MO Dewji ni kubwa sana, hospitali zetu zinamahitaji makubwa sana na kwa hili ambalo wamefanya ni mfano wa kuigwa na watu wengine, tunawashukuru sana na tunawaomba muwe tayari kutusaidia kwa muda mwingine," amesema Mongella. Kwa upande wa Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kemirembe Lwota amesema aliomba Taasisi ya MO Dewji kuwasaidia baada ya kuona changaoto nyingi ambazo zinawakabili wanawake ambao wanakwenda kujifungua katika Hospitali ya Sekou Toure na watoto ambao wanazaliwa.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kemirembe Lwota akieleza sababu ya kuiomba msaada Taasisi ya MO Dewji ili iwasaidie vitanda, magodoro na mashuka kwa ajili ya wodi ya wazazi.

"Rais Magufuli alikuja hapa na hata yeye aliona changamoto ambazo zinatukabili na mimi kama mbunge niliamua kwenda kuzungumza na watu wa MO Dewji Foundation na napenda kuwashukuru kwa kukubali kutusaidia na naamini msaada huu utasaidia kupunguza baadhi ya changamoto ambazo zilikuwa zinatukabili," alisema Lwota.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. Leonard Subi akitoa taarifa ya Hospitali ya Sekou Toure.

Nae Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. Leonard Subi amesema hospitali hiyo licha ya changamoto ambazo zinawakabili inahudumia wagonjwa 500 kwa siku na kwa wanawake ambao wanafika kujifungua kwa siku wanakadiriwa kuwa kati ya 30 na 40.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akipokea msaada wa vitanda 20, magodoro 20 na mashuka 100 kutoka Taasisi ya MO Dewji.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akimshukuru Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez kwa msaada ambao wamewapatia.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Sekou Toure Dk. Rweyendela Onesmo akitoa neno la shukrani.Mmoja wa wanawake ambao wamejifungua katika Hospitali ya Sekou Toure, Eveline Francis akiishukuru MO Dewji Foundation kwa msaada ambao wametoa kwenye hospitali hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kemirembe Lwota na Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez wakimjulia hali Zuwena Mohammed baada ya hafla ya kukabidhi msaada.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kemirembe Lwota, Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez, Mwenyekiti wa UWT Mwanza, Ellen Bagohe na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. Leonard Subi wakiwa katika picha ya pamoja.Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kemirembe Lwota, Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez, Mwenyekiti wa UWT Mwanza, Ellen Bagohe na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. Leonard Subi wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Hospitali ya Sekou Toure.
Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella. Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kemirembe Lwota.
Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella.

MO DEWJI FOUNDATION YATOA MSAADA WA VITANDA, MAGODORO NA MASHUKA KATIKA HOSPITALI YA SEKOU TOURE

January 05, 2017
Katika kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano ya kuboresha hudumza za afya kwa mama na mtoto, Taasisi ya MO Dewji imetoa msaada wa vitanda 20, magodoro 20 na mashuka 100 kwa Hospitali ya SekouToure iliyopo mkoani Mwanza. Akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada huo, Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez amesema msaada huo ni sehemu ya malengo ya taasisi hiyo ya kuhakikisha inasaidia sehemu zenye uhitaji katika sekta ya afya, elimu na ustawi wa jamii. Amesema msaada huo unalenga kusaidia kupunguza vifo vya wanawake na watoto kwani kwa sasa idadi ni kubwa hivyo msaada huo utawezesha mkoa wa Mwanza kuongeza kasi ya mapambano ili kumaliza kabisa vifo vya wanawake na watoto. 
Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez akizungumza kuhusu juhudi ambazo zinafanywa na taasisi hiyo kwa ajili ya kusaidia jamii na malengo ya kutoa msaada katika Hospitali ya Sekou Toure.

"Tunafahamu kwamba asilimia 32 ya vifo vya watoto chini ya miaka mitano vinatokea katika siku 28 za mwanzo lakini pia tunaelezwa kuwa kila mwaka cha wanawake 8,000 hufariki dunia wakati wa ujauzito na wakati wa kujifungua kwa sababu ambazo zinaweza kuzuilika na sisi kitu cha kwanza tunachotaka ni kusaidia mapambano ya kupunguza vifo vya watoto na wanawake," amesema Barbara. Nae mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella ameitaja Taasisi ya MO Dewji kuwa mfano wa kuigwa kwa msaada ambao wameutoa kwa hospitali ya mkoa huo na kuwaomba kuendelea kuwasaidia pindi wanapohitaji msaada zaidi.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akizungumzia mipango ya Serikali kuboresha huduma za afya lakini pia kuishukuru Taasisi ya MO Dewji kwa msaada ambao wamewapatia.

"Ukimpa mama afya bora, umesaidia jamii nzima, jambo lililofanywa na Taasisi ya MO Dewji ni kubwa sana, hospitali zetu zinamahitaji makubwa sana na kwa hili ambalo wamefanya ni mfano wa kuigwa na watu wengine, tunawashukuru sana na tunawaomba muwe tayari kutusaidia kwa muda mwingine," amesema Mongella. Kwa upande wa Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kemirembe Lwota amesema aliomba Taasisi ya MO Dewji kuwasaidia baada ya kuona changaoto nyingi ambazo zinawakabili wanawake ambao wanakwenda kujifungua katika Hospitali ya Sekou Toure na watoto ambao wanazaliwa.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kemirembe Lwota akieleza sababu ya kuiomba msaada Taasisi ya MO Dewji ili iwasaidie vitanda, magodoro na mashuka kwa ajili ya wodi ya wazazi.

"Rais Magufuli alikuja hapa na hata yeye aliona changamoto ambazo zinatukabili na mimi kama mbunge niliamua kwenda kuzungumza na watu wa MO Dewji Foundation na napenda kuwashukuru kwa kukubali kutusaidia na naamini msaada huu utasaidia kupunguza baadhi ya changamoto ambazo zilikuwa zinatukabili," alisema Lwota.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. Leonard Subi akitoa taarifa ya Hospitali ya Sekou Toure.

Nae Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. Leonard Subi amesema hospitali hiyo licha ya changamoto ambazo zinawakabili inahudumia wagonjwa 500 kwa siku na kwa wanawake ambao wanafika kujifungua kwa siku wanakadiriwa kuwa kati ya 30 na 40.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akipokea msaada wa vitanda 20, magodoro 20 na mashuka 100 kutoka Taasisi ya MO Dewji.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akimshukuru Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez kwa msaada ambao wamewapatia.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Sekou Toure Dk. Rweyendela Onesmo akitoa neno la shukrani.Mmoja wa wanawake ambao wamejifungua katika Hospitali ya Sekou Toure, Eveline Francis akiishukuru MO Dewji Foundation kwa msaada ambao wametoa kwenye hospitali hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kemirembe Lwota na Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez wakimjulia hali Zuwena Mohammed baada ya hafla ya kukabidhi msaada.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kemirembe Lwota, Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez, Mwenyekiti wa UWT Mwanza, Ellen Bagohe na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. Leonard Subi wakiwa katika picha ya pamoja.Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kemirembe Lwota, Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez, Mwenyekiti wa UWT Mwanza, Ellen Bagohe na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dk. Leonard Subi wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Hospitali ya Sekou Toure.
Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella. Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kemirembe Lwota.
Mkuu wa Taasisi ya MO Dewji, Barbara Gonzalez akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella.