MWENYEKITI WA ZAMANI WA CCM MKOA WA MWANZA ALIYEUWAWA KUZIKWA SIKU YA ALHAMISI

December 17, 2013
Marehemu Clement Mabina.
MAZISHI ya aliyekuwa mwenyekiti wa CCM na Diwani wa Kata ya Kisesa wilayani Magu Clement Mabina, aliyeuawa kikatili na kundi la wananchi, yanatarajiwa kufanyika Alhamisi.
 
Taarifa iliyotolewa na msemaji wa familia ya marehemu Mabina, Timothy Gregory ambaye ni mdogo wa marehemu, alisema kwamba, mipango ya mazishi imekamilika na zaidi ni pamoja na kusubilia mtoto wa kike wa marehemu aliyoko njiani kutokea nchini Uingereza marehemu waliokuwa nje ya nchi.
 
Gregory alisema, Kijana mdogo wa marehemu (mtoto ) tayari amewasili jana jioni, hivyo mazishi marehemu Mabina yatafanyika kesho kutwa Kisesa wilayani Magu baada ya mtoto wake mkubwa wa kike kuwasili kutoka Uingereza.
 
Mwenyekiti wa Kamati ya mazishi hayo, Henry Matata ambaye ni Meya wa Manispaa ya Ilemela, amesema kuwa, taratibu za maziko ya marehemu Mabina, zinaendelea kufanyika nyumbani kwa marehemu na kupokea wageni mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara, wanasiasa wa Kada mbalimbali kutoka vyama vya siasa na serikali pamoja na ndugu na rafiki wa karibu na marehemu wa sehemu tofauti nchini kote na nje ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

KONGAMANO LA VIONGOZI WANAWAKE AFRIKA KUFANYA BONANZA LEO UWANJA WA TAIFA

December 17, 2013
IMEWEKWA DESEMBA 18,2013 SAA 7:14 ASUBUHI.
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mh. Amosi Makala (kushoto) akipongezwa na mmiliki wa Taasisi ya Right to Play, Dr. Dennis Bright (kulia) baada yakufungua kongamano la wanawake wa Afrika viongozi wa michezo linalofanyika nchini



Nahodha wa timu ya Taifa ya wanawake, ‘Twiga stars’, Sophia Mwasikili akiwatambulisha wachezaji wenzake (hawapo kwenye picha) kwenye kongamano la wanawake wa Afrika viongozi wa michezo

Mmiliki wa Anita Foundation, Dr. Anita White akizungumza kwenye kongamano la wanawake wa Afrika viongozi wa michezo lililofanyika nchini. Waliokaa wa pili kushoto ni Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mh. Amosi Makala kushoto ni Kaimu katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt Ole Gabriel na mmiliki wa Taasisi ya Right to Play, Dr. Dennis Bright na mwisho ni Mkurugenzi wa Michezo, Leonard Thadeo

WASHIRIKI wa kongamano la wanawake viongozi wa Afrika linalofanyika nchini leo watafanya bonanza la michezo yote katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Mkurugenzi wa Michezo wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, ambaye ndiye mwandaaji wa kongamano hilo  Juliana Yasoda alisema kuwa watafanya bonanza hilo ambalo litajumuisha michezo yote katika Uwanja wa Taifa kuanzia saa 3:00 asubuhi.
“leo) tutafanya bonanza ambalo litahusisha michezo yote kwani hapa kuna viongozi na wanamichezo wa michezo yote na baadae timu za Taifa ya Twiga na ile U-20 watacheza mchezo wa kirafiki”, alisema Juliana.
Michezo ambayo itachezwa ni soka, riadha, kikapu, mikono, wavu, magongo, kurusha tufe na kisahani pamoja na kuvuta kamba.
Pia alisema kongamano hilo limesaidia kutoa mwanga na dira kwenye michezo miongoni mwa washiriki kutokana na kila mmoja kuelezea uzoefu wake katika michezo ukilinganisha na sera za nchi anayotoka.
Awali juzi wakati akifungua kongamano hilo Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mh. Amos Makala aliwataka washiriki hao kupigania michezo katika nchi wanazotoka  kwani wanawake ni chachu ya mafanikio kwenye michezo mbalimbali hasa wakipewa elimu ya maendeleo ya michezo.
Kongamano hilo lilikuwa la siku mbili na lilishirikisha viongozi wanawake toka nchi za Msumbiji, Burundi, Rwanda, Kenya, Uganda, Zambia na  Ghana  pamoja na wageni wengine toka Finland na Marekani

SABA WATIWA MBARONI KWA MAUAJI YA MWENYEKITI WA ZAMANI WA CCM NA ALIYEKUWA DIWANI WA KATA YA KISESA.

December 17, 2013
IMEWEKWA DESEMBA 17 SAA 3:14.
Kilima cha Kanyama lilicho sababisha mauti, kilichokuwa kinamilikiwa na marehemu Mabina kwa kuridhiwa na serikali ya kijiji iliyotoa hati ya umiliki.
Kutoka barabara kuu ya Mwanza - Musoma kona ya kuelekea kijiji na kilima cha Kanyama, kwa kawaida eneo hili huwa lina changamka sana likiwa na watu na pilika pilika za biashara lakini limepwaya kana ndiyo kunakucha vile kumbe laa! 
Njia yenyewe ndiyo hii ambayo pia marehemu aliitumia kupita wakati akikimbia kujiokoa baada ya kundi la watu waliokuwa wakishambulia.
Ni kona ambayo ndipo shambulizi lilianzia huku marehemu akijivuta taratibu kuelekea eneo la msaada.
Marehemu alifika eneo hili akijaribu kukimbilia katika moja ya nyumba zinazo onekana mbele ili kupata msaada wa kujiokoa.
Lakini kabla hajafika katika nyumba hizo eneo lililo zungushiwa duara ndipo alipo anguka baada ya kupigwa jiwe kichwani na kuanguka chini nakuanza kushambuliwa kwa mawe hadi mauti yalipomkuta. 
Kwa ukaribu zaidi na pembeni ni baadhi ya mawe yaliyo tumika kumshambulia.
Ndivyo alivyokutwa na mauti mwenyekiti huyo wa zamani CCM.
Nyumbani kwa marehemu na sehemu ya waombolezaji.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Injinia Evarist Ndikilo (kulia) pamoja na Mkuu wa Usalama mkoa (kushoto) wakimfariji mjane wa marehemu Clement Mabina.
Meya wa Manispaa ya Ilemela Henry Matata (mwenye tai) ambaye alikuwa rafiki mkubwa wa marehemu Mabina ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mazishi na hapa akizungumza na baadhi ya wajumbe wa Kamati hiyo.
Baadhi ya waombolezaji.
Huzuni kubwa imetawala kwa wafanyakati wa Mamlaka ya maji safi na maji taka jijini Mwanza (MWAUWASA) nyumbani kwa marehemu.
Na. PETER FABIAN MWANZA.

WATU saba wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Mwanza wakituhumiwa kuhusika na mauaji ya kinyama ya aliyekuwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza na Diwani wa Kata ya Kisesa, Clement Mabina.

Watu hao wamekamatwa wakati hofu ikiwa imewakumba wakazi wa maeneo ya Kisesa na Kanyama, eneo ambalo marehemu Mabina aliuawa na watu wenye hasira katika kile kilichoelezwa kuwa mgogoro wa mashamba.

ASAA SIMBA,MOHAMED BAWAZIR WAONGEA NA WANA CCM KATA YA JANGWANI KUIMARISHA CHAMA

December 17, 2013

IMEWEKWA DESEMBA 17 SAA 3:05

Mwenyekiti wa CCM  Kata ya Jangwani Mohamed Bawazir katikati akizungumza wakati wa kufungua kikao cha kujadili kelo mbalimbali zinazowakabili katika kata hiyo kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Ilala Asaa Simba ambaye pia ni Diwani wa Vingunguti na kulia  ni katibu wa kata ya jangwani, Majala Balawa
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala Asaa Simba kushoto akizungumza na Mwenyekiti wa CCM  Kata ya Jangwani Mohamed Bawazir
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala Asaa Simba kushoto akizungumza na Mwenyekiti wa CCM  Kata ya Jangwani Mohamed Bawazir wakingia katika ukumbi wa mkutano
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala Asaa Simba kushoto akiongea na baadhi ya wanachama wa CCM wa kata ya Jangwani wakati alipotembelea kwa ajili ya kujadili kelo mbalimbali zinazo ikabili kata hiyo kulia ni Mwenyekiti wa Chama Hicho Kata ya Jangwani Mohamed Bawazir

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala Asaa Simba kushoto akiongea na baadhi ya wanachama wa CCM wa kata ya Jangwani wakati alipotembelea kwa ajili ya kujadili kelo mbalimbali zinazo ikabili kata hiyo kulia ni Mwenyekiti wa Chama Hicho Kata ya Jangwani Mohamed Bawazir
Baadhi ya wanachama wa CCM wakisikiliza mada mbalimbali katika mkutano huo

*MATUKIO YA MICHEZO YA BANDARI ‘INTER-PORTS'

December 17, 2013
Tuesday, December 17, 2013  
 Katibu Mkuu wa Dowuta Taifa, Bw. Jonathan Msoma akizungumza na Wanamichezo wa Bandari, katika siku ya kufunga michezo iliyofanyika hivi karibuni katika viwanja vya Sigara Chang’ombe. Kulia ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Bw. Awadhi Massawe na Mganga Mkuu wa Mamlaka, Dkt. Mkunde Mlay.
Katibu Mkuu wa Dowuta Taifa, Bw. Jonathan Msoma akisaini mprira kama kumbukumbu ya kufunga michezo ya Bandari iliyofanyika hivi karibuni katika viwanja vya Sigara Chang’ombe. Kushoto ni mwamuzi wa Kimataifa, Othaman Kazi na katikati ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Bw. Awadhi Massawe.
 Timu ya soka ya Makao Makuu ikiwa katika picha ya pamoja.
Mganga Mkuu wa Mamlaka, Dkt. Mkunde Mlay akisalimiana na wachezaji kabla ya kuanza kwa mechi ya mpira wa miguu.
 Mashabiki wa timu ya Bandari ya Dar es Salaam wakishangilia.
Mstahiki Meya wa wilaya ya Temeke, Maabad Hoja akisoma hotuba yake wakati wa kufungua michezo ya Bandari iliyofanyika katika viwanja vya Sigara hivi karibuni.

Mashabiki wa timu ya Makao Makuu wakishangilia.

MAISHA BORA HAYAPATIKANI KWA KUKAA VIJWENI-KISAUJI.

December 17, 2013
IMEWEKWA DESEMBA 17,2013 SAA 2:15.
Na Oscar Assenga,Tanga.

MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (MNEC) wilaya ya Tanga,Salim Kassim Kisauji amesema maisha bora kwa kila mtanzania yataenda na ufanyaji wa kazi na sio kukaa vibarazani kwa kupiga soga.


Kisauji ambaye pia ni Meya  wa zamani wa Jiji la Tanga alitoa kauli hiyo wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Ngamiani kusini ikiwa ni ziara ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana Mkoa wa Tanga(UVCCM) Abdi Makange wilayani hapa ulioendana sambamba na ufunguzi wa matawi.

VIONGOZI WA DINI WAKIRI ELIMU NI KIKWAZO CHA UNYANYAPAA KWA WAATHIRIKA

December 17, 2013
IMEWAKWA DESEMBA 17  Na Dege Masoli, Korogwe.
Baadhi  ya viongzi  wa madhehebu mbalimbali ya dini Wilayani hapa, wamekiri kuwa ukosefu wa elimu ya ushauri nasaha  kuhusu  VVU  na  Ukimwi  na jinsi ya kuwahudumia  waathirika  wa ungonjwa  huo iliwafanya kuwa  kikwazo katika mapambano ya unyanyapaa.
Viongozi hao walieleza hayo wakati wa mafunzo ya jinsi ya kushughulikia unyanyapaa,madhara na faida za kutokuwepo kwa unyanyapaa  yaliyoambatana na kupima afya zao kwa hiari, walidai kuwa  kukosa elimu hiyo ili kuliwafanya wawe  kikwazo bila ya wao kujijua.
 
Katika mafunzo hayo ya siku mbili viongozi 30  wa madhehebu ya dini   kutoka maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Korogwe  walipima afya zao  kwa hiari ambapo mtaalamu wa upimaji afya, Joice Mwanga  alisema kuwa maambukizi yalikuwa asilimia 0%  ya washiriki wote.
Wakizungumza na Blog hii, Viongozi hao  walieleza kuwa  zoezi la upimaji wa afya limefanikiwa kutokana na elimu  waliyoipata kuwapa  mwanga wa kujitambua tofauti na walivyokuwa awali ambapo suala la kupima afya lilikuwa ni kinyume na imani na taratibu za dini zao.
“Tumejifunza mengi lakini kubwa ni kutambua  jinsi ya kushughulikia unyanyapaa ndani ya jamii, madhara na faida za kutokuwepo kwa unyanyapaa huo…….  huu ni mwanga kwetu”  alisema Yahaya Yussuph.
Naye  Richard  David  yeye alieleza kuwa  .inawezekana wao walikuwa kikwazo  cha  kupunguza kama siyo kuondoa kabisa tatizo hilo bila ya wao kujua na kwamba sasa wataendeleza  mapambano ya unyanyapaa na upimaji afya kwa hiari huku wakiwa mfano  kwa wengine.
Janeth  Mshana   alibainisha kuwa ukosefu wa elimu ya unyanyapaa na faida za upimaji wa afya  lilikuwa tatizo si kwa waumini pekee lakini pia hata kwa viongozi wa dini lilikuwa ni jambo la miujiza ambalo halikuwa rahisi kulitangaza bayana mbele ya jamii zaidi ya kuegemea katika masuala ya kiimani pekee.
Omari Abdalah   alisema kuwa tatizo hilo lilikuwa kikwazo katika mapambano ya harakati za unyanyapaa na kupima afya  na kwamba baada ya kupata mafunzo hayo  watahakikisha mabadiliko  ndani ya nyumba za ibada na jamii kwa ujumla katika maeneo yao yanapatikana.
Hata hivyo Mwajuma Athuman  alidai kuwa kutokana na elimu waliyoipata wameweka  mkakati wa  kubadilisha mtazamo wa waumini wao  kwa  kutoa elimu  juu  ya  athari za unyanyapaa  kwa  waathirika wa ukimwi  na utambuzi na faida ya kupima afya zao kwa hiari.