CHUO CHA BANDARI CHAJIVUNIA KUTOA WATAALAMU BORA NCHINI

November 21, 2022

Afisa Msajili katika Chuo cha Bandari Pendo Mtinangi akizungumza na waandishi wa Habari Jijini Tanga katika viwanja vya Bandari kunakoendelea Mashindano ya Shimuta kuhusu umuhimu wa chuo hicho

Afisa Msajili katika Chuo cha Bandari Pendo Mtinangi akizungumza na waandishi wa Habari Jijini Tanga katika viwanja vya Bandari kunakoendelea Mashindano ya Shimuta kuhusu umuhimu wa chuo hicho

Afisa Uhusiano wa Chuo cha Bandari Edda Mmari akizungumza na waandishi wa habari leo


Afisa Utawala Mwandamizi katika chuo hicho Halima Kagobe akizungumza

Mratibu wa mafunzo ya muda mfupi John Leonard akizungumza




Chuo cha Bandari kimejivuna kutoa wataalamu bora wengi ambao wamekuwa ni chachu ya mafanikio katika sekta ya uchukuzi na nyingine hapa nchini.

Hatua hiyo inatokana na takwimu kuonyesha kuwa fursa ya ajira kwa wahitimu wake ni zaidi ya asilimia 90 huajiriwa katika maeneo mbalimbali ya sekta ya uchukuzi Nchini .

Hayo yalibainishwa Leo naAfisa Utawala Mwandamizi katika chuo hicho Halima Kagobe wakati wakizungumza na waandishi wa Habari Jijini Tanga katika viwanja vya Bandari kunakoendelea Mashindano ya Shimuta

Ambapo alisema kuwa Kutokana na umahiri wa uwepo miundombuni bora ya kujifunza umefanya chuo hicho kuweza kutoa wanafunzi ambao wanahitajika katika soko la ajira.

Alisema kuwa kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia ambayo chuo hicho kinakwenda sambamba Kwa kuweka mitambo ya kisasa pamoja masomo ambayo ya yanaendana na hitajio la soko la ajira.

"Chuo chetu kinajukumu la kuandaa wataalamu ambao wataweza kutumika na TPA pamoja na sekta nzima ya uchukuzi kutokana na mafunzo ambayo wanayatoa Kwa Wanafunzi wao"Alisema Kagobe

Awali akizungumza Mratibu wa mafunzo ya muda mfupi John Leonard alisema kuwa kozi za uendeshaji wa mitambo Kwa kipindi cha miaka ya hivi karibu imepata mwitikio mkubwa na vijana wa jinsia ya kike.

Alisema kuwa mafunzo yanayotolewa katika chuo hicho sio tuu yameweza kunufaisha wananchi wa hapa nchini pekee hadi nje ya nchi hususani zilizoko katika ukanda wa Afrika ya Mashariki.

Alisema wanatoa kozi za utalaamu katika maeneo ya Bandari na usimamizi wa shughuli za forodha wanayo makundi mawili ya kozi za muda mfupi ambazo wanayatoa kwenye chuo cha Bandari .

Mratibu huyo alisema kwamba upande wa kozi ya vyombo vya kuendesha mashine mbalimbali zinazotumika Bandari ikiwmo uendeshaji wa vyombo vya winch na vyengine ambavyo zimefungwa kwenye Bandari kubwa hapa nchini ikiwemo za Dar na Mtwara.

Naye kwa upande wake Afisa Uhusiano wa Chuo cha Bandari Edda Mmari alisema wameshiriki kwenye mashindano ya Shimuta yanayoendelea Jijini Tanga ili kutangaza chuo hicho ambacho kimekuwa kikitoa wataalamu mbalimbali katika sekta ya uchukuzi hapa nchini

Alisema pia Michezo hiyo inaunganisha taasisi mbalimbali na wao ni sehemu yao na wanatoa huduma kwa wananchi hivyo wamekuja kutangaza chuo cha Bandari ambacho kinatoa kozi za muda mrefu na mfupi hivho waliona ni muhimu kushiriki ili kuwaelezea umuhimu wake na uwepo wake hivyo wanawakaribisha watu wote kufika kujiunga na chuo hicho na wao wapo tayari kuwahudumia .


Mwisho