February 20, 2014

MWANAMKE ATAPELIWA MILIONI 5 HOTELI YA FRESH COACH MOSHI

Bi. Shembusho akilia kwa uchungu baada ya kudangasnywa na watu wawili, wa kike na wakiume ambao majina yao bado hayajafahamika. watu hao walimpeleka katika Hoteli maarufu mjini moshi, Fresh Coach na kumtapeli shilingi milioni 5.4 ambazo alikuwa ametoka kutoa Benki ya Uchumi ya mjini Moshi.
Askari wa Hoteli hiyo inayodaiwa kutumika kumtapeli mwanamke huyo akimtuliza Mama huyo ambaye alionekana kuchanganyikiwa na tukio hilo.
Akilia kwa Uchungu
February 20, 2014

*PSPF YAWAPIGA MSASA WANAHABARI DAR, WENGI WAVUTIWA WAJIUNGA NA MFUKO

 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu akiaga baada ya kumalizika kwa semina aliyowaandalia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, kuhusu utendaji wa mfuko huo pamoja na kuwahamasisha kujiunga nao. Waliohudhuria semina hiyo ni wachora katuni, wamiliki wa mitandao ya kijamii na wahabari kutoka vituo vya televisheni, redio na magazeti.
 Ofisa wa PSPF akiwaelekeza baadhi ya wanahabari kujza fomu za kujiunga na mfuko huo katika mfumo wa hiari ambapo kiingilio ni sh. 10,000. 
 Wanahabari wakiwa katika semina hiyo
Wanahabai wakiwa beze kunasa notes....
 Wanahabari wakiwemo wamiliki wa mitandao ya kijamii wakishiriki katika semina hiyo

BREAKING NEWZ!!! KIPANYA NA ROLI USO KWA USO

February 20, 2014

WATU wanne wapo katika hali mbaya na wengine saba wamejeruhiwa baada ya lori scania namba T653 BFD  (scania 380) kugongana uso kwa uso na baso dogo la abiria Toyota Hiace T613 CPG iliyokuwa inatoka mbagala kwenda mkuranga.
Kwa mujibu wa shuhuda ya ajali hiyo iliyotokea Mwandege, Dominic Kubhota, ameiambia blogu hii usiku huu kwamba chanzo cha ajali hiyo ni ovateki isiyotumia akili ya lori hilo .
Majeruhi hao wamefikishwa katika hospitali ya Mkuranga, lakini muda mfupi baadaye walianza kukimbizwa kuleta dare s salaam kw amatibabu zaidi.
Abiria wawili waloikuwa mbele  ya daladala walikatika miguu.

Majeruhi wengine walioweza kuzungumza ni:
Mustafa mfungapoa wa mkuranga
Abdul Ally wa mwandege
Ramadhani rajab
Theofrida Mwinuka ( alikuwa mbele amevunjika miguu)
Jamal  mbaraka ( aliyekwanguka ngozi ya kichwa)
Abraham Mohamed
Swalehe salum
NA LUKWANGULE
MAFUNZO YA TEHAMA KWA SIMU YASISITIZWA KUKUZA DEMOKRASIA VIJIJINI.

MAFUNZO YA TEHAMA KWA SIMU YASISITIZWA KUKUZA DEMOKRASIA VIJIJINI.

February 20, 2014
IMAG0271
Mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya Kilombero, Hassan Masala, akifungua mafunzo ya matumizi ya simu kwa habari katika ukumbi wa Mazingira Kibaoni, Ifakara 03 Februari 2014 yanayolenga kukuza taaluma ya upashaji habari kwa kutumia simu. Kushoto ni Afisa Tawala wa Wilaya ya Kilombero Bi. Christa Njovu na Kulia ni Mkufunzi kutoka UNESCO Mama Rose Haji Mwalimu.
Na. Mwandishi wetu
Demokrasia vijijini itapatikana iwapo vyombo vya habari jamii vitatumika kikamilifu na kutekeleza wajibu wake wa kupasha habari kwa kutumia teknolojia mpya.
Akifungua mafunzo ya wiki moja katika Ukumbi wa Mazingira, Kibaoni Ifakara yanayowashirikisha wanahabari jamii kutoka Pemba, Unguja, Pangani, Ifakara na Kyela, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Hassan Masala amesema mbinu za kisasa zinahitajika kuelimisha jamii na mambo gani yafanyike ili kupata uongozi bora vijijini na taifa kwa ujumla.
February 20, 2014

*BENKI YA BARCLAYS YAKABIDHI ZAWADI KWA WASHINDI WA KAMPENI ZA MAISHA BOMBA NA DOUBLE YOUR SAVINGS

 Ofisa wa Benki ya Barclays Tanzania, Valence Luteganya (katikati) kikabidhi mfano wa hundi ya shs milioni moja kwa mmoja wa washindi wa droo ya pili ya promosheni ya ‘Double your Savings ’ ya benki hiyo, Anthony Noah Mwakyombe ,  jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Wateja wa Maalumu wa Benki ya Barclays, Neema Rwehumbiza.
 Mkuu wa Kitengo cha Wateja wa Maalumu wa Benki ya Barclays, Neema Rwehumbiza (katikati) akikabidhi mfano wa hundi ya shs milioni 10 mshindi wa zawadi kubwa ya kampeni  ya “Maisha Bomba na Barclays Golden Briefcase” Bi. Moza Ally Mohamed huku  Ofisa wa benki hiyo, Valence Luteganya akishuhudia jijini Dar es Salaam leo.  
February 20, 2014

MAMA ASHA BILALI AJIUNGA NA MFUKO WA HIFADHI YA JAMII WA PPF LEO KWENYE TAMASHA LA WANAWAKE NA AKIBA

 Mke wa Makamu wa Raisi Bi Asha Bilali akipata maelezo ya Kujiunga na Mfuko wa hifadhi ya Jamii wa PPF Kutoka kwa Meneja Mahusiano na Masoko wa Mfuko huo wa PPF Bi Lulu Mengele wakati alipofika katika banda la PPF kwenye Tamsha la Wanawake na Akiba katika Ukumbi wa Dar Live mapema leo
Mgeni rasmi wa tamasha la Wanawake na Akiba na ambae ni Mke wa Makamu wa Raisi Tanzania Bi Asha Bilali akijaza fomu ya Kujiunga na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PPF wakati alipotembelea banda la PPF kwenye Tamasha la wanawake na Akiba lililofanyika leo Katika Ukumbi wa Dar Live, Wanaoshuhudia ni Maafisa wa Mfuko wa PPF.

MUME NA MKE WAZUA BALAA BUNGE LA KATIBA

February 20, 2014

 Bunge la katiba likiendelea mjini Dodoma. Picha na Maktaba 

Chama cha National League for Democracy (NLD) Zanzibar kimemtaka, Rais Jakaya Kikwete kufuta uteuzi wa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kupitia chama hicho kwa madai kuwa walioteuliwa katika chama hicho ni mtu na mkewe na kufanya uteuzi huo kukosa sura ya Muungano.
Tamko hilo limetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa NLD - Zanzibar, Khamis Haji Mussa katika taarifa aliyoisambaza kwa vyombo vya habari mjini hapa juzi, kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Dk Emmanuel Makaidi amewasilisha majina mawili, la kwake na la mkewe, Modesta Ponera kwa ajili ya uteuzi.
Alisema NLD - Zanzibar kilianza kufuatilia taratibu za uwasilishaji wa barua tangu Desemba 27, mwaka jana kwa kumwandikia barua Katibu Mkuu Kiongozi wa SMZ baada ya kupokea maelekezo ya Ikulu ya Tanzania kwamba majina ya Zanzibar yatafanyiwa kazi visiwani na ya Bara yangepelekwa Ikulu Dar es Salaam.