ZIMWI LA TEGETA ESCROW LAMTISHA PROFESA TIBAIJUKA, AKATAA KUPOKEA DOLA 300,000 BAADA YA KUPEWA TUZO YA KIMATAIFA

September 29, 2016
 
 Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka akionesha tuzo ya kimataifa (UN) ya Maendeleo Endelevu ya Mwana Mfalme Khalifa Bin Salman Al Khalifa aliyotunukiwa hivi karibuni New York Marekani wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo.
 Profesa Anna Tibaijuka akionesha cheti alichokabidhiwa sanjari na tuzo hiyo.
 Profesa Tibaijuka akisisitiza jambo katika mkutano huo na wanahabari. Kulia ni Mratibu wa mkutano huo, Mussa Ally.
 wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.

Na Dotto Mwaibale


MBUNGE wa Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka amekacha kuchukua dola 300,000 alizopewa baada ya kutunukiwa tuzo ya  Maendeleo Endelevu aliyopewa na Umoja wa Mataifa (UN), kutokana na sakata la fedha za Escrow Tegeta.


Tuzo hiyo aliipokea Septemba 23 mwaka huu New York Marekani ambayo mfadhili wa tuzo hiyo ni wa waziri mkuu wa Bahrain mwana mfalume Khalifa bin Al Khalifa.

Akizungumza jana Dar es Salaam Profesa Tibaijuka alisema kwa sasa umoja wa mataifa umeingia katika awamu ya pili ya maendeleo, ambao umekuja kupisha yale malengo 17 ya mileniam ambayo yote yeye alikuwepo, hivyo aliokuwa wanatoa tuzo walinona kwa namna alivyoshiriki kwa kiasi kikubwa.

"Tuzo hizi si za kuomba, ni watu wanakaa na kupendekeza mtu wa kupewa, na hii ni mara ya pili, mara ya kwanza   nilipewa mwaka 2009 nchini Swideni," alisema na kuongeza.

"Tuzo zinatoka kwa niaba ya jamii inayotoka au kuitumikia na kufanya nayo kazi, hivyo wamatambua mchango wangu katika kuwatumikia wananchi wa Muleba," alisema.

Aidha Profesa tibaijuka alitaja sababu zilizpokekea yeye kutochua dola 300,000 za Marekeni za tuzo hiyo.

"Sikuichukua kwa sababu ya yaliyonikuta hapo mapema, kulikuwa na uwezekano wa kuichukua lakini nikasema kwa hali halisi ya nyumbani, hatuna sheria ya kupokea tuzo, michango na zawadi kwa hiyo mimi nikaicha mezani wao wafanye wanayotaka," alisema na kuongeza. 

"Unapoona mtu kama mimi nafanya kazi nakwenda kuchafulia kwenye kitu ambacho siusiki nacho, sasa Unapoipokea hapa utaonekana kama umevunja maadili au umejinufaisha kwa kuwa ndio mambo ya kwetu, hivyo nikawaachia," alisema.

Aliongeza kwa sasa umeshapeleka mswada binafsi bungeni wa kuweka sheria ya michango ili vitu vya hiari kama hivi vinapokuja katika jamii visimamiwe na si kupotoshwa kisiasa.

"Kwa maana jambo hili halina kificho, yaani huwezi kumzungumzia Anna Tibaijuka bila kutaja suala la Escro, hayo hayakwepeki kwa sababu yalitengenezwa yakawa hivyo, mtu asiyehusika anavalishwa joho lisilo muhusu.

"Lakini kwa sababu jamii haina uwezo wa kuchimba chini, unabaki kuwa uongo na kushindwa kujua ukweli umesimama wapi, lakini wao (UN) wanajua hii ni propanda la sivyo nisingesimama hapa na tuzo," alisema.

Aliongeza licha ya yeye kuwa mstaafu wa umoja wa mataifa bado wanamfuatilia katika shughuli za kimaendeleo ambazo anazifanya akiwa ndani na nje ya nchi.

"Kama ukijikwaa, ukianguka na kusimama watu wanaangalia kulikoni, na huu ni utamaduni wao, kwa hiyo pale uongo na fitina havina nafasi," alisema kwa msisitizo wakati akizungumza na wanahabari.

Diwani wa Kata ya Karambi ambaye pia ni Mjumbe wa mkutano Mkuu wa Taifa wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM),  Felix Bwahama ambaye aliongozana na  Profesa Tibaijuka alishukuru UN kwa kumtunuku tuzo hiyo ambapo alisema ni fahari kwa wanakagera na taifa kwa ujumla licha ya baadhi ya watu nchini kubeza kazi anazizifanya ambazo zinaonekana kimataifa.



DC MWILAPWA AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA MAJI KUHUSU MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA

September 29, 2016
Mkuu wa wilaya ya Tangaa,Thobias Mwilapwa akifungua mkutano wa akifungua mkutano wa wadau kuhusu mkataba wa huduma kwa mteja iliyoandaliwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) uliofanyika kwenye ukumbi wa Veta Jijini Tanga kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi na kulia ni Afisa Tarafa ,Suleiman Zumo anayefuatia ni Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji hiyo,Haika Ndalama
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Mhandisi Zena Saidi akizungumza wakati wa kikao hicho kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa akimsikiliza kwa umakini 
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa),Haika Ndalama akzingumza wakati wa kikao hicho cha wadau

Wananchi wa Jiji la Tanga wakiongozwa na madiwani wao waki fuatilia kikao hicho kwa umakini mkubwa katikati ni Naibu Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga ,Mohamed Haniu
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga,Mustapha Selebosi akiuliza swali kwenye mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa Chuo cha Veta mjini hapa

Diwani wa Kata ya Msambweni (CUF)Abdurahamani Hassani akiuliza swali kwenye mkutano huo
Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa)Dorah Ilo kulia aakiteta jambo na Afisa Tarafa Suleimani Zumo wakati wa kikao hicho cha wadau
Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa)Dorah Ilo akifuatilia hoja mbalimbali zilizokuwa zikijiri kwenye kikao hicho
Kushoto ni Maafisa wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini na wananachi wakifuatilia kikao hicho wa kwanza kushoto ni Meneja wa Huduma kwa Mteja wa Mamlaka hiyo,Mohamed Pima


Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa akisaliana na Afisa Tarafa,Suleiman Zumo kabla ya kufungua mkutano huo katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi

Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa kushoto akisalimiana na Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga (CCM)Mustapa Selabosi kabla ya kuanza kikao hicho katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa)Haika Ndalama
Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa kushoto akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua kikao hicho

RAIS DKT MAGUFULI AONGOZA BARAZA LA MAWAZIRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

RAIS DKT MAGUFULI AONGOZA BARAZA LA MAWAZIRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

September 29, 2016
joh1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Mhe. Kassim
 Majaliwa kabla ya kuanza kwa Baraza la Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 29, 2016
joh2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongoza 
 Baraza la Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 29, 2016
joh3
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongoza
Baraza la Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 29, 2016
joh4
Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiongea mara baada ya kumalizika kwa Baraza la Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 29, 2016
PICHA NA IKULU
TAIFA STARS WATAKAOIVAA ETHIOPIA HAWA HAPA

TAIFA STARS WATAKAOIVAA ETHIOPIA HAWA HAPA

September 29, 2016
Kocha Mkuu wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Tanzania (Taifa Stars), Charles Boniface Mkwasa ametaja majina ya nyota 24 watakaounda kikosi ambacho kitasafiri mwishoni mwa wiki ijayo kwenda Addis Ababa, Ethiopia kucheza na wenyeji wetu kwenye mchezo wa kirafiki wa kimataifa utakaofanyika Oktoba 8, mwaka huu.
Mkwasa maarufu kwa jina la Master amesema wachezaji aliowaita wataingia kambini Oktoba 2, 2016 kabla ya kuanza kukiandaa kuanzia Oktoba 3, 2016 ikiwa mara baada ya michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara ya mwishoni mwa wiki hii ambako Mwadui itacheza na Azam huku Mbao ikishindina na JKT Ruvu Oktoba 2, mwaka huu.

Nyota wa Stars walioitwa na Mkwasa ni:
Makipa
Deogratius Munishi – Young Africans
Said Kipao – JKT Ruvu
Aishi Manula – Azam FC

Mabeki
Shomari Kapombe – Azam FC
Juma Abdul – Young Africans
Vicent Andrew - Young Africans
Mwinyi Haji - Young Africans
Mohamed Hussein – Simba SC
David Mwantika - Azam FC
James Josephat – Tanzania Prisons

Viungo wa Kati
Himid Mao - Azam FC
Mohammed Ibrahim – Simba SC
Jonas Mkude – Simba SC
Muzamiru Yassin – Simba SC

Viungo wa Pembeni
Shiza Kichuya – Simba SC
Simon Msuva - Young Africans
Juma Mahadhi - Young Africans
Jamal Mnyate – Simba
Hassan Kabunda – Mwadui FC

Washambuliaji
Ibrahim Ajib – Simba SC
John Bocco - Azam FC
Mbwana Samatta - CK Genk ya Ubelgiji
Elius Maguli – Oman
Thomas Ulimwengu – TP Mazembe Congo

TIGO YAWAKUMBUKA WAHANGA WA TETEMEKO MKOANI KWA KUTOA SARUJI MIFUKO 2424

September 29, 2016


Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Salum Kijuu(kushoto) akipokea sehemu ya mifuko ya saruji 2424 yenye thamani ya Sh 40 Milioni kutoka kwa Mkurugenzi wa Mtandao wa Tigo kanda ya ziwa Ali Mswanya,kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.


Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Salum Kijuu(kulia) akipeana mkono na Mkurugenzi wa Mtandao wa Tigo kanda ya ziwa Ali Mswanya alipomkabidhi sehemu ya mifuko ya saruji 2424 yenye thamani ya Sh 40 Milioni ,kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera,wa pili kulia ni Meneja wa Tigo Mkoani humo Sadock Phares.

Mkurugenzi wa Mtandao wa Tigo kanda ya ziwa Ali Mswanya akizungumza na  waanidishi wa habari mkoani Kagera alipomkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Salum Kijuu     sehemu ya mifuko ya saruji 2424 yenye thamani ya Sh 40 Milioni ,kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera

KAULI NZITO YA MAKOCHA SERENGETI BOYS

September 29, 2016
Shime maarufu kama Mchawi Mweusi, amezungumza hayo wakati anaendelea kufanya maandalizi ya mwisho ya mchezo dhidi ya Jamhuri ya Congo utakaofanyika Jumapili Oktoba 2, kwenye Uwanja wa Alphonse Massamba-Débat ulioko kwenye Makutano ya Barabara za Nkolo na Boko, hapa jijini Brazzaville.

Katika mazungumzo yake, Shime anasema: “Timu iko vizuri. Tumejiandaa vizuri kwa yale ya msingi yote tumekamilisha. Kwa hivyo, kila kitu kiko sawa, kama tulivyokusudia. Tupo hapa Congo kwa sasa kumalizia au kukumbushia mambo mawili au matatu hivi...
“Lakini pia tupo hapa Congo kuzoea hali ya hewa. Kwa bahati nzuri si tofuati na ya nyumbani Tanzania,” anasema Shime kwa kujiamini kabisa leo mchana Septemba 29, 2016 huku akijiandaa kwenye mazoezi.
Shime anasema kwamba mfumo atakaoutumia ni wa 4-4-2 katika mchezo huo wa kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana. Fainali hizo zitafanyika jijini Antananarivo, Madagascar mwezi Aprili, mwakani.
Anasema kwamba mfumo huo ni rafiki kwa Serengeti Boys kwani katika michezo takribani 15 ya kimataifa hajapoteza hata mmoja, “Kwa hivyo siwezi kubadili mfumo huu. Ni mfumo wa kushambulia na kulinda tusifungwe. Vijana wanauelewa zaidi na ndio mfumo wetu.”
Shime aliyekuwa mchezaji zamani kabla ya ndoto zake za kusonga mbele kufutwa kwa majeruhi, anasema kwamba benchi nzima la ufundi linafahamu kuwa mchezo wa Jumapili dhidi ya Congo ni mgumu kwa sababu ya umuhimu wake.
Na akiwaelezea Congo - wapinzani wake, Kocha Shime anasema: “Ni timu ya kawaida kwa maana wanafungika. Kwenye mchezo huu ukiangalia kwa makini sisi ndio tunahitaji zaidi ushindi kuliko Congo. Lakini nataka uwaambie Watanzania kwamba pamoja na hayo, nawaheshimu Congo, najua wako nyumbani lakini mwisho wa siku ni wachezaji 11 kila upande ndio watakaoingia uwanjani.”
Amesema kwamba amekiandaa kikosi chake vema kabisa katika eneo la mbinu, ufundi na saikolojia. “Akili za vijana wangu wooooote ni kuhakikisha tunafanya vema kwenye mchzo wa Jumapili.”
Naye Kocha wa Makipa, Muharami Mohammed au Shilton, alisema: “Silaha zangu ziko tayari kwa vita, makipa wangu wangu wote akiwamo Kelvin Kayego, Ramadhani Kabwili na Brazio wote wako fiti. Ye yote kati yao anaweza kucheza.”

MCHUNGAJI DKT.DANIEL KULOLA KURINDIMA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA INJILI JIJINI MWANZA.

September 29, 2016

Kanisa la EAGT Posta “B” Mabatini Jijini Mwanza chini ya Mchungaji Lameck Nkumba, linawakaribisha watu wote kwenye mkutano mkubwa wa injili utakaofanyika katika viwanja vya kanisa hilo vinavyotizamana na geti la polisi Mabatini nyuma ya iliyokuwa Orange Tree Hotel.

Mhubiri wa kitaifa na kimataifa ambaye amehubiri mataifa mbalimbali duniani ikiwemo Marekani, Canada, Uingereza, Ireland, Wales , Scotland, Ujerumani, Dernmark, Swirtzland, Afrika Kusini, DRC Congo na mengine mengi, Dkt.Daniel Moses Kulola (pichani), atahudumu kwenye mkutano huo akishirikiana na wahubiri wengine.

Ni wiki moja yenye miujiza na uponyaji wa nguvu ya Mungu, kuanzia jumapili tarehe 9.10.2016 hadi jumapili tarehe 16.10. 2016 muda ni kuanzia saa 9.00 mchana hadi saa 12 jioni, kila siku.

Waimbaji mbalimbali akiwemo Mwanyamaki kutoka Morogoro, Emannuel Mgogo kutoka Dar es salaam pamoja na kwaya zinatotamba Jijii Mwanza kama vile Havillah Gospel Singers kutoka EAGT Lumala Mpya, na kwaya ya EAGT Posta “B” zitahudumu kwenye mkutano huo.

Ewe baba, mama, kaka, dada, ndugu, jamaa na marafiki, fika kwenye mkutano huo ili ukutane na nguvu ya Mungu ambapo wagonjwa mbalimbali, wenye mapepo, mikosi na waliofungwa na vifungo vya ibirisi watafunguliwa kwa jina la Yesu, bila malipo.
Kwa msaada wa Kiroho, piga simu nambari 0784 43 77 82 
Bonyeza HAPA Kusikiliza, Au Bonyeza Play hapo chini .

Paul Mashauri awataka vijana kufanya kazi kwa bidii ili kuondokana na umaskini

September 29, 2016

Katika kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa nchi yenye maendeleo na iliyo na watu ambao wamefanikiwa kimaisha, vijana nchini wametakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kujikomboa na janga la umaskini lakini pia kulisaidia taifa kupata maendeleo.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HiTech International, Paul Mashauri wakati akizungumza na vijana ambao wanajifunza ujasiriamali na kuwambia ni vyema wakaongeza bidii katika ndoto wanazotamani kuzifikia ambazo pia zitawasaidia kuondokana na umaskini ambao umekithiri nchini.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HiTech International, Paul Mashauri akizungumza na vijana kuhusu ujasiriamali.
Alisema ili mtu kufanikiwa kimaisha haitaji zaidi elimu ya darasani bali ni muhusika mwenyewe kujiongeza kwa kufanya kazi kwa bidii katika jambo ambalo anatamani kulifikia na akiwatolea mfano yeye mwenyewe kuwa tangu amalize masomo yake katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hajawahi kurudi chuoni kuchukua cheti chake lakini amefanikiwa kimaisha.
"Mimi simchukii mtu ila nauchukia umaskini alionao, ukiwa na juhudi katika biashara na kujituma hata Rais Magufuli hatakufikia mshahara watu wanaweza kusema unafanya biashara ya kawaida lakini inakulipa sana, ni wewe tu na juhudi zako unazofanya ili ufanikiwe,
"Maisha hayana formula kuwa kufanikiwa ni lazima uwe na masters ndiyo upate mafanikio, masters ya maisha ni kuwa mtaani maisha yakupige alafu uinuke upambane na uyashinde hapo ndiyo umeyashinda maisha, ukitaka kufanikiwa lazima ufanye kazi kwa bidii hata mimi natumia muda wangu mwingi kujifunza ili nizidi kufanikiwa," alisema Mashauri.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HiTech International, Paul Mashauri akiwaeleza vijana jinsi wanavyoweza kufanikiwa kimaisha kwa kufanya biashara.

Washiriki kutoka Rwanda na Burundi wapigana ndani ya kijiji cha Maisha Plus.

September 29, 2016





Katika hali isiyotarajiwa katika kijiji cha Maisha Plus, jana washiriki wawili, KAREKEZI Jean kutoka Rwanda na BASWARI Nibigira kutoka Burundi walipigana hadharani huku wakirekodiwa na camera zilizofungwa kijijini hapo. 

Ilikua hivi;

SOLANGE kawakuta KAREKEZI na PATRICK wamekaa wanapiga stori akawaambia kwamba BASWARI alikua anamsema KAREKEZI kwa watu. 

KAREKEZI hakuonyesha kufurahishwa na ile hali, akapata hasira, PATRICK akachochea, akamwambia asikubali kudharauliwa, lazima akapigane. 

"Muacheni, kwani nyie hamjui BASWARI anavyojifanya anajua kila kitu?" SOLANGE akahoji.

PATRICK akaendelea kushauri kwamba KAREKEZI asikubali kuliacha liishie hapo.. Akampige BASWARI. 

Baada ya kuona KAREKEZI anashawishika kwenda kupigana 
SOLANGE akamzuia asiende ili isijulikane kwamba yeye ndio ameleta hizo taarifa. 

KAREKEZI akiwa amekasirika akasema, "Mimi sipendi dharau... awe anawadharau nyie wanawake sio sisi wanaume." 

PATRICK akazidi kuchochea.. 'Nenda kampige asituchukulie hivyo... Kwanini atuseme vibaya?'

SOLANGE: "Usimdanganye mwenzio aende kupigana... Be gentle, men can't act like that... be gentle..''

Baada ya kuona mambo hayataishia pale, SOLANGE akaomba wasiseme kama yeye ndio ameleta hayo maneno.

KAREKEZI akamfuata BASWARI. Akamshika. BASWARI naye akamshika. Wakavutana. KAREKEZI akamwambia BASWARI, "Usiwe unaingilia maisha yangu, haunijui, wala sipendi unavyonisema kwa watu..." 

KAREKEZI akamtukana BASWARI kwa kifaransa. 

Ugomvi ukaendelea kwa muda.

SOLANGE akakasirika akatoka eneo la tukio akaona kama amesalitiwa... "Kwanini umenifanyia hivi, watu wakijua mimi ndio nimesema hayo maneno nitakua na bad image kwenye society.."

"Unaharibu reputation yetu kwa kugombana kijijni."

BABU hapendagi Ujinga. Kuna kikao cha kijiji asubuhi hii. Mjadala mkali unaendelea juu ya hatima ya hawa washiriki. Tukutane Azam Two saa 3.30 usiku kujua kitakachojiri. 

#VijanaNdioNgazi #HapaKaziTu