UN YASHINDA KWENYE MAONYESHO YA 40 YA BIASHARA YA KIMATAIFA YA DAR ES SALAAM 2016

UN YASHINDA KWENYE MAONYESHO YA 40 YA BIASHARA YA KIMATAIFA YA DAR ES SALAAM 2016

July 04, 2016
Shirika la Umoja wa Mataifa limenyakua tuzo ya mwoneshaji bora kwenye kategori ya habari, machapisho, uchapishaji na vifaa vya ofisini katika sherehe za uzinduzi wa maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.

Tuzo hiyo imekabidhiwa na mgeni rasmi Rais wa Rwanda Mh. Paul Kagame na kupokelewa na Mkuu wa Masharika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Bw. Alvaro Rodriguez.

Umoja wa Mataifa umekuwa kinara wa kuelimisha wananchi, kupitia njia mbalimbali ikiwemo redio, magazeti mitandao ya kijamii na pia kushiriki katika maonyesho ya sabasaba kila mwaka kwa Zaidi ya miaka 6 na kwa miaka 5 mfululizo wamekuwa wakishinda tuzo hizo.

Umoja wa Mataifa mwaka huu umekuja na kampeni ya uhamasishaji wa Malengo ya dunia (Global Goals) na umuhimu wa watanzania kuyaelewa malengo hayo na kuwa mabalozi katika kuhakikisha malengo hayo mapya ya maendeleo endelevu (SDGs) yanatekelezeka.

Banda la Umoja wa Mataifa linapatikana katika ukumbi wa Karume yanakoendelea maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa almaarufu 'sabasaba' katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Rais wa Rwanda Paul Kagame, (wa pili kulia) akiwa na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli, (wa kwanza kulia), akimkabidhi tuzo ya mwoneshaji bora kwenye kategori ya habari, machapisho, uchapishaji na vifaa vya ofisini, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Bw. Alvaro Rodriguez, wakati wa uzinduzi wa maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam Julai 1, 2016. Wapili kushoto ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mh. Charles Mwijage.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Bw. Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wakiwa na tuzo ya ushindi katika banda lao. Kulia Felister Bwana wa Shirika la UNFPA Tanzania, Didi Nafisa (wa pili kulia) pamoja na Hoyce Temu (kushoto).
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Bw. Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wakiwa na tuzo ya mwoneshaji bora kwenye kipengele cha habari, machapisho, uchapishaji na vifaa vya ofisini katika banda lao. Kulia Felister Bwana wa Shirika la UNFPA Tanzania, Didi Nafisa (wa pili kulia), Hoyce Temu (katikati) pamoja na Edgar Kiliba (kushoto).
Wataalamu wa mawasiliano na Uhamasishajii (Communications, Advocacy and Partnership-COAP) wa ofisi ya Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini wakifurahia ushindi huo katika banda lao. Kutoka kushoto ni Edgar Kiliba, Hoyce Temu na Didi Nafisa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Bw. Alvaro Rodriguez (kulia) katika picha ya pamoja na vijana wanaojifunza kazi 'Intern' katika ofisi za Umoja wa Mataifa, Edgar Kiliba (katikati) na Msafiri Manongi.
Wananchi wakisaini kitabu cha wageni katika banda la Umoja wa Mataifa lililopo ukumbi wa Karume kwenye Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa almaarufu Sabasaba katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Barabara ya Kilwa jijni Dar es Salaam.
Kijana Msafiri Manongi anayejifunza kazi 'Intern' (kushoto) wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM), akitoa maelezo ya kazi mbalimbali zinazofanywa na mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini sambamba na elimu ya Malengo ya Dunia (Global Goals) kwa Maendeleo Endelevu kwa kijana mwenzake (jina halikuweza kupatikana) aliyetembelea banda UN kwenye maonyesho ya Sabasaba yanaoendelea kutimua vumbi jijini Dar es Salaam.
Kijana Msafiri Manongi anayejifunza kazi 'Intern' kwenye Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) (kushoto) akipozi na kijana mwenzake aliyetembelea banda la UN kujifunza shughuli mbalimbali za UN Tanzania na kujinyakulia zawadi ya tisheti.
Kijana Edgar Kiliba anayejifunza kazi 'Intern' katika kitengo cha Mawasiliano katika Ofisi ya Mkuu wa Umoja wa Mataifa Tanzania (kulia), akitoa elimu ya Malengo ya Dunia (Global Goals) kwa Maendeleo Endelevu kwa wananchi wanaoendelea kufurika kwenye banda la Umoja wa Mataifa katika maonyesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Ofisa wa Mawasiliano na Ushirikiano NUNV kutoka Ofisi ya Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Didi Nafisa akitoa maelezo ya kazi mbalimbali za Umoja wa Mataifa kwa Bw. Rehani Athumani wa NHIF (kulia) aliyetembelea banda la UN Tanzania katika maonyesho ya Sabasaba yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Katikati ni Kijana Edgar Kiliba anayejifunza kazi 'Intern' katika kitengo cha Mawasiliano katika Ofisi ya Mkuu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa Tanzania.
Makamu wa Rais wa Powerline Technologies Limited, Bw. Tumu Kaisi (kushoto) akibadilishana uzoefu na Kijana Msafiri Manongi anayejifunza kazi 'Intern' (kushoto) wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) alipotembelea banda la Umoja wa Mataifa kwenye maonyesho ya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Ofisa wa Mawasiliano na Ushirikiano NUNV kutoka Ofisi ya Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Didi Nafisa akimbandika zawadi ya beji ya' HE 4 SHE' ya Shirika la UN Women katika kampeni ya kuhamasisha wanaume waweze kuwasapoti wanawake katika nyanja mbalimbali kwa mmoja wa wananchi wanaoendelea kutembelea banda la Umoja wa Mataifa katika maonyesho ya Sabasaba yanayoendelea kushika kasi jijini Dar es Salaam.
Pichani juu na chini ni Baadhi ya wananchi wakisoma vipeperushi na majirada mbalimbali katika banda la Umoja wa Mataifa lililopo katika ukumbi wa Karume kwenye maonyesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

Mtoto akisoma moja ya vitabu vyenye michoro ya katuni ambacho kilimvutia akisome alipotembelea banda la Umoja wa Mataifa na wazazi wake.
Mmoja wa wananchi aliyetembelea banda la Umoja wa Mataifa kwenye maonyesho ya Sabasaba akifurahia zawadi ya tisheti yenye ujumbe mzito wa kukomesha ukatili wa kijinsia inayosomeka "FUNGUKA" Tumia malaka yako KUZUIA UKATILI WA KIJINSIA. Kulia ni Ofisa wa Mawasiliano na Ushirikiano NUNV kutoka Ofisi ya Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Didi Nafisa.
Mmoja wa Wakurugenzi wa Kampuni ya Zaidi Enterprises, Eng. Allen Kimambo katika picha na mabango ya Malengo ya Dunia (Global Goals) ambayo ni sehemu anayoyafanyia katika utekelezaji wa kuhakikisha malengo hayo yanafanikiwa.
Mtaalamu wa Mawasiliano Mwandamizi wa Ukanda wa Afrika wa Jhpiego, Bw. Charles Wanga akiwa na mabango ya Malengo ya Dunia (Global Goals) kwa Maendeleo Endelevu katika banda la UN Tanzania.

Mkutubi wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Harriet Macha katika picha ya pamoja na mmoja wa vijana aliyetembelea banda la Umoja wa Mataifa kwenye maonyesho ya Sabasaba.


Baadhi ya wananchi na familia zao waliotembelea banda la Umoja wa Mataifa wakipiga picha na mabango ya Malengo ya Dunia (Global Goals) ikiwa ni kampeni ya Umoja wa Mataifa katika utekelezaji wa malengo hayo kwa kila nchi mwananchama wa Umoja wa Mataifa.



Watoto nao waliwakilisha Malengo ya Dunia kwa Maendeleo Endelevu. Kulia ni Msafiri Manongi kutoka Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM).
Vijana wanaojifunza kazi katika Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini 'Intern' Edgar Kiliba (kushoto) na Msafiri Manongi (kulia) katika picha ya pamoja na wananchi wanaotembelea banda la Umoja wa Mataifa kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa na Mashirika hayo nchini.
-- Zainul A. Mzige, Operation Manager, MO BLOG, www.modewjiblog.com +255714940992.

BINTI WA MCHUNGAJI DANIEL KULOLA WA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA APATA MWENZA.

July 04, 2016
Bwana Harusi, Richard Jeremiah Gwapulukwa (kushoto) wa Kasamwa mkoani Geita, amefunga ndoa na Happness Daniel Kulola (kulia) ambae ni binti wa Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza.

Ndoa imefungwa katika Kanisa hilo hii leo na Mchungaji Paul Thomas Bagaka ambae pia ni msajili wa ndoa Manispaa ya Ilemela. Hafla ya ndoa hiyo inafanyika katika Ukumbi wa New Sun City Hotel Jijini Mwanza.
Na BMG
Maharusi wakiingia Kanisani kwa ajili ya Kufunga ndoa leo mchana
Maharusi wakiingia Kanisani kwa ajili ya Kufunga ndoa leo mchana
Maharusi wakisalimia. Pembeni ni wasimamizi/wapambe wao
Mchungaji Paul Thomas Bagaka ambae pia ni msajili wa ndoa Manispaa ya Ilemela, akitoa somo la ndoa kabla ya kuwafungisha maharusi ndoa
Mchungaji Paul Thomas Bagaka ambae pia ni msajili wa ndoa Manispaa ya Ilemela, wakiwafungisha maharusi ndoa
Bwana harusi akimvalisha bibi harusi pete ya ndoa
Bibi harusi akimvalisha bwana harusi pete ya ndoa
Maharusi wakiombewa na viongozi wa dini pamoja na wazazi
Maharusi pamoja na wasimamizi/wapambe wao
Kutoka kulia ni Mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya, Dkt.Daniel Moses Kulola, Mama Mchungaji, Mercy Daniel Kulola, Mama mzazi na mchungaji na viongozi wa kanisa.
Brighters wakiingia ukumbini
Ndoa ilishuhudiwa na ndugu, jamaa na marafiki wakiwemo waumini wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya.

CUF YAZINDUA TAWI LA WANAFUNZI WANACHAMA WA CUF LA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (JIVICUF UDSM)

July 04, 2016
 Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa , Juvicuf, ambaye pia ni Mbunge wa Mchinga Hamidu Bobal (kushoto), akizungumza na wanafunzi wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (JIVICUF UDSM), Dar es Salaam jana wakati akizindua tawi la wanafunzi hao katika chuoni hapo.
 Mbunge wa Kilwa Kusini Seleman Bungara maarufu Bwege (CUF), akizungumza na wanafunzi hao katika uzinduzi huo.
 Mbunge wa Liwale Zubeir Kuchauka (CUF), akichangia jambo kwenye mkutano huo wa uzinduzi.
Mwongozaji wa uzinduzi wa tawi hilo, akiwa kazini.
 Mbunge wa Viti Maalumu (CUF) kutoka Pangani akichangia jambo.
 Taswira meza kuu katika uzinduzi huo.
 Wanafunzi hao wakiwa katika hafla hiyo ya uzinduzi.
 Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa , Juvicuf, ambaye pia ni Mbunge wa Mchinga Hamidu Bobal (kushoto), akikabidhi kadi kwa wanafunzi hao.
 Kadi zikitolewa.
 Kadi zikiendelea kutolewa.


 Hapa ni wanafunzi hao wakiwa na furaha baada ya kukabidhiwa kadi
 Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa , Juvicuf, ambaye pia ni Mbunge wa Mchinga Hamidu Bobal (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi hao baada ya kuzindua tawi hilo.

Picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa kadi za kujiunga na umoja huo.

Na Mwandishi Wetu

CHAMA cha Wananchi (CUF), kimezindua Tawi la Wanafunzi wanachama wa CUF la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Jivicuf UDSM), ikiwa ni moja ya mikakati ya kujitanua kisiasa kwa chama hicho.

Uzinduzi huo umefanywa na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa , Juvicuf, ambaye pia ni Mbunge wa Mchinga Hamidu Bobal, Dar es Salaam jana ambapo aliwataka vijana kutumia ujana kupigania haki na demokrasia nchini

Alisema pamoja na kupigiani haki hasa za wanyonge vijana pia wanapaswa kushika nafasi mbalimbali za uongozi ili kusimamia rasilimali za nchini na wananchi.

"Nimezindua tawi hili la Juvicuf UDSM, nawataka mfanye siasa za nidhamu lakini msiwe waoga kwani sisi tumechelewa katika hizi harakati naamini mtaendana na kasi ambayo tunataka ya kuitanga CUF kila mahali." alisema

Alisema atawapigania vijana wote ambao watashiriki katika nafasi za uongozi kuanzia ngazi ya mitaa, vijiji, kata, wilaya, jimbo, mkoa na taifa ili kuendeleza chama chao.

Bobal aliwapa tahadhari vijana hao kuwa siasa si jambo la lelemama wanahitajika kujituma ili kuweza kufikia mafanikio kwani yeye mwenyewe amepitia changamoto nyingi hadi kufikia hapo alipo.

Mbunge huyo alisema historia yake alikuwa mwalimu wa Sekondari ambapo alipotangaza kujihusisha na siasa alipata changamoto kutoka kwa walimu wenzake ila leo amefanikiwab kuwa mbunge na kutumikia wananchi wa Mchinga.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mbunge wa Kilwa Kusini Seleman Bungara maarufu Bwege CUF, aliwataka vijana hao kujikita katika kutetea wanyonge kwani ndio njia ambayo itawasaidia kuchaguliwa na wananchi.

"Mimi nilifanikiwa kushinda ubunge kwa sababu nilikuwa natetea watu wanyonge nilipambana na watu matajiri lakini niliwashinda kwa sababu wananchi waliangalia mtu sahihi na si fedha," alisema.


Mbunge wa Liwale Zubeir Kuchauka CUF, alisema siasa ndio kila kitu katika maisha hivyo ni vigumu kutenganisha siasa na wananchi.

Kuchauka aliwataka vijana hao kuwa wavumilivu katika kupigania maslahi ya nchi kwa kuweka uzalendo mbele na haki.

Mwenyekiti wa Juvicuf UDSM, Jidawi Chande, alisema, tawi hilo kwa sasa lina vijana wanachama wa CUF zaidi ya 100.

Alisema changamoto walizonazo ni ukosefu wa ofisi hivyo kuwaomba wabunge hao kuwasaidia kupata ofisi ili waweze kufanya kazi cha chama kwa uhuru.