DC MUHEZA APIGA MAFUKURU MATUMIZI YA SIMU ZA MIKONONI KWA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI.

August 11, 2013

NA SELEMANI KIBUGO,MUHEZA.

MKUU wa wilaya ya Muheza, Subira Mgalu amepiga marufuku matumizi ya simu za mkononi kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani humo kwa madai kuwa zinachangia matokeo mabaya ya mitihani

Wito huo umetolewa na mkuu huyo wa wilaya katika kikao cha wazazi wa wanafunzi hao kuwakumbusha juu ya ulipaji wa ada kwa wakati katika shule ya sekondari ya Mang’enya wilayani humo.

Amesema kuwa mwanafunzi yeyote akikutwa na simu walimu wazichukuwe wazipeleke  ofisini kwake kwa ajili ya kuuzwa ili ichangie ujenzi wa maabara.

Mkuu huyo wa wilaya pia amewataka wazazi kulipa ada kwa wakati mpaka tarehe 30 mwezi huu wawe wazazi wamelipa ada zote wanazodaiwa.

Hata hivyo mkuu wa wilaya huyo amesema kuwa viboko virudishwe katika shule ya Mang’enya na mwanafunzi aadhibiwe kulingana na kosa lenyewe kama vile utoro,utovu wa nidhamu na kukutwa na simu.

Amesema atachangia katika shule huyo shilingi Laki tano kwa ajili ya ujenzi wa maabara huku akiwaomba wafadhili kujitokeza kuchangia ukarabati wa majengo utakoanza mwezi wa 9 mwaka huu.


MUHEZA YAWEKA MIKAKATI YA KUJENGA VITUO VYA AFYA KILA KATA.

August 11, 2013



Na Selemani Kibugo,Muheza

SERIKALI wilayani Muheza imeweka  mpango mkakati wa kuhakikisha wanajenga vituo vya Afya kila kata wilayani humo ili kusogeza huduma za Afya karibu na wananchi wake

Hayo yamesemwa na Mbunge wa jimbo la Muheza, Herbert Mntangi wakati akizungumza na wananchi wa vijiji vya Mashewa,Kilongo,Tingeni na  Kisiwani Kata ya Kisiwani.

Amesema kuwa serikali inampango wa kujenga vituo vya Afya kata zote pamoja na Zahanati ambapo hiyo ni ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM natayari vituo vitatu vimeshaanza kujengwa ambako ni Songa,Ubwari naMisalai ambavyo ni vya kisasa.

Kwa upande wa elimu amesema kuwa wanakusudia kuipandisisha hadhi shule ya sekondari Shebomeza kuwa ya kidato cha tano na sita na watajenga kila Tarafa sekondari moja ya kidato cha tano na sita na kuahidi walimu wamsingi na sekondari kuboreshewa huduma za nyumba na maslahi.

HANDENI WASHAURIWA KUHIFADHI CHAKULA.

August 11, 2013

Na Oscar Assenga,Handeni
WANANCHI wa wilaya ya Handeni mkoani Tanga wameshauriwa kuhifadhi chakula cha kutosha ili kujihadhari na upungufu wa chakula unaoweza kujitokeza kutokana na wilaya hiyo kutopata mavuno ya kutosha.

Ushauri huo ilitolewa na Kaimu Ofisa Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wa wilaya hiyo, Yibarila Kamele wakati akizungumza na mwandishi wa blog hii kuhusiana na maendeleo ya kilimo wilayani humo.

Kamele amesema kukosekana kwa mvua ya kutosha mwishoni mwa msimu huu kume sababisha wakulima kukosa mavuno ya kutosha kama walivyotegemea hali ambayo inaweza kuleta ukosefu wa chakula kama wananchi hawatakuwa makini na kuuza chakula hicho kidogo walichopata.

Amesema kuwa ni muhimu kila mwananchi ahifadhi chakula cha kutosha kwa msimu wote ujao ambapo kila kaya ya watu sita inatakiwa kujiwekea jumla ya magunia 18 ambayo ndio kadili la chakula kwa kaya.

Aidha pia Kamele amesema kuwa wananchi wote ambao watauza mahindi wauze kwa wakala wa taifa wa kuhifadhi chakula (NFRA) ambao kwa sasa wameshaingia Handeni na wananunua kilo moja ya mahindi kwa shilingi 530 na sio kama wanavyonunua wachuuzi wengine ambao wao wananunua kilo 350 ambayo inamuumiza mwananchi.

WAKULIMA WA KOROSHO KATA YA BWITI MKINGA WAITAKA SERIKALI KUCHUKUA HATUA ZA HARAKA ZA KUKAMILISHA MALIPO.

August 11, 2013

NA OSCAR ASSENGA,MKINGA
WAKULIMA wa Korosho wa Kata ya Bwiti wilayani Mkinga wameitaka Serikali kuchukua hatua za haraka kukamilisha malipo ya  korosho ili kuondoa uwezekano wa kutokea vitendo vya uvunjifu wa amani kama ilivyokuwa kwa wananchi wa Mtwara.

Wananchi hao wamesema kwa muda mrefu wamekuwa wakizungushwa kuhusu malipo stahili ya korosho zao na kumpa siku tatu Diwani wa Kata hiyo, Peter Kimweri kuhakikisha wanalipwa fedha hizo.

Wamesema ni jambo la kushangaza kuona hadi sasa bado hawajalipwa fedha zao za korosho huku kukiwa hakuna taarifa yoyote kutoka Serikalini.

Akizungumza na blogg hii,Diwani wa Kata hiyo, Kimweri amekiri kuwepo kwa malalamiko hayo ya wakulima na kumtaka Mkuu wa wilaya ya Mkinga kuingilia kati ili kunusuru kutokea vitendo vya uvunjifu wa amani.

Kimweri amesema kwa muda mrefu wakulima hao wamekuwa wakilalamikia fedha zao na kwamba Serikali imekuwa kimya hali inayopandikiza chuki miongoni mwa wakulima dhidi ya Serikali yao.

LIGI YA WILAYA YA KOROGWE KUTIMUA VUMBI OCTOBA 10 MWAKA HUU.

August 11, 2013
(Katibu wa Chama cha Soka wilaya ya Korogwe Zaina Kassama wa Tatu anayemfuatia Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa)

Na Safari Chuwa,Korogwe.
LIGI ya soka wilaya ya Korogwe inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Octoba 10 mwaka huu ambapo itachezwa katika viwanja ambavyo vitatangazwa baadae na chama cha soka wilaya ya Korogwe (KDFA).

Katibu wa Chama hicho,Zaina Hassani alisema maandalizi ya ligi hiyo yanaendelea vizuri na kueleza mpaka wakati huu timu nane zimejitokeza kuchukua fomu za kushiriki huku timu zaidi ya ishirikini zikitarajiwa kushiriki.

Hassani alizitaja timu ambazo zimechukua fomu ni Kilole,New Cap,Ngombezi,Nyota SC, Kwamndolwa, Liver Pool,Mombo Shooting na Millan FC na kutoa wito kwa timu nyengine kujitokeza kushiriki mashindano hayo.

Alisema ligi hiyo itachezwa kwenye vituo mbalimbali wilayani humo ambapo washindi kila kituo watakutana kwenye kituo kimoja ili kuweza kumpata bingwa wa wilaya hiyo.

Katibu huyo alisema baada ya kupatikana bingwa wa wilaya hiyo atapata fuksa ya kuungana na mabingwa wengine kutokana wilaya mbalimbali kucheza ligi ya mkoa.

AFRICAN SPORTS KUKUTANA NA WANACHAMA WAKE KESHO.

August 11, 2013
NA OSCAR ASSENGA,TANGA.
TIMU ya African Sports "Wanakimanumanu"wanatarajiwa kuwa na mkutano na wanachama wao kesho saa kumi na moja jioni makao makuu ya klabu hiyo barabara 12 jijini Tanga lengo likiwa ni kujadili maendeleo ya timu hiyo.

Kwa mujibu wa Msemaji wa Klabu hiyo,Said Karsandas alisema kwenye kikao hicho kutakuwa na agenda

mbalimbali ambazo zitajadiliwa kwa ajili ya mustakabali wa timu hiyo kongwe hapa nchini.

Karsandas alisema licha ya kuzungumzia maendeleo lakini pia watatumia muda huo kujadili suala la uchaguzi mkuu wa timu hiyo ambao utafanyika katikati ya mwezi huu .

Alisema wanachama pekee ndio ambao wataruhusiwa kushiriki katika mkutano huo ambao ni muhimu sana kwa ajili ya maendeleo yao pamoja na kupanga mikakati ya ushiriki wao kwenye ligi ya mkoa msimu huu.
 

PONDAMALI :MZIKI UNALIPA ZAIDI KULIKO MPIRA.

August 11, 2013

Na Oscar Assenga,Tanga.
MSANII Mpya wa Muziki wa BongoFleva hapa nchini,Juma Pondamali “Mensa”amesema mziki huo unalipa sana kuliko hapa mchezo wa mpira wa miguu ila itatagemea na umahiri ulionao katika kutoa mashairi mazuri.

Akizungumza na Tanga Raha,Pondamali ambaye hivi sasa anatamba na wimbo wake “Pesa baba yako nani”ambao ameirekodi kwenye studio za Suleshi alisema ameamua kuingia kwenye mziki huo sio kwa kutania bali ni dhamiri yake aliyekuwa nayo muda mrefu.

Pondamali alienda mbali zaidi na kueleza anamshukuru mwenyezi mungu kwa kumjalia kipaji cha utunzi mzuri na uimbaji kitu ambacho kitampa wakati mzuri wakati akiwa katika harakati zake za kuachia album lakini akisema wakati huu amepanga kuachia single tu.
    
“Ninamshukuru mwenyezi mungu amenijali kipaji kizuri cha utunzi na sio kama ninatania nimedhamiri kweli kufanya mziki kwa sababu unalipa kuliko ilivyo soka na unaweza kuuza single moja tu ukapata fedha nzuri “Alisema Mensa.

Aidha aliongeza kuwa licha ya kuimba mziki hatoweza kuiacha kazi yake aliyokuwa nayo hivi sasa kwani anaiheshimu na kuithamini hivyo atafanya mziki na kufundisha soka kwani kila kitu hapo kinawakati wake na muda.

Pondamali ambaye pia ni Kocha wa Makipa kwenye timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa Stars”na timu ya Coastal Union ya Tanga alisema malengo yake makubwa ni kuhakisha anafanya vizuri kwa kutoa nyimbo mzuri ambazo zitaweza kumpa mafanikio zaidi.

SEMINA YA MAKAMISHNA YAANZA DAR, MWANZA

August 11, 2013
NA BONIFACE WAMBURA,DAR ES SALAAM.
Semina kwa ajili ya makamishna wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) pamoja na mtihani wa utimamu wa mwili (physical fitness test) kwa  waamuzi wote wa daraja la kwanza (Class I) wanaotaka kuchezesha VPL msimu wa 2013/2014 vinaanza kesho (Agosti 12 mwaka huu) katika vituo vya Dar es Salaam na Mwanza.

Mafunzo hayo yatakayomalizika Agosti 14 mwaka huu yatakuwa chini ya wakufunzi Leslie Liunda, Joan Minja na Riziki Majara kwa kituo cha Dar es Salaam wakati kituo cha Mwanza kitakuwa na Alfred Rwiza na Omari Kasinde.

Kwa Dar es Salaam mafunzo yatafanyika Uwanja wa Taifa wakati Mwanza itakuwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba.
 

Kituo cha Mwanza kitakuwa na makamishna na waamuzi kutoka mikoa ya Geita, Kagera, Katavi, Kigoma, Manyara, Mara, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Singida na Tabora.

Kituo cha Dar es Salaam kitahusisha waamuzi na makamishna kutoka mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Kilimanjaro, Lindi, Mbeya, Morogoro, Mtwara, Njombe, Pwani, Ruvuma na Tanga.

Washiriki wote wanakumbushwa kuwa ni lazima wafuate utaratibu huo wa vituo, na si vinginevyo.

MAKOCHA 32 KUSHIRIKI KOZI YA FIFA COPA COCA-COLA

August 11, 2013
NA BONIFACE WAMBURA,DAR ES SALAAM.

Makocha 32 kutoka mikoa ya Tanzania Bara na Visiwani wanashiriki kozi ya Copa Coca-Cola inayoanza kesho (Agosti 12 mwaka huu) jijini Dar es Salaam chini ya Mkufunzi kutoka Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Mpira wa Miguu (FIFA).

Kozi hiyo itakayomalizika Agosti 17 mwaka huu itafunguliwa saa 3 kamili asubuhi kwenye ukumbi wa Msimbazi Centre na washiriki wote tayari wameshawasili Dar es Salaam. Mkufunzi wa kozi hiyo ni Govinder Thondoo kutoka Mauritius.


Washiriki wa kozi hiyo ni Ahazi Ibrahim Kasegese (Mbeya), Aloyce Mayombo (Pwani), Andrew Zoma (Tabora), Asuri Msakamali (Simiyu), Bakari Khamis Kilambo (Kaskazini Pemba), Chacha Sambulo (Mara), Charles Rwezaura (Kagera), Daniel Sambala (Njombe), Dudu Haruni (Iringa) na Emmanuel Kapurata (Rukwa).


Faki Makame Haji (Kaskazini Unguja), Fatawi Khamis Sheha (Kusini Pemba), Hamisi Omary Mabo (Kigoma), Hussein Maulid (Morogoro), Issa Lugaza (Kilimanjaro), James Gaspar (Shinyanga), James Wambura (Arusha), Jomo Jackson Puccey (Lindi), Joseph Sihaba (Dodoma), Kelvin Haule (Ruvuma) na Kessy Juma Abdallah (Tanga).


Kessy Mziray (Mwanza), Menswi Mchwampaka (Kinondoni), Mohamed Abdallah Kweka (Singida), Nurdin Gogola (Temeke),  Pius Kamande (Rukwa), Ramadhan Abrahman Ramadhan (Mjini Magharibi), Ramadhan Salum Mnyoti (Manyara), Raphael Ngeleja (Geita), Samuel Edgar Maokola (Ilala), Shaweji Nawanda (Mtwara) na Vuai Abdul Haji (Kusini Unguja).


Fainali za U15 Copa Coca-Cola ngazi ya Taifa zitafanyika Septemba mwaka huu jijini Dar es Salaam.