UAMUZI WA MATOKEO KUNDI C KUTOLEWA KAMATI YA NIDHAMU

UAMUZI WA MATOKEO KUNDI C KUTOLEWA KAMATI YA NIDHAMU

February 17, 2016
Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi ya Ligi (Kamati ya Saa 72) imekutana jana (Februari 16, 2016) kupitia taarifa za mechi mbili za Kundi C la Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes kati ya JKT Kanembwa na Geita Gold SC, na Polisi Tabora na JKT Oljoro ambapo Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) lilisimamisha matokeo yake hadi taarifa hizo zitakapopitiwa.

JKT Kanembwa ilifungwa mabao 8-0 na Geita Gold SC katika mechi iliyofanyika Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma, wakati Polisi Tabora ilishinda mabao 7-0 dhidi ya JKT Oljoro kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.

Baada ya kupitia taarifa hizo na vielelezo vingine, Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imeonyesha mashaka kutokana na kuwepo viashiria vya upangaji wa matokeo (match fixing).

Kwa vile suala hilo linahusisha masuala ya kinidhamu, na kwa kuzingatia Ibara ya 50(1) na (11) ya Katiba ya TFF na Ibara ya 69 ya Kanuni za Nidhamu za TFF, Kamati ya Saa 72 imemuelekeza Katibu Mkuu wa TFF apeleke suala kwenye Kamati ya Nidhamu ya TFF kwa ajili ya uchunguzi na hatimaye kufanya uamuzi.

BIOTEKNOLOJIA YA KILIMO NCHINI KUFANYIWA UTAFITI

February 17, 2016


Mkuu wa Idara ya Uchumi na Uzalishaji Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Ndaro Kulwijila (katikati), akiwakaribisha mkoani humo watafiti wa kilimo kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), ambao walifika ofisini kwake kujitambulisha kabla ya kwenda kutoa mafunzo kwa watafiti, wakulima na wadau wa kilimo kuhusu matumimizi ya kilimo cha  bioteknolojia ambacho kinafanyiwa utafiti na watafiti wa kilimo kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech.


Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ukiruguru kilichopo jijini Mwanza, Dk.Evelyne Lukonge (wa pili kulia), akifurahi wakati akisalimiana na Mtafiti Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia, Dk.Emmarold Mneney alipo wasili na maofisa wenzake watafiti katika ofisi yake kujitambulisha kabla ya kutoa mafunzo kwa watafiti wa kituo hicho na wadau wa kilimo. Kulia ni Mtafiti Kiongozi kutoka Costech, Dk.Nicholaus Nyange na wa pili kushoto ni Mratibu Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia Afrika, Daniel Utunge kutoka nchini Kenya.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ukiruguru kilichopo jijini Mwanza, Dk.Evelyne Lukonge, akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni Mtafiti Kiongozi wa Costech, Dk.Nicholaus Nyange.
Mtafiti Kiongozi wa Costech, Dk.Nicholaus Nyange (kulia), akisisitiza jambo kwenye mafunzo hayo ya matumizi ya bioteknolojia.
Mtafiti Mkuu kutoka Jukwaa la Bioteknolojia, Dk.Emmarold Mneney (kushoto), akifundisha kuhusu matumizi ya teknolojia mpya ya bioteknolojia katika semina hiyo iliyofanyika Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ukiruguru cha jijini Mwanza.
Watafiti na washiriki wakiwa kwenye semina hiyo.
Semina ikiendelea.

Mratibu Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia Afrika, Daniel Utunge kutoka nchini Kenya (kushoto), akiwa kwenye semina hiyo. Wa pili kushoto ni Ofisa kutoka Costech, Mohamed Nyamka na kulia ni mshiriki wa semina hiyo.
Mafunzo yakiendelea.
Watafiti na washiriki wakiwa katika semina hiyo.
Washiriki wakifuatilia kwa karibu mafunzo hayo.
Mtafiti kutoka ARI -Ukiriguru, Maganga Joseph akiuliza swali katika semina hiyo.
Taswira ya ukumbi wa semina hiyo.

Na Dotto Mwaibale, Mwanza

MTAFITI Kiongozi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech) Dk.Ncholaus Nyange amesema Bioteknojia ya kilimo nchini itafanyiwa utafiti ili kukabiliana na changamoto ya mazao kuharibika.

Hayo aliyaelezwa jijini Mwanza katika semina ya siku moja ya Jukwaa la Bioteknojia iliyoandaliwa mahsusi kwa watafiti na wadau wa kilimo.

Alisema ni muhimu bioteknojia ya kilimo kufanyiwa utafiti ili kwenda sanjari ya dunia ya kilimo ambayo inahitahi watafiti.

Katika hatua nyingine Dk. Nyange amewataka wananchi na wataalamu mbalimbali kuthamini tafiti za kilimo za bioteknolojia zinazofanywa na watafiti wetu wa ndani badala ya kusikiliza propoganda za nje kuwa hazifai.

"Bioteknolojia au uandisijemi ni teknolojia ambayo inakubalika lakini kuna taasisi kadhaa za nje hazilali usingizi zinaeneza propoganda kuwa haifai wakati wao wanaitumia" alisema Nyange.

Alisema teknolojia hiyo inayotumika kwa kilimo cha pamba imeleta mafanikio makubwa katika nchi za Bakinafaso, India, Marekani na nyingine nyingi ambazo hivi sasa zimekuwa zikiongoza kwa utengenezaji wa nguo za kotoni duniani lakini nchi hizo zimekuwa mstari wa mbele kuzuia isitumike hapa nchini.

Mtafiti Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia, Dk.Emmarold Mneney alisema teknolojia hiyo mpya ambayo ina zaidi ya miaka 20 imesaidia kukabiliana na changamoto ya mabadiliko ya tabianchi kutokana na kuwepo kwa ukame, magugu na wadudu waharibifu wa mazao na ndio maana wameamua kuipeleka kwa wakulima ili waijue.

"Tumeamua kuwafuata watafiti mikoani ili kuendesha mafunzo ya teknolojia hii mpya ambapo tumeanza hapa Mwanza na tutaenda Bunda na Butihama mkoani Mara na watu tuliowalenga ni watafiti wa kilimo, walimu ambao tunaamini wakiilewa nao watatoa elimu hiyo kwa makundi mengine" alisema Dk.Mneney.

Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ukiruguru, Dk. Evelyne Lukonge alisema katika ukanda huo wa ziwa changamoto kubwa waliyonayo ni magonjwa ya mazao ya pamba, ndizi, viazi na mihogo hivyo njia pekee ni kwa watafiti kutumia teknolojia hiyo ili kuwa komboa wakulima.

Dk. Lukonge alisema changamoto nyingine kubwa ni fedha za kusaidia kufanya tafiti hizo ambapo aliiomba serikali kuliangalia suala hilo kwa karibu zaidi.

Mkuu wa Idara ya Uchumi na Uzalishaji Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Ndaro Kulwijila akiwakaribisha mkoani humo watafiti hao kutoka Costech alisema hivi sasa duniani hakuna kilimo kitakachofanikiwa bila ya kuwa na watafiti hivyo aliiomba serikali kutenga fedha za kutoka ili kuwawezesha watafiti kwa ajili ya  kufanya tafiti mbalimbali za kilimo.

Kulwijila alisema mkoani humo changamoto kubwa waliyonayo ni kupanda kwa gharama kubwa ya kilimo cha pamba kwani bei yake imeendelea kuporomoka kutoka sh.1200 kwa kilo hadi kufikia sh. 800 hadi 700 jambo linalowakatisha tamaa wakulima.

GERMANY DONATE SURVEILLANCE AIRCRAFT TO SERENGETI NATIONAL PARK

February 17, 2016
Minister for Natural Resources and Tourism Prof. Jumanne Maghembe (right) receive Germany Ambassador in Tanzania Egon Kochanke during the handing over event of the Husky Surveillance aircraft to Serengeti National Park over the weekend.
The Husky surveillance aircraft donated by Germany to Serengeti National Park to enhance patrol activities
 Minister for Natural Resources and Tourism Prof. Jumanne Maghembe greet Serengeti National Park Tourism Warden Godson Kimaro during the handing over event.
  Germany Ambassador in Tanzania Egon Kochanke (2nd left) delivering his speech during the handing over event. Others in the picture from left are Serengeti Chief Park Warden William Mwakilema,  Minister for Natural Resources and Tourism Pro. Jumanne Maghembe and Director General of TANAPA Allan Kijazi.
  Germany Ambassador Hon. Egon Kochanke (2nd left) handing over a certificate of ownership of the Husky surveillance aircraft donated to Serengeti National Park to the Minister for Natural Resources and Tourism Pro. Jumanne Maghembe. Others in the picture are FZS Program Manager for Africa Gerald Bigurube, Acting Director General of TAWA Martin Loibooki, TANAPA Director General Allan Kijazi, Serengeti Chief Park Warden William Mwakilema and TANAPA Director of Tourism and Marketing Ibrahim Mussa. 

   
                                    
                                                                   






 Joint Press release by Tanzania National Parks, German Embassy Tanzania, and Frankfurt Zoological Society

A Husky to help watch over the Serengeti

Seronera, 15 February 2016 – Today, the German Ambassador to Tanzania handed over an aircraft to the Tanzanian Minister of Natural Resources and Tourism. The Husky aircraft will be deployed by Frankfurt Zoological Society (FZS) for surveillance of the Serengeti National Park to support TANAPA’s fight against poaching.

„We are seeing the large mammals of our protected areas under a severe threat of local extinction because of poaching,“ said Minister Jumanne Maghembe on the occasion of the handover in Seronera. He thanked the German government for the support in countering the recent upsurge in poaching.

“Stringent law enforcement, community involvement and ecosystem management are key in the fight against poaching”, said the German Ambassador Egon Kochanke. “I am very proud to be able to hand this aircraft over to the Tanzanian authorities and FZS. This is an important cornerstone of our close and longstanding cooperation.”

Frankfurt Zoological Society will operate the aircraft in close cooperation with the Serengeti National Park Authority. With aerial support, poacher camps and illegal activities can be detected and the pilots can provide critical information to reaction forces on the ground.

Tanzanian wildlife authorities are faced with a dramatic upsurge of poaching threatening the country’s populations of elephants and rhinos. To counter this threat and to support wildlife and habitat monitoring, the German Government through the German Federal Ministry for Economic Cooperation and Development (BMZ) has provided funding for the acquisition of three aircraft.

The other two Husky A-1C Aircraft will be deployed in the Tanzanian Selous Game Reserve and the Zambian North Luangwa National Park. The Husky is well suited for monitoring and anti-poaching surveys as it operates at low heights and slow speeds.

This support is part of longer-term financial and technical development cooperation measures implemented by FZS, GIZ, KfW, in collaboration with Tanzania Wildlife Authority TAWA, Tanzania National Parks TANAPA, and the Zambian Department of National Parks and Wildlife DNPW.


For further information, please contact:

Paschal Shelutete
Corporate Communications Manager
Tanzania National Parks
Tel.: 0754 313 248
shelutete@yahoo.com
John Merikion
Communications officer
German Embassy
Tel +255 (0)755 696 366
Pr-100@dare.diplo.de
Patrick Eickemeier
Africa Communications Manager
Frankfurt Zoological Society
Tel.: 0732 985 768
patrick.eickemeier@fzs.org




“UKAGUZI WA VYOMBO MAJINI KUHAKIKISHA UBORA NA USALAMA”

February 17, 2016
MAMLAKA ya Udhibiti Usafiri wa nchi kavu na Majini Mkoani Tanga (Sumatra) wakishirikiana na Jeshi la Polisi kikosi cha Maji mkoani hapa wameanza ukaguzi maalumu wa siku saba kwa vyombo vya majini ili kudhibiti ubora na usalama kitendo ambacho kitasaidia pia kupunguza ajali zinazoweza kutokea kutokana na ubovu kwa baadhi yao.

Zoezi hilo litasimamiwa na Afisa mfawidhi wa SUMATRA Tanga Dr.
  Walukani Luhamba, Maafisa wakaguzi wa vyombo vya majini Captain Alex Katama, Mhandisi Christopher Mlelwa waliotokea makao makuu.

Akizungumza na Tanga Raha Blog, Ofisa Mfawidhi wa Sumatra mkoani Tanga, Dkt Walukani
  Luhamba alisema hali hiyo itasaidia pia kudhibiti wimbi la uingizwaji wa madawa ya kulevya unaopitishwa na vyombo ikiwemo ubora wa vifaa vya
usalama na kuhakikisha vinafanya kazi kwa mujibu wa sheria na
vitakavyobainika kukiuka viwango vya ubora kisheria kuzuiwa kufanya
kazi.

Alisema sambamba na hilo itasaidia kuvifanya vyombo vinavyofanya
  biashara zisizokuwa halali kuhofia iwapo vitafanya hivyo vitakumbana na adhabu kali ikiwemo kukamatwa na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria zilizopo. 

Vyombo visivyosajiliwa na Sumatra vitachukuliwa hatuaya kisheria ikiwa ni pamoja na faini ya shilingi 500,000/= au faini
pamoja na kifungo kulingana na sheria. (Merchant shipping act 2003)
   “Mara nyingi vyombo ambavyo vinafanya kazi zao majini hasa katika bandari bubu visivyokuwa na leseni vimekuwa vikijihusisha na uingizaji wa madawa ya kulevya hivyo ukaguzi huu utawezesha kusaidia kupunguza wimbi la uingizwaji wa madawa ya kulevya kupitia bandari hizo “Alisema Dkt Luhamba.

Aidha alisema kuwa ukaguzi huo utakwenda sambamba na kutoa elimu kwa
  wamiliki na watumiaji ikiwemo kuangalia kama wamiliki wa vyombo vya majini wanafuata sheria za majini kama ilivyoelekezwa.
  “Unajua sheria ya udhibiti wa vyombo vya majini (Merchant Shipping Act, 2003 inayoelekeza vyombo vyote vya usafirishaji majini lazima vikaguliwe na kusajiliwa kupitia mamlaka husika Sumatra “Alisema Dkt Walukani.

“Lakini vitu vya kuzingatia kabla ya chombo kusajiliwa ni kwanza

kinatakiwa kukaguliwa sambamba na kuwepo kwa vifaa vya kujiokolea, kiwe na Nanga na Injini kwa ajili ya kuendesha shughuli zao “Alisema
 
Alisema kuwa ukaguzi huo wa mara kwa mara licha ya kusaidia kupunguza  ajali lakini pia utawezesha kuondoa ongozeko la uingizaji wa madawa ya kulevya mkoani Tanga kwa sababu baadhi ya waingizaji wa bidhaa hizo wanatumia bandari bubu zilizopo kufanya biashara hizo.

Hata hivyo aliwataka wananchi waliopo maeneo mbalimbali mkoani hapa
  kutoa ushirikiano kwa maafisa wa Sumatra watakaokuwa wakipita kwenye maeneo yao kwa ajili ya kaguzi hizo zenye lengo la kukabiliana na hali hiyo.

MO DEWJI FOUNDATION YAKABIDHI MILIONI 100 KWA WAFUGAJI WA KUKU, KIJIJI CHA MSOGA, CHALINZE

MO DEWJI FOUNDATION YAKABIDHI MILIONI 100 KWA WAFUGAJI WA KUKU, KIJIJI CHA MSOGA, CHALINZE

February 17, 2016


Mo Dewji Foundation
Afisa Mahusiano wa Mo Dewji Foundation, Zainul Mzige (wa pili kulia) akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 100 kwa Mwenyekiti wa mradi ufugaji kuku wa kienyeji katika kijiji cha Msoga, Michael Mkindo (wa tatu kushoto). Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Mh. Ridhiwani Kikwete (wa pili kushoto), Mkuu wa Wilaya ya ya Bagamoyo, Mh. Majid Mwanga (kushoto) na Diwani wa kata ya Msoga, Hassan Mwinyikondo (kulia).
IMG_2999Afisa Mahusiano wa MO Dewji Foundation, Zainul Mzige akisoma hotuba wakati wa makabidhiano ya mfano wa hundi kwa wafugaji wa kuku wa kienyeji chotara kutoka kijiji cha Msoga, Chalince mkoa wa Pwani. Wa kwanza kushoto ni mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Chalinze, Majid Mwanga, wa kwanza kulia ni Diwani wa Kata ya Msoga, Hassan Mwinyikondo.
Mfuko wa MO Dewji umeupatia mradi wa ufugaji wa kuku wa kienyeji chotara wa kijiji cha Msoga mkoani Pwani shilingi milioni 100 kufanikisha uendeshaji wa mradi huo awamu ya kwanza.
Mradi huo unaokisiwa kuwa na makisio ya uzalishaji ya sh 2,777,901,500 ulibuniwa mwaka 2013 kwa lengo la kukabiliana na umaskini kijijini hapo.
Kwa mujibu wa taarifa za mradi makisio ya mapato kutokana na mauzo ya mayai, vifaranga na kuku baada ya kukoma kutaga zinakadiriwa kuwa sh 4,913,708,000
Aidha mradi huu unasimamiwa na kufadhiliwa na rais Mstaafu Dk Jakaya Mrisho Kikwete.
Akikabidhi hundi hiyo ya sh milioni 100, Afisa Mahusiano wa Mo Dewji Foundation, Zainul Mzige alisema kwamba fedha hizo zitaumika kujenga mabanda 200, ununuzi wa vifaranga, ununuzi wa chakula cha kuku, chanjo na dawa na malipo kwa wataalamu.
IMG_3008
Afisa Mahusiano wa MO Dewji Foundation, Zainul Mzige akisoma hotuba wakati wa makabidhiano ya mfano wa hundi kwa wafugaji wa kuku wa kienyeji chotara kutoka kijiji cha Msoga.
Mambo mengine ni utawala, mawasiliano, ununuzi wa chachu za mpunga na vifaa vya chakula na maji.
Mzige alisema pamoja na kutoa fedha hizo kuunga mkono juhudi za Msoga Poultry Farming Project (MPFP) kuendesha na kuuendeleza mradi kibiashara, aliwataka wahisaniwa kutambua kwamba maendeleo ya mradi wao yatategemea sana namna wanavyokuwa makini kutumia fursa mbalimbali kujiimarisha.
Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita Mo Dewji Foundation imetumia zaidi ya dola za Marekani milioni 3 kwa ajili ya kusaidia miradi mbalimbali ya kijamii nchini.
Aidha hivi karibuni Mfuko wa MO Dewji kwa kushirikiana na kampuni ya Darecha Limited walizindua shindano la Mo Mjasiriamali lenye lengo la kusaidia kukuza ujasirimali miongoni mwa vijana.
Shindano ya Mo Mjasiriamali litatoa fursa ya ukuzaji wa mitaji, ulezi wa wajasiriamali na mitandao ya biashara kuongeza mwanga, ujasiri na kuzalisha wajasiriamali Tanzania.
Ili kufanikisha nia ya kuwa na wajasiriamali wengi, shindano hilo linatarajiwa kuwa daraja kwenda kwa Ofisa Mtendaji, Mohammed Dewji (MeTL Group na mwenyekiti wa Mo DewjiFoundation) ambapo vijana ambao wanaonekana wana kitu cha kufanya, lakini hawana msaada watashiriki kwa lengo la kupata msaada katika mfumo wa mtaji, mtandao na usimamizi wa ukuaji wa shughuli wanayofanya au kutaka kuifanya ili kuianzisha na kuikuza.
Kwa niaba ya wananchi wa Msoga, mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete alimshukuru Mwenyekiti wa Taasisi ya Mo Dewji, Mohammed Dewji kw ufadhili ambao ameufanya kwa wananchi wa kijiji cha Msogo na kumtaka kuwa na moyo wa kutoa zaidi ili azidi kusaidia wananchi walio na mahitaji.
Mo Dewji Foundation
Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete akitoa neno la shukrani kwa MO Dewji Foundation mara baada ya kukabidhiwa mfano wa hundi ya shilingi 100 kwa ajili ya ufugaji wa kuku wa kienyeji Chotara.
Alisema kuwa kupitia mradi huo wa ufugaji wa kuku wa kienyeji chotara, wananchi wa kijiji cha Msoga wataweza kujikwamua na janga la umasikini na wataendelea kuwa wakiandika maombi ya miradi mbalimbali ambayo wanataka kuifanya ili kuzidi kutengeza ajira zaidi kwa wananchi wa Mzoga.
“Tunamshukuru Mohammed Dewji kwa msaada huu tunaimani utasaidia wananchi wa Mzoga na namuomba asisite kutupokea muda mwingine tunapokuwa na miradi mingine,” alisema Kikwete.
Nae Mratibu wa Mradi wa ufugaji wa kuku wa kienyeji chotara (Msoga Poultry Farming Project), Novatus Kailembo alisema wazo la kuanzisha mradi huo lilitolewa na Rais wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Kikwete mwaka 2013 ili kusaidia kuboresha maisha ya wananchi wa Msoga kama kiuchumi, kielimu na kiafya.
Alisema wanataraji kuanza na wanakijiji 300 ukiwa ni mradi wa mfano, awamu ya kwanza ambao wanataraji kuanza kufanyika katika vitongoji tisa ambavyo ni Hospital, Takalagame, Kota, Mnazi Mmoja, Tumbi Juu, Tumbi Chini, Kingugi, Mkundi na Mokela.
Mo Dewji Foundation
Mkuu wa Wilaya ya Chalinze, Majid Mwanga akimshukuru Mwenyekiti wa MO Dewji Foundation, Mohammed Dewji kwa ufadhili ambao ameutoa kwa wilaya yake kwa ajili ya ufugaji wa kuku wa kienyeji chotara ambapo ufugaji huo unataraji kufanyika katika kijiji cha Msoga.
REGIONAL WORKSHOP ON MAKING AN IMPACT WITH HUMAN DEVELOPMENT REPORTING STARTS

REGIONAL WORKSHOP ON MAKING AN IMPACT WITH HUMAN DEVELOPMENT REPORTING STARTS

February 17, 2016
Tanzania human development report 2014/2017

The host of the workshop, Executive Director of ESRF, Dr. Tausi Kida, presents a paper; The Tanzania human development report experience. The session highlighted the Tanzania report experience in producing the Tanzania human development report 2014/2017.

Tanzania human development report 2014/2017

UN Resident Coordinator and UNDP Resident Representative in Tanzania, Mr.Alvaro Rodriguez, delivers his speech when opening a four-day regional workshop on making an impact with human development reporting at Ramada Resort in Dar es Salaam, February 16, 2016.

regional workshop on making an impact with human development reporting at Ramada Resort in Dar es Salaam, February 16, 2016

Executive Director of Economic and Social Research Foundation, ESRF, Dr.Tausi Kida congratulates the UN Resident Coordinator and UNDP Resident Representative in Tanzania, Mr.Alvaro Rodriguez, after he had delivered his opening remarks.

National Human Development Reporting A Regional Workshop 2016

Rodgers Dhliwayo, Economics Adviser/Senior Economist UNDP Tanzania Country Office, presents a paper; Influence of the National Human Development Reports (NHDRs)-Why Produce NHDRs?, during the morning session of four-day regional workshop on making an impact with human development reporting at Ramada Resort in Dar es Salaam, February 16, 2016.

National Human Development Reporting A Regional Workshop 2016

Head of the United Nations Development Programme (Human Development Reports Unit), in New York, Mr. John Hall, presents a paper; The Human Development Approach: An overview of the human development approach, 1990 onwards.

human development reporting regional workshop on making an impact with human development reporting at Ramada Resort in Dar es Salaam, February 16, 2016

Ice breaker exercise, delegates knowing each other before the start of the crucial session.

human development reporting

Delegate from UNDP-Mozambique, Manuel Filipe, makes his contribution following papers presentation.

regional workshop on making an impact with human development reporting at Ramada Resort in Dar es Salaam, February 16, 2016

A cross section of participants attend the morning session.

regional workshop on making an impact with human development reporting at Ramada Resort in Dar es Salaam, February 16, 2016

UN Resident Coordinator and UNDP Resident Representative in Tanzania, Mr.Alvaro Rodriguez, (R), exchanges ideas with the, Head of the United Nations Development Programme (Human Development Reports Unit), in New York, Mr. John Hall, during the opening day of four-day regional workshop on making an impact with human development reporting at Ramada Resort in Dar es Salaam Tuesday February 16, 2016.

regional workshop on making an impact with human development reporting at Ramada Resort in Dar es Salaam, February 16, 2016

Mr.Alvaro Rodriguez (seated-R), ESRF Chief, Dr.Tausi Kida, (seated centre), and Rodgers Dhliwayo, in a group photo with some delegates.

regional workshop on making an impact with human development reporting at Ramada Resort in Dar es Salaam, February 16, 2016

UN Resident Coordinator and UNDP Resident Representative in Tanzania, Mr.Alvaro Rodriguez, (L), is being escorted by ESRF Executive Director, Dr. Tausi Kida, as he leaves the workshop venue.

 

KATIBU WA CWT MANISPAA YA IRINGA AMETANGAZA MGOGORO NA MKURUNGEZI WA MANISPAA YA IRINGA

February 17, 2016

 katibu wa cha walimu manispaa ya iringa mwalimu Fortunate Njalali akiwa ofisini kwake

DAWASCO KUZIMA MTAMBO WA MAJI WA RUVU CHINI

February 17, 2016
TAARIFA KWA UMMA
KUZIMWA KWA MTAMBO WA MAJI WA RUVU CHINI
SHIRIKA LA MAJI SAFI NA MAJITAKA DAR-ES-SALAAM (DAWASCO),  LINAWATANGAZIA  WAKAZI WA JIJI LA DAR-ES-SALAAM NA MJI WA BAGAMOYO MKOANI PWANI  KUWA, MTAMBO WA KUZALISHA MAJI WA RUVU CHINI UTAZIMWA  KWA SAA 36 KWA SIKU YA ALHAMIS TAREHE 18.02.2016.

KUZIMWA KWA MTAMBO HUO KUMETOKANA NA MATENGENEZO KATIKA BOMBA KUU LENYE UKUBWA WA INCHI 54 LINALOSAFIRI MAJI KUTOKA BAGAMOYO MPAKA KWENYE MATENKI YA MAJI YALIYOPO CHUO KIKUU ARDHI . 

MATENGENEZO HAYO YATAFANYIKA ENEO LA LUGALO JESHINI NA KUANZIA SAA 12 ASUBUHI YA TAREHE 18/02/2016

 KWASABABU HIYO MAENEO YAFUATAYO YATAKOSA MAJI:

MJI WA BAGAMOYO, VIJIJI VYA MAPINGA, KEREGE NA MAPUNGA. BUNJU, BOKO, TEGETA, KUNDUCHI, SALASALA, JANGWANI, MBEZI BEACH NA KAWE.

MAENEO MENGINE NI MLALAKUWA, MWENGE, MIKOCHENI, MSASANI, SINZA, MANZESE, MABIBO, KIJITONYAMA, KINONDONI, OYSTERBAY, MAGOMENI, UPANGA, KARIAKOO, CITY CENTRE, ILALA, UBUNGO MAZIWA, KIGOGO, MBURAHATI, HOSPITALI YA RUFAA MUHIMBILI, BUGURUNI, CHANGOMBE NA KEKO.      

WASILIANA NASI KUPITIA KITUO CHA HUDUMA KWA WATEJA NAMBA 022-2194800 AU 0800110064

DAWASCO INAWAOMBA RADHI KWA USUMBUFU UTAKAOJITOKEZA

IMETOLEWA NA OFISI YA UHUSIANO
DAWASCO-MAKAO MAKUU
“DAWASCO TUTAKUFIKIA”.

MWENYEKITI WA BODABODA MKOANI MWANZA ATOA TAHADHARI JUU YA VITENDO VYA UKWAPUAJI JIJINI MWANZA.

February 17, 2016
Mwenyekiti wa Chama cha Waendesha Pikipiki Mkoani Mwanza Makoye Kayanda (pichani), amewataharisha wakazi wa Jiji la Mwanza kuwa makini wawapo barabarani, ili kuepukana na vitendo vya ukwapuaji wa Mikoba na Mabegi vinavyofanywa na baadhi ya wahalifu kwa kutumia pikipiki.

Kayanda alitoa tahadhari hiyo jana Jijini Mwanza baada ya kupokea malalamiko ya kukithiri kwa vitendo vya ukwapuaji vinavyofanywa na baadhi ya watu wanaojifanya waendesha pikipiki, jambo linalochafua taswira ya waendesha pikipiki Mkoani Mwanza.

Tayari watu kadha wamefikisha malalamiko yao kwa uongozi wa bodaboda Mkoani Mwanza, baada ya kukumbwa na kadhia ya kukwapuliwa mikoba pamoja na mabegi yao, ambapo mmoja wa wahanga wa matukio hayo Diana Abdallah ameeleza kukwapuliwa mkoba wake uliokuwa na pesa pamoja na vito vya thamani wakati akitokwa kwenye shughuli zake.

"Nilikuwa maeneo ya Nyegezi ambapo nilikuwa nikitoka kwenye shughuli zangu, nilikwapuliwa mkoba wangu ambao ulikuwa na pesa shilingi Laki Nane, Simu ya shilingi Laki mbili na nusu, Pete sita za Silver zenye thamani ya shili laki moja na elfu ishiri na sita pamoja na miwani ya macho ya shilingi Laki nne. Watuhumiwa waliweza kukamatwa na kesi iko polisi katika kituo cha Igogo".Alisema Abdallah

Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari wanaopiga Vita matumizi ya dawa za kulevya na uhalifu nchini Edwin Soko, analaani Vitendo hivyo vya ukwapuaji wa Mikoba na Mabegi ya watu kwa kutumia bodaboda ambavyo vimekuwa vikiwakumba watembea kwa miguu Jijini Mwanza, ambapo ameomba jeshi la polisi kutoa ushirikiano wake kwa ajili ya kuvikomesha.
Imeandaliwa na George Binagi-GB Pazzo @BMG.

WANACHACHAMA WA CCM MKOANI MWANZA WAONYA VITEGA UCHUMI VYA CHAMA KUTUMIKA VIBAYA.

February 17, 2016
Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM, Kata ya Kirumba Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza, wameonya juu ya baadhi ya Wawekezaji nchini wanaotumia Vitega uchumi vya chama hicho bila kufuata mikataba wanayopewa.

Wanachama hao walitoa kauli hiyo wiki hii baada ya Wawekezaji wanaotumia majengo ya CCM Kata ya Kirumba, kudaiwa kukiuka masharti yao na hivyo kutumia majengo hayo bila kuyalipia kodi ya pango kwa muda mrefu.

Ni kutokana na hatua hiyo, Wanachama hao walichukua maamuzi ya kufunga Majengo hayo ambayo yanatumiwa na Tasisi ya Mikopo ya Wadoki pamoja na Hotel ya Kirumba Resort, huku taratibu nyingine za kisheria zikiendelea, lengo likiwa ni kuhakikisha kwamba watumiaji wa majengo hayo wanayalipia kodivwanayodaiwa vinginevyo watafurushwa nje ya majengo hayo.

Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kirumba Abubakary Francis Kweyamba alithibitisha kwamba wanachama hao wamefikia maamuzi hayo, kutokana na kutumia majengo ya chama katika kata hiyo huku wakiwa hawayalipii kodi na hivyo kukisababishia chama usumbufu mkubwa wa kuendesha shughuli zake za kiofisi huku akisisitiza msimamo wa kuendelea kuyafunga majengo hayo.

Katibu Mwenezi wa CCM Kata ya Kirumba Juma Wesa pamoja na Katibu wa Chama hicho Wilaya ya Ilemela Acheni Maulidi, walisema kuwa maamuzi yaliyochukuliwa na wanachama hayo ni sahihi kwa kuwa malalamiko ya wawekezaji hao yaliishajadiliwa hadi ngazi ya Mkoa ya Chama hicho na kuonekana kwamba wawekezaji hao hawatii makubaliano yaliyofikiwa.

Suala hilo lilifikishwa katika Kituo cha Polisi Kirumba na kila upande umetakiwa kuwasilisha vielelezo vyake ili kutambua wanaokiuka makubaliano ya mkataba wa upangaji kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

Meneja wa Kirumba Resort hakutaka kuzungumzia malalamiko hayo kwa madai kwamba mzungumzaji ni Mkurugenzi wake ambae alisema amesafiri huku Uongozi wa Wadoki Saccos ukishindwa kupatikana.
Imeandaliwa na George Binagi-GB Pazzo @BMG.