Wanachama na wafuasi wa Chadema
wakiandamana katika mitaa mbalimbali ya kigoma ili kupinga ziara ya
Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Slaa mkoani humo pamoja na kupinga maamuzi
yanayofanywa na Kamati kuu ya Chadema. Maandamano hayo yanaendelea hivi
sasa
KENYA YATINGA NUSU FAINALI KWA KUIFUNGA RWANDA 1-0, SASA KUCHEZA NA KILI STARS
Na Mahmoud Zubeiry, Mombasa
TANZANIA
Bara, Kilimanjaro Stars itamenyana na wenyeji, Kenya, Harambee Stars
katika Nusu Fainali ya Kwanza ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na
Kati, CECAFA Challenge Desemba 10, mwaka huu Uwanja wa Nyayo, Nairobi,
Kenya.
Hiyo inafuatia Kenya kuifunga Rwanda 1-0 katika Robo Fainali ya pili CECAFA Challenge jioni hii Uwanja wa Manispaa, Mombasa Kenya, bao pekee la beki wa Azam FC ya Dar es Salaam, Joackins Atudo kwa penalti dakika ya 56.
Mapema katika Robo Fainali ya kwanza, Stars iliwatoa mabingwa watetezi, Uganda kwa penalti 3-2 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90.
Robo Fainali nyingine zitachezwa kesho, Ethiopia na Sudan na Zambia na Burundi, Uwanja wa Manispaa pia.
Mshambuliaji wa Kenya, Haambee Stars, Jacob Keli akiwatoka mabeki wa Rwanda, AmavubiBayisenge Emery kulia na Tubane James kushoto Uwanja wa Manispaa, Mombasa leo. |
Hiyo inafuatia Kenya kuifunga Rwanda 1-0 katika Robo Fainali ya pili CECAFA Challenge jioni hii Uwanja wa Manispaa, Mombasa Kenya, bao pekee la beki wa Azam FC ya Dar es Salaam, Joackins Atudo kwa penalti dakika ya 56.
Mapema katika Robo Fainali ya kwanza, Stars iliwatoa mabingwa watetezi, Uganda kwa penalti 3-2 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90.
Robo Fainali nyingine zitachezwa kesho, Ethiopia na Sudan na Zambia na Burundi, Uwanja wa Manispaa pia.
MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI MAHAFALI YA KWANZA YA CHUO KIKUU BAGAMOYO
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, akikata keki ya mahafali ya kwanza ya chuo kikuu cha Bagamoyo
yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es salaam
leo Disemba 7-2013, kulia Mkuu wa Chuo hicho Petired Bishop Elinasa
Sendoro, kushoto Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Costa Ricky Mahalu.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, akihutubia kwenye mahafali ya kwanza ya chuo kikuu cha Bagamoyo
yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es salaam
leo Disemba 7-2013.
UVCCM TANGA KUANZA ZIARA KESHO MKOANI TANGA.
IMEWEKWA JUMAMOSI:DESEMBA 7 SAA 6:45 JIONI.
JUMUIYA wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Tanga(UVCCM) inatarajia kuanza ziara yake kesho kwa mkoa mzima wa Tanga kukutana na viongozi wa umoja huo ngazi za wilaya pamoja na kufanya mikutano ya hadhara.
Akizungumza leo na Blog hii,Mwenyekiti wa Umoja huo,Abdi Makange amesema ziara hiyo itakuwa na
lengo la kukutana na mabaraza ya umoja wa vijana kila wilaya ili kuwekeana mikakati mbalimbali ya kuufanya
umoja huo uzidi kuwa imara pamoja na kuwashukuru wajumbe wa umoja huo.
Amesema suala lengine watakalolifanya katika ziara
hiyo ni kuangalia uhai wa jumuiya hiyo kwenye wilaya hizo utakaoendena sambamba
na ufunguzi wa matawi ya umoja huo lengo likiwa ni kuuimarisha
Makange amesema ziara hiyo
kwa kila wilaya zitakuwa zikihitimishwa na ufanyikaji wa mikutano ya hadhara
ambapo wananchi wa wilaya husika watapata nafasi ya kupata sera makini za umoja
huo ambazo zitakuwa zikitolewa na viongozi wake.
Subscribe to:
Posts (Atom)