February 07, 2014

KAMISHNA WA SENSA ATOA SOMO KWA WADADISI NA WAHARIRI WA MADODOSO YA UTAFITI WATU WENYE UWEZO WA KUFANYA KAZI 2014

Wadadisi na Wahariri wa madodoso ya watu wenye uwezo wa kufanya Kazi kutoka mikoa ya Dar es salaam, Pwani, Morogoro, Lindi na Mtwara wakiwa  kwenye mafunzo ya siku  mjini Morogoro.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Na. Veronica Kazimoto na Aron Msigwa – Morogoro.

Wadadisi na Wahariri wa madodoso ya Utafiti wa Watu Wenye Uwezo wa Kufanya Kazi  mwaka 2014 wametakiwa kuzingatia maadili na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao ili kuepuka kuliletea taifa hasara  kwa kutoa takwimu zisizosahihi.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Morogoro na Kamishna wa Sensa ya Watu na   Makazi Bi. Hajjat Amina Mrisho Said wakati akizungumza  na Wadadisi na Wahariri wa madodoso yaUtafiti wa Watu wenye uwezo wa kufanya kazi kutoka mikoa ya Dar es salaam, Pwani, Morogoro, Lindi na Mtwara walio katika mafunzo ya siku 16 mjini Morogoro.
February 07, 2014

MKUTANO MKUU WA TASWA WASOGEZWA MBELE, SASA KUFANYIKA MACHI 2 MWAKA HUU

UCHAGUZI Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), uliokuwa umepangwa kufanyika Februari 16 umesogezwa mbele kwa wiki mbili na sasa utafanyika Machi 2, mwaka huu jijini Dar es Salaam.
 
Uamuzi wa kusogeza mbele tarehe ya kufanyika uchaguzi huo imechukuliwa na Sekretarieti ya TASWA kutokana na sababu mbalimbali, lakini kubwa ni kutoa nafasi kwa wanachama wengi zaidi kulipia ada zao kwa ajili ya kushiriki mkutano huo wa uchaguzi.
 
Hadi kufikia leo mchana idadi ya wanachama waliokuwa wamelipia ada ni 57 kati ya wanachama karibu 150 waliopo katika leja na kati ya waliolipa ni wanne tu ndiyo wamelipia ada ya miaka mitatu kama walivyotakiwa wakati waliobaki wamelipia mwaka mmoja.
February 07, 2014

KAMATI YA ARDHI, MALIASILI NA MAZINGIRA YATEMBELEA HIFADHI YA TARANGIRE

Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya ardhi, maliasili na mazingira wakijiandaa kwa safari ya kuelekea katika hifadhi ya Tarangire, iliyoko wilayani Babati, mkoa wa Manyara

Mbunge wa Luchoto, Dkt. Henry Daffa Shekifu (katikati) akisalimiana na askari muda mfupi kabla ya kuanza safari ya kuelekea Hifadhi ya Tarangire, kushoto kwake ni Mkurugenzi mkuu wa TANAPA, Allan Kijazi
February 07, 2014

KIKAO MAALUMU CHA BARAZA LA VYAMA VYA SIASA VYENYE USAJILI CHAFANYIKA DAR JANA


 Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam akisoma dua kabla ya kikao hicho cha Baraza la Vyama Vya Siasa vyenye usajili kuanza katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaa
 Sehemu ya viongozi wa vyama vya siasa wakiomba dua katika kikao hicho cha Baraza la Vyama Vya Siasa vyenye usajili kabla ya kuanza katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam
  Sehemu ya viongozi wa vyama vya siasa katika kikao hicho cha Baraza la Vyama Vya Siasa vyenye usajili  katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam
   Sehemu ya viongozi wa vyama vya siasa katika kikao hicho cha Baraza la Vyama Vya Siasa vyenye usajili kuanza katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam
   Sehemu ya viongozi wa vyama vya siasa katika kikao hicho cha Baraza la Vyama Vya Siasa vyenye usajili katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam
   Mwenyekiti wa Baraza la Vyama Vya siasa ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama cha APPT-Maendeleo, Mhe Peter Mziray akisoma hotuba yake katika  kikao hicho cha Baraza la Vyama Vya Siasa vyenye usajili  katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea risala toka kwa Mwenyekiti wa Barza la Vyama vya Siasa Mhe. Peter Mziray

RC GALLAWA AWAFARIJI WANANCHI WALIEZULIWA NYUMBA ZAO KOROGWE NA MUHEZA

February 07, 2014
Picha namba 9274 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa
kushoto akitoa maelekezo kwa Mwenyekiti wa Kijiji Lusanga kata ya Mnyuzi wilayani Korogwe Thabiti Selemani mwenye kofia jinsi ya kuutumia msaada huo wa unga kwa wananchi walioathirika.
Afisa Rasilimali wa Kiwanda cha Unga jijini Tanga cha Pembe, Salele Masoudy kushoto akimkabidhi Msaada wa Unga kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Lusanga kata ya Mnyunzi,Thabiti Selemani katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa kushoto na Mkuu wa wilaya ya Korogwe Mrisho Gambo wakishuhudia makabidhiano hayo
MKUU wa Mkoa wa Taga,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa akisisitiza jambo kwa wananchi wa Kijiji cha Lusanga kata ya Mnyuzi wilayani Korogwe  kilichokumbwa na maafa ya wananchi wake kuezuliwa mabati kwenye nyumba za kaya 83 wilayani humo uliotokana na upepo mkali ulioaambatana na mvua juzi ukushoto ni Afisa Rasilimali wa Kiwanda cha Unga cha Pembe jijini TangaSalele Masoudy  na kulia ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe Mrisho Gambo