BODI ya Ligi imesema kuwa ipo mbioni kukamilisha mchakato wa kuzipatia ufadhili klabu zinazoshiriki michuano ya ligi daraja la kwanza hapa nchini ili kuweza kuyafanya mashindano hayo kuwa na msisimuko ikiwemo ushindani kama ilivyokuwa kwenye ligi kuu.
Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi, Hamadi Yahaya wakati akizungumza na MTANDAO HUU ambapo alisema kuwa hivi sasa wapo kwenye mazungumzo na Kampuni ya Azam Media ambapo kwa asilimia kubwa mafanikio yanaweza kupatikana kutokana na hatua nzuri walioifikia.
Yahaya alisema kuwa mwaka uliopita walichagua kampuni kwa ajili ya kutafuta ufadhili lakini ilishindwa kuifanya kazi hivyo lakini wanaona kuangalia namna ya kufanya ili kufanikisha jambo hilo kwa kampuni ya Azam Media.
Kauli ya Mwenyekiti huyo inatokana na baadhi ya maombi yaliyotolewa na vilabu vinavyoshiriki michuano kuitaka bodi hiyo kuhakikisha wanavitafutia ufadhili ili kuweza kuondokana na utegemezi ambao wakati mwengine unachangia kuwepo kwa maandalizi hafifi jambo ambalo linapelekea kuikosesha ladha michuano hiyo.
Hata hivyo vilabu hivyo vilitaka pia mechi zao kuchezwa mwishoni mwa wiki badala ya katikati ya wiki kama ilivyokuwa hivi sasa ili kuweza kuzipa fursa kufanya matayarisho ya kutosha kama ilivyokuwa vilabu vya ligi kuu hapa nchini.
Akitolea ufafanuzi suala hilo, Mwenyekiti huyo alisema kuwa ligi hiyo inachezwa katikati ya wiki kutokana na wingi wa mechi hivyo
zisipochezwa kwa staili hiyo itachukua muda mrefu kumalizika kwa
michuano hiyo .
Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi, Hamadi Yahaya wakati akizungumza na MTANDAO HUU ambapo alisema kuwa hivi sasa wapo kwenye mazungumzo na Kampuni ya Azam Media ambapo kwa asilimia kubwa mafanikio yanaweza kupatikana kutokana na hatua nzuri walioifikia.
Yahaya alisema kuwa mwaka uliopita walichagua kampuni kwa ajili ya kutafuta ufadhili lakini ilishindwa kuifanya kazi hivyo lakini wanaona kuangalia namna ya kufanya ili kufanikisha jambo hilo kwa kampuni ya Azam Media.
Kauli ya Mwenyekiti huyo inatokana na baadhi ya maombi yaliyotolewa na vilabu vinavyoshiriki michuano kuitaka bodi hiyo kuhakikisha wanavitafutia ufadhili ili kuweza kuondokana na utegemezi ambao wakati mwengine unachangia kuwepo kwa maandalizi hafifi jambo ambalo linapelekea kuikosesha ladha michuano hiyo.
Hata hivyo vilabu hivyo vilitaka pia mechi zao kuchezwa mwishoni mwa wiki badala ya katikati ya wiki kama ilivyokuwa hivi sasa ili kuweza kuzipa fursa kufanya matayarisho ya kutosha kama ilivyokuwa vilabu vya ligi kuu hapa nchini.
Akitolea ufafanuzi suala hilo, Mwenyekiti huyo alisema kuwa ligi hiyo inachezwa katikati ya wiki kutokana na wingi wa mechi hivyo
zisipochezwa kwa staili hiyo itachukua muda mrefu kumalizika kwa
michuano hiyo .