NORWAY YAIHAKIKISHIA TANZANIA USHIRIKIANO KATIKA SEKTA YA KILIMO

March 23, 2023

 Serikali ya Norway imeihakikishia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ushirikiano katika sekta za kilimo, usalama wa chakula, nishati, biashara na uwekezaji pamoja na mabadiliko ya tabianchi.

Ahadi hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Norway anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa Mhe. Bjørg Sandkjær alipokutana kwa mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Balozi Mbarouk alisema kuwa Norway imekuwa mdau mkubwa wa Tanzania katika sekta ya afya na imekuwa ikisaidia katika masuala mbalimbali katika sekta hiyo.

“Katika hii ziara Mhe. Naibu Waziri anatagemea kufanya ziara ya kutembelea hospitali ya Kiluteri ya Hydom ambayo imekuwa ikifadhiliwa na Serikali ya Norway……… madhumuni ya zaira hiyo ni kuangalia ni kwa namna gani Norway inaweza kuongeza ushirikiano na kuisaidia hospitali hiyo,” alisema Balozi Mbarouk.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Norway anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa Mhe. Bjørg Sandkjær amesema kuwa ameitembela Tanzania kutokana na ushirikiano imara uliopo baina yake na Serikali ya Norway uliodumu kwa muda mrefu na ulianza kama ushirikiano wa maendeleo.

“Lengo la ziara yangu hapa Tanzania ni kuangalia ushirikiano katika sekta ya afya kwa sababu Norway imekuwa ikifadhili sekta, Mashirika ya Umoja wa Mataifa, mifuko ya kimataifa, wadau wengine wanaohusika katika sekta ya afya pamoja na asasi za kiraia zinazofanya kazi na Serikali ya Tanzania katika kuboresha huduma za afya,” alisema Mhe. Sandkjær.

Hivyo nitaitembelea Hospitali ya Kilutheri ya Haydom ili kujionea shughuli zinavyofanyika na kuangalia zaidi maeneo ya ushirikiano katika sekta hiyo.

Tanzania na Norway zimekuwa zikishirikiana katika sekta za afya, elimu, uvuvi, nishati jadidifu, kilimo, ushafirishaji na utalii pamoja na masuala ya bahari.










WAANDISHI WA HABARI CHUO KIKUU HURIA TZ WAPEWA MAFUNZO, WAASWA KUWA NA JICHO LA KIJINSIA

March 23, 2023

 

MTANDAO wa jinsia Tanzania (TGNP) wakishirikiana na Internews kupitia Mradi wa Boresha Habari watoa mafunzo kwa Wanachuo wanaosoma Masomo ya Uandishi wa habari katika Chuo Kikuu Cha Huria Tanzania ili waweze kuwa na jicho la kijinsia kwenye habari.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Machi 23, 2023 na waandishi wa habari, Mwezeshaji kutoka Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP), Deogratius Temba amesema kuwa lengo la ni kuwaweka waandishi wa habari sehemu nzuri mapema kabla hawajawa na msongamano wa majukumu pale watapomaliza chuo.

“Tunataka waandishi waweze kuzingatia usawa wa kijinsia katika Uandishi wa habari mbalimbali katika jamii.”

Amesema zipo habari nyingi kwenye jamii ambazo hazijaandikwa kuhusiana na wanawake pamoja na makundi ya watu wenye ulemavu ambazo zinaonekana hazina maana katika uuzaji kwenye vyombo vyao vya habari.

“Habari hizo ndizo tunazojaribu kuwaeleza waandishi wa habari vijana ili wajue ni namna gani wanazipa kipaumbele wanapokuwa wanafanya kazi zao.” Ameeleza Temba

Amesema kuwa ili kuleta maendeleo lazima habari ziwe zuri na ziweze kuandikwa kwa kukwepa uzalilishaji wowote wa jinsi ya ME au KE ili kuleta maendeleo katika shughuli zozote za maendeleo.

Amesema kuwa habari inayozingatia sauti za jinsi zote mbili ya wanawake na wanaume .

Kwa upande wa Mratibu wa mafunzo wa Mradi wa Boresha Habari kutoka 'Internews', Mariam Oushoudada amesema mafunzo hayo yataenda kusaidia wanafunzi katika kuhakikisha kunakuwa na uwiano wa uongozi katika tasnia ya habari.

"Mafunzo haya tumeona tuyatoe kwa wanachuo wakiwa chuoni yaani mwanzoni kabisa ili wawe na uelewa wa masuala ya jinsia pale wanapo andika habari katika vyombo vyao vya habari pale watapomaliza masomo." Amesema Mariam.

Amevitaj vyuo ambavyo vitanufaika na mafunzo hayo kuwa ni Chuo Kikuu cha Tumaini, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ,Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino(SAUT) na Practical School of Journalism.

Amesema Mradi huo utatanua uelewa wa jamii kuhusiana na usawa wa kijinsia pamoja na kutoa uelewa kwa waandishi wa habari chipukizi ili waweze kuandika na kuzipa kipaumbele habari za jinsia.

Amesema mafunzo hayo yatakuwa endelevu pia kutakuwa na atamizi kwaajili ya kuendelea kuwa nao pamoja ili waweze kuandika habari ambazo zitakuwa na usawa wa kijinsia bila kukandamiza jinsi yeyote katika jamii.

Kwa upande wa Mwezeshaji kutoka TGNP Ester Wilium amesema mafunzo hayo yanawajengea uelewa waandishi wa habari chipukizi kuweza kuandika habari ambazo hazipendelei na zinaangalia jinsi zote ‘Mwanamke na mwanaume’ ili uandishi wa habari wa sasahivi uwe tofauti na uandishi wa zamani.

Kwa upande wa mnufaika wa mafunzo hayo, kutoka Chuo Kikuu Huria Tanzania, Aniva Mwongola amesema kuwa mafunzo hayo atayafanyia kazi kwa vitendo kwani kumekuwa na changamoto ya waandishi kuandika habari ambazo hazina sauti za jinsia zote.

“Mafunzo haya yamenijengea uelewa wa masuala mapana na namna ambavyo nitaweza kuisaidia jamii kuelewa uhalisia wa jinsia hasa ukiangalia masuala ya kutambua haki ya kila mwanadamu na kupata fursa mbalimbali.” Amesema Aniva

Akizungumzia fursa hizo amesema kila mwanadamu anatakiwa kupata fursa za kiuchumi, Uongozi na fursa za elimu, amesema ingawa serikali imewezesha jamii kupata fursa mbalimbali lakini kama mwandishi wa habari anafursa ya kufanya kwa nafasi yake ili kuwe na usawa katika jamii kwa ujumla.
Mwezeshaji kutoka Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP), Deogratius Temba akizungumza na wanachuo Kikuu Huria cha Tanzania wakati wa kutoa mafunzo ya usawa wa kijinsia wakati wa kuripoti habari. Mafunzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam leo Machi 23, 2023.
Mratibu wa mafunzo wa Mradi wa Boresha Habari kutoka 'Internews', Mariam Oushoudada akizungumza na wanachuo Kikuu Huria cha Tanzania wakati wa kutoa mafunzo ya usawa wa kijinsia wakati wa kuripoti habari. Mafunzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam leo Machi 23, 2023.
upande wa Mwezeshaji kutoka TGNP Ester Wilium akizungumza na wanachuo Kikuu Huria cha Tanzania wakati wa kutoa mafunzo ya usawa wa kijinsia wakati wa kuripoti habari. Mafunzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam leo Machi 23, 2023.
Baadhi ya wanachuo Kikuu Huria cha Tanzania wakiuliza maswali wakati wa mafunzo ya uandishi wa habari za jinsia kutoka Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP) wakishirikiana na Internews kupitia Mradi wa Boresha habari. Mafunzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam leo Machi 23, 2023.




Baadhi ya wanachuo Kikuu Huria cha Tanzania wakipata mafunzo ya uandishi wa habari za jinsia kutoka Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP) wakishirikiana na Internews kupitia Mradi wa Boresha habari. Mafunzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam leo Machi 23, 2023.


WAZIRI MKUU KIKAO CHA KIKUNDI KAZI CHA KITAIFA CHA MAWAZIRI CHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

WAZIRI MKUU KIKAO CHA KIKUNDI KAZI CHA KITAIFA CHA MAWAZIRI CHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

March 23, 2023

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiongoza Kikao cha Kikundi Kazi cha Kitaifa cha Mawaziri cha Nishati safi ya Kupikia, kilichofanyika katika ukumbi wa Hazina jijini Dodoma, Machi 23, 2023. Kushoto ni Waziri wa Nishati Januari Makamba na kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) George Simbachawene. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

HOSPITALI YA RUFAA YA BOMBO KUANZISHA KLINIKI ZA KIBINGWA ZA JIONI

March 23, 2023



Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhan

Na Oscar Assenga, TANGA.

HOSPITALI ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo inatajia kuanzisha huduma za Kliniki za Kibingwa wakati wa muda wa ziada wa jioni itakayoanza kuanzia Aprili 9 mwaka huu katika hospitali hiyo.

Akizungumza leo Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhan amesema huduma hizo zitaaza saa tisa na nusu jioni mpaka muda ambao wagonjwa watamalizika ambao watapata fursa ya kuonana na madaktari bingwa waliopo kwenye hospitali hiyo.

Dkt Juma alisema kwamba katika kliniki hiyo huduma mbalimbali za kibingwa ikiwemo magonjwa ya ndani,magonjwa ya ya upasuaji,magonjwa ya wakina mama,magonjwa ya watoto,magonjwa wa koo,pua pamoja na sikio .

Aidha alisema kwamba huduma hizo zitatolewa kwa wagonjwa wote wenye bima bila kujalia aina gani ya bima lakini pia wale wagonjwa wanaofanya malipo ya keshi yatapokelewa.

Hata hivyo alisema huduma hiyo itatolewa siku Jumatatu mpaka Ijumaa kuanzia saa tisa na nusu mpaka pale watakapomalizika.

Dkt Juma aliwahimiza wananchi wa mkoa wa Tanga kujitokeza kwa wingi kuhudhuria kliniki hizo ili kuweza kukutana na madaktari bingwa wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga

Hata alisema uwepo wa kliniki hiyo utasaidia kutoa fursa kwa wagonjwa kuweza kukutana na madaktari bingwa ambao wataweza kuwasaidia hivyo watumie nafasi hiyo kuweza kuonana na madaktari hao bingwa waliopo kwenye hospitali hiyo.