Serikali ya Tanzania na Mauritius kuendeleza ushirikiano katika Sekta ya Sanaa na na Utamaduni.

December 06, 2016
 Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa,na Michezo Mhe. Anastazia Wambura(wa pili kulia) akizungumza na Ujumbe  wa Serikali ya Mauritius pamoja na  baadhi ya viongozi wa Wizara  leo Jijini Dar es Salaam  alipokutana na Waziri wa Sanaa na Utamaduni Mhe. Santaram Baboo (wa kwanza kulia) kuhusu ushirikiano baina ya nchi hizo mbili katika sekta ya Sanaa na Utamaduni.Wa tatu kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel.
 Viongozi wa Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo  wakiwa katika mazungumzo na Uongozi wa Mauritius kuhusu kuimarisha sekta ya Sanaa na Utamaduni leo Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Sanaa na Utamaduni wa Mauritius Mhe.Santaram Baboo (wa kwanza Kulia) akizumgumza na baadhi ya viongozi wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo wakati wa majidiliano ya  kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili  katika Sekta ya Sanaa na Utamaduni yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Anastazia Wambura.
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel(aliyesimama) akiongea jambo wakati wa mazungumzo  kati ya Wizara yake na Serikali ya Mauritius katika  Sekta ya Sanaa na Utamaduni.
 Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa,na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akipokea zawadi kutoka kwa Waziri wa Sanaa na Utamaduni wa Mauritius Mhe.Santaram Baboo baada ya mazungumzo baina yao kuhusu ushirikiano katika Sekta ya Sanaa na Utamaduni yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa,na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Wizara yake na viongozi wa Serikali ya Mauritius baada ya mazungumzo kuhusu ushirikiano katika Sekta ya Sanaa na Utamaduni yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

MATUKIO YA UHAKIKI WA WASTAAFU WANAOLIPWA NA HAZINA MKOANI ARUSHA

December 06, 2016


Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Msaidizi Bw. Stanslaus Mpembe (kushoto)  akitoa ufafanuzi kwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango namna zoezi zima la uhakiki wa wastaafu kanda ya kaskazini linavyokwenda kabla ya uzinduzi wa zoezi hilo. Zoezi hili ni kwa mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga. 
Zoezi la kuhakiki wastaafu likiendelea katika Ofisi za Makao Makuu, Halmashauri ya jiji la Arusha, Pichani ni baadhi ya wastaafu wakifanyiwa uhakiki.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Doroth Mwanyika akifurahia jambo na baadhi ya wastaafu wanaolipwa pensheni zao na Hazina, waliojitokeza kuhakikiwa wakati wa uzinduzi wa zoezi hilo katika Ofisi za halmashauri ya Jiji la Arusha, zoezi litakalo dumu kwa siku tano hadi Ijumaa wiki hii katika mikoa ya Kanda ya Kaskazini ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Doroth Mwanyika akiongea na baadhi ya wastaafu waliofika katika Ofisi za Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa ajili ya uhakiki ambapo wastaafu hao wameiomba serikali iwaongezee kiwango cha pensheni wanacholipwa ili waweze kukabiliana na hali ngumu ya maisha.
Baadhi ya Wastaafu wanaolipwa Pensheni yao na Hazina, waliofika katika Ofisi za Makao Makuu, Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa ajili ya kuhakikiwa.
Baadhi ya Wastaafu wanaolipwa Pensheni yao na Hazina, Livingstone Kisanga (kulia) na Allen Kijazi, wakazi wa Arusha, wakisubiri kuhakikiwa katika Ofisi za Halmashauri ya Jiji la Arusha, wakati wa zoezi la uhakiki wa wastaafu hao linalofanyika katika mikoa ya Kanda ya Kaskazini (Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara). 
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Doroth Mwanyika akihojiwa na baadhi ya waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali mara baada ya kuongea na wastaafu waliofika kwa ajili ya uhakiki, ambopo wastaafu wengi wameridhishwa na zoezi hili la wanashukuru zoezi hili linaenda kwa haraka kwani wengi wao wana nyaraka zote muhimu zinazohitajika.
Wawezeshaji wa zoezi la uhakiki wakibadilishana mawazo na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Doroth Mwanyika. Kushoto kwake ni Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Msaidizi Bw. Stanslaus Mpembe na Mkaguzi wa Ndani Mkuu Bw. Paison Mwamnyasi.
Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Bw. Mohamed Mtonga, akitoa ufafanunuzi kwa wanahabari wa mkoa wa Arusha kuhusu masuala mbalimbali ya uhakiki wa wastaafu wanaolipwa na Hazina, unaoendelea katika kanda ya Kaskazini, mikoa ya Arusha, Manyara, Tanga na Kilimanjaro.
Mstaafu, Mwanakombo Yusuph, mkazi wa eneo la Kaloleni, Jijini Arusha, akihojiwa na Wanahabari mara baada ya kuhakikiwa katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha ambapo ameipongeza Serikali kwa kuendesha uhakiki huo utakaosaidia kuhuisha daftari la wastaafu na kwa uamuzi wake wa kuwalipa wastaafu kila mwezi badala ya miezi mitatu mitatu.
Bi. Amina Msigiti (kulia) ambaye ni mstaafu anayelipwa na Wizara ya Fedha na Mipango, akijiandaa kutia saini fomu yake ya uhakiki mbele ya Afisa wa Hazina, Winfrida Moshi, kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha.
RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN, KATIBU MKUU PAMOJA NA NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN, KATIBU MKUU PAMOJA NA NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

December 06, 2016
a1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwakaribisha Naibu Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo aliyeambatana na Katibu Mkuu wa TAMISEMI Mhandisi Mussa Iyombe  kabla ya kuanza kwa kikao chao cha pamoja na Makamu wa Rais  Samia Suluhu Hassan.
a2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika kikao cha pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Naibu Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo pamoja na  Katibu Mkuu wa TAMISEMI Mussa Iyombe.
a3
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na  Makamu wa Rais Samia Suluhu mara baada ya kutoka kwenye kikao cha pamoja kilicho wahusisha Naibu Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo pamoja na  Katibu Mkuu wa TAMISEMI Mussa Iyombe Ikulu jijini Dar es Salaam
a5
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan mara baada ya kumaliza kikao chao kilicho wahusisha Naibu Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo pamoja na  Katibu Mkuu wa TAMISEMI Mussa Iyombe Ikulu jijini Dar es Salaam.
PICHA NA IKULU
WAZIRI MAKAMBA AKUTANA NA WATUMISHI WA IDARA YA MAZINGIRA

WAZIRI MAKAMBA AKUTANA NA WATUMISHI WA IDARA YA MAZINGIRA

December 06, 2016

s1
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akiongea na watumishi wa Idara ya Mazingira katika Ofisi yake (hawapo pichani). Kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Mbarak Abdulwakil.
s2
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (kulia) akiwa katika kikao kazi kati ya Idara ya Mazingira na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira Bw. Richard Muyungi.
s3
Sehemu ya Watumishi kutoka Idara ya Mazingira wamkimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba (hayupo pichani) katika kikao kazi kilichofanyika Mtaa wa Luthuli jijini Dar es Salaam.
s4
Waziri Makamba (wa kwanza kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu Bw. Mbarak Abdul Wakil wakati wa kikao na Idara ya Mazingira.