MAGUFULI AHUTUBIA KISIWANI PEMBA LEO,AAHIDI KUULINDA MUUNGANO KWA NGUVU ZOTE.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya chama cha Mapinduzi,Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa Pemba jioni ya leo kwenye kutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Gombani ya Kale mjini Pemba.
Katika mkutano huo wa Kampeni,Dkt
Magufuli ameahidi kuwa akichaguliwa kuwa Rais wa awamu ya tano,atadumisha na
kuulinda Muungano wa Zanzibar na Tanganyika ulioanzishwa na Waasisi wetu
akiwemo Baba wa Taifa Hayati Julius Kambarage Nyerere pamoja na Abeid Amani
Karume.Dkt Magufuli kesho atahutubia kwenye mkutano mkubwa wa kampeni mjini
Unguja.
Wananchi wa Kisiwani Pemba wakiwa wamekusanyika katika uwanja wa Gombani ya Kale ,wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli alipokuwa akijinadi na kuomba kura kwa wananchi hao.
Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt
Mohamed Shein akiwahutubia
wakazi wa Pemba jioni ya leo kwenye kutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja
wa Gombani ya Kale mjini Pemba.Dkt Shein amewataka wakazi wa Kisiwani Pemba
kuilinda amani iliyopo ndani ya kisiwa hicho na kuwa Wananchi wakajitokeze kwa
wingi kupiga kura siku ya Oktoba 25 kwenye uchaguzi mkuu Mwaka huu.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar Dkt Mohamed Shein
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana Mama Shadia Karume mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Gombani ya Kale kwa ajili ya kuwahutubia wananchi kwenye mkutano wa kampeni.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza kwa makini Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar Dkt Mohamed Shein kabla ya mkutano wa kampeni kuanza jioni ya leo kisiwani Pemba.
Umati wa wakazi wa kisiwani Pemba kwenye mkutano wa kampeni.
Wananchi wa kiswani Pemba wakifuatilia mkutano wa kampeni
uliofanyika jioni ya leo,kwenye uwanja wa Gombani ya kale kisiwani humo.
Wananchi
wa kiswani Pemba wakishangilia jambo kwenye mkutano wa kampeni
uliofanyika jioni ya leo,ambapo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi Dkt John Pombe Magufuli pamoja na
Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt Mohamed Shein
walitumia jukwaa na mkutano huo kuwaomba kura za kutosha ili wakaiongoze
Tanzania katika kipindi cha awamu ya tano.
PICHA NA MICHUZI JR-PEMBA
MKUTANO WA BARAZA LA VYAMA VYA SIASA TANZANIA.ZANZIBAR
Viongozi
wa Meza Kuu wakiwa wamesimama wakati wa kuomba Dua Mkutano huo wa
Baraza la Viongozi wa Vyama vya Siasa Tanzania uliovikutanisha Viongozi
wa Vyama 22 vya Siasa Tamzania uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya
bwawani Zanzibar.wa kwanza Jaji Lubuva Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya
Siasa Mzirai na Msajili Msaidi wa Vyama vya Siasa Tanzani Mhe Ibrahim
Mkwawa.
Mmoja
wa Viongozi wa Vyama vya Siasa Tanzania akiuombea Mkutano huo wa Baraza
la Vyama vya Siasa Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya
Bwawani Zanzibar. ukizungumzia maadili ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania .
Katibu
wa Baraza la Vyama vya Siasa Mhe. Jaji Francis S.K. Mutungi,
akizungumza kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya
Siasa Tanzania Mhe Peter Mzirai kuaza kwa kikao hicho kilichofanyika
katika ukumbi wa hoteli ya Bwawani Zanzibar na kuwashirikisha Viongozi
wa Vyama 22 vya Siasa Tanzania.
Viongozi
wa Vyama vya Siasa wakimsikiliza Mtoa Mada Msaidizi Msaidi wa Vyama vya
Siasa Tanzania Mhe Ibrahim Mkwawa, akiwasilisha mada ya Maadili
iliotiwa saini na Viongozi wa Vyama vya Siasa kuhusiana na Uchaguzi Mkuu
wa Tanzania unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.
Msajili
Msaini wa Vyama vya Siasa Tanzania Mhe Ibrahim Mkwawa akiwasilisha Mada
ya Maadili ya Vyama vya Siasa kuhusiana na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania
mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa hoteli ya bwawani Zanzibar na
kuwashirikisha Viongozi wote wa Vyama vya Siasa vinavyoshiriki Uchaguzi
Mkuu mwezi huu.
Viongozi wa Vyama vya Siasa wakifuatilia Mkutano Huo. katika ukumbi wa hoteli ya bwawani Zanzibar.
Viongozi
wa Vyama vya Siasa wakiwa makini wakifuatilia mkutano huo wa Baraza la
Vyama vya Siasa Tanzania ukizungumzia Maadili ya Uchaguzi Mkuu wa
Tanxzania unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.
Viongozi wa Chama cha TADEA wakifuatila mkutano huo wa Baraza la Vyama vya Siasa Tanzania.
Viongozi
wa Chama cha AFP wakifuatilia mkutano huo kwa makini unaozungumzia
Maadilidi ya Uchaguzi kwa Vyama vya Siasa Tanzania uliofanyika katika
ukumbi wa hoteli ya bwawani Zanzibar.
Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot Zanzinews.com.
Mobeli No 0777 424152 or 0715424152
Email, othmanmaulid@gmail.com.
RAIS JAKAYA KIKWETE KUWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UJENZI WA BANDARI YA BAGAMOYO
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akizungumza na waandi wa habari wapo picha juu ya ujenzi
wa bandari ya Bagamoyo utakaokuwa wa aina yake Afrika Mashariki na
Kati, unatarajiwa kugharimu dola za Marekani bilioni 10 na kukamilika kati ya miaka mitano hadi saba ijayo. kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa CMHI ambaye pia ni Makamu wa Rais Mtendaji wa kampuni ya China Merchant Group Dk Hu Jianhua.kikao hichi kimefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akizungumza juu ya ujenzi huo na Mjumbe
kutoka China Mkurugenzi Mtendaji wa CMHI ambaye pia ni Makamu wa Rais
Mtendaji wa kampuni ya China Merchant Group Dk Hu Jianhua.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akiagana na Mjumbe
kutoka China Mkurugenzi Mtendaji wa CMHI ambaye pia ni Makamu wa Rais
Mtendaji wa kampuni ya China Merchant Group Dk Hu Jianhua.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbarimbari na Mjumbe
kutoka China Mkurugenzi Mtendaji wa CMHI ambaye pia ni Makamu wa Rais
Mtendaji wa kampuni ya China Merchant Group Dk Hu Jianhua.
(Picha na Emmanuel Massaka wa Global ya jamii)
WAZIRI
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe
amewathibitishia wakazi wa Bagamoyo kuwa wale wote watakaoguswa na mradi
wa ujenzi wa bandari mpya watalipwa fidia na wengine watajengewa nyumba
kwenye maeneo ya mji huo.
Akizungumza
na wandishi wa habari badaa ya kukutana na Mkurugenzi wa Kampuni ya
China Merchants Group itakayosimamia ujenzi huo, Dk Hu Jianhao, Membe
alisema katika ujenzi huo utakaochukua hekta 2400, wananchi wote
watakaohuswa hawataachwa bure.
“Mradi
huo ni mkubwa sana unaoshirikisha kampuni hii ya China Merchants Group,
wawekezaji kutoka Oman ambao wataalamu wao pia wameshafika na Serikali
ya Tanzania. Tunatarajia kuwa utaibadilisha Bagamoyo kwa kiasi kikubwa
na kuufannya kuwa mji wa viwanda, hatua itakayovuta wawekezaji wengi
zaidi na kuzalisha ajira nyingi,” alisema.
Mradi
mzima wa ujenzi utajumuisha eneo hekta 800 kwa ajili ya ujenzi wa
bandari na eneo la hekta 1,700 kwa ajili ya ukanda wa viwanda.
Mazungumzo
hayo ni sehemu ya awali ya maandalizi kwa ajili ya kuweka jiwe la
msingi la ujenzi wa bandari hiyo, katika sherehe inayotarajiwa
kuongozwana Rais Jakaya Kikwete leo.
Mradi
huo wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo utakaokuwa wa aina yake Afrika
Mashariki na Kati, unatarajiwa kugharimu Dola za Marekani bilioni 10 na
kukamilika kati ya miaka mitano hadi saba ijayo.
Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu,
Ofisi ya Waziri Mkuu Dk Florens Turuka jana, Rais Kikwete ataweka jiwe
hilo la msingi kwa ajili ya uzinduzi wa awamu ya kwanza ya mradi huo.
Eneo
hilo litaendelezwa chini ya makubaliano ya Serikali ya Tanzania,
Kampuni ya China ya Merchants Holdings International (CMHI) na Mfuko wa
Taifa wa Dharura wa Oman (SGRF).
Chini
ya ushirikiano huo, Serikali inawakilishwa na Mamlaka ya Bandari ya
Tanzania (TPA) na Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uwekezaji kwa Mauzo ya Nje
(EPZA), Oman itawakilishwa na SGRF na China CMHI.
Dk
Turuka alisema mradi huo pia utahusisha ujenzi wa miundombinu kama vile
reli, mitandao ya barabara, umeme, umeme, gesi na mitandao ya
mawasiliano.
Mradi
huo unatarajiwa kuibadili Tanzania na kuwa kituo kikuu cha usafirishaji
kwa wafanyabiashara wa ndani na wa kimataifa ambao wataunganishwa na
viwanda vitakavyozalisha bidhaa zilizoongezewa ubora.
Kwa
mujibu wa Dk Turuka, wazo la kuwepo mradi huo, limetokana na uhusiano wa
muda mrefu wa kidiplomasia baina ya Tanzania, China na Oman katika
kuhamasisha uimarishaji wa viwanda Afrika jambo litakalosaidia kuongeza
ajira nchini.
mwaka 2008, Rais Kikwete alipotembelea China na kuzungumza na Rais wa nchi hiyo, Hu Jintao, na kuafikiana kujenga bandari hiyo.
Sherehe za kuweka jiwe la msingi zitahudhuriwa na wageni wa kimataifa na wa ndani wakiwemo wawekezaji katika mradi huo.
Wengine
wanoatarajiwa kuhudhuria ni wanadiplomasia na ujumbe kutoka kwa Sultani
wa Oman utakaoongozwa na Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano nchini humo,
Shehe Abdullah Al Saadi.
DK. MAGUFULI APOKELEWA KWA NDEREMO NA VIFIJO KISARAWE NA UKONGA WAKATI WA MKUTANO WA KUOMBA KURA
Wananchi wa Jimbo la Kisarawe, mkoani Pwani wakishangilia hotuba ya Dk Magufuli wakati wa mkutano wa kampeni mjini Kisarawe leo. Picha zote na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Dk Magufuli akimnadi mgombea ubunge Jimbo la Kisarawe, Seleman Javo wakati wa mkutano wa kampeni mjini Kisarawe leo.
Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akiwanadi wagombea wa viti maalum wa Kisarawe.
Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akionyesha picha aliyochorwa.mm
Wakazi wa Mombasa, Ukonga, Dar es Salaam wakiuzuia msafara wa Dk Magufuli ulipokuwa ukitoka Kisarawe kwenda eneo Moshi Bar kuendelea na kampeni.
Shamra shamra za kumpokea Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli mapema leo, wakati akielekea Ukonga katika barabara ya Moshi - Bar.
Msafara wa Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli ukipokelewa kwa nderemo na vifijo.
Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akiingia Ukonga katika mkutano wake wa kuomba kura.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ndg. Ramadhan Madabida akimnadi Dk. Magufuli kwa wakazi wa Ukonga.
Akina mama wakiwa na nyuso za furaha.
Umati wa watu waliohudhuria mkutano huo.
Kila mmoja akitaka kumuona mgombea.
Dk. Magufuli akitoa ahadi ya ujenzi wa Barabara ya Mombasa hadi Moshi Baa kwa kiwango cha Lami.
Mmoja ya wafuasi wa CCM akisiliza sera za mgombea Urais wa Tanzania, Dk. John Magufuli huku akiwa amebeba mboga mboga zake.
Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akinyooshewa vidole gumba na wakazi wa Jimbo la Ukonga ikiwa ni ishara ya kukubali kumpigia kura ya ndiyo , wakati wa mkutano wa kampeni eneo la Moshi Bar, Ukonga Dar es Salaam.
Dk. Magufuli akimnadi Mgombea ubunge Jimbo la Ukonga kupitia CCM, Jerry Silaa wakati wa mkutano wa kampeni jimboni humo leo. Dk. Magufuli akiwanadi wagombea wa viti maalum wa Jimbo la Ukonga kupitia CCM wakati wa mkutano wa kampeni jimboni humo leo. -- ---- Cathbert Angelo Kajuna, Founder and Mananging Director Kajunason Blog, P.O Box 6482, Dar es Salaam. Tel: +255 787 999 774 Alt: +255 765 253 445 www.kajunason.blogspot.com "Everything is Possible Through Peace & Stability''
Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akiwanadi wagombea wa viti maalum wa Kisarawe.
Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akionyesha picha aliyochorwa.mm
Wakazi wa Mombasa, Ukonga, Dar es Salaam wakiuzuia msafara wa Dk Magufuli ulipokuwa ukitoka Kisarawe kwenda eneo Moshi Bar kuendelea na kampeni.
Shamra shamra za kumpokea Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli mapema leo, wakati akielekea Ukonga katika barabara ya Moshi - Bar.
Msafara wa Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli ukipokelewa kwa nderemo na vifijo.
Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akiingia Ukonga katika mkutano wake wa kuomba kura.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ndg. Ramadhan Madabida akimnadi Dk. Magufuli kwa wakazi wa Ukonga.
Akina mama wakiwa na nyuso za furaha.
Umati wa watu waliohudhuria mkutano huo.
Kila mmoja akitaka kumuona mgombea.
Dk. Magufuli akitoa ahadi ya ujenzi wa Barabara ya Mombasa hadi Moshi Baa kwa kiwango cha Lami.
Mmoja ya wafuasi wa CCM akisiliza sera za mgombea Urais wa Tanzania, Dk. John Magufuli huku akiwa amebeba mboga mboga zake.
Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akinyooshewa vidole gumba na wakazi wa Jimbo la Ukonga ikiwa ni ishara ya kukubali kumpigia kura ya ndiyo , wakati wa mkutano wa kampeni eneo la Moshi Bar, Ukonga Dar es Salaam.
Dk. Magufuli akimnadi Mgombea ubunge Jimbo la Ukonga kupitia CCM, Jerry Silaa wakati wa mkutano wa kampeni jimboni humo leo. Dk. Magufuli akiwanadi wagombea wa viti maalum wa Jimbo la Ukonga kupitia CCM wakati wa mkutano wa kampeni jimboni humo leo. -- ---- Cathbert Angelo Kajuna, Founder and Mananging Director Kajunason Blog, P.O Box 6482, Dar es Salaam. Tel: +255 787 999 774 Alt: +255 765 253 445 www.kajunason.blogspot.com "Everything is Possible Through Peace & Stability''
Subscribe to:
Posts (Atom)