Naibu
Waziri Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira Mh Luhaga Mpina
akitolea ufafanuzi namna ambayo fukwe ya Pangani imeathirika na athari
zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi.
kushoto
meneja mkuu wa kiwanda cha maziwa cha tanga fresh Bw. Michael Kalata,
akimuonyesha mh Naibu Waziri wa Nchi ofisi ya makamu wa Raisi Muungano
na Mazingira Luhaga Mpina, moja nya bidhaa ya maziwa inayozaliswa katika
kiwanda hicho. mh Mpina alitembelea baadhi ya viwanda jijini tanga
kujionea namna ambavyo vinatekeleza sheria ya mazingira ya 2004 na
kanuni zake.
Mh
Luhaga Mpina Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya makamu wa Rais Muungano na
Mazingira mwenye nguo nyeusi akipata maelezo toka kwa mtaalam katika
kiwanda cha Twiga cement alipokitembelea leo jijini tanga kuona namna
ambavyo kiwanda hicho kinatekeleza sheria ya mazingira ya mwaka 2004 na
kanuni zake.
Pichani
Namna ambavyo fukwe ya Pangani Jijini Tanga ilivyoliwa na maji ya
bahari, kutokana na kuongezeka kwa kina cha bahari ikiwa ni athari
zitokanano na madhara ya mabadiliko ya tabia nchi. na baaadhi ya visiwa
nchini viko hatarini kumezwa na bahari.
Picha zote na Evelyn Mkokoi wa Ofisi ya Makamu wa Raisi
…………………………………………………………………………………………….
NA EVELYN MKOKOI TANGA
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na
Mazingira Mh. Luhaga Mpina (MB) amekifungia kiwanda cha kuzalisha cement
na chokaa kilichopo jijini Tanga cha Rhino Cement,
leo jioni kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni uharibu na uchafuzi wa
mazingira na kuvunja sheria ya usimamizi wa mazingira ya mwaka 2004 na
kanuni zake.
Mh. Mpina amechukua uamuzi huo, baada ya kupokea malalamiko
kutoka kwa wananchi wa kata ya maweni kupitia diwani wa kata hiyo Bw.
Joseph Colvas na kujionea mwenyewe namna ambavyo kiwanda hicho kinavyo
achilia moshi mzito kwenda angani, pamoja na vumbi lisilovumilika
kusambaa katika maeneo ya makazi ya wanachi wa kata hiyo ikiwa ni pamoja
na kusambaa katika maeneo ya shule ya sekondari ya Don Bosco ambapo,
Mh. Mpina ameelezwa kuwa athari zitokanazo na uachiachi wa hewa hiyo
chafu angani si tu kwa watoto wa shule zinazozunguka kata hiyo bali pia
ni kwa viumbe hai na mazingira.
“Hawa jamaa wamekuwa wakiachilia vumbi jingi na moshi mzito
kutoka katika kiwanda hiki mara kwa mara, hivi tangu jana wamezima
mitambo yao wakijua kabisa kuwa kuna ugeni wa Naibu Waziri kutoka Ofisi
ya Makamu wa Rais, Alisisitiza Bw. Joseph.”
Kwa upande wake Afisa Afya wa jiji la tanga aliyejulikana kwa
jina moja la bwana Kizito alimuelezea Naibu Waziri Mpina kuwa ni kweli
kiwanda hicho kimekuwa kikifanya uchafuzi huo wa mazingira, na Afisa
uendeshaji kutoka Baraza la Taifa na HIfadhi ya Mazingira NEMC Bw.
Novatus Mushi ameeleza kuwa kiwanda hicho kimeshawahi kutozwa faini ya
shilingi milioni kumi na saba (17) kwa kosa la kuchelewa kulipa ada ya
mwaka ya mazingira pamoja na uharibifu wa mazingira uliokuwa ukifanywa
na kiwanda hicho kwa upande wa kuzalisha chokaa.
Mh. Mpina ameelekeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa
Mazingira ( NEMC) kukifunga kiwanda hicho kisiendelee na uzalishaji kwa
muda usiopungua miezi mitatu, na kulitaka baraza hilo lijiridhishe na
kufuatilia namna kiwanda hicho kinavyotakiwa kutekeleza sheria ya
mazingira kwa kujenga mfumo wa kisasa wa kutoa taka zitokanazo na
uzalishaji kiwandani hapo pamoja, na kupima vumbi na moshi utokao
kiwandani hapo kama hautakuwa na madhara na athari kwa mazingira na
viumbe hai. Kinyume na hapo kiwanda hicho kitafungiwa moja kwa moja.
Aidha, akitolea mfano wa kiwanda cha bonite bottles cha mjini
moshi kwa kuwa kinara katika upandaji miti na utunzaji wa mazingira, mh
Mpina alivitaka viwanda vingine viige mfano wa kiwanda hicho cha coke
cola.
Ziara ya Mh. Mpina Jijini Tanga ilihusisha pia kuangalia namna
ukuta wa fukwe ya Pangani uliojengwa enzi za mkoloni, ulivyo athirika na
madhara yatokanayo na athari za mabadiliko ya tabia nchi na kusema
kuwa, ukuta huo huko kwenye mchakato wa kujengwa na kuboreshwa upya,
ifikapo mwezi wa nne mwaka huu mradi wa ujenzi wa ukuta huo utaanza
kutekelezeka kwa kuwa tenda imeshatangazwa na jumla ya kiasi cha fedha
za kimarekani dola milioni 1,400 zimepatikana kupitia mfuko wa nchi
maskini zaidi duniani (LDCf).
Mh. Mpina aliwaasa wakazi wa mji wa Tanga na viunga vyake
kutunza mazingira kwa kupanda miti na kufanya usafi kama ilivyoagizwa na
serikali, ili kuhepukana na nchi kuwa janga na magonjwa yatokanayo na
uchafu.
Waziri Mpina Pia alitembelea kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh
na kiwanda cha Tanga Cement na kuridhirishwa na namna ambayo
wanatekeleza sheria ya mazingira ya mwaka 2004 na kanuni zake.