Wakuu wa Mikoa wapewa jukumu la kutoa vibali vya kuchangia Elimu

Wakuu wa Mikoa wapewa jukumu la kutoa vibali vya kuchangia Elimu

March 03, 2016

01 
Na Eleuteri Mangi- MAELEZO
Serikali imeongeza wigo wa utoaji wa kibali cha uchangiaji wa elimu msingi bila malipo hadi kwa Wakuu wa Mikoa baada ya kujiridhisha kuwa taratibu zilizowekwa zimefuatwa kikamilifu.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo jijini Dar es salaam Msemaji wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Rebecca Kwandu amesema kuwa awali vibali hivyo vilitolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) pekee ikiwa na lengo la kudhibiti michango holela.
Taarifa hiyo imesisitiza kuwa azma ya Serikali ya kutoa elimu msingi bila malipo haizuii wadau mbalimbali wa elimu kuchangia maendeleo ya elimu kwa hiari ambapo wadau wakiamua kuchangia kwa nia ya kushughulikia kero fulani iliyopo katika shule yao au shule zao baada ya kupata kibali wanaruhusiwa kufanya hivyo.
Katika kutekeleza dhana ya utoaji wa elimumsingi bila malipo, hadi kufika mwishoni mwa mwezi Januari, 2016   Serikali inatoa elimu hiyo kwa jumla ya wanafunzi 9,771,902.
Kati ya wanafunzi hao, 8,301,759 ni wa elimu ya msingi na 1,470,143 ni wa sekondari ambao wanapatiwa elimumsingi bila malipo kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne.
Serikali inasisistiza kuwa viongozi wanahusika katika kusimamia utekelezaji wake ambapo kwa upande wa wazazi au walezi, kamati na Bodi ya shule pamoja na jamii wao nao wanajukumu la kuelewa majukumu yao ipasavyo.
Aidha, juhudi za makusudi zinapaswa kufanywa na viongozi na watendaji wa elimu ili kuwezesha jamii kufahamu wajibu wao katika utekelezaji wa elimumsingi bila malipo na hatimaye kufikiwa kwa malengo yaliyokusudiwa.
Katika kutekeleza wajibu wake, Serikali ya Awamu ya Tano (SAT) kuanzia mwezi Januari, mwaka huu imeanza kutoa elimumsingi bila malipo imetoa waraka wa Elimu Namba 6 wa Mwaka 2015 ambao unaofafanua na kubainisha majukumu ya serikali na wadau mbalimbali katika utekelezaji wa elimu msingi bila malipo.

DIWANI ATAKA MSHIKAMANO NDANI YA VIKOBA

March 03, 2016




Tangakumekuchablog
Korogwe, DIWANI wa kata ya Kerenge halmashauri ya Korogwe mjini, Shebila Said Shebila (CCM), amewataka wanachama wa Vikoba Upendo Tupendane cha Mazinde Tarafa ya Mombo kushikamana na umoja wao na kuyafikia malengo waliyojiwekea.
Akizungumza katika mkutano mkuu wa wanachama wa vikoba Mazinde jana, Shebila alisema umoja huo ni mfano kwa wanawake wengine kujiunga kwani mbali ya maendeleo waliyopata pia wamekuwa chachu ya maendeleo Mombo.
Ameitaka Serikali kutuma wataalamu wa elimu ya vikoba ili wakulima na wajasiriamali wa kazi za mikono kujiunga na kuweza kufaidika na mikopo ya kukopa na kulipa.
“Kabla ya kuja hapa nilikuwa nazisikia sifa zenu na najua nini mumefanya na leo mumesimama hapa, kwa jitihada zenu na umoja wenu nina imani kila mmoja hapa baada ya mwaka mmoja atakuwa ni tajiri wa mfano” alisema Shebila na kuongeza
“Muko wanachama zaidi ya mia na ukiangalia kuna wengine wanajiunga huu ni mtaji tunaoweza kusema jiunge utajirike hongereni sana” alisema
Diwani huyo amevishauri vikundi hivyo kuwa wabuni miradi mengine zaidi na halmashauri itawasaidia kwa hali na mali kuhakikisha unakomesha umasikini majumbani.
Alisema Tarafa ya Mombo vijijini vya Mazinde viko na rasilimali nyingi za kujikwamua na umasikini kikiwemo kilimo cha matikiti maji na zao la mkonge hivyo kujiunga na vikundi ni njia rahisi kujipatia fursa za mikopo.
Kwa upende wake wa Kikoba Tupendane, Issa Sigge,  amemtaka diwani huyo kupata asilimia 20 ya halmashauri kwa vijana na vikundi ili kuimarisha vikundi vyao na kupunguza wimbi la watu wasio na kazi.
Alisema kuna vijana wengi wamekaa bila kazi ya kufanya hivyo kuipata asilimia hiyokuanweza kuwavutia vijana na kuondosha wimbi la wasio na kazi Mazinde jambo ambalo litawasukuma katika kazi za ujasiriamali.
“Mhshimiwa diwani hebu katupigie chapuo kule katika mabaraza yenu ya madiwani kuipata ile asilimia 20 ya halmashauri, hii itawasukuma vijana na wasio na kazi kujiunga na vikundi” alisema Segga
Segga aliwataka wanachma wa vikoba kudumisha umoja na mshikamano ili kuweza kuyafikia malengo yao na kuhakikisha kila mwanachama anawasilisha michango yake kwa wakati.
                                          

 Wanachama wa Vikoba Tupendane Mazinde Wilayani Korogwe Mkoani Tanga wakionyesha pesa walizochanga wakati wa mkutano mkuu wa Umoja huo uliofanyika Mazinde jana. Jumla ya shilingi milioni moja laki mbili zilichangwa.
Serikali yavipongeza vyombo vya Habari kwa kuhabarisha Jamii vyema.

Serikali yavipongeza vyombo vya Habari kwa kuhabarisha Jamii vyema.

March 03, 2016

bar1
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Anastazia Wambura akisalimiana na Mkurugenzi mkuu National Media Group  Bw.Joe Muganda wakati wa tafrija fupi iliyoandaliwa na kampuni ya Mwananchi Communications limited kwa ajili ya Bodi ya  Mwananchi,wateja wake na wadau wa Habari.
bar2
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Anastazia Wambura akiwasili katika hoteli ya Serena kwa ajili ya tafrija fupi iliyoandaliwa na kampuni ya Mwananchi Communications limited kwa ajili ya Bodi ya  Mwananchi,wateja wake na wadau wa Habari.
bar3
Mkurugenzi Idara ya Habari Maelezo Bw.Assah Mwambene (kushoto) akifurahia jambo na Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Mwananchi Communications Limited Bakari Machumu wakati wa tafrija fupi iliyoandaliwa na kampuni ya hiyo kwa ajili ya Bodi ya  Mwananchi,wateja wake na wadau wa Habari.
bar4
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Anastazia Wambura akizungumza na wadau wa Habari wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na kampuni ya Mwananchi Communications Limited.Mheshimiwa wambura alivishukuru vyombo vya habari kwa kuhabarisha watanzania kipindi cha uchaguzi na pia katika siku mia za kwanza za Rais wa awamu ya tano na Mhe.John Pombe Magufuli na kuwapongeza kwa kuonyesha weledi na ukomavu katika uandishi wa Habari.
bar5
Wadau wa Habari wakifatilia hotuba ya Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Anastazia Wambura.Kutoka kushoto ni Bi.Teddy Mapunda na Mwisho kulia ni Maria Sarungi
bar6
Afisa Mtendaji mkuu wa Star Times Tanzania Bw.Leo Liofang(wa kwanza Kulia) pamoja na makamu wa Rais wa kampuni ya Star Times Bi. Zuhura Hanif(wa pili Kulia) wakifatilia jambo wakati wa tafrija fupi iliyoandaliwa na kampuni ya Mwananchi Communications limited kwa ajili ya Bodi ya  Mwananchi,wateja wake na wadau wa Habari.
Picha na Daudi Manongi.
……………………………………………………………………………………………………………………………
Na Daudi Manongi-WHUSM
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura amevipongeza Vyombo vya Habari kwa kuwahabarisha watanzania vyema katika mchakato wote wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na katika kipindi cha siku mia za kwanza za awamu ya tano ya utawala wa Mheshimiwa Dr. John Joseph Pombe Magufuli.
Naibu Waziri uyo ameyasema hayo alipokuwa akiongea na wadau wa Habari katika tafrija fupi iliyoandaliwa na kampuni ya Mwananchi Communications Limited.
“Hakika mmeonesha uwezo mkubwa, weledi na ukomavu mkubwa wa kisiasa na uzalendo kwa nchi yetu”.Alisema Bi.Wambura.
Mhe.Wambura pia alieleza kuwa Serikali ya awamu ya tano ina dhamira ya dhati kabisa ya kushirikiana na wadau wote vikiwemo Vyombo vya Habari, ambapo pia mchakato wa Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari ambao ulishasomwa kwa mara ya kwanza bungeni bado Serikali inaendelea kupokea maoni ya wadau mbalimbali juu ya namna bora ya kuboresha Muswada huo.
Naibu Waziri uyo alikazia umuhimu wa upashaji habari na kusema ni jambo muhimu sana katika nchi yetu na kwaiyo Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo iko tayari kufanya kazi na wadau wote.
“Kama Serikali hatuwezi kuwakwepa wadau na ndio maana hata utaratibu wetu wa kushughulikia makosa kwenye Vyombo vya Habari umebadilika. Tumekuwa ni walezi zaidi badala ya kuwa viranja. Tunashauriana zaidi kuliko kutoa adhabu. Tunaelimisha zaidi kuliko kusubiliana”
Naibu Waziri uyo pia aliupongeza uongozi mpya wa jukwaa la wahariri na kuhaidi kuwapa ushirikiano wa karibu katika kutatua masuala mbalimbali ya Habari.
Kwa upande wake Mwenyekiti Mtendaji wa Bodi ya Magazeti ya Mwananchi Bw.Francis Nanai aliipongeza serikali kwa kuweka jitihada zaidi katika kuboresha mahusiano mazuri na vyombo vya Habari na pia kwa afrika mashariki Tanzania iko katika nafasi nzuri ukilinganisha na wenzetu katika suala la uhuru wa vyombo vya habari.

WAKALA YA SERIKALI MTANDAO YAZISHAURI TAASISI ZA SERIKALI KUFUATA MIONGOZO NA VIWANGO KATIKA MATUMIZI YA TEHAMA

March 03, 2016


 Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wakala ya Serikali Mtandao Bi. Suzan Mshakangoto akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa Habari kuhusu taratibu zinazotakiwa kuzingatiwa na taasisi za Serikali katika kuimarisha matumizi sahihi na salama ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika kuendesha mifumo ya Tehama Serikalini. Kushoto ni Mkurugenzi wa Usimizi wa Huduma za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Wakala hiyo. 
 Waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano huo.
 Mkurugenzi wa Usimamizi wa Huduma za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Wakala hiyo Bw. Benedict Ndomba akifafanua kuhusu mpango wa Serikali wa kuimarisha mawasiliano katika mifumo ya TEHAMA Serikalini.

Na Beatrice Lyimo - Dar es Salaam
 
Wakala ya Serikali mtandao (e-Government Agency) imezishauri Taasisi zote za Umma ,Wizara, Idara zinazojitegemea, Sekreterieti za Mikoa, Wakala na Mamlaka za Serikali ,Bodi, Tume, Mabaraza, Mifuko, Mashirika ya umma na Mamlaka za Serikali za Mitaa kufuata miongozo na viwango vilivyotolewa Wakala hiyo katika uanzishaji na usimamizi wa mifumo ya Tehama Serikalini.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wakala ya Serikali Mtandao Bi. Suzan Mshakangoto alipokuwa akitoa maelekezo na ufafanuzi wa taratibu zinazotakiwa kuzingatiwa na taasisi hizo kwa lengo la kuimarisha matumizi sahihi na salama ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika kuendesha mifumo ya Tehama Serikalini.

Bi. Mshakangoto amesema kuwa miongozo na viwango hivyo vinalenga kuziwezesha taasisi za umma kujenga mifumo inayoendana na mahitaji halisi ya taasisi husika na kuepuka mifumo inayojengwa kwa shinikizo la wafanyabiashara, wafadhili au kwa matakwa ya mtu binafsi.

“ Taasisi zote zikitumia miongozo ya viwango tuliyoweka, Serikali itakuwa na uwezo wa kuepuka urudufu wa mifumo na kupunguza gharama kubwa za uendeshaji kwa kuwa na mifumo endelevu yenye gharama halisi inayofuata viwango vya Usalama katika kulinda taarifa na data za Serikali”  Alifafanua Meneja huyo.

Amezishauri taasisi hizo kuwasilisha maandiko ya mifumo mipya ya TEHAMA na kujaza taarifa za mifumo au miradi ya TEHAMA iliyopo katika mfumo wa kukusanya na kutunza taarifa za miradi ya TEHAMA Serikali ili iweze kuthibitishwa iwapo imefuata miongozo na viwango vilivyowekwa kabla ya kujengwa na kusakinishwa.

Akitoa ufafanuzi kuhusu wafanyabiashara wanaojihusisha na miradi au utengenezaji wa mifumo ya TEHAMA Serikalini amesema kuwa wanashauriwa kufuata miongozo na viwango hivi ili kujua mahitaji halisi ya Serikali na kuweza kujenga mifumo ya TEHAMA endelevu na inayoleta tija kwa umma.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Usimizi wa Huduma za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Wakala hiyo Bw. Benedict Ndomba ameeleza kuwa mpango wa Serikali ni kuhakikisha kuwa mifumo yote ya TEHAMA ya Serikali inakuwa na mawasiliano na kubadilishana taarifa mbalimbali.

Amesema kuwa Serikali imekuwa ikiweka msisitizo wa matumizi ya TEHAMA kwa lengo la kupunguza gharama za uendeshaji kwa kuwawezesha wananchi na wadau mbalimbali kupata huduma za Serikali kwa gharama nafuu kwa njia ya Mtandao.

Wakala ya Serikali Mtandao (e-Government Agency) ni Taasisi ya Serikali iliyoanzishwa mwaka 2012 kwa sheria ya Wakala za Serikali Na. 30, Sura ya 245 ya mwaka 1997. Wakala hii ina majukumu na mamlaka ya kuratibu, kusimamia na kukuza jitihada za Serikali Mtandao nchini Tanzania.
TWIGA STARS TAYARI KUWAVAA ZIMBABWE KESHO

TWIGA STARS TAYARI KUWAVAA ZIMBABWE KESHO

March 03, 2016
Kikosi cha timu ya Taifa ya Wanawake ya Mpira wa Miguu (Twiga Stars), leo kimefanya mazoezi ya mwisho tayari kwa kuwakabili timu ya Taifa ya Wanawake kutoka Zimbabwe (Mighty Warriors) katika mchezo wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa ya Afrika kesho Ijumaa katika uwanja wa Azam Complex Chamazi jijini Dar es salaam.
Twiga Stars inayonolewa na kocha mzawa mwanamke, Nasra Juma imekamilisha ratiba yake leo asubuhi kwa kufanya mazoezi mepesi katika uwanja wa Karume ofisi za TFF, huku kocha wake Nasra akisema vijana wake wote wapo katika hali nzuri kuelekea kwenye mchezo huo.
Akiongea na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa TFF uliopo Karume, Nasra amesema ana waheshimu Zimbabwe wana timu nzuri, ndani ya miaka minne wameshacheza nao zaidi ya mara nne, mapungu yaliyojitokeza katika michezo iliyopita wamefanyi kazi na hivyo kesho ana imani watafanya vizuri.
Aidha kocha Nasra, amewaomba watanzania kujitokeza kwa wingi kesho Ijumaa katika uwanja wa Azam Complex Chamazi kuwapa sapoti Twiga Stars katika mchezo huo utakaonza majira ya saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
Naye nahodha wa kikosi hicho Sophia Mwasikili, amesema wachezaji wote wapo katika hali nzuri, wana ana ari na morali ya hali ya juu kuelekea kwenye mchezo huo wa kesho, na kuwaomba watanzania kuwapa sapoti kwa kujitokeza kwa wingi kuja kuwashangilia uwanjani watakapokuwa wakipeperusha bendera ya Tanzania.
Wapinzani wa Twiga Stars, timu ya taifa ya Zimbabwe wanawasili leo jioni tayari kwa mchezo huo, huku waamuzi wa mchezo huo kutoka nchini Ethiopia wakiwa tayari wameshawasili leo mchana kwa shirika la ndege la Kenya (KQ).

Semina ya kujadili masuala ya kodi kwenye sekta ya vinywaji vyenye kilevi yafanyika Dar

Semina ya kujadili masuala ya kodi kwenye sekta ya vinywaji vyenye kilevi yafanyika Dar

March 03, 2016


MER1
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dkt.Adelhelm Meru, (kushoto) akibadilishana mawazo na  Mkurugenzi  Mkuu wa TBL Group ,Roberto Jarrin  wakati  wa semina ya kujadili masuala ya kodi kwenye sekta ya vinywaji iliyofanyika  jana katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam.
MER2
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo,Maji na Mifugo Dk.Mary Nagu (kushoto) akibadilishana mawazo na   Mkurugenzi  Mkuu wa TBL Group ,Roberto Jarrin  wakati  wa semina ya kujadili masuala ya kodi kwenye sekta ya vinywaji iliyofanyika  jana katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam.
MER3
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dkt.Adelhelm Meru, (kushoto)  akizungumza  wakati wa uzinduzi wa   semina hiyo ambapo alikuwa mgeni rasmi. Kutoka kulia ni  Mkurugenzi  Mkuu wa TBL Group ,Roberto Jarrin , wa pilia ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Tanzania (SBL) Kalpesh Mehta na Mkurugenzi Mkuu wa Heineken Tanzania, Michael Mbungu.
MER4
Mkurugenzi  Mkuu wa TBL Group ,Roberto Jarrin akizungumza katika mkutano huo.
MER5
Baadhi ya wadau mbalimbali waliohudhuria  kwenye mkutano wa Alcoholic Drinks and  Beer Sector Taxation  Workshop uliofanyika leo katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam, wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye semina hiyo
MER6
Baadhi ya wadau mbalimbali waliohudhuria  kwenye mkutano wa Alcoholic Drinks and  Beer Sector Taxation  Workshop uliofanyika leo katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam, wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye semina hiyo
MER7
Baadhi ya wadau mbalimbali waliohudhuria  kwenye mkutano wa Alcoholic Drinks and  Beer Sector Taxation  Workshop uliofanyika leo katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam, wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye semina hiyo
MER8
Mkurugenzi Mkuu wa Heineken Tanzania, Michael Mbungu, akifafanua jambo wakati wa mkutano wa  Alcoholic Drinks and  Beer Sector Taxation Workshop ,uliofanyika jana katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam. Wengine kutoka kushoto ni  Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Tanzania (SBL) Kalpesh Mehta ,   , Christopher  Mgifi kutoka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji   na Mkurugenzi  Mkuu wa TBL Group ,Roberto Jarrin  
MER9
Baadhi ya wadau wakuu walioshiriki katika semina hiyo wakiwa katika picha ya pamoja
Serikali kujenga machinjio ya kisasa Vingunguti

Serikali kujenga machinjio ya kisasa Vingunguti

March 03, 2016

Na Raymond Mushumbusi, MAELEZO

IL
Serikali imejipanga kujenga machinjio ya kisasa katika eneo la Vingunguti  Jijini Dar es Salaam ili kuondoa changamoto zilizopo machinjioni hapo ikiwa ni pamoja na kulinda afya za wachinjaji na walaji wa nyama.
.
Akiongelea mipango hiyo kwa njia ya simu Msemaji wa Manispaa ya Ilala Bi.Tabu Shahibu amesema Halmashauri iko katika mchakato wa kutangaza zabuni kwa makampuni yatakayoweza kujenga machinjio hayo kwa kiwango kinachotakiwa.
“Tupo katika harakati za kutafuta mkandarasi wa kujenga machinjio na hivi karibuni tutatangaza zabuni kwa ajili ya ujenzi huo”
“ Napenda kuwahakikishia kwamba tutafanya jitihada zote za kumpata mkandarasi mapema ili tuanze mapema ujenzi huu wa machinjio mapya na kuondokana na changamoto zinazokabili machinjio yaliyopo”Alisema Bi Tabu.
Aidha, Bi Tabu Shaibu amesema kuwa kabla ya kujenga machinjio mapya wanaendelea na ujenzi wa mabanda ya machinjio, njia za kushushia ng’ombe ,bucha na kupanua eneo la machinjio na wameshapima na kufanya tathimini ya gharama ambazo zitatumika katika marekebisho hayo.
Mpango huu umekuja mara baada ya ya agizo la mawaziri, akiwemo Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mhe. Mwigulu Nchemba, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Hamis Kigwangalla na Waziri wa Nchi ofisi ya Raisi TAMISEMI MHE. George Simbachawene walipotembelea machinjio ya Vingunguti Januari 2 mwaka huu.
Machinjio ya Vingunguti yalianza kutumika tangu miaka ya 1950 ikiwa inahudumia idadi ya watumiaji wa mazao ya wanyama waliokuwa kwa wakati ule. Machinjio hayondio bado  yanatumika hadi sasa wakati idadi ya watumiaji wa mazao ya nyama wameongezeka  hivyo kukumbana na changamoto mbalimbali. Ili kukabiliana na changamoto hiyo Serikali imepanga kuyarekebisha yaliyopo na kujenga mapya na ya kisasa.

SHULE DIRECT YASHIRIKI KILI MARATHON KUSAIDIA WANAFUNZI WASIOSIKIA (VIZIWI) KUJIFUNZA

March 03, 2016


Mgeni Rasmi Afisa Elimu Manispaa ya Moshi, Bw. Deo Tulo Fundi (pichani kulia) akifafanua jambo wakati wa hafla fupi ya kukabidhi kompyuta zenye matini ya masomo tisa ya Sekondari (kidato cha kwanza – sita), kompyuta hizo zilitolewa na Shule Direct kwa ajili ya kusaidia wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia katika Shule ya Ufundi Sekondari Moshi. (Kushoto ni Bw. Erasmus Kyara, Mkuu wa Shule ya Ufundi Moshi).
Afisa Elimu wa Elimu ya Mahitaji Maalum Manispaa ya Moshi akitoa neno wakati akishuhudia tukio la makabidhiano ya kompyuta zenye matini za kujifunzia zilizotolewa na Shule Direct kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia katika Shule ya Ufundi Sekondari Moshi.
Baadhi ya wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia katika Shule ya Ufundi Sekondari Moshi na mwalimu wao Mwl. Raphael Lukumai (aliyekaa kulia) wakifurahia pamoja na baadhi ua wageni waliofika shuleni kwao kukabidhi kompyuta zenye masomo tisa ya Sekondari ndani yake.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya ufundi sekondari Moshi wakielekezana jambo katika mojawapo ya kompyuta walizokabidhiwa na Shule Direct, shuleni kwao,
Aneth Gerana, mtanzania wa kwanza mwenye ulemavu wa kusikia kupata shahada ya Chuo Kikuu, ambaye pia alijitokeza kuunga mkono jitihada za Shule Direct, akiongea na baadhi ya wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia katika shule ya ufundi sekondari Moshi wakati wa hafla fupi ya kukabidhi kompyuta shuleni hapo.
Aneth Gerana na baadhi ya wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia kutoka shule ya ufundi sekondari Moshi, wakifurahia kompyuta zilizotolewa na Shule Direct ili kuwasaidia wanafunzi hao kujifunza kwa urahisi zaidi.
Faraja Nyalandu, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mkuu wa Shule Direct na Aneth Gerana wakikimbia mbio za kilometa 21.1 wakati wa mbio za Kili Marathon. Shule Direct walishiriki mbio hizo kwa ajili ya kuchangisha fedha kuwezesha upatikanaji wa kompyuta zenye matini ya masomo tisa ya Sekondari kwa ajili ya kusaidia wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia katika shule za Ufundi Sekondari Moshi na Njombe Sekondari ya viziwi.
Wakiwa wenye nyuso za furaha, Faraja Nyalandu, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mkuu wa Shule Direct, Aneth Gerana na wengine kutoka Shule Direct na marafiki wa Shule Direct mara baada ya kumalizi mbio za kilometa 21.1 wakati wa Kili Marathon.

Namna bora ya kufundisha wanafunzi wenye ulemavu ni kuwafundisha wakiwa wamechanganyika darasa moja na wanafunzi wasio na ulemavu. Hii inamaanisha kwamba kwa wanafunzi wasiosikia ni muhimu walimu watakaofundisha hilo darasa wawe ni wataalamu wa lugha ya ishara ili waweze kufundisha kwa matamshi na ishara ili kukidhi mahitaji ya wote. Hii ni ngumu kwasababu si walimu wengi wenye utaalamu wa lugha ya ishara. Matokeo yake wale wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia wanaachwa nyuma bila kuelewa na hatimaye kufeli masomo yao.

Shule Direct ilitambua umuhimu wa kutafuta mifumo mingine ya kuwasaidia wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia, kuweza kujifunza. Masomo yakiwa ndani ya Kompyuta ni rahisi kwa mwanafunzi huyo kusoma na kujifunza katika kasi yake na kulingana na uelewa wake.
Hivyo, Shule Direct ikaazimia kushiriki mbio za Kili Marathon 2016 ili kuchangisha fedha kwa ajili ya Shule ya Sekondari ya Moshi Technical na Njombe Shule ya Sekondari ya Viziwi (Shule pekee ya Sekondari ya viziwi Tanzania). Fedha hizo ni kwa ajili ya kuwapatia ‘Content Lab’ kila shule. ‘Content Lab’ inakuwa na kompyuta 20, masomo tisa ya Shule Direct yaliyotengenezwa kwa mujibu wa ‘Syllabus’ ya Tanzania yanayowekwa moja kwa moja kwenye kompyuta hizo kurahisisha upatikana ji bila ‘internet’ na kamusi ya lugha ya ishara ya signwiki.

Tarehe 27 Februari 2016, Mgeni rasmi, Afisa Elimu wa Manispaa ya Moshi Bw. Deo Tulo Fundi akiwa na Afisa Elimu wa Elimu ya Mahitaji maalumu wa Manispaa ya Moshi, Bi. Joyce Sawuo walishuhudia awamu ya kwanza ya utoaji wa vifaa hivyo katika Shule ya Sekondari ya Moshi Tech.

Kabla ya makabidhiano hayo, timu ya ufundi ya Shule Direct iliweza kutoa mafunzo ya namna ya kutumia nyenzo hizo kwa walimu na wanafunzi wa Moshi Technical, hususan wale walimu wanaosimamia wanafunzi wenye ulemavu. 

Wakitoa shukrani zao za dhati wakiongozwa na Mwalimu Mkuu wa Moshi Tech Mwl. Erasmus Kyara na Mwalimu msimamizi wa anayesimamia mafunzo ya wanafunzi wenye ulemavu walielezea furaha yao kupata kompyuta hizo zenye nyenzo za kujifunzia, walisema kwa kipindi kirefu sasa wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia wamekuwa wakiwasindikiza tu wenzao kwa maana matokeo yao huwa hayavuki daraja la nne, wanakumbuka kwa jina, mwanafunzi mmoja tu mwenye ulemavu wa kusikia aliyewahi kupata daraja la tatu katika shule hiyo. 

Akiongea kwa niaba ya wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia shuleni hapo, mwanafunzi wa kidato cha nne, Raphael, alielezea furaha yake kuwa wanafunzi wenye tatizo kama lake wameweza kupatiwa msaada wa kompyuta zenye masomo zitakazowawezesha kujisomea na kuelewa masomo yao zaidi, alishukuru sana kupata nafasi ya kupata mafunzo ya vitendo ya jinsi kutumia kompyuta hizo, zaidi alishukuru kwa fursa ya pekee ya kukutanishwa na mwanadada Aneth Gerana ambaye aliongozana na timu ya Shule Direct. Aneth ni mtanzania wa kwanza mwenye ulemavu wa kusikia aliyefanikiwa kupata shahada ya Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam, naye ni miongoni mwa wadau waliojitokeza kujiunga na Shule Direct katika zoezi hili kwa kuwashirikisha wanafunzi maisha yake na kuwaasa kuwa wafanye bidii katika masomo yao ili waweze kufaulu katika maisha.

Zoezi la kusaidia wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia la Shule Direct lililopatiwa jina la #KiliShuleThon 2016 lilifanikishwa kwa kiasi kikubwa sana na mchango wa wadau mbali mbali wa elimu na maendeleo waliojitokeza kuchangia, pia zoezi hili liliwezeshwa kwa mchango mkubwa na ushirikiano na waandaaji wa Kili Marathon, Benki ya NMB, Freedom Computers Limited na Lensmark Studios.

CCM MKOA WA ARUSHA YAMCHAGUA LEKULE KUWA MWENYEKITI ,HUKU SHABANI MDOE AKIIBUKA KATIBU MWENEZI

March 03, 2016


SAM_7665
Mwenyekiti mpya wa ccm mkoa wa Arusha   Maiko Lekule aliyepata kura 515akizungumza mara baada ya kutangazwa mshindi wa kiti hicho hivi karibuni jijini Arusha(Habari  Picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
SAM_7696
Katibu mwenezi wa chama hicho Mkoa wa Arusha Shabani Mdoe aliyeshinda na fasi hiyo kwa kupata kura 36 ambaye kwa taaluma ni mwandishi wa habari akitoa neno la shukurani kwa wajumbe wa mkutano huo mara baadaa  ya kutangazwa rasmi kushinda nafasi hiyo
SAM_7636
Msimamizi wa uchaguzi huo ambaye ni mjumbe wa kamati kuu ya ccm taifa Stephen Wassiraakitangaza rasmi nafasi ya mwenyekiti wa mkoa ambapo pia aliwataka wanaccm kuhakikisha wanashirikiana
SAM_7656
Mjumbe wa NEC taifa toka wilaya ya Monduli Namelock Sokoine akizungumza katika mkutano huo mara baada ya uchaguzi kuisha ambapo aliwataka wanaccm kuchapa kazi na kuhakikisha wanawashuhulikia mamluki waliopo ndani ya chama hicho
SAM_7676
Mjumbe wa NEC taifa toka wilaya ya Monduli Namelock Sokoineakiteta jambo na Mbunge viti maalum Catherine Magige katika mkutano huo
SAM_7680
Emanuel Makongoro ambaye alikuwa akiwania nafasi wa uwenyekiti wa mkoa akifurahia jambo na katibu wa wazazi mkoa wa Arusha Mayasa Kimbau 
SAM_7689
Semi Kiondo ambaye alikuwa akiwania nafasi ya ukatibu mwenezi akizungumza mara baada ya uchaguzi kuisha ambapo alihaidi kutoa ushirikiano wake kwa chama cha mapinduzi huku akishirikiana na viongozi waliochaguliwa
SAM_7684
viongozi wa chama cha mapinduzi wakiwa katika pozi la picha
SAM_7630

Wajumbe wa mkutano
 CHAMA cha Mapinduzi ( CCM)mkoa wa arusha kimefanya uchaguzi wa mwenyekiti wa mkoa  na kufanikiwa kumchagua  Maiko Lekule aliyepata kura 515 dhidi ya mgombea mwenza Emanuel Makongoro aliyepata kura 338,huku katibu mwenezi wa chama hicho akichaguliwa kuwa ni Shabani Mdoe aliyeshinda na fasi hiyo kwa kupata kura 36.

Aidha katika uchaguzi huo wa mwenyekiti  wajumbe  halisi waliopaswa kuhudhuria  ni 960 ambapo waliohudhuria ni 903 huku wajumbe halisi waliopiga kura wakiwa ni 861.
Akitangaza matokeo hayo jana msimamizi wa uchaguzi huo ambaye ni mjumbe wa kamati kuu ya ccm taifa Stephen Wassira alisema kuwa uchaguzi huo umefanyika kwa huru na amani na hivyo ana imani kuwa uongozi huo utakiletea mabadiliko makubwa chama cha mapindizi katika mkoa huo.
Alisema kuwa katika mkoa wa arusha matatizo ya umoja  na tofauti yapo na kwamba atakayemaliza mzizi huo ni mwenyekiti aliyepatikana kwa kuhakikisha kuwa anawaunganisha wana ccm ili wawe kitu kimoja.
“hapa arusha yapo matatizo sana naomba tu nitumie fursa hii kumtaka mwenyekiti aliyeshinda kuhakikisha kuwa anakijenga chama na ndie atakayeifanya arusha iungwe mkono na watu wote hatutaki kusikia tena kuwepo kwa makundi ya kuvunja chama muda wa uongozi wa mwaka mmoja ni mkubwa sana katika kukirejesha chama sehemu yake”alisema Wassira.
Alileleza kuwa kwa arusha hawataki  kusikia ccm  inayoendeshwa kwa fedha ya mtu binafsi wala kampuni bali wanaitka ccm yao irudishe kwa wananchi na jamii iweze kunufaika na rasilimali zake sio kwa ajili ya watu binafs ambao  ndio wamekuwa wakikisaliti chama.
Kwa upande wake mwenyekiti aliyechaguliwa Maiko Lekule  akitoa neno la shukrani  alisema kuwa anawashukuru wajumbe hao kwa kumchagua na kwamba nafasi aliyopewa hataweza mwenyewe kuimaraisha chama hicho ambacho kipo mahututi hivyo anaomba ushirikiano uwepo.
Lekule alisema kuwa chama hicho kinahitaji kufanyiwa ukarabati mkubwa sana hivo kamati za siasa ,wenyeviti na kamati inabidi waungane kwa pamoja kukijenga chama hicho kwa upya ili kirudi katia hali yake.
“mimi nahidi tu ntakiimarisha chama hiki kwa kushirikiana na wenzangu ila niwaombe tu mamluki wote walioko kwenye hiki chama ambao ndio wasaliti wakuu waondoke mapema wenyewe na kama hawataondoka tutawaondoa sisi”alisema Lekule.

Nae katibu mwenezi Shabani mdoe ambaye ni mwandishi mwandamizi wa gazeti la Uhuru  aliwashukuru wajumbe hao kwa kumuamini kwa kumchagua na kuahidi kuwa atatumia taaluma yake ya uhabari kuimarisha chama hicho kwani waandishi wana nguvu kubwa ya kujenga palipobomoka.
MFUKO WA HIARI WA PSPF WANUFAISHA MAMIA YA WAKAZI WA UKONGA

MFUKO WA HIARI WA PSPF WANUFAISHA MAMIA YA WAKAZI WA UKONGA

March 03, 2016


Afisa Uendeshaji kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bw. Delphin Richard akizungumza na wananchi wa Ukonga pamoja na maeneo mengine ya mji wa Dar es Salaam kuhusu Mfuko wa Hiari wa PSPF wakati wa Semina ya Ujasiriamali Ukonga jana jijini Dar es Salaam.
Afisa Uendeshaji kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bw. Delphin Richard akifafanua jambo kwa wajasiriamali kuhusu Mfuko wa Hiari wa PSPF jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mjasiriamali kwanza Enterprises Dr. Didas Lunyungu.
Wajasiriamali kutoka maeneo ya Ukonga na maeneo mengine ya mji wa Dar es Salaam wakisikiliza kwa makini elimu iliyokuwa ikitolewa kuhusu uchangiaji wa hiari katika Mfuko wa Hiari wa PSPF wakati wa semina ya wajasiriamali jana jijini Dar es Salaam
Afisa Masoko kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bibi. Sarah Adebe akitoa elimu kwa wachangiaji wa hiari katika Mfuko wa Hiari wa PSPF wakati wa kuandikisha wachangiaji wapya wa mfuko huo jana jijini Dar es Salaam.
Afisa Masoko kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bibi. Sarah Adebe akitoa elimu kwa wachangiaji wa hiari katika Mfuko wa Hiari wa PSPF wakati wa kuandikisha wachangiaji wapya wa mfuko huo jana jijini Dar es Salaam.
Afisa kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bw. Mrisho Ngongo (kulia) akitoa fomu za kujisajiri kwa wachangiaji wapya wa hiari katika Mfuko wa Hiari wa PSPF jana jijini Dar es Salaam
Baadhi ya wanachama wa hiari katika Mfuko wa Hiari wa PSPF wakiwa katika mstari kwa ajili ya kukamilisha hatua za mwisho za kujisajiri katika mfuko huo jana jijini Dar es Salaam.
Afisa Masoko kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bibi. Sarah Adebe (kushoto) akikagua fomu za uanachama wa hiari katika Mfuko wa Hiari wa PSPF baada ya kusajili wanachama wapya jana jijini Dar es Salaam.Picha na: Genofeva Matemu – Maelezo
…………………………..

Na: Genofeva Matemu – Maelezo


Wananchi zaidi ya 500 kutoka zoni ya ukonga jijini Dar es Salaam wamejitokeza na kujisajiri kuwa wanachama wa hiari katika mfuko wa hiari wa PSPF ili kuweza kunufaika na mafao yatolewayo na mfuko huo.

Wananchi hao walipata fursa ya kujisajiri wakati wa semina ya ujasiriamali iliyofanyika siku ya jana maeneo ya Ukonga jijini Dar es Salaam na kuudhuriwa na wananchi wapatao 1600 kutoka zoni ya Ukonga na maeneo mengine ya jiji la Dar es Salaam na mikoa ya jirani.

Akizungumza wakati wa semina hiyo Afisa Uendeshaji kutoka Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) Bw. Delphin Richard amesema kuwa mfuko wa hiari wa PSPF uliundwa kwa ajili ya kutoa fursa kwa wananchi kuwa na akiba ya ziada kwa kutoa uhuru kwa mwanachama kuchangia kwa kutegemea upatikanaji wa kipato cha ziada kitakachomwezesha kujiwekea akiba.

Bw. Richard amesema kuwa lengo la PSPF ni kushiriki katika masuala mbalimbali ya kijamii ili kuweza kutoa elimu ya mfuko wa hiari wa PSPF hivyo kutoa nafasi kwa wajasiriamali, wakulima, wafugaji, wafanyabiashara, na watu binafsi kuchangia katika mfuko wa hiari kipato chao cha ziada kwa ajili ya akiba ya ziada.

Kwa upande wake Afisa Masoko Bibi. Sarah Adebe amesema kuwa jamii imekua na muitikio mkubwa wa kujisajiri katika mfuko wa hiari wa PSPF kwani mfuko huo unatoa huduma kwa kuchangia gharama ndogo hivyo kuwanufaisha wanachama hasa wa kipato cha chini.

Naye Mjasiriamali kutoka zoni ya Ukonga Bi. Doris Kimaro amesema kuwa ujio wa elimu ya mfuko wa hiari wa PSPF ni mafanikio makubwa katika familia yake kwani atatumia nafasi aliyoipata kwa kuchangia kipato chake cha ziada ili aweze kunufaika na fao la elimu litakalomuwezesha kukidhi mahitaji yake ya baadae.

Mfuko wa hiari wa PSPF umelenga kusaidia jamii kwa kuwa na mafao saba ambayo ni fao la elimu, fao la ujasiriamali, fao la uzeeni, fao la kifo, fao la ugonjwa/ulemavu, fao la kujitoa na fao la matibabu.

MFUMO DUME NI KIKWAZO CHA WANAWAKE KUTOKUMILIKI ARDHI - ANNA MGHWIRA

March 03, 2016
Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Anna Mghwira

Na Fredy Njeje-Blogs za Mikoa
Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Anna Mghwira amesema umiliki wa ardhi kwa wanawake hapa nchini bado unasuasua kutokana na mfumo dume uliopandikizwa tokea miaka ya nyuma.

Bi Mghwira ambaye alikuwa mwanamke pekee aliyegombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2015 kupitia ACT Wazalendo, ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Blogs za Mikoa kuhusu sababu za wanawake wengi nchini kutomiliki raslimali muhimu ya ardhi.

Kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2012 idadi ya wanawake hapa nchini ni asilimia 51% lakini wanaomiliki ardhi ni asilimia 19% tuu jambo ambalo linaonyesha wazi kuwa wanawake wengi bado hawamiliki ardhi ukilinganisha na wanaume.

''Tatizo lililopo hapa nchini ni tatizo la kitamaduni, ilikuwa kazi ya mwanamke akishazaliwa ni alelewe na baadaye akiolewa anaendeleza kizazi huko alikoolewa lakini kumiliki ardhi ni mfumo mpya ambao unatoa fursa sawa katika kumiliki raslimali hiyo muhimu kwa ajili ya kuitumia katika shughuli za kiuchumi''Amesema Mghwira.

Bi Mghwira ameenda mbali zaidi na kuona tatizo la umiliki wa ardhi pia lipo kwa upande wa wanaume hasa inapotokea suala la makubaliano na mwekezaji ndiyo maana kuna kesi nyingi kuhusiana na wawekezaji na wananchi katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
Baadhi ya wanaume waliopo katika mmoja ya Kijiji Wilayani Lushoto Mkoani Tanga wakiongea na Blogs za Mikoa kutoa maoni yao ya namna ambavyo walikuwa hawakubaliani na wanawake kumiliki Ardhi

Katika jitihada za kuunga mkono Serikali katika jitihada mbalimbali za kutatua kero kwa wananchi Bi Mghwira amesema kwamba mara kwa mara amekuwa akielimisha wanawake hapa nchini katika kutambua haki zao na kujikwamua na umasikini.

Hata hivyo ameitaka serikali kutizama upya sheria ya ardhi na pia kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na umiliki wa ardhi ili kuwezesha wananchi kutambua kuwa umiliki wa ardhi ni wa haki kwa pande zote kwa upande wa wanaume na wanawake.
Regards Tone Multimedia Company Limited Plot No.223/225 Block 46, Umoja Street Kijitonyama P.O Box 32529 Dar es salaam Tanzania Tel +255 22 2772919 Fax +255 22 2772892 E-Mail info@tonemg.com Facebook: www.facebook.com/blogszamikoa Web: www.tonemg.com