HOME GUARD FC, SMALL PRISON ZAAGA MASHINDANO ULINZI CUP TANGA
Na Oscar Assenga, TANGA.
TIMU za soka Small Prison na Home Guard zimeaga Mashindano ya Ulinzi Cup baada ya kila mmoja kufungwa katika mchezo wa hatua ya mtoano inayoendelea kwenye viwanja vya Ziwani Pongwe Jijini Tanga.
Mashindano hayo yanaratibiwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga yakiwa na lengo la kutoa elimu kwa vijana kujiepusha na vitendo vya uhalifu katika jamii wanazoishi ikiwemo kuwa mabalozi wa amani kwenye maeneo yao
Katika mchezo wa awali wa ufunguzi wa mashindano hayo timu ya soka TFC waliigaragaza Home Guard bao 1-0 bao ambalo lilifungwa na Mohamed Saidi dakika ya 5 hya mchezo huo ambao ulikuwa na upinzani.
Huku mchezo wa pili uliochezwa Agosti 21 mwaka huu timu ya Chote FC waliweza kuwapigisha kwata maafande wa Jeshi la Magereza Small Prison bao 1-0 ambalo lilifungwa na Boniface Majere dakika ya 47.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mashindano hayo,Diwani wa Kata ya Pongwe (CCM) Mbaraka Sadi alilipongeza Jeshi la Polisi kwa kazi kubwa anayoifanya kwa kuhakikisha Jeshi la Polisi linakuwa karibu na Jamii jambo ambalo ni muhimu katika kuhakikisha kuimarisha ulinzi.
Mbaraka alisema kwamba kufanyika kwa mashindano hayo katika maeneo mbalimbali yanasaidia na kuwawezesha vijana kuweza kuyatumia kama njia muhimu ya ajira,kujenga afya pamoja na kusaidia kuwaondoa vijana kwenye masuala ya uhalifu na dawa za kulevya na wanaamini mashindan hayo yatakuwa chachu kubwa ya kuinua vipaji vya wachezaji.
Naye kwa upande wake Mratibu wa Mashindano hayo Sophia Wakati alivitaka vilabu vinavyoshiriki kwenye mashindano hayo kuhakikisha wanazingatia sheria 17 za mpira wa miguuu zilizowekwa ikiwemo kuacha kuwachukia waamuzi.
“Lengo la Mashindano hayo ni kujenga undugu baina ya Jeshi la Polisi na Jamii lengo kujenga urafiki msijengeane chuki hakikisheni mnacheza kwa kuzingatia nidhamu ambayo itakuwa chachu ya mafanikio kwenye jambo lolote lile lakini msiwachukie waamuzi kutokana na kwamba wakati mwengine kunakuwa na makosa ya kibinadamu”Alisema
Naibu Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii avutiwa na Kamati ya Ulinzi wa Mtoto Stendi ya Nyegezi, Mwanza
MAJALIWA: TAASISI ZA SERIKALI ZINAZODAIWA NA TEMESA KUKIONA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Lazaro Kilahala, kuwasilisha Ofisini kwake orodha ya Taasisi zote za Serikali zinazodaiwa na Wakala huo ili aweze kuwaandikia baraua ya kusisitiza kulipa madeni yao.
TOENI ELIMU ZAIDI KWA WANANCHI JUU YA UGONJWA WA MPOX;WAZIRI MHAGAMA
Na WAF, Namanga- Arusha
Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Mhagama amewataka wataalamu wa Afya nchini kuongeza kasi ya kutoa elimu ya ugonjwa wa Mpox ili wananchi wawe na uelewa mpana dhidi ya ugonjwa huo.
Waziri Mhagama ametoa agizo hilo leo Agosti 21, 2024 wakati wa ziara kwenye Kituo cha Forodha cha Mpaka wa Namanga Halmashauri ya Wilaya ya Longido mkoani Arusha alipofika kuona utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa Mpox.
“ Nimezungumza na mmoja wa wasafiri lakini hajui dalili za za ugonjwa wa Mpox hivyo ipo haja ya kuongeza kasi ya utoaji elimu kwa wananchi ili kuwa na uelewa juu ya ugonjwa huo”, ameeleza Mhe. Mhagama na kuongeza
“Kuwe na mabango na vipeperushi vinavyotoa elimu juu ya ugonjwa kuelezea Dalili, unaambukizwaje na namna ya kujikinga ili kila msafiri anayeingia na kutoka nchini awe na uelewa mpana” amesisitiza Waziri Mhagama.
Mhe. Mhagama amesema kwa sasa mpaka Tanzania ni Salama na hakuna mgonjwa yeyote aliyebainika kuwa na ugonjwa huo hivyo wananchi waendelee kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa wa Mpox .
“ Natoa wito kwa wananchi kila mmoja awe mlinzi kwa mwenzake pale atakapo ona dalili za ugonjwa huo kwa mtu basi atoe taarfa kwa wataalamu wa afya, Kituo cha kutolea huduma za afya kilichopo karibu yake au kuwasiliana na Wizara ya Afya kwa Namba ya 199 ili kuhakikisha nchi inakuwa salama”, ametoa wito.
Akihitisha ziara yake Waziri Mhagama amewahakikishia watanzania kuwa Wizara yake imejipanga kikamilifu kwa kuimarisha Huduma za uchunguzi na maabara maeneop ya mipakani ili kuhakikisha ugonjwa huo hauingii nchini