Mkoa Wa Tanga Wajipanga Kutokomeza Vifo Vya Wamama Wajawazito

July 15, 2014


Serikali kwa kushirikiana na wadau wa afya imechukua hatua mbalimbali katika kuboresha huduma ya afya hususani katika kupunguza vifo vya akina mama wajawazito.
 Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa waTanga Mhe. Chiku Gallawa leo wakati akifungua Kikao cha mwaka cha tathmini ya namna ya kupunguza vifo vya akina mama na watoto chini yamiaka mitano kilichohusisha Wakuu wa Wilaya za Tanga, Wakurugezi na Waganga wa Wilaya kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mkuu wa Mkoa.
Amesema kuwa tatizo linalowakabili akinamama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano halina budi kupungua ikiwezekana kuzibitiwa kabisa.
Hatua zinazochukuliwa na Serikali ni pamoja na kutoa mafunzo kwa watendaji, kuongeza ajira za watumishi wa kada za afya na kuongeza upatikanaji wa dawa na vifaa tiba.
Wakichangia mada kwa wakati tofauti, watumishi kutoka kada ya afya wameishauri Serikali kuhakikikisha kuna kuwepo na vyumba vya kupumzikia wamamama wajawazito (Maternity home) kwenye vituo vya afya wakati wakisubiria kujifungua ili kupunguza uwezekano wa wamama hao kujifungulia majumbani/njiani.
Wananchi pia wameonywa kuacha tabia ya kuzipa nafasi mila na desturi ambao hupelekea ucheleweshwaji wa mama wajawazito kufikishwa katika vituo vya afya kwa mfano mama kutoa taarifa ya uchungu katika hatua ya mwisho .
 Mratibu wa Chanjo kutoka hospitali ya Rufaa ya Bombo Bw. Seif Shaibu akitoa mada inayohusu masuala ya chanjo 
Katibu Tawala Mkoa Tanga  Bw. Salum M. Chima  ( Alhaji ) akichangia mada
Washiriki wa Kikao


Mhe. Subira Mgalu, Mkuu wa Wilaya ya Muheza akichangia mada
Kaimu Mganga Mkuu Mkoa wa Tanga Dr. Asha Mahita akitoa ufafanuzi wa nini kifanyike ili kuboresha huduma za afya katika hospitali na vituo vya afya Mkoani Tanga