MATUKIO YA PICHA KATIKA FAINALI ZA MASHINDANO YA KOMBE LA MKONGE CUP LEO UWANJA WA MKWAKWANI

December 06, 2013


TAARIFA KUTOKA SHIRIKISHO LA SOKA TFF LEO

December 06, 2013
Release No. 206
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Desemba 6, 2013

TUMEJIANDAA VIZURI KWA MECHI- TANZANITE
Tanzanite imesema iko vizuri kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kwa wasichana wenye umri chini ya miaka 20 dhidi ya Afrika Kusini (Basetsana) inayochezwa kesho Jumamosi (Desemba 7 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kocha Mkuu wa Tanzanite, Rogasian Kaijage amesema wamejiandaa vizuri kwa mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili itakayochezwa kuanzia saa 10 kamili jioni.

KWAHERI MADIBA [1918-2013

KWAHERI MADIBA [1918-2013

December 06, 2013

-nelson-mandela

Leo hii dunia nzima inaomboleza kifo cha Nelson Mandela “Madiba”.Mandela ambaye alizaliwa tarehe 18 Julai mwaka 1918  huko Mvezo, Afrika Kusini amefariki akiwa na miaka 95.
Tangazo la kifo cha Mandela lilitolewa rasmi jana usiku [kwa saa za Afrika Kusini] na Rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma akisema;
“Our nation has lost its greatest son. Our people have lost a father. Although we knew that this day would come, nothing can diminish our sense of a profound and enduring loss, His tireless struggle for freedom earned him the respect of the world. His humility, his compassion and his humanity earned him their love”
 TANGA RAHA inaungana na watu wote duniani katika kuomboleza msiba huu mkubwa. Mandela alikuwa na atabia kuwa ishara au alama ya ushujaa, amani,demokrasia na utumishi wa umma uliotukuka.Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

*KIDUMU ATUA NCHINI KUWASHA MOTO CLUB E LEO

December 06, 2013

Msanii kutoka nchini Burundi, Jean Pierre “Kidum” akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julias Nyerere jana usiku kuja kutumbuiza katika Shererhe ya Kampuni ya Sigara Tanzania(TCC) “CLUB E” inayotarajiwa kufanyika leo katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Msanii kutoka nchini Burundi, Jean Pierre “Kidum”(kulia) akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julias Nyerere jana usiku kuja kutumbuiza katika Shererhe ya Kampuni ya Sigara Tanzania(TCC) “CLUB E” inayotarajiwa kufanyika leo katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Kushoto ni mwenyeji wake, Ather.
Msanii kutoka nchini Burundi, Jean Pierre “Kidum” (katikati) akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julias Nyerere jana usiku na waimbaji wake kuja kutumbuiza katika Shererhe ya Kampuni ya Sigara Tanzania(TCC) “CLUB E” inayotarajiwa kufanyika leo katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

KIGOMBE BINGWA WA KOMBE LA MKONGE CUP 2013

December 06, 2013


Na Oscar Assenga,Tanga.

TIMU ya Shamba la Mkonge la Kigombe mkoani Tanga leo wameibuka na ubingwa wa Kombe la Mkonge Cup mara baada ya kuibamiza China Farm ya Morogoro mabao 4-3 katika mchezo wa fainali uliochezwa kwenye dimba la soka Mkwakwani.



Katika mchezo ambao ulikuwa mkali na wenye upinzani mkubwa ambapo mpaka timu zote zinakwenda mapumziko hakuna timu iliyoweza kuona lango la mwenzie,kipindi cha pili kilianza kwa kasi ya mashambulizi kwa timu zote.



Wakionekana kujipanga na kujiimarisha vilivyo,Kigombe waliweza kufanya mashambulizi ya kushtukiza langoni mwa China Farm na kufanikiwa kuandika bao lao la kwanza dakika ya 56 kupitia Said Yasin kwa njia ya penati iliyotokana na mshambuliaji wa China Farm kumchezea faulu eneo la hatari Abdallah Maduba.


*MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA KIFO CHA MZEE MANDERA

December 06, 2013
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisaini kitabu cha maombolezo ya kifo cha Rais wa zamani wa Afrika ya Kusini, Nelson Mandera, aliyefariki usiku wa kuamkia leo wakati alipofika kwenye Ofisi za Ubalozi wa Afrika ya Kusini zilizopo Masaki  jijini Dar es salaam leo. Mzee Nelson Mandela (95) alifariki Dunia jana usiku nyumbani kwake Houghton, Jouhannesburg. Kushoto ni Balozi wa Afrika ya Kusini Nchini, Henry Thanduyise Chilize.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa heshima za mwisho mbele ya picha ya marehemu Nelson Mandera baada ya kusaini kitabu cha maombolezo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Afrika ya Kusini Nchini Tanzania, Henry Thanduyise Chiliza (kulia) na baadhi ya Viongozi wa Ubalozi huo kwenye ofisi za Ubalozi wa Afrika ya kusini Masaki jijini Dar es salaam leo, baada ya kusaini kitabu cha maombolezo.