WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI WAAGIZWA KUWA NA KIWANGO CHA UFAULU KUANZIA ASILIMIA 41

September 21, 2016
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe Deogratius Ndejembi akisisitiza jambo wakati wa kikao chake na Wakuu wa Shule za sekondari Wilayani humo

DC HANDENI.MH GONDWE AFANIKIWA KUTATUA MGOGORO WA MPAKA ULIOKUWA UKIVIHUSISHA VIJIJI VIWILI WILAYANI HANDENI

September 21, 2016

 Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Gdwin GOndwe akisalimiana na mkazi wa kijiji cha nyasa.

 Mkuu waa Wilaya ya Handeni,Mh Godwin Gondwe  Jana alifanikiwa kusuluhisha mgogoro wa mpaka uliokuwa ukivihusisha vijiji viwili vya kata ya kang'ata wilayani Handeni .Vijiji hivyo ni Madebe na Nyasa ambao walikua hawafahamu mpaka wao unaishia wapi,suluhu hiyo ilifanikiwa kumalizwa na mkuu wa wilaya na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Handeni ,Bwa.William Makufwe.

DC Gondwe pia aliwataka wananchi na viongozi wajikite katika shughuli za kimaendeleo badala ya kujikita kwenye suala la mipaka ,Kwa madai  wapate maeneo ya kulima wakati wakigombania maeneo ili wauze. Amewaonya wasiuze ardhi kiholela  na kufanya vizazi vijavyo kuwa watumwa kwenye ardhi yao.
 Mkuu wa wilaya Mh.Godwin Gondwe akimsikiliza Mkurugenzi mtendaji wa wilaya ya Handeni,Ndugu William Makufwe (pichani kushoto) akitoa ufafanuzi kwa wananchi wa vijiji vya nyasa na madebe.
 Mwenyekiti wa kijiji cha nyasa  na madebe wakipeana pongezi baada ya kujua mipaka yao huku wakisistizwa kujikita zaidi katika masuala ya maendeleo.
Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Gondwe akipeana mkono wa pongezi na Mwenyekiti wa kijiji cha Nyasa baada ya kupata mpaka wa maeneo yao.
Mkuu wa wilaya ya handeni Mh.Gondwe akizungumza na wananchi wa vijiji vya nyasa na madebe akiwakataza wasiuze ardhi kiholela na wasigombanie maeneo ili wayauze.

DC MTATURU: SERIKALI ITAVISAIDIA VIKUNDI VITAKAVYO KUWA TAYARI KUJIHUSISHA NA KILIMO CHA UMWAGILIAJI

September 21, 2016
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisisitiza umakini kwa wananchi waliojitokeza kwenye Kikao cha Mafunzo ya namna bora ya kushiriki katika kilimo chambogamboga na matunda kupitia umwagiliaji
Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ayub Sengo akiwasihi wananchi kutumia njia za kisasa katika kilimo cha umwagiliaji na kufuata taratibu wanazoelekezwa na wataalamu wa kilimo
Baadhi ya viongozi wa vikundi mbalimbali vya ujasiriamali sawia na wajumbe washiriki kwenye mafunzo hayo wakifatilia kwa makini Muelimishaji
Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya kiserikali ya RIWADE Mhandisi Ayubu Massau, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu, Moses Msai Mratibu wa RIWADE mkoa wa Singida na Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ayub Sengo
Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu na kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bi Haika Massawe wakifatiliakwa makini mafunzo ya namna bora ya kujishughulisha na kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia Gree House
Kutoka Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Hassan Tati, Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya kiserikali ya RIWADE Mhandisi Ayubu Massau, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bi Haika Massawe, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu, Moses Msai Mratibu wa RIWADE mkoa wa Singida na Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ayub Sengo
Dc Mtaturu akisisitiza jambo wakati wa kufunga mafunzo hayo

Na Mathias Canal, Singida

Uongozi wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida umeahidi kuvisaidia vikundi mbalimbali ambavyo vitakubali kujihusisha na kilimo cha mbogamboga na matunda (Perishable Crops) sambamba na kilimo hicho kwa kutumia Kitalu Nyumba (Green House).

Kauli ya serikali imetolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Miraji Jumanne Mtaturu wakati akifunga mafunzo kwa wajasiriamali, wakulima na wafugaji yaliyoendeshwa na Asasi isiyo ya kiserikali ya Right Way For Development (RIWADE) kwenye ukumbi wa Mikutano katika Shule ya Sekondari Ikungi na kuhudhuriwa na watu 115 ambao wanatokea katika Kata 24 kati ya Kata 28 zilizopo Wilayani humo.

Katika Mafunzo hayo jumla ya Vikundi 39 vimehudhuria ambavyo vimetakiwa kujishughulisha zaidi kukimbia kilimo cha mazoea ambacho wakulima hulima msimu mmoja hadi mwingine na hatimaye kujihusisha na kilimo cha umwagiliaji ambacho kinatumia muda mchache kukamilika na kuanza kwa mavuno.

DC Mtaturu amevitaka vikundi hivyo kwa pamoja kutumia vyema fursa ya Makao makuu ya serikali kuhamia Mjini Dodoma kwani itakuwa taswira chanya katika kukuza soko la mazao yao pasina kupata ugumu wa uuzaji.

Amesema kuwa Mkoa wa Singida mara nyingi umekuwa ukitajwa kama mkoa masikini nchini Tanzania kati ya mikoa 10 ambayo ipo mkiani katika maendeleo ya kiuchumi kwa sababu ya wananchi wenyewe kutofanya ubunifu katika kilimo chao jambo ambalo linasababisha uzalishaji mdogo na kupelekea kipato kuendelea kuwa duni ilihali maandalizi ya mashamba ni makubwa.

Mtaturu amesema kuwa wananchi wanapaswa kutoa ushirikiano kwa serikali katika kukamilisha adhma yake katika uwekezaji na Tanzania ya viwanda kwani endapo watakubali kulima kilimo cha kisasa na kuwa na uzalishaji mkubwa itakuwa rahisi kwa serikali kuanzisha viwanda vya kusindika mazao.

Kwa upande wake muwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya kiserikali ya RIWADE ambayo imesajili kwa lengo la kiwasaidia vijana wasio na ajira waweze kufanya kilimo, Ufugaji, Uvuvi na Mazingira Mhandisi Ayubu Massau alisema kuwa wananchi wanapaswa kufikia kilimo cha kuachana na kuuza mazao yao kwa madalali badala yake kuuza moja kwa moja kwa mtumiaji jambo ambalo litatoa fursa chanya ya mafanikio makubwa katika pato la mwananchi mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Hata hivyo amepigia chepuo zaidi kilimo cha Kitalu Nyumba (Green House) na kusema kuwa ndicho kilimo pekee chenye uwezo wa kuwatoa wananchi kwenye kadhia ya umasikini kwani kilimo hichp kupitia umwagiliaji wa kisasa unatumia maji machache na matokeo yake ni makubwa kama wakulima watafuata taratibu zote za utunzaji wa shamba.

Massau alisema kuwa umefika wakati wa wananchi kuachana na vyama vya kufa na kuzikana badala yake kujihusisha zaidi na vyama vya kujikwamua kiuchumi kupitia vikundi mbalimbali.

Naye Moses Msai ambaye ni Mratibu wa RIWADE mkoa wa Singida alisema kuwa wakulima wanapaswa kutambua kuwa sekta pekee yenye uwezo wa kuajiri watu wengi na kuwatoa kwenye lindi la umasikini ni Sekta ya Kilimo hivyo ni vyema kufanya kilimo cha kisasa kwani ndicho kitakacho wanufaisha wananchi.

Ametoa fursa kwa wananchi kujiunga na RIWADE kwani watapata fursa ya kuunganishwa na wataalamu ili kuelekezwa namna bora ya kulima kilimo cha umwagiliaji.

Hata hivyo Mjasiriamali na mkulima aliyeshika nafasi ya Kwanza kanda ya kati katika sekta ya kilimo Hassan Tati aliwasihi wakulima hao waliopatiwa mafunzo kuwa mafanikio kwenye kilimo ni makubwa endapo wakulima watafuata taratibu za kilimo na kuwasikiliza wataalamu.

Tati amesema kuwa hakuna ajira nzuri duniani kama kuwekeza kwenye kilimo lakini amewasihi wananchi kuing'ang'ania Asasi ya RIWADE kwani ni taasisi muhimu kwa kila mmoja kwa kujitolea kutoa mafunzo ya kilimo na ufugaji.

Asasi isiyo ya kiserikali ya Right Way For Development (RIWADE) ilianzishwa Mwezi June 2016, ikiwa ni dhima ya kutengeneza na kutoa fursa kwa watanzania wote ili waweze kupata elimu ya ujasiriamali na namna ya kutengeneza mitaji kwa ajili ya ukuaji endelevu wa kijamii na kiuchumi.

Kampuni ya Tigo yakabidhi madawati 435 mkoani Tanga leo

September 21, 2016



Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani, Goodluck Charles akiongea na wanahabari na wanafunzi ya shule ya msingi Mabawa leo, kwenye hafla ya kukabidhi madawati. Kushoto kwake ni mkuu wa wilaya ya Tanga, Thobias Mwilapwa, Katibu tawala wilaya ya Tanga Bi. Faidha Salim na kushoto ni Meneja wa Tigo mkoani Tanga, Patricia Sempinge






Katibu tawala wilaya ya Tanga Bi. Faidha Salim akiongea na wanahabari na wanafunzi ya shule ya msingi Mabawa leo, kwenye hafla ya kukabidhi madawati. Kulia kwake ni mkuu wa wilaya ya Tanga Mhe. Thobias Mwilapwa, Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani, Goodluck Charles na Meneja wa Tigo mkoani Tanga Patricia Sempinge. Na kushoto kwake mwalimu mkuu Zuwena Msembo.


Mkuu wa wilaya ya Tanga Mhe. Thobias Mwilapwa (kulia)akipokea  dawati toka kwa mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani, Goodluck Charles(kushoto). Katikati ni mwalimu mkuu wa shule ya mabawa, Zuwena Msembo, Jumla ya madawati 435 yenye thamani ya shilingi milioni 72  yalitolewa na kampuni ya Tigo mkoani Tanga kwenye hafla iliyofanyika shule ya msingi Mabawa leo.

Mkuu wa wilaya ya Tanga Mhe. Thobias Mwilapwa (kulia) akiwa ameketi na mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani(mwenye miwani) na wanafunzi  Amir Kibwana na Pili Ali(kushoto) wa shule ya msingi Mabawa, mara baada ya kampuni ya Tigo kukabidhiwa  435 yenye thamani ya shilingi milioni 72 kwa mkoa wa Tanga leo.


Wanafunzi wa shule ya msingi Mabawa mkoani Tanga wakiwa wameketi kwenye madawati .waliyokabidhiwa na kampuni ya Tigo leo

MADEREVA 10 WA TANZANIA WALIOTEKWA NCHINI CONGO WAREJEA NCHINI NA KUSEMA WALIPONEA TUNDU LA SINDANO KUUAWA

September 21, 2016
 Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Suzan Kolimba (katikati), akizungumza na madereva 10 wa Tanzania waliotekwa na watu wanaodaiwa kuwa ni waasi Jamhuri ya Demokrasia ya Conco (DRC), wakati wa hafla fupi ya kuwapokea iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam leo jioni. Kulia ni Balozi wa Congo nchini, Jean Mutamba na kushoto ni Mkurugenzi  Idara ya Afrika katika wizara hiyo, Balozi Samweli Shelukindo.
 Balozi wa Congo nchini, Jean Mutamba (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo.
 Mmiliki wa Kampuni ya Simba Logistic ambayo magari yake na madereva walitekwa, Azim Dewj (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo ya kuwapokea madereva hao.
 Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakisubiri kuchukua taarifa za kuwapokea madereva hao.
 Madereva hao wakipokelewa uwanjani hapo.
 Madereva hao wakiwa chumba cha mkutano cha uwanja huo wakati wa mapokezi yao.
Dereva  Mbwana Said (kulia), akielezea jinsi walivyotekwa.
 Dereva Kumbuka Seleman (kulia), akisimulia jinsi alivyotoroka na kutoa taarifa ya kutekwa kwao.
Dereva  Athuman Fadhili (kulia), akisimulia walivyookolewa na majeshi ya Congo na jinsi walivyojificha porini na kutembea umbali mrefu kwa kutambaa ambapo ilifika wakati waliomba bora wafe kuliko mateso waliyokuwa wakipata.
 Hapa ni furaha ya kukutana na ndugu jamaa na wafanyakazi wenzao.
 Picha ya pamoja na viongozi waliowapokea.
 Ndugu, Jamaa, marafiki na wafanyakazi wenzao wakiwa nje ya jengo la VIP uwanjani hapo wakisubiri kuwapokea.
 Mapokezi yakiendelea.
Ni furaha ya kukutana na wapendwa wao.
Hapa Dereva Mbwana Said akikumbatia na mjomba wake Kassim Salim katika hafla hiyo kwa Mbwana ilikuwa ni furaha na majonzi. 
Mbwana Said (katikati), aamini macho yake baada ya kukutana na mke wake Mariam pamoja na mtoto wake Kauzari.

Na Dotto Mwaibale

MADEREVA 10 wa Tanzania waliotekwa na watu  wanaodhaniwa ni waasi Jamhuri ya Demokraia ya Congo (DRC) wamesema waliponea tundu la sindano kuuawa.

Kauli hiyo imetolewa na madereva hao katika hafla ya kuwapokelewa iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam leo jioni.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake Mbwana Said alisema analishukuru jeshi la Congo kwa jitihada kubwa walioifanya kwa ajili ya kuokoa maisha yao." 

" Tunaishukuru serikali ya Congo kwa kutuokoa kwani tulikuwa katika wakati mgumu na leo kuungana tena na ndugu zetu" alisema Said.

Alisema walilazimia kutembea kwa muda mrefu huku risasi zikirindima kati ya majeshi ya serikali na waasi hao hadi walipofanikiwa kutuokowa kutoka kwenye mikono ya waasi hao. 

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Suzan Kolimba aliishukuru serikali ya Congo kwa jitihada iliyoifanya na kufanikiwa kuwaokoa madereva hao.

Balozi wa Congo nchini Jean Mutamba aliwataka madereva hao kuacha viza na nyaraka zao ubalozini pindi wanapo safiri na kurudi ili iwe rahisi kuwatambua pale wanapopata matatizo.

"Tukio hilo limetokea kwa bahati mbaya na kutoa wito kuwa waendelee kusafiri kwa kufuata taratibu zilizopo," alisema Mutamba.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712727062)

TAMKO KUHUSU TAKA HATARISHI

September 21, 2016


­­­­



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA MAKAMU WA RAIS




TANGAZO KWA UMMA
UZUIAJI WA UTUPAJI OVYO   USIO WA KITAALAMU WA TAKA ZA MAHOSPITALI.

Sheria ya usimamizi  wa Mazingira ya mwaka 2004  inapiga marufuku uchafuzi wa mazingira ikiwa ni pamoja na unaotokana na taka za mahospitali.  Aidha Kanuni za Taka Hatarishi za mwaka 2009, zinasisitiza utenganishi wa taka mbali mbali  zitokazo kwenye mahispotitali kwa kuzitibu katika namna ambayo haitaleta athari katika mazingira na afya ya binadamu. Pia Kanuni zinahimiza matumizi ya teknologia sahihi kama vile matumizi ya incinerators ambazo huchoma taka za mahospitali na  kuziteketeza kabisa.

 Ofisi yangu imefuatilia na kugundua kuwa taka nyingi za mahopitali, taka kutoka katika maduka ya  madawa zilizoisha muda wake zinatupwa ovyo  au kuharibiwa kwa utaratibu usio kubalika kitalaamu. Tumefuatalia na kukuta malundo ya madawa chakavu na vifaa vya hospitali vilivyotumika   katika maeneo ya visiwa vya Bongoyo na Mbudya. Aidha madawa chakavu yanatumpwa holela katika dampo la Pungu Kinyamwezi.  Hii ni hatari sana kwa mazingira na kwa afya ya binadamu. 

Kuanzia sasa ni marufuku  kutupa taka hizi katika utaratibu usio wa kawaida. Kila hospitali na zahanati  au kituo cha afya kihahakikishe kinatumia incinerators  au utaratibu mwingine ulio sahihi kwa mujibu wa sheria ya mazingira na kanuni zake. Aidha ninaiagiza NEMC kuanzia sasa wafanye msako mkali kubaini mahospitali na watu wanaokiuka agizo hili. Nimewapa mwezi mmoja na   kwa  wale wanaofanya hivyo waache mara moja.   Kwa msako huu atakayebainika kukiuka hatua kali za kisheria zinachukuliwa dhidi yake.

Nichukue fursa hii kutoa tena pole kwa wezentu wa Mkoa wa Kagera na maeneo ya jirani kwa athari za tetemeko la ardhi.
Baada ya tatetemeko kuna athari kubwa za kimazingira  ambazo zimejitokeza. Hivyo mimi binafsi ninafuatilia suala hili kwa ukaribu na kuhakikisha  athari ambazo zimejotokeza na zinazoendelea kujitokeza zinashughulikiwa kwa haraka.  Nimeagiza Ofisi yangu pamoja na NEMC washirikiane kwa ukaribu sana na watendaji wa Mkoa na Kamati mbalimbali zilizoundwa kushughulikia maafa haya na kufanya  tathmini  ya athari za mazingira zilizojitokeza na kuelekeza hatua za haraka kuchukuliwa ilikupunguza madhara kwa mazingira na binadamu.

Pia, napenda kutumia fursa hii  kuukumbusha umma  juu ya dhamira ya Serikali ya kupiga marufuku matumizi ya mifuko na vifungashio vya ya plastiki ifikapo Januari Mosi 2017.

Adhma ya Serikali ya kupiga marufuku matumizi ya mifuko  na vifungashio vya plastiki ni kuepusha athari za kiafya na mazingira zinazoendelea kujitokeza kutokana na matumizi ya mifuko hiyo. Hivyo basi wazalishaji, waagizaji, wasambazaji, wauzaji  na watumiaji  wa mifuko hiyo wanakumbushwa kuendelea na zoezi la kuondosha pamoja na kusitisha uzalishaji wa mifuko hii.


IMETOLEWA NA
JANUARY  Y. MAKAMBA (MB.)
WAZIRI WA NCHI OFISI YAMAKAMU WA RAIS
 MUUNGANO NA MAZINGIRA
21/9/2016 

RC KILIMANJARO SAID MECKY SADICK ATEMBELEA KIWANDA CHA TANGAWIZI

September 21, 2016
 Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadick akiwahutubia wananchi kwenye mkutano wake wa kazi alipozuru wilaya ya Same
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadick akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Wilaya ya Same kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki
 Wananchi wakisikiliza kwa makini mkutano wa mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro

WATU 283 WAJITOKEZA KUPIMA VVU/UKIMWI KWENYE MKESHA WA MWENGE WILAYANI IKUNGI

September 21, 2016
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akikimbia na baadhi ya watumishi wa Wilaya yake ishara ya kuukabidhi Mwenge wa uhuru Manispaa ya singida mara baada ya kumaliza mbio zake Wilayani Ikungi
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Ikungi Hassan Tati akizungumza wakati wa kuwashukuru wananchi kwa kujitokeza kupima Virusi Vya Ukimwi
Wananchi wa Manispaa ya Singida wakiusubiri Mwenge wa Uhuru kwa shauku kubwa muda mchache kabla ya kuwasili katika eneo lao ukitokea Wilaya ya Ikungi

MAJALIWA AZINDUA MPANGO MKAKATI NA MRADI WA MABORESHO YA HUDUMA ZA MAHAKAMA YA TANZANIA.

September 21, 2016


 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi  Evarest Ndikilo baada ya kuwasili kwenye eneo inapojenjwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Pwani na Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kuzindua Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania Septemba 21, 2016. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman  baada ya kuwasili kwenye eneo inapojenjwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Pwani na Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kuzindua Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania Septemba 21, 2016.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Naibu Spika wa Bunge  Dkt, Tulia Ackson baada ya kuwasili kwenye eneo inapojenjwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Pwani na Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kuzindua Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania Septemba 21, 2016. 
 Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarest Ndikilo akizungumza  katika   uzinduzi  Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania ulifanywa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini Kibaha Septemba 21, 2016.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji  akizungumza katika   uzinduzi  Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania ulifanywa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini Kibaha Septemba 21, 2016.

SERIKALI YAREJESHA ENEO LA HEKELI 50 KWA WANANCHI WA KIJIJI CHA KIPARA MPAKANI MKOANI PWANI.

September 21, 2016


 WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe (kulia) akisalimiana na Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, baada ya kuwasili katika kijiji cha Kipara Mpakani kwa ajili ya kukabidhi eneo la hekali 50 kwa wanakijiji hicho, Mkuranga, Mkoani Pwani.
 WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, akisaini kitabu cha wageni kabla ya mkutano na wanakijiji cha Kipara Mpakani. Kushoto ni Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega.
  Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, akihutubia wanakijiji cha Kipara Mpakani kabla ya Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Maghembe kukabidhi eneo la hekali 50 kwa kijiji hicho kwa ajili ya huduma za kijamii.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, akihutubia wanakijiji cha Kipara Mpakani katika mkutano huo kabla ya makabidhiano.
  Mzee wa Kijiji cha Kipara Mpakani akimshukuru Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe na Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, kwaniaba ya wanakijiji hicho.
 Wanakijiji wakimpongeza Mbunge wao, Ulega baada kufanikiwa kupewa eneo hilo la hekali 50.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe (kushoto) na Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, wakikata majani kuashiria kukabidhi rasmi eneo hilo kwa ajili ya huduma za kijamii.


Na Mwandishi Wetu.
SERIKALI imerejesha eneo la hekeli 50 Kwa wananchi wa kijiji cha kipara mpakani kilichopo Kata ya Mwandege,Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani ili wajenge huduma za kijamii.

Akikabidhi eneo hilo Waziri wa Maliasi na Utalii Profesa  Jumanne Maghembe aliwaeleza wananchi hao ambo walijitokeza Kwa wingi katika mkutano amesema kuwa wamponge Mbunge  wa Jimbo hilo Abdallah Ulega kwani amefanya jitihada kubwa za kuhakikisha Serikili inatoa Kwa wananchi eneo hilo.

Amesema kuwa wakati wako Bungeni mbunge huyo pamoja na baadhi viongozi wa kata  hiyo walikwenda Bungeni na kuiomba Serikali kuwapa eneo hilo ambapo lilikuwa pori tengefu la  maliasili ili wananchi wa kata ya Mwandege waweze kujenga Masoko.Shule,na miundombinu mingine.

"Nawapa eneo hili leo kwaniaba ya Serikali kwani najuwa Mh.rais Dkt.Magufuli wakati wakampeni alipita hapa nakuzungumzia eneo hili hivyo tunahitaji mjenge huduma mbalimbali na sio baadae watu wajitokeze na kusema eneo la kwenu."amesema Profesa Maghembe.

Naye Mbunge Ulega akizungumza katika mkutano huo amesema kuwa wananchi hao niwastaratibu kwani.mbali na kukosa maeneo ya kujenga huduma za jamii bado walikuwa wamekituza eneo hilo hadi leo Serikali wanapoamua kuwapa wananchi.