DC HANDENI.MH GONDWE AFANIKIWA KUTATUA MGOGORO WA MPAKA ULIOKUWA UKIVIHUSISHA VIJIJI VIWILI WILAYANI HANDENI
Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Gdwin GOndwe akisalimiana na mkazi wa kijiji cha nyasa.
Mkuu waa Wilaya ya Handeni,Mh Godwin Gondwe Jana alifanikiwa kusuluhisha mgogoro wa mpaka uliokuwa ukivihusisha vijiji viwili vya kata ya kang'ata wilayani Handeni .Vijiji hivyo ni Madebe na Nyasa ambao walikua hawafahamu mpaka wao unaishia wapi,suluhu hiyo ilifanikiwa kumalizwa na mkuu wa wilaya na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Handeni ,Bwa.William Makufwe.
DC Gondwe pia aliwataka wananchi na viongozi wajikite katika shughuli za kimaendeleo badala ya kujikita kwenye suala la mipaka ,Kwa madai wapate maeneo ya kulima wakati wakigombania maeneo ili wauze. Amewaonya wasiuze ardhi kiholela na kufanya vizazi vijavyo kuwa watumwa kwenye ardhi yao.
Mkuu wa wilaya Mh.Godwin Gondwe akimsikiliza Mkurugenzi mtendaji wa wilaya ya Handeni,Ndugu William Makufwe (pichani kushoto) akitoa ufafanuzi kwa wananchi wa vijiji vya nyasa na madebe.
Mwenyekiti wa kijiji cha nyasa na madebe wakipeana pongezi baada ya kujua mipaka yao huku wakisistizwa kujikita zaidi katika masuala ya maendeleo.
Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Gondwe akipeana mkono wa pongezi na Mwenyekiti wa kijiji cha Nyasa baada ya kupata mpaka wa maeneo yao.
Mkuu wa wilaya ya handeni Mh.Gondwe akizungumza na wananchi wa vijiji vya nyasa na madebe akiwakataza wasiuze ardhi kiholela na wasigombanie maeneo ili wayauze.
DC MTATURU: SERIKALI ITAVISAIDIA VIKUNDI VITAKAVYO KUWA TAYARI KUJIHUSISHA NA KILIMO CHA UMWAGILIAJI
Mkuu wa
Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisisitiza umakini kwa wananchi waliojitokeza kwenye Kikao cha Mafunzo ya namna bora ya kushiriki katika kilimo chambogamboga na matunda kupitia umwagiliaji
Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ayub Sengo akiwasihi wananchi kutumia njia za kisasa katika kilimo cha umwagiliaji na kufuata taratibu wanazoelekezwa na wataalamu wa kilimo
Baadhi ya viongozi wa vikundi mbalimbali vya ujasiriamali sawia na wajumbe washiriki kwenye mafunzo hayo wakifatilia kwa makini Muelimishaji
Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya
kiserikali ya RIWADE
Mhandisi Ayubu Massau, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Mkuu wa
Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu, Moses Msai Mratibu wa RIWADE
mkoa wa Singida na Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ayub Sengo
Kulia ni Mkuu wa
Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu na kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bi Haika Massawe wakifatiliakwa makini mafunzo ya namna bora ya kujishughulisha na kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia Gree House
Kutoka Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Hassan Tati, Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya
kiserikali ya RIWADE
Mhandisi Ayubu Massau, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bi Haika Massawe, Mkuu wa
Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu, Moses Msai Mratibu wa RIWADE
mkoa wa Singida na Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ayub Sengo
Dc Mtaturu akisisitiza jambo wakati wa kufunga mafunzo hayo
Na Mathias Canal, Singida
Uongozi wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida umeahidi kuvisaidia vikundi
mbalimbali ambavyo vitakubali kujihusisha na kilimo cha mbogamboga na
matunda (Perishable Crops) sambamba na kilimo hicho kwa kutumia Kitalu
Nyumba (Green House).
Kauli ya serikali imetolewa na Mkuu wa
Wilaya hiyo Mhe Miraji Jumanne Mtaturu wakati akifunga mafunzo kwa
wajasiriamali, wakulima na wafugaji yaliyoendeshwa na Asasi isiyo ya
kiserikali ya Right Way For Development (RIWADE) kwenye ukumbi wa
Mikutano katika Shule ya Sekondari Ikungi na kuhudhuriwa na watu 115
ambao wanatokea katika Kata 24 kati ya Kata 28 zilizopo Wilayani humo.
Katika Mafunzo hayo jumla ya Vikundi 39 vimehudhuria ambavyo vimetakiwa
kujishughulisha zaidi kukimbia kilimo cha mazoea ambacho wakulima
hulima msimu mmoja hadi mwingine na hatimaye kujihusisha na kilimo cha
umwagiliaji ambacho kinatumia muda mchache kukamilika na kuanza kwa
mavuno.
DC Mtaturu amevitaka vikundi hivyo kwa pamoja kutumia
vyema fursa ya Makao makuu ya serikali kuhamia Mjini Dodoma kwani
itakuwa taswira chanya katika kukuza soko la mazao yao pasina kupata
ugumu wa uuzaji.
Amesema kuwa Mkoa wa Singida mara nyingi umekuwa
ukitajwa kama mkoa masikini nchini Tanzania kati ya mikoa 10 ambayo ipo
mkiani katika maendeleo ya kiuchumi kwa sababu ya wananchi wenyewe
kutofanya ubunifu katika kilimo chao jambo ambalo linasababisha
uzalishaji mdogo na kupelekea kipato kuendelea kuwa duni ilihali
maandalizi ya mashamba ni makubwa.
Mtaturu amesema kuwa wananchi
wanapaswa kutoa ushirikiano kwa serikali katika kukamilisha adhma yake
katika uwekezaji na Tanzania ya viwanda kwani endapo watakubali kulima
kilimo cha kisasa na kuwa na uzalishaji mkubwa itakuwa rahisi kwa
serikali kuanzisha viwanda vya kusindika mazao.
Kwa upande wake
muwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya
kiserikali ya RIWADE ambayo imesajili kwa lengo la kiwasaidia vijana
wasio na ajira waweze kufanya kilimo, Ufugaji, Uvuvi na Mazingira
Mhandisi Ayubu Massau alisema kuwa wananchi wanapaswa kufikia kilimo cha
kuachana na kuuza mazao yao kwa madalali badala yake kuuza moja kwa
moja kwa mtumiaji jambo ambalo litatoa fursa chanya ya mafanikio makubwa
katika pato la mwananchi mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.
Hata
hivyo amepigia chepuo zaidi kilimo cha Kitalu Nyumba (Green House) na
kusema kuwa ndicho kilimo pekee chenye uwezo wa kuwatoa wananchi kwenye
kadhia ya umasikini kwani kilimo hichp kupitia umwagiliaji wa kisasa
unatumia maji machache na matokeo yake ni makubwa kama wakulima
watafuata taratibu zote za utunzaji wa shamba.
Massau alisema
kuwa umefika wakati wa wananchi kuachana na vyama vya kufa na kuzikana
badala yake kujihusisha zaidi na vyama vya kujikwamua kiuchumi kupitia
vikundi mbalimbali.
Naye Moses Msai ambaye ni Mratibu wa RIWADE
mkoa wa Singida alisema kuwa wakulima wanapaswa kutambua kuwa sekta
pekee yenye uwezo wa kuajiri watu wengi na kuwatoa kwenye lindi la
umasikini ni Sekta ya Kilimo hivyo ni vyema kufanya kilimo cha kisasa
kwani ndicho kitakacho wanufaisha wananchi.
Ametoa fursa kwa
wananchi kujiunga na RIWADE kwani watapata fursa ya kuunganishwa na
wataalamu ili kuelekezwa namna bora ya kulima kilimo cha umwagiliaji.
Hata hivyo Mjasiriamali na mkulima aliyeshika nafasi ya Kwanza kanda ya
kati katika sekta ya kilimo Hassan Tati aliwasihi wakulima hao
waliopatiwa mafunzo kuwa mafanikio kwenye kilimo ni makubwa endapo
wakulima watafuata taratibu za kilimo na kuwasikiliza wataalamu.
Tati amesema kuwa hakuna ajira nzuri duniani kama kuwekeza kwenye kilimo
lakini amewasihi wananchi kuing'ang'ania Asasi ya RIWADE kwani ni
taasisi muhimu kwa kila mmoja kwa kujitolea kutoa mafunzo ya kilimo na
ufugaji.
Asasi isiyo ya kiserikali ya Right Way For Development
(RIWADE) ilianzishwa Mwezi June 2016, ikiwa ni dhima ya kutengeneza na
kutoa fursa kwa watanzania wote ili waweze kupata elimu ya ujasiriamali
na namna ya kutengeneza mitaji kwa ajili ya ukuaji endelevu wa kijamii
na kiuchumi.
Kampuni ya Tigo yakabidhi madawati 435 mkoani Tanga leo
Wanafunzi wa shule ya msingi Mabawa mkoani Tanga wakiwa wameketi kwenye madawati .waliyokabidhiwa na kampuni ya Tigo leo |
MADEREVA 10 WA TANZANIA WALIOTEKWA NCHINI CONGO WAREJEA NCHINI NA KUSEMA WALIPONEA TUNDU LA SINDANO KUUAWA
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Suzan Kolimba (katikati), akizungumza na madereva 10 wa Tanzania waliotekwa na watu wanaodaiwa kuwa ni waasi Jamhuri ya Demokrasia ya Conco (DRC), wakati wa hafla fupi ya kuwapokea iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam leo jioni. Kulia ni Balozi wa Congo nchini, Jean Mutamba na kushoto ni Mkurugenzi Idara ya Afrika katika wizara hiyo, Balozi Samweli Shelukindo.
Balozi wa Congo nchini, Jean Mutamba (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo.
Mmiliki wa Kampuni ya Simba Logistic ambayo magari yake na madereva walitekwa, Azim Dewj (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo ya kuwapokea madereva hao.
Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakisubiri kuchukua taarifa za kuwapokea madereva hao.
Madereva hao wakipokelewa uwanjani hapo.
Madereva hao wakiwa chumba cha mkutano cha uwanja huo wakati wa mapokezi yao.
Dereva Mbwana Said (kulia), akielezea jinsi walivyotekwa.
Dereva Kumbuka Seleman (kulia), akisimulia jinsi alivyotoroka na kutoa taarifa ya kutekwa kwao.
Dereva Athuman Fadhili (kulia), akisimulia walivyookolewa na majeshi ya Congo na jinsi walivyojificha porini na kutembea umbali mrefu kwa kutambaa ambapo ilifika wakati waliomba bora wafe kuliko mateso waliyokuwa wakipata.
Hapa ni furaha ya kukutana na ndugu jamaa na wafanyakazi wenzao.
Picha ya pamoja na viongozi waliowapokea.
Ndugu, Jamaa, marafiki na wafanyakazi wenzao wakiwa nje ya jengo la VIP uwanjani hapo wakisubiri kuwapokea.
Mapokezi yakiendelea.
Ni furaha ya kukutana na wapendwa wao.
Hapa Dereva Mbwana Said akikumbatia na mjomba wake Kassim Salim katika hafla hiyo kwa Mbwana ilikuwa ni furaha na majonzi.
Mbwana Said (katikati), aamini macho yake baada ya kukutana na mke wake Mariam pamoja na mtoto wake Kauzari.
Na Dotto Mwaibale
MADEREVA 10 wa Tanzania waliotekwa na watu wanaodhaniwa ni waasi Jamhuri ya Demokraia ya Congo (DRC) wamesema waliponea tundu la sindano kuuawa.
Kauli hiyo imetolewa na madereva hao katika hafla ya kuwapokelewa iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam leo jioni.
Akizungumza kwa niaba ya wenzake Mbwana Said alisema analishukuru jeshi la Congo kwa jitihada kubwa walioifanya kwa ajili ya kuokoa maisha yao."
" Tunaishukuru serikali ya Congo kwa kutuokoa kwani tulikuwa katika wakati mgumu na leo kuungana tena na ndugu zetu" alisema Said.
Alisema walilazimia kutembea kwa muda mrefu huku risasi zikirindima kati ya majeshi ya serikali na waasi hao hadi walipofanikiwa kutuokowa kutoka kwenye mikono ya waasi hao.
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Suzan Kolimba aliishukuru serikali ya Congo kwa jitihada iliyoifanya na kufanikiwa kuwaokoa madereva hao.
Balozi wa Congo nchini Jean Mutamba aliwataka madereva hao kuacha viza na nyaraka zao ubalozini pindi wanapo safiri na kurudi ili iwe rahisi kuwatambua pale wanapopata matatizo.
"Tukio hilo limetokea kwa bahati mbaya na kutoa wito kuwa waendelee kusafiri kwa kufuata taratibu zilizopo," alisema Mutamba.
(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712727062)
(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712727062)
TAMKO KUHUSU TAKA HATARISHI
OFISI YA MAKAMU WA RAIS
TANGAZO KWA UMMA
UZUIAJI WA UTUPAJI
OVYO USIO WA KITAALAMU WA TAKA ZA
MAHOSPITALI.
Sheria ya usimamizi wa
Mazingira ya mwaka 2004 inapiga marufuku
uchafuzi wa mazingira ikiwa ni pamoja na unaotokana na taka za mahospitali. Aidha Kanuni za Taka Hatarishi za mwaka 2009, zinasisitiza utenganishi wa taka mbali mbali zitokazo kwenye mahispotitali kwa kuzitibu
katika namna ambayo haitaleta athari katika mazingira na afya ya binadamu. Pia
Kanuni zinahimiza matumizi ya teknologia sahihi kama vile matumizi ya incinerators
ambazo huchoma taka za mahospitali na kuziteketeza
kabisa.
Ofisi yangu imefuatilia na kugundua
kuwa taka nyingi za mahopitali, taka kutoka katika maduka ya madawa zilizoisha muda wake zinatupwa
ovyo au kuharibiwa kwa utaratibu usio kubalika
kitalaamu. Tumefuatalia na kukuta malundo ya madawa chakavu na vifaa vya
hospitali vilivyotumika katika maeneo
ya visiwa vya Bongoyo na Mbudya. Aidha madawa chakavu yanatumpwa holela katika
dampo la Pungu Kinyamwezi. Hii ni hatari
sana kwa mazingira na kwa afya ya binadamu.
Kuanzia sasa ni marufuku kutupa
taka hizi katika utaratibu usio wa kawaida. Kila hospitali na zahanati au kituo cha afya kihahakikishe kinatumia
incinerators au utaratibu mwingine ulio
sahihi kwa mujibu wa sheria ya mazingira na kanuni zake. Aidha ninaiagiza NEMC
kuanzia sasa wafanye msako mkali kubaini mahospitali na watu wanaokiuka agizo
hili. Nimewapa mwezi mmoja na kwa wale wanaofanya hivyo waache mara moja. Kwa msako huu atakayebainika kukiuka hatua
kali za kisheria zinachukuliwa dhidi yake.
Nichukue fursa hii kutoa tena pole kwa wezentu wa Mkoa wa Kagera na
maeneo ya jirani kwa athari za tetemeko la ardhi.
Baada ya tatetemeko kuna athari kubwa za kimazingira ambazo zimejitokeza. Hivyo mimi binafsi
ninafuatilia suala hili kwa ukaribu na kuhakikisha athari ambazo zimejotokeza na zinazoendelea
kujitokeza zinashughulikiwa kwa haraka.
Nimeagiza Ofisi yangu pamoja na NEMC washirikiane kwa ukaribu sana na
watendaji wa Mkoa na Kamati mbalimbali zilizoundwa kushughulikia maafa haya na
kufanya tathmini ya athari za mazingira zilizojitokeza na
kuelekeza hatua za haraka kuchukuliwa ilikupunguza madhara kwa mazingira na
binadamu.
Pia, napenda kutumia fursa hii kuukumbusha
umma juu ya dhamira ya Serikali ya
kupiga marufuku matumizi ya mifuko na vifungashio vya ya plastiki ifikapo
Januari Mosi 2017.
Adhma ya Serikali ya kupiga marufuku matumizi ya mifuko na vifungashio vya plastiki ni kuepusha athari
za kiafya na mazingira zinazoendelea kujitokeza kutokana na matumizi ya mifuko
hiyo. Hivyo basi wazalishaji, waagizaji, wasambazaji, wauzaji na watumiaji wa mifuko hiyo wanakumbushwa kuendelea na zoezi
la kuondosha pamoja na kusitisha uzalishaji wa mifuko hii.
IMETOLEWA NA
JANUARY Y. MAKAMBA (MB.)
WAZIRI WA NCHI OFISI
YAMAKAMU WA RAIS
MUUNGANO NA MAZINGIRA
21/9/2016
RC KILIMANJARO SAID MECKY SADICK ATEMBELEA KIWANDA CHA TANGAWIZI
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadick akiwahutubia wananchi kwenye mkutano wake wa kazi alipozuru wilaya ya Same
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadick akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Wilaya ya Same kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki
Wananchi wakisikiliza kwa makini mkutano wa mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro
WATU 283 WAJITOKEZA KUPIMA VVU/UKIMWI KWENYE MKESHA WA MWENGE WILAYANI IKUNGI
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akikimbia na baadhi ya watumishi wa Wilaya yake ishara ya kuukabidhi Mwenge wa uhuru Manispaa ya singida mara baada ya kumaliza mbio zake Wilayani Ikungi
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Ikungi Hassan Tati akizungumza wakati wa kuwashukuru wananchi kwa kujitokeza kupima Virusi Vya Ukimwi
Wananchi wa Manispaa ya Singida wakiusubiri Mwenge wa Uhuru kwa shauku kubwa muda mchache kabla ya kuwasili katika eneo lao ukitokea Wilaya ya Ikungi
MAJALIWA AZINDUA MPANGO MKAKATI NA MRADI WA MABORESHO YA HUDUMA ZA MAHAKAMA YA TANZANIA.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi
Evarest Ndikilo baada ya kuwasili kwenye eneo inapojenjwa Mahakama ya
Hakimu Mkazi wa Pwani na Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kuzindua Mpango
Mkakati na Mradi wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania
Septemba 21, 2016.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed
Chande Othman baada ya kuwasili kwenye eneo inapojenjwa Mahakama ya
Hakimu Mkazi wa Pwani na Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kuzindua Mpango
Mkakati na Mradi wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania
Septemba 21, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Naibu Spika wa Bunge Dkt, Tulia Ackson baada
ya kuwasili kwenye eneo inapojenjwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Pwani
na Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kuzindua Mpango Mkakati na Mradi wa
Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania Septemba 21, 2016.
Mkuu
wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarest Ndikilo akizungumza katika
uzinduzi Mpango Mkakati na Mradi wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya
Tanzania ulifanywa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini Kibaha
Septemba 21, 2016.
Naibu
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji akizungumza katika
uzinduzi Mpango Mkakati na Mradi wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya
Tanzania ulifanywa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini Kibaha
Septemba 21, 2016.
SERIKALI YAREJESHA ENEO LA HEKELI 50 KWA WANANCHI WA KIJIJI CHA KIPARA MPAKANI MKOANI PWANI.
WAZIRI
wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe (kulia) akisalimiana
na Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, baada ya kuwasili katika kijiji
cha Kipara Mpakani kwa ajili ya kukabidhi eneo la hekali 50 kwa
wanakijiji hicho, Mkuranga, Mkoani Pwani.
WAZIRI
wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, akisaini kitabu cha
wageni kabla ya mkutano na wanakijiji cha Kipara Mpakani. Kushoto ni
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega.
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, akihutubia wanakijiji cha Kipara
Mpakani kabla ya Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Maghembe
kukabidhi eneo la hekali 50 kwa kijiji hicho kwa ajili ya huduma za
kijamii.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, akihutubia wanakijiji cha Kipara Mpakani katika mkutano huo kabla ya makabidhiano.
Mzee
wa Kijiji cha Kipara Mpakani akimshukuru Waziri wa Maliasili na Utalii,
Profesa Jumanne Maghembe na Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega,
kwaniaba ya wanakijiji hicho.
Wanakijiji wakimpongeza Mbunge wao, Ulega baada kufanikiwa kupewa eneo hilo la hekali 50.
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe (kushoto) na Mbunge wa
Mkuranga, Abdallah Ulega, wakikata majani kuashiria kukabidhi rasmi
eneo hilo kwa ajili ya huduma za kijamii.
Na Mwandishi Wetu.
SERIKALI
imerejesha eneo la hekeli 50 Kwa wananchi wa kijiji cha kipara mpakani
kilichopo Kata ya Mwandege,Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani ili wajenge
huduma za kijamii.
Akikabidhi
eneo hilo Waziri wa Maliasi na Utalii Profesa Jumanne Maghembe
aliwaeleza wananchi hao ambo walijitokeza Kwa wingi katika mkutano
amesema kuwa wamponge Mbunge wa Jimbo hilo Abdallah Ulega kwani
amefanya jitihada kubwa za kuhakikisha Serikili inatoa Kwa wananchi eneo
hilo.
Amesema
kuwa wakati wako Bungeni mbunge huyo pamoja na baadhi viongozi wa kata
hiyo walikwenda Bungeni na kuiomba Serikali kuwapa eneo hilo ambapo
lilikuwa pori tengefu la maliasili ili wananchi wa kata ya Mwandege
waweze kujenga Masoko.Shule,na miundombinu mingine.
"Nawapa
eneo hili leo kwaniaba ya Serikali kwani najuwa Mh.rais Dkt.Magufuli
wakati wakampeni alipita hapa nakuzungumzia eneo hili hivyo tunahitaji
mjenge huduma mbalimbali na sio baadae watu wajitokeze na kusema eneo la
kwenu."amesema Profesa Maghembe.
Naye
Mbunge Ulega akizungumza katika mkutano huo amesema kuwa wananchi hao
niwastaratibu kwani.mbali na kukosa maeneo ya kujenga huduma za jamii
bado walikuwa wamekituza eneo hilo hadi leo Serikali wanapoamua kuwapa
wananchi.
Subscribe to:
Posts (Atom)