WAZAZI SAFI

April 14, 2013
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi chama cha Mapinduzi taifa,Abdallah Bulembo akisalimiana na wanachama wa chama hicho mkoani Tanga mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Mkwakwani akifuatiwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi mkoa wa Tanga,Dr,Edmund Mndolwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga,Gustav Mubba,Picha na Mwandishi Wetu.

WAZAZI SAFI.

April 14, 2013
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa,Abdalla Bulembo akisailiana na viongozi mbalimbali wa chama hicho mkoani Tanga na Pemba mara baada ya kuwasili mkoani Tanga wakati wa maadhimisho ya wiki ya Wazazi ambapo kitaifa ilifanyika uwanja wa Tangamano jijini Tanga,Picha na Mwandishi Wetu,Tanga.
Kampira:Mgambo haitishiki na Yanga.

Kampira:Mgambo haitishiki na Yanga.

April 14, 2013
Na Oscar Assenga, Tanga.

KOCHA Mkuu wa timu ya Mgambo Shooting, Mohamed Kampira amesema mchezo wao wa Dar es Salaam Yanga Africa hauwapa wasiwasi wale kuwanyima usingizi kwani kwao wanauona kama mchezo wa kawaida katika ligi hiyo.

Kampira aliyasema hayo jana mara baada ya kumalizika kwa mazoezi yao ya asubuhi ambapo alisema maandalizi ya mechi hiyo licha ya wapenzi na mashabiki wa soka hapa nchini kuitabiria kuwa itakuwa ni ngumu lakini wao wanaiona kama yakawaida sana kutokana na uimara wa kikosi chao.

Alisema kuwa kikosi hicho hivi sasa kipo imara kwa ajili ya kupambana na timu yoyote ili iweze kutimiza malengo yao ambayo wamejiwekea ya kuhakikisha wanamalizia ligi hiyo wakiwa kwenye nafasi tano za juu kwenye msimamo.

    “Sisi tunajua Yanga ina ubora wake wanawachezaji wakulipwa na makocha lakini vyote hivyo haviwezi kutuzuia kuchukua pointi tatu muhimu mbele yao wani nasi pia tumejipanga na kujithatiti kikamilifu katika mechi hiyo “Alisema Kampira.

Kocha huyo alisema kile wachezaji wake waliochokifanya kwenye mechi yao na Simba kwenye mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo watazidisha zaidi yake ili kuhakikisha timu hiyo inapata ushindi wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani.

Wakati huo huo, Umoja wa Wanachama wa Klabu ya Yanga mkoa wa Tanga umeanza shamra shamra za kuwapokea viongozi wa timu hiyo ambao watawasili mkoani hapa siku moja kabla ya kuchezwa mechi hiyo ambayo inatarajiwa kuwa yenye ushindani mkubwa.

Akizungumza na gazeti hili,Katibu wa Matawi ya Yanga mkoa wa Tanga,David Manyilizu alisema mapokezi ya viongozi hao yanatarajiwa kufanyika katika njia ya Panda ya Segera wilayani Handeni na Pongwe jijini Tanga ambapo wapenzi na wanachama wa klabu hiyo wataungana ili kuilaki timu yao.

Mwisho.