Mhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Amina Sanga akitoa mada kwenye kongamano la siku moja la vijana wasomi kutoka makanisa mbalimbali ya kikristo lilifanyika Hoteli ya Landmark jijini Dar es Salaam jana lenye lengo wasomi hao kutumia taaluma walizonazo katika kuitumikia jamii na taifa kwa ujumla.
Vijana wasomi wakiwa kwenye kongamano hilo.
Kongamano likiendelea.
Wanakwaya wa Haleluya Celebration wakiwa kwenye kongamano hilo.
Muonekano wa ukumbi katika kongamano hilo.
Meza kuu katika kongamano hilo. Kutoka kulia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Philip Sanga, Mgeni rasmi wa Kongamano hilo, Askofu Mkuu wa Kanisa la Abundant Bressing Centre (ABC), Flaston Ndabila , Mchungaji John Kanafunzi na Mratibu wa kongamano hilo, Ephraim Mwambapa.
Wanakwaya wa Haleluya Celebration wakitoa burudani ya nyimbo za kusifu.
Burudani ikiendelea.
Maombi yakifanyika.
Waratibu wa kongamano hilo wakijitambulisha. Kutoka kushoto ni Sarafina Kabwe, Irene Sadock, Michael Mhagama na Yona Kilindu.
Katibu Mkuu wa Kongamano hilo, Lendian Bigoli, akitoa mada.
Mratibu wa Kongamano hilo, Ephraim Mwambapa akitoa mada katika kongamano hilo.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Abundant Bressing Centre (ABC), Flaston Ndabila, akizungumza kwenye kongamano hilo.
Maombi yakifanyika.
Maombi yakiendelea.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Dk.Philip Sanga akihutubia kwenye kongamano hilo.
Mgeni rasmi wa kongamano hilo,Askofu Mkuu wa Kanisa la Abundant Bressing Centre (ABC), Flaston Ndabila akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine na waratibu wa kongamano hilo.
Picha ya pamoja
Na Dotto Mwaibale
Na Dotto Mwaibale
ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Abundant Bressing Centre (ABC), Flaston Ndabila amewataka Vijana wasomi na wanataalumu nchini kumsaidia Rais Dk.John Magufuli kuliletea Taifa maendeleo.
Ndabila ametoa mwito huo jijini Dar es Salaam jana wakati akiwahutubia wasomi wanataaluma katika kongamano la siku moja la vijana wasomi kutoka makanisa mbalimbali ya kikristo lilifanyika Hoteli ya Landmark lenye lengo kwa wasomi hao kutumia taaluma walizonazo katika kuitumikia jamii na taifa kwa ujumla.
"Ninyi wasomi mmesomeshwa kwa ajili ya kuwatumia wananchi na taifa msaidieni Rais wetu John Magufuli kuliletea taifa la Tanzania na kanisa maendeleo kwani hakuna mtu mwingine tunaye mtegemea zaidi yenu" alisema Askofu Ndabila.