Katibu
Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia) akiwa na
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Malawi,
Burundi na Msumbiji Bi. Bella Bird, wakielekea kusaini Mkataba wa mkopo
nafuu wa Dola za Marekani milioni 150 (Sh. bilioni 340) kwa ajili ya
kufungua utalii katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania, Jijini Dar es
Salaam
Baadhi
ya Maafisa waandamizi wa Wizara ya Fedha na Mipango, na Katibu Mkuu
Wizara ya maliaasili na Utalii( wa kwanza kushoto) wakifuatilia kwa
makini tukio la kusainiwa kwa Mkataba wa mkopo nafuu wa Dola za Marekani
milioni 150 (Sh. bilioni 340) kwa ajili ya kufungua utalii katika
Ukanda wa Kusini mwa Tanzania, Jijini Dar es Salaam.
Sehemu
ya Ujumbe wa Benki ya Dunia walioshiriki tukio la Tanzania na Benki
hiyo kutiliana saini mkataba wa mkopo nafuu wa Dola za Marekani milioni
150 (Sh. bilioni 340) kwa ajili ya kufungua utalii katika Ukanda wa
Kusini mwa Tanzania, Jijini Dar es Salaam
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi,
akitoa neon la shukurani wakati wa kusainiwa kwa Mkataba wa Mkopo Nafuu
kati ya Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia wenye thamani ya Dola za
Marekani milioni 150 (Sh. bilioni 340) kwa ajili ya kufungua utalii
katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania, Jijini Dar es Salaam. Kulia kwake
ni Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Malawi,
Burundi na Msumbiji Bi. Bella Bird.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (wa pili kulia) na
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Malawi,
Burundi na Msumbuji, Bi. Bella Bird, wakisaini Mkataba wa Mkopo wenye
masharti nafuu wa Sh. Dola za Marekani milioni 150 sawa na Shilingi
bilioni 340 kwa ajili ya Mradi wa kuibua fursa za Utalii Ukanda wa
Kusini mwa Tanzania, huku Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Meja
Jenerali Gaudence Milanzi (wa pili kulia waliosimama-tai nyekundu)
akishuhudia, katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es
Salaam.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (wa pili kulia) na
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Malawi,
Burundi na Msumbuji, Bi Bella Bird, wakisaini Mkataba wa Mkopo wenye
masharti nafuu wa Sh. Dola za Marekani milioni 150 sawa na Shilingi
bilioni 340 kwa ajili ya Mradi wa kuibua fursa za Utalii Ukanda wa
Kusini mwa Tanzania, katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini
Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa-TANAPA, Bw. Allan Kijazi na
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Malawi,
Burundi na Msumbuji, Bi Bella Bird, wakisaini Makubaliano ya utekelezaji
wa Mkataba wa Mradi wa kuibua fursa za Utalii Ukanda wa Kusini mwa
Tanzania utakao gharimu Shilingi bilioni 340 zilizotolewa kama mkopo
wenye masharti nafuu na Benki hiyo kwa Tanzania, Ofisi za Wizara ya
Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa-TANAPA, Bw. Allan Kijazi na
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Malawi,
Burundi na Msumbuji, Bi Bella Bird, wakisaini Makubaliano ya utekelezaji
wa Mkataba wa Mradi wa kuibua fursa za Utalii Ukanda wa Kusini mwa
Tanzania utakao gharimu Shilingi bilioni 340 zilizotolewa kama mkopo
wenye masharti nafuu na Benki hiyo kwa Tanzania, Ofisi za Wizara ya
Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia nyuma ni Katibu
Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James, (wa pili kulia
waliosimama akifuatiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Meja
Jenerali Gaudence Milanzi, Jijini Dar es Salaam.
Katibu
Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia) na Mwakilishi
Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Malawi, Msumbiji na
Burundi Bi. Bella Bird (kushoto) wakibadilishana Mkataba wa Mkopo wenye
masharti nafuu wa Sh. bilioni 340 kwa ajili ya Mradi wa kuibua fursa za
Utalii katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania, katika Ukumbi wa Wizara ya
Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Katibu
Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia) na Mwakilishi
Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Malawi, Msumbiji na
Burundi Bi. Bella Bird (kushoto) wakibadilishana Mkataba wa Mkopo wenye
masharti nafuu wa Sh. bilioni 340 kwa ajili ya Mradi wa kuibua fursa za
Utalii katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania, katika Ukumbi wa Wizara ya
Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Katibu
Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia) na Mwakilishi
Mkazi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Malawi, Msumbiji na
Burundi Bi. Bella Bird (kushoto) wakionesha Mkataba wa Mkopo wenye
masharti nafuu wa Sh. bilioni 340 kwa ajili ya Mradi wa kuibua fursa za
Utalii katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania, baada ya kusainiwa katika
Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango)
Benny Mwaipaja, Dar es Salaam
BENKI
ya Dunia imeipatia Tanzania Mkopo wenye masharti nafuu wa Dola za
Marekani milioni 150, sawa na takriban Shilingi bilioni 340 kwa ajili ya
kutekeleza mradi mkubwa wa kufungua fursa za utalii katika Ukanda wa
Kusini mwa Tanzania.
Mkataba
wa mkopo huo umetiwa saini Jijini Dar es Salaam kati ya Katibu Mkuu
Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James na Mwakilishi Mkazi wa Benki
ya Dunia anayehudumia nchi za Tanzania, Malawi, Msumbiji na Burundi, Bi.
Bella Bird.
Bw.
James alisema kuwa mkopo huo umelenga kuimarisha miundombinu ya utalii
katika ukanda huo wa kusini ikiwemo ujenzi wa barabara, viwanja vya
ndege, madaraja pamoja na kuibua fursa nyingi za utalii ili kuvutia
watalii wengi zaidi.
Alisema
pia kwamba mradi huo umelenga kuwajengea uwezo wananchi wanaozunguka
maeneo ya utalii kwa kuanzisha miradi itakayo chochea maendeleo yao ya
kijamii na kiuchumi pamoja na kuendeleza uhifadhi katika maeneo yao.