Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
akipokea shada la maua kutoka kwa kaimu Mkurugenzi wa Utawala wa Ofisi
ya Waziri Mkuu, Savera Kazaura (kulia) Baada ya kuwasili ofisini kwake
Novemba 23, 2015. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt,
Florence Turuka. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim
Majaliwa akitia saini kitabu baada ya kuingia ofisini kwake , Magogoni
jijini Dar es salaam, Novemba 23, 2015. Kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya
Waziri Mkuu, Dkt. Florence Tiruka.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya
Waziri Mkuu wakimsikiliza Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majliwa wakati
alipozungumza nao katika mkutano wa kujitambulisha , Ofisini kwa Waziri
Mkuu jijini Dar es salaam Novemba 23, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu)
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya
Waziri Mkuu wakimsikiliza Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majliwa wakati
alipozungumza nao katika mkutano wa kujitambulisha , Ofisini kwa Waziri
Mkuu jijini Dar es salaam Novemba 23, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu)
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim
Majaliwa akimsikiliza Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt.
Florence Turuka ambaye alitoa taarifa ya jumla kuhusu Ofisi ya Waziri
Mkuu baada ya Waziri Mkuu kuwasili Ofisini na kujitambulisha kwa
watumishi wa Ofisi yake Novemba 23, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu)
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim
Majaliwa akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu katika mkutano
wa kujitambulisha alioufanya baada tu ya kuwasili ofisni Novemba 23,
2015. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim
Majaliwa na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Florence Turuka
wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Waziri
Mkuu baada ya kuzungumza nao katika mkutano wa kujitambulisha
alioufanya baada ya kuwasili ofisini kwake Novemba 23, 2015. (Picha na
Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim
Majaliwa akizungumza na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu,Dkt Florence
Turuka baada ya kuwasili Ofisini Novemba 23, 2015. (Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim
Majaliwa na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Florence Turuka
wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Waziri
Mkuu baada ya kuzungumza nao katika mkutano wa kujitambulisha
alioufanya baada ya kuwasili ofisini kwake Novemba 23, 2015. (Picha na
Ofisi ya Waziri Mkuu)
…………………………………………………………………….
WAZIRI MKUU Majaliwa Kassim
Majaliwa amewataka wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu watambue jukumu
walilonalo la kuwahudumia wananchi kutokana na majukumu ya ofisi hiyo
ambayo yanagusa maisha ya kila siku ya Watanzania.
“Ofisi ya Waziri Mkuu ni kubwa na
pana sana na inahusika na shughuli za kila siku za Watanzania. Kwa hiyo
tuna kazi kubwa ya kukidhi matarajio yao,” alisema.
Ametoa kauli hiyo leo mchana
(Jumatatu, Novemba 23, 2015) wakati akizungumza na wakuu wa taasisi,
wakurugenzi na watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwenye mkutano
uliofanyika ofisini kwake, Magogoni, jijini Dar es Salaam. Leo ndiyo
ameripoti kwa mara ya kwanza tangu alipoapishwa Ijumaa iliyopita kwenye
Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma.
Pamoja na kazi nyingine tunayo
majukumu makubwa ambayo ni udhibiti, usimamizi na ufuatiliaji wa masuala
mbalimbali humu Serikalini. Ninataraji kupata mpango kazi kutoka kwa
Mkuu wa kila idara na kila taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu.
Nitakwenda pia ofisi za TAMISEMI ili kuweka vipaumbele vyetu sawa,”
alisema.
Aliwataka watumishi hao wawe
tayari kutekeleza kaulimbiu ya ‘Hapa Kazi Tu’ ambayo imekuwa
ikisisitizwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli ili kuweza kumudu kasi ya
utendaji kazi Serikali ambayo anaihimiza hivi sasa.
Alisema ana imani kuwa watumishi
hao watampa ushirikiano kama ambavyo walikuwa wakiutoa kwa mtangulizi
wake, Mhe. Mizengo Pinda ambaye amestaafu hivi karibuni.