TANZANITE ROYAL GIN YAZIDI KUPAMBA MANYARA TANZANITE MARATHON 2026
burudani habari






JESCA SIMUCHILE FT EV. DANIEL SAFARI WAACHIA VIDEO MPYA YA INJILI “TUIMBE TUMEPONA”
burudani

HALIMA – A CROSS-AFRICAN LOVE MELODY BY EKUNRAWO AND JUX
burudani

SERIKALI KUTOA MIRAHABA YA BILIONI 1 KWA WASANII MWAKANI
burudaniNA MASHAKA MHANDO
WIZARA ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, kupitia Taasisi ya Hakimiliki nchini (COSOTA), inatarajia kuweka historia mpya kwa kugawa zaidi ya shilingi bilioni moja kama mirabaha kwa wasanii wa makundi mbalimbali nchini ifikapo Januari 23, 2026.
Hatua hiyo inakuja baada ya majadiliano ya kimkakati kati ya Naibu Waziri wa sekta hiyo, Mhe. Hamis Mwinjuma (MwanaFA), na uongozi wa COSOTA, yaliyolenga kujibu kiu ya muda mrefu ya wasanii kuhusu malipo ya haki zao.
Akizungumza katika mahojiano maalum, MwanaFA alisema kuwa Serikali imejipanga kufanya ugawaji huo kuwa shughuli kubwa na ya kihistoria kutokana na kiwango kikubwa cha fedha kilichokusanywa.
"Kama msanii na kama Naibu Waziri, nimekuwa nikipokea maswali mengi kutoka kwa wasanii wenzangu wakitaka kujua hatma ya mirabaha yao. Nimefanya majadiliano (discussion) nzuri na COSOTA na tumekubaliana kuwa Januari 23 mwakani, tunakwenda kutoa zaidi ya shilingi bilioni moja na ushee. Hiki ni kiwango kikubwa ambacho hakijawahi kutokea nchini," alisema MwanaFA.
MwanaFA alibainisha kuwa mafanikio hayo yametokana na hatua ya Bunge kubadilisha sheria inayoruhusu kuanzishwa kwa Taasisi za Pamoja za Kusimamia Hakimiliki (Collective Management Organizations - CMOs).
Alieleza kuwa hadi sasa, leseni mbili zimetolewa kwa kampuni za CMO ambazo zimeshirikiana na taasisi za kimataifa, ikiwemo Taasisi ya Afrika Kusini inayosimamia mirabaha ya kidijitali (CAPASSO) kupata fedha hizo zinazokwenda kutolewa Januari.
Aidha, alitaja kuwa miongoni mwa vyanzo vikuu vya fedha hizo ni pamoja na kodi ya vifaa vinavyobeba kazi za sanaa na ada zinazotokana na Vibali vya Jumla vya kupiga nyimbo kwenye Redio na Televisheni (Blanket License).
"Tumepata zaidi ya shilingi bilioni moja kupitia mfumo wa Blanket License. Fedha hizi zitawanufaisha wasanii, huku sehemu ikiongoza Mfuko wa Utamaduni na Sanaa, COSOTA, pamoja na kodi ya Serikali," aliongeza.
Alifafanua kuwa tofauti na zamani, safari hii wigo umepanuliwa ambapo wanufaika watatoka katika makundi ya Muziki, Filamu, Sanaa za Maonyesho, Sanaa za Ufundi, pamoja na Waandishi wa Vitabu.
Hata hivyo, MwanaFA alitoa rai kwa wasanii wote: "ili unufaike na fedha hizi, ni lazima usajili kazi zako COSOTA. Usajili ndio utambulisho pekee utakaorahisisha utaratibu wa wewe kupata mirabaha yako pindi kazi zako zinapotumika au kuchezwa."
Mwisho
ENIOLA FALASE: THE NIGERIAN STAR SETTING HIS SIGHTS ON EAST AFRICA’S MUSIC SCENE
burudani
WEWE NI NGUVU YANGU WIMBO KUTOKA KWA GRACE OF AFRICA
burudani
Grace of Africa rasmi wameachia wimbo mpya wa injili, “Wewe ni Nguvu Yangu (You’re My Strength)”, unaohamasisha imani, tumaini, na nguvu ya ndani.
🔴🔴 WALIMBWENDE WA MISS GRAND TANZANIA WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HIFADHI YA PANDE
burudaniNa Beatus Maganja,
Dar es Salaam
Walimbwende 24 wanaoshiriki mashindano ya Miss Grand Tanzania 2025 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara, wamefanya ziara ya siku moja katika Hifadhi ya Pande iliyopo jijini Dar es Salaam tarehe 13 Agosti 2025 kwa lengo la kujifunza masuala ya uhifadhi na utalii wa ndani.
Ziara hiyo iliandaliwa kwa ushirikiano kati ya waandaaji wa Miss Grand Tanzania na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), ikiwa ni sehemu ya kuwawezesha walimbwende hao kujifunza masuala ya uhifadhi na utalii na kuwa mabalozi wa vivutio vya utalii wa ndani, hususan Hifadhi ya Pande.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Kaimu Kamanda wa Hifadhi ya Pande, PC Suleiman Keraryo, alisema hifadhi hiyo ni kivutio cha kipekee kilichopo katikati ya Jiji la Dar es Salaam, ambapo wageni hupata fursa ya kutalii na kujionea vivutio mbalimbali ikiwa ni pamoja na kujifunza kuhusu historia ya hifadhi hiyo, bioanuwai na mchango wake katika uhifadhi wa mazingira na viumbe hai.
“Karibuni sana katika Hifadhi yetu ya Pande, hifadhi iliyo katikati ya Jiji la Dar es Salaam, ikiwa na wanyamapori wa aina mbalimbali na vivutio vingine lukuki. Hapa ni mahali sahihi kwenu kujifunza na kujionea rasilimali za nchi yenu,” alisema Keraryo.
Aidha, alibainisha kuwa mshindi wa Miss Grand Tanzania 2025 atateuliwa kuwa Balozi wa Hifadhi ya Pande, ambapo atashirikiana na TAWA katika juhudi za kuitangaza hifadhi hiyo pamoja na kuchochea utalii wa ndani, sambamba na kuunga mkono juhudi za Serikali katika sekta ya maliasili na utalii.
Mashindano ya fainali ya Miss Grand Tanzania yanatarajiwa kufanyika tarehe 16 Agosti 2025 katika Ukumbi wa Superdome, Masaki – Dar es Salaam.
Uongozi wa Hifadhi ya Pande pia umeeleza dhamira yake ya kuendeleza ushirikiano na waandaaji wa Miss Grand Tanzania kwa kuhakikisha kuwa walimbwende wanapata fursa ya kulala ndani ya hifadhi hiyo na kufanya mazoezi katika mazingira ya asili, ili kuongeza uelewa wao kuhusu uhifadhi wa mazingira.
Kwa upande wao, walimbwende wameeleza kufurahishwa na ziara hiyo, hususan kupata fursa ya kuona kwa ukaribu aina mbalimbali za wanyamapori waliopo hifadhini humo, sambamba na mapokezi mazuri kutoka kwa maofisa wa TAWA. Pia waliahidi kuwa mabalozi wa kuitangaza hifadhi hiyo kwa jamii.
Ziara hiyo imeelezwa kuwa ni mwanzo wa ushirikiano endelevu kati ya TAWA na taasisi za kijamii, hususan zinazowalenga vijana, kwa lengo la kuongeza uelewa juu ya umuhimu wa kulinda mazingira na kuendeleza utalii wa ndani kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho
Vipindi vya Miss Universe Tanzania 2025 Kuanza Leo, Fainali Agosti 23
burudaniJOKAT E ATAJWA SHINDANO LA MISS TANGA 2024 LIKIZINDULIWA
burudani
SHINDANO la Miss Tanga 2024 limezinduliwa rasmi huku Mratibu wa Shindano la Miss Tanga 2024 Victoria Martin akisema suala warembo sio uhuni bali ni fursa ambayo inaweza kuwabadilishia watu maisha yao.
Katika kusisitiza umuhimu wa tasnia ya urembo kwamba sio uhuni alimtolea mfanoaliyewahi kuwa Miss Tanzania Jokati Mwogelo manufaa aliyokuwa nayo kupitia tasnia ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu UVCCM Taifa Bara.
Victoria ambaye aliwahi kuwa Miss Tanga 2007 aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa uzinduzi wa Shindano hilo lililofanyika kwenye Ukumbi wa Tanga Beach Resort Jijini Tanga na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa tasnia hiyo
Uzinduzi huo ulikwenda sambamba na usajili wa warembo ambao watawania taji hilo huku akitoa wito kwamba usaili bado unaendelea kujitokeza kushiriki kwenye shindano hilo ambalo mwaka huu ltakuwa la aina yake.
Victoria alisema lengo la kuandaa shindano hilo ni aliona ni muda wa kurudi nyumbani ,kuridisha ari na thamani ya urembo ili kuhamasisha ushiriki kwenye shindano hilo ambalo limesheheni fursa mbalimbali.
“Kupitia urembo watu wanaweza kubadilisha maisha yao kwa mfano wapo watu wengi wamenufaika kupiti huku kama ilivyo kwa Jokate Mwegelo ambayo wa sasa ni Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Bara lakini wapo wengi wametoka kutokana na tasnia hiyo”Alisema
“Lakini kupitia Miss Tanga tunaweza kubadilisha maisha hivyo ni muhimu wadau kuendelee kuisapoti tasnia hiyo kutokana na kuwa sehemu ya ajira kwa vijana wanaoshiriki kutokana na baadhi yao kupata nafasi katika maeneo mbalimbali ambazo zinawakwamua kiuchumi na hivyo kuchochea maendeleo kwenye jamii zao”Alisema
“Tunaomba tujitokeze kwa wingi kusapoti urembo kwani sio uhuru bali ni ajira tumekuwa tukipigwa bunduki kubwa tukiambiwa kwamba urembo ni uhuni sio sahihi maana asilimia kubwa washiriki wanatokea vyuoni “Alisema Victoria
Aidha Mratibu huyo alisema kwamba warembo ambao wanawania taji hilo wanatarajia kuingia kambini Mei 2 mwaka huu Shindano hilo lilitarajiwa kufanyika Mei 11 mwaka huu katika Hotel ya Tanga Beach Resort Jijini humo.
ZIFF, EU WALETA FILAMU MIKOA MITATU YA TANZANIA BARA
burudaniNa Andrew Chale, Dar es Salaam.
TAMASHA la Kimataifa la filamu za Nchi za Majahazi (Zanzibar International Film Festival-ZIFF) kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya (EU), Nchini wametangaza rasmi uoneshaji wa filamu katika Vyuo Vikuu kwenye mikoa mitatu ya Tanzania Bara linalokwenda kwa jina la “ZIFF Goes Mainland 2023”.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa ZIFF aliyemaliza muda wake ambaye anaratibu mpango huo, wa "ZIFF Goes Mainland 2023" amesema mpango huo umeendelea kuimarika na kuanzia Novemba 3, 2023, filamu tano zilizoshinda tuzo kutoka msimu wa 26 wa ZIFF na filamu teule za Ulaya zitaonyeshwa.
‘’Filamu hizi zitaoneshwa katika Mikoa ya Dar es Salaam ikiwemo Chuo cha Kampala KIU, Pwani Wilaya ya Bagamoyo katika Chuo cha TaSUBa, na Morogoro katika chuo kikuu Mzumbe. Wanafunzi watashiriki katika majadiliano baada ya kutazama kuhusu filamu na mbinu zao za kutengeneza filamu.
Tamasha hilo litafungua filamu ya "EONII" ya mwongozaji Mtanzania, na pia kutakuwa na filamu kutoka nchi za Ulaya kuangazia utofauti wa kitamaduni tajiri.’’ Amesema Prof. Martin Mhando.
Aidha, Mwaka huu, ili kuonyesha mshikamano kati ya vita vinavyoendelea na Urusi, filamu kutoka Ukraine, Pia filamu kutoka Afrika Kusini, Kenya, Misri na Tanzania.
‘’#TeamEurope - EU, taasisi zake na nchi wanachama - imekuwa muhimu katika kuimarisha tamasha la ZIFF.
Ushirikiano wetu na shughuli za zamani ikiwa ni pamoja na kusaidia warsha za mafunzo, kufadhili programu za ZIFF, ili kuwasilisha fursa za utayarishaji wa pamoja”. Amesema Prof. Martin Mhando
Kwa upande wake, Mkuu wa Ujumbe wa EU nchini Tanzania, Mhe. Balozi Bi. Christine Grau amesema; "Ulaya imechangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa tamasha zaidi ya kuonyesha filamu binafsi. Kusaidia wadau wanaohusika na utamaduni, na kuanzisha miundomsingi inayosaidia wasanii kujitahidi na kuhamasisha jamii zao.
Katika mkutano huo, wawakilishi kutoka Balozi tisa zikiwemo nchi za Spain, Belgium, Germany, Ireland, France, Poland, Finland, Italy na Sweden zinazochangia mpango huo wa ZIFF kwenda Bara 2023’’, wameweza zilizohudhuria, wakisisitiza ari ya #TeamEurope na jukumu la Diplomasia ya kitamaduni katika kukuza amani katika Ulaya na Afrika.
Baadhi ya filamu hizo tano ni pamoja na N8, MWANDISHI,NEB TAWY, 9MEMEZA na EONII




MADJS WA DAR KUUWASHA MOTO CLUB BEN BISTRO LOUNGE MKESHA WA MWAKA MPYA
burudaniMeneja wa Club Benbistro Hamisi Hassan akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusu walivyojipanga kuaga mwaka 2022 na kuukaribisha mwaka 2023 kwa staili ya aina yake ikiwemo kuwashukuru wateja wao kushoto ni Marton wa Club hiyo Sarah Patrick
Meneja wa Club Benbistro Hamisi Hassan akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusu walivyojipanga kuaga mwaka 2022 na kuukaribisha mwaka 2023 kwa staili ya aina yake ikiwemo kuwashukuru wateja wao kushoto ni Marton wa Club hiyo Sarah Patrick
Marton wa Club hiyo Sarah Patrick akizungumza namna walivyojipanga kushoto ni Msimamizi wa Club hiyo Silvester Kasembe
Marton wa Club hiyo Sarah Patrick akizungumza namna walivyojipanga kushoto ni Msimamizi wa Club hiyo Silvester Kasembe
Msimamizi wa Club Ben Bistro Lounge Silvester Kasembe
MADJS Maarufu kutoka Jijini Dar es Salaam na wakishirikiana na wenyeji wa Jiji la Tanga wanatarajia kuuwasha moto Club Maarufu Jijini Tanga “BEN BISTRO” siku ya mkesha wa kuuaga mwaka 2022 na kuukaribisha mwaka 2023 kwa staili ya aina yake ikiwemo kuwashukuru wateja wao
Akizungumza leo na waandishi wa Habari Jijini Tanga Meneja wa Benbistro Hamisi Hassan alisema kwamba burudani hizo zitaanza siku ya kuuaga mwaka na kuukaribisha mwaka 2023 na wamejiandaa kikamilifu kuhakikisha wateja wao wanapata burudani kali.
Alisema kwamba Pamoja na uwepo wa burudani hizo lakini wanawashukuru wateja na wadau wao tokea walipoanza mpaka sasa na kikubwa wamejiandaa kikamilifu na vitu ni vingi upande wa jikoni na club huku akieleza watahakikisha pia usalama unaimarishwa lengo kuwawezesha wadau wao na wateja kusheherekea mwaka mpya
“Kikubwa ni shukrani kwa wateja wetu na wadau wanaotusapoti tokea tumeanza mpaka sasa na tunawaambia mkesha wa Jumamosi na Jumampili kutokuwa na burudani kutoka kwa madjs kutoka Dar na tunaufunga mwaka “Alisema
Aidha alisema kwamba wanawahaidia wateja wao kuendelea kuboresha huduma zao ikiwemo kuhakikisha suala la usalama wao linaendelea kuwepo kila wakati na muda wote.
Awali akizungumza Mdau wa Club Benbistro Kamafa Forever alisema kwamba uwepo wa Club hiyo ambayo imekuwa tofauti na zile za awali umewasaidia wapenda burudani Jijini Tanga kupata ladha za uhakika ambazo hapo awali walikuwa wakizikosa
“Kinachofanyika Club Benibistro ni spesho sana na sehemu nzuri ambayo wadau wa burudani wataendea kupata burudani ya kuufunga mwaka na sababu za kupeleka uwepo wa madjs wapya ni kupata ladha tofauti ambazo zitakuwa na vionjo vya aina yake “Alisema
Naye kwa upande wake Matron wa Club hiyo Sarah Patrick alisema kwamba upande wa huduma ipo vizuri sana na wamejipanga kuhakikisha wanawahudumia wateja wao kama ilivyokuwa kawaida na kuhakikisha hakuna mtu ambaye anakosa vinywaji kutokana na aina ya wahudumu wachangamfu waliopo.
Hata hivyo msimamizi wa Club hiyo Silvester Kasembe alisema kwamba mwaka 2023 wanatarajia kufanya mambo makubwa Zaidi na sehemu hiyo ni nzuri ya Kwenda kupata burudani hivyo wanawakaribisha wateja wao kutoka ndani na nje ya Jiji la Tanga.
WAZIRI MCHENGERWA KUUNDA KAMATI MAALUMU YA KUANDAA MDUNDOWA KITANZANIA
burudani









.jpg)










.jpg)