SERIKALI YATAKA WANANCHI KUITAMBUA NA KUITUAMINI MIRADI YA MAENDELEO KATIKA MAENEO YAO
UBALOZI WA TANZANIA NCHINI UHOLANZI WATIA FORA TAMASHA LA MABALOZI MJINI THE HAGUE
Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi Mhe. Caroline Kitana Chipeta akipongezwa na Mstahiki Meya wa Mji wa The Hague Mhe. ~Jan Van Hanen kwa Tanzania kuwa kivutio kikubwa kwenye Tamasha la Mabalozi 2024 (Embassy Festival) nchini Uholanzi lililovutia watazamaji zaidi ya 50,000 mjini The Hague.
UBALOZI wa Tanzania umetia fora kwenye Tamasha la Mabalozi 2024 (Embassy Festival) nchini Uholanzi lililovutia watazamaji zaidi ya 50,000 wikiendi iliyopita mjini The Hague.
Idadi hiyo ya wahudhuriaji nkatika Tamasha hilo ni pamoja na makumi ya wana Diaspora wa Tanzania waishio nchini humo pamoja na wawekezaji wakubwa kutoka Tanzania kama vile PetroBas NL.
“Tamasha hilo ni fursa ya kipekee kuonyesha utajiri wa utamaduni wa Tanzania, nasi nafasi hiyo hatukuipoteza hata kidogo,” Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi Mhe.Caroline Kitana Chipeta amesema.
Balozi Chipeta amesema fursa zilizojitokeza kwenya tamasha hilo ni kuanzia kukuza utalii na lugha ya Kiswahili hadi mchanganyiko wa mitindo ya zamani na ya kisasa, ambapo Tanzania iliibuka kuwa kivutia kikubwa.
Amesema Banda la Tanzania, likiwa na vyakula vya kuvutia na vifaa vya kitamaduni, lilikuwa kivutio kikubwa kiasi ya kwamba Mstahiki Meya wa The Hague, Jan Van Zanen, alifika na kulisifia huku akiongeza heshima zaidi ya Tanzania kwenye tukio hilo.
“Ujio wa Meya Zanen bandani kwetu kunaonyesha jinsi uwepo wa kitamaduni wa Tanzania ulivyothaminiwa sana huko The Hague”, amesema Balozi Chipeta
Katika tamasha hilo Tanzania ilifanya onyesho la mitindo na mbunifu wa Kitanzania la kuvutia sana, hasa kwa kuchanganya mavazi ya zamani na ya sasa ambako kulileta athari kubwa.
Balozi Chipets, ambaye yeye mwenyewe alishiriki akiwa kavalia vazi la mwanamke wa kimwambao la khanga na baibui na kushangiliwa sana, anasema, onesho hilo pia lilikuwa ni njia bora ya kuendeleza tamaduni za jadi huku zikifanywa ziwe za kisasa.
Banda la Tanzania pia lilikuwa kivutio cha pekee hasa kwa kucheza muziki pendwa wa Bongo Fleva ambapo kila aliyepita alifurahia, hasa hasa ilipopigwa ngoma ya Coma Cava ya Diamond Platinumz ambaye Septemba 30, 2024 atafanya onesho jijini Amtserdam.
TUVUMILIANE NA KUHESHIMIANA KAMA WATANZANIA - DKT. BITEKO
MSIGWA AIPONGEZA TBS KWA KUHAMASISHA MICHEZO MAENEO YA KAZI
WAZIRI MAVUNDE AIPONGEZA TUME YA MADINI KWA KUVUNJA REKODI YA UKUSANYAJI WA MAPATO
Waziri wa Madini Anthony Mavunde akizungumza leo wakati akifungua kikao kazi na Menejimenti ya Tume ya Madini Jijini Tanga |
Naibu Waziri wa Madini Dkt Steven Kiruswa akizungumza wakati wa kikao hiho |
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Mhandisi Yahaya Samamba akizungumza wakati wa kikao kazi hicho |
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akizungumza |
Na Oscar Assenga,TANGA
WAZIRI wa Madini Anthony Mavunde ameipongeza Tume ya Madini kwa kuvunja rekodi kukusanya kiasi cha Sh Bilioni 196 kwa kipindi cha siku 75 huku akieleza jambo hilo ni kubwa na inaonyesha wamedhamiria kuifanya sekta ya madini inachangia kwenye uchumi wa nchini.
Mavunde aliyasema hayo leo Jijini Tanga wakati akifungua kikao kazi na Menejimenti ya Tume ya Madini Jijini Tanga ambapo alisema kiwango hicho kimepokelewa mpaka leo 15 Septemba ndani ya miezi miwili ya mwaka huu na hilo linatokana na .
Alisema kiwango hicho kimeifanya kuvunja rekodi ya makusanyo ilihali mwaka 2015/2016 ilichukua mwaka mzima kukusanya Bilioni 161 lakini leo ndani ya siku 75 tume hiyo imeshakusanya kiasi hicho na hivyo kuvunja rekodi kwani waliojiwekea makusanyo ya Bilioni 60 mpaka Bilioni 65 kwa kila miezi na mwili iliyopita mmekusanya Bilioni 83 kila mwezi mmevuka malengo yao.
“Niwatie moyo na wakikaza buti na kuendelea na usimamizi huo mzuri na makusanyo wakifika mwakani mwezi wa saba watakuwa mmeandika historia kubwa”Alisema
Katika hatua nyengine Waziri Mavunde amewataka maafisa madini wakazi wa mikoa kuhakikisha wanashughulikia migogoro kwenye maeneo yao kwa haraka inapojitokeza badala ya kusubiri mpaka wafike viongozi wakubwa ikiwemo Waziri.
Alisema haiwezekani wao wapo kwenye mikoa na wanashindwa kutatua migogoro iliyopo hivyo wabadilike wahakikishe wanaishughulia na utatuzi wake unapatikana haraka bila kumuonea mtu.
Alisema anajisikia vibaya kuona mgogoro inapotokea mpaka aende waziri au Naibu Waziri wakati wapo maafisa madini wakazi mpaka umshinde ndio uvuke uende ngazi lakini kazi yenu hya kwanza ni utatuzi wa migogoro labda mniembie nyie ni sehemu ya migogoro lakini kama sio sehemu ya migogoro tatueni migogoro,
“Niwaambieni kipimo chenu cha kazi kitakuwa ni namna mnavyotatua migogoro tatueni na sio mpaka msubiri ufike hatua ya juu anzeni nao lakini mtatue migogoro katika haki asionewe mtu simamieni haki ndugu zangu”Alisema Waziri Mavunde
Udhibiti wa Utoroshwaji wa Madini
WAZIRI Mavunde aliwataka maafisa hao kuhakikisha wanadhibiti utoroshwaji wa madini katika maeneo yao hususani ile ya mipakani
“Mmeona hivi karibuni kuna kesi nyingi sana zinapelekwa mahakamani na juzi tumewakamata watu Bandari Dar na kilo 15 za dhahabu na tumezitaifisha ela dhahabu na wanakwenda mahakamani,huko kwenye maeneo yenu hakikisheni mnashirikiana kwenye task force kudhibiti hili lisitokee”Alisema Waziri Mavunde
Aidha Waziri Mavunde aliutaja Mkoa wa Madini wa Kahama ndio unaongoza kwa shughuli za za utoroshaji wa madini na mbinu hivi sasa zimebadilika wanasikie wale ambao wanakwenda kuuziana kwenye mashine za Mpunga ambapo alimtaka Afisa Madini Mkazi wa Mkoa huo kuhakikisha anaimarisha eneo hilo.
Mavunde alitoa agizo hilo leo Jijini Tanga ambapo alisema haiwezekani wao wapo kwenye mikoa na wanashindwa kutatua migogoro iliyopo hivyo wabadilike wahakikishe wanaishughulia na utatuzi wake unapatikana haraka bila kumuonea mtu.
Alisema anajisikia vibaya kuona mgogoro inapotokea mpaka aende waziri au Naibu Waziri wakati wapo maafisa madini wakazi mpaka umshinde ndio uvuke uende ngazi lakini kazi yenu hya kwanza ni utatuzi wa migogoro labda mniembie nyie ni sehemu ya migogoro lakini kama sio sehemu ya migogoro tatueni migogoro,
“Niwaambieni kipimo chenu cha kazi kitakuwa ni namna mnavyotatua migogoro tatueni na sio mpaka msubiri ufike hatua ya juu anzeni nao lakini mtatue migogoro katika haki asionewe mtu simamieni haki ndugu zangu”Alisema Waziri Mavunde
Udhibiti wa Utoroshwaji wa Madini
WAZIRI Mavunde aliwataka maafisa hao kuhakikisha wanadhibiti utoroshwaji wa madini katika maeneo yao hususani ile ya mipakani
“Mmeona hivi karibuni kuna kesi nyingi sana zinapelekwa mahakamani na juzi tumewakamata watu Bandari Dar na kilo 15 za dhahabu na tumezitaifisha ela dhahabu na wanakwenda mahakamani,huko kwenye maeneo yenu hakikisheni mnashirikiana kwenye task force kudhibiti hili lisitokee”Alisema Waziri Mavunde
Aidha Waziri Mavunde aliutaja Mkoa wa Madini wa Kahama ndio unaongoza kwa shughuli za za utoroshaji wa madini na mbinu hivi sasa zimebadilika wanasikie wale ambao wanakwenda kuuziana kwenye mashine za Mpunga ambapo alimtaka Afisa Madini Mkazi wa Mkoa huo kuhakikisha anaimarisha eneo hilo.
“Lakini pia nimemwambia Katibu Mkuu waifanye Kahama kama Kanda Maalumu kwa maana dhahabu nyingi inatoroshewa kupitia Kahama nimekuona RMO mara mbili mara tatu mnatoka mnakamata endeleee na mikoa mingine hasa mikoa ya Mipakani”Alisema Waziri huyo.
Waziri huyo aliwataka maafisa hao kila mmoja katika eneo lake ahakikishe anakuwa sehemu ya udhibti wa utoroshaji wa madini kwa maana utoroshwaji huo unasababisha kupoteza mapato mengi.
Hata hivyo Waziri huyo aliitaka Ofisi ya Kamishna wa Madini kushirikiana na RMO kuwalea wachimbaji wadogo na kuwaendeleza katibu mkuu pale wizara wawekezaji wakubwa wana meneja wake ndani ya wizara wa kuyasimamia katibu mkuu kupitia Ofisi ya Kamishna natoa maelekezo tengenezeni utaratibu kushirikiana na RMO kuwaibua watanzania wawekezaji wa sekta ya madini kupitia ofisi ya Kamishna wawelee nao wagraduate kutokana na kwamba hivi sasa wenyewe hawana muangalizi.
Alisema ili siku moja waweze kutengeneza mabilioni wengi kupitia wachimbaji wadogo hivyo wakikaa nao na kuwasaidia kama wanavikwazo waone namna ya kuyatatua ili kuweza kuongeza mapato.
Katika hatua nyengine Waziri Mavunde aliwataka kuhakikisha wanadhibiti upotevu wa mapato waende wakazibe mianya na makusanyo yaweze kuongezeke huku akieleza hiyo ni sehemu ya kazi yako ya msingi.
“RMOs kila mtu amewekewa malengo ya kuwafikia kwa mwaka wa fedha huu kama unahisi kwako unashindwa kufikia malengo kwa jambo ambalo halihusiani na wewe ni tatizo la kimfumo,kimundo lipo nje ya uwezwa