UKINYIMWA UNYUMBA NDANI YA NDOA NENDA KASHITAKI DAWATI LA JINSIA POLISI

December 10, 2016

 Mkuu wa Wilaya ya Temeke,  Felix Lyaniva (katikati), ambaye alikuwa mgeni rasmi akihutubia wakati akizindua maonyesho ya dawati la jinsia na watoto Wilaya ya Temeke viwanja vya Mwembe Yanga Dar es Salaam leo asubuhi. Kutoka kulia Mkuu wa Polisi wa Kituo cha Chang'ombe (OCD) Msuya, Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa (UN), Lucy Tesha, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP), Gilles Muroto na Kamishna Msaidizi wa Polisi, Vedastus Chambu kutoka Kamisheni ya Polisi Jamii Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Nchini.
 Mkuu wa Wilaya ya Temeke,  Felix Lyaniva (Wa pili kushoto), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa maonesho wa  maonyesho ya dawati la jinsia na watoto Wilaya ya Temeke katika viwanja vya Mwembe Yanga Dar es Salaam leo asubuhi. Kutoka kulia Mkuu wa Polisi wa Kituo cha Chang'ombe (OCD) Msuya, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Vedastus Chambu kutoka Kamisheni ya Polisi Jamii Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Nchini, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP), Gilles Muroto na Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa (UN), Lucy Tesha. 
 Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa (UN), Lucy Tesha akihutubia kwenye uzinduzi huo.
 viongozi mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Wadau na wananchi wakifuatilia hutuba za mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaniva.

Maofisa Wanawake wa Jeshi la Polisi  Dawati la Jinsia wakiwa kwenye Maonyesho hayo. 


 Wananchi na wadau wengine wakifuatilia hutuba ya mgeni rasmi
 Wananchi na wadau wengine wakiwa kwenye maonyesho hayo.
 Hapa ni kazi tu.
 Mrakibu wa Jeshi la Polisi, (SP), Faidha Suleiman (kushoto), ambaye anashughulikia dawati la jinsia Makao Makuu ya jeshi hilo akimkabidhi Mgeni rasmi DC wa Temeke machapisho mbalimbali ya ukatili wa kijinsia ikiwemo miongozo ya uanzishaji wa dawati la jinsia na watoto ndani ya jeshi hilo.
  Mrakibu wa Jeshi la Polisi, (SP), Faidha Suleiman (kushoto), akimuelekeza Mkuu wa Wilaya ya Temeke kuhusu kazi kubwa inayofanywa na jeshi hilo kwenye idara ya dawati la jinsia.
Wananchi wakipata machapisho mbalimbali.

Na Dotto Mwaibale

WANANDOA wanaojimwa ujumba na wenza wao wametakiwa kwenda kushitaki dawati la jinsia yaliyopo vituo mbalimbali vya polisi ili kupatiwa utatuzi wa changamoto hiyo.

Mwito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva wakati akizindua maonyesho ya dawati la jinsia na watoto katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke Dar es Salaam leo ambayo yalishirikisha wadau mbalimbali kutoka Hospitali ya Amana wilayani Ilala na wananchi.

"Ukatili wa kijinsia si kupigana na kutukana hata mume na mke wakinyimana unyumba pia ni ukatili wa kijinsia hivyo anayejimwa hasione aibu aende kushitaki dawati la jinsia katika kituo chochote cha polisi" alisema Lyaniva.

Lyaniva aliwataka wananchi wanao fanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenda kwenye dawati hilo kupata ushauri kutoka kwa maofisa wa polisi waliopatiwa mafunzo ya kutatua changamoto hiyo.

Katika hatua nyingine Lyaniva aliwaagiza maofisa wa polisi wa dawati hilo kutotoa nje siri za watu wanaopeleka malalamiko yao katika dawati hilo kwa kufanya hivyo ni kukiuka utaratibu wa kazi.

Aliwaasa wanandoa kuwa na mshikamano na upendo ili kuwa na familia bora na yenye maadili jambo litakalosaidia kutokuwepo kwa watoto waliokosa maadili na kujiingiza kwenye makundi ya kiovu kama panya road.

Lyaniva aliwaomba wanawake pale wanapopata mafanikio ya maisha kupata fedha au kupanda vyeo kuacha kuwadharau waume zao ili kuepusha kuvinjika kwa ndoa zao.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Temeke Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, (SACP), Gilles Muroto amewataka wananchi wasiogope kwenda kutoa taarifa za ukatili wa kijinsia katika vituo vya polisi kwani malalamiko yao yatasikilizwa kwa faragha na maofisa maalumu wa jeshi hilo.

Maonyesho hayo yamedhaminiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa (UN).

Ziara ya Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano nas Mazingira Mhe Luhaga Mpina Zanzibar

December 10, 2016


Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe Luhaga Mpina akimsikiliza Mratibu wa Kituo cha Tume ya Sayansi na Teknolojia Zanzibar Bi Afua Mohammed akitowa maelezo ya utendaji wa Tume hiyo wakati akiwasilisha Ripoti ya Utafiti iliofanywa na Tume hiyo wakati wa ziara ya Mhe Luhaga, Mkutano huo umefanyika katika Ofisi za Tume hiyo maruhubi Zanzibar.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe Luhaga Mpina akipitia Ripoti ya Tume ya Sayansi na Teknolijia Zanzibar wakati wa ziara yake kutembelea miradi inayosimamiwa na Tume hiyo ilioko Zanzibar.
Mratibu wa Kituo cha Tume Sayansi na Teknolojia Zanzibar Bi Afua Mohammed akitowa maelezo kwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe, Luhaga Mpina alipofika katika Kituo hicho maruhubi Zanzibar akiwa katika ziara yake kutembelea miradi inayosimamiwa na Tume ya Sayansi na Teknolojia Zanzibar.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akizunhgumza na waandishi wa habari Zanzibar baada ya kumalizia mazungumzo yake na kupoata taarifa ya Utendaji wa Kituo cha Tume ya Sayansi na Teknolojia Zanzibar katika ofisi zake ziliko maruhubi Zanzibar.  
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muunganio na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akiwasili katika viwanja vya Kituo cha Utafiti wa Kilimo Kizimbani Zanzibar kutembelea kituo hicho kujionea shughuli zinazofanywa katika kazi za Utafiti wa Zao la Kilimo Zanzibar. 
Mkuu wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo Kizimbani Zanzibar Ndg Khatib Juma akitowa maelezo kwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe Luhaga Mpina alipofika Kituoni hapo kutembelea na kujionea shughuli za utafiti zinazofanya na Kituo hicho.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe Luhaga Mpina akizungumza wakati wa ziara yake katika Kituo cha Utafiti wa Kilimo Kizimbani Zanzibar akiwa katika ziara yake Zanzibar.
Mratibu wa Tume ya Sayansi na Teknolijia Zanzibar Bi Afua Mohammed akitowa maelezo kwa Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina alipotembelea Kituo cha Utafiti wa Kilimo Kizimbani Zanzibar.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akizungumza wakati wa ziara yake na wafanyakazi wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo Kizimbani akiwa katika ziara yake kisiwani Zanzibar kutembelea Miradi inayofadhiliwa na Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania. 
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe, Luhaga Mpina akitembelea Kituo cha Utafiti wa Kilimo Kizimbani Zanzibar akiwa na Mkuu wa Kituo hicho Ndg.Khatib Juma. 
Mkuu wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo Kizimbani Zanzibar Ndg Khatib Juma akitowa maelezo kwa Naibu Waziri Ofisi Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina wakiwa katika maabara ya kituo hicho kizimbani Zanzibar wakati wa ziara yake. 
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe Luhaga Mpina akiangalia mpunga unaofanyiwa utafiti katika Kituyo cha Utafiti wa Kilimo Kizimbani Zanzibar, akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Kituo hicho Ndg Juma Khatib katikati.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe Luhaga Mpina akitoka katika Jengo la Kituo cha Utafiti wa Kilimo Kizimbani Zanzibar akiwa katika ziara yake kutembelea Miradi ilinayodhaminiwa na Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Tanzania katika utafiti wake.
Imeandaliwa na OthmanMapara.Blogspot.
othmanmaulid@gmail.com
Zanzinews.com 
0715 424152.or 0777424152.
Zanzibar.

MASAUNI AZINDUA MASHINDANO NAGE MAPINDUZI CUP ZANZIBAR, ACHANGIA VICOBA JIMBONI KWAKE

December 10, 2016


 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na mamia ya wananchi kabla ya kuzindua Mashindano maarufu ya Nage Mapinduzi Cup katika Viwanja vya Matumbaku, Wilaya ya Mjini, Unguja, Zanzibar. Mashindano hayo yanawahusisha wasichana kutoka majimbo mbalimbali ya mjini humo yameandaliwa kwa ajili ya Maadhimisho ya Sherehe ya Miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar yanayotarajiwa kufanyika mwezi ujao mwakani.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Chama cha Kuweka na Kukopa (Vicoba-Together) katika sherehe iliyofanyika Skuli ya Chekechea, Miembeni, Zanzibar. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mjini, Unguja. Masauni alikichangia chama hicho shilingi milioni tatu.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akimkabidhi Mkurugenzi wa Redio ya Coconut mjini Unguja, Zanzibar, Ally Dai, jezi kwa ajili ya Mashindano maarufu ya Nage Mapinduzi Cup ambayo yamezinduliwa na kiongozi huyo katika Viwanja vya Matumbaku mjini humo. Mashindano hayo yanawahusisha wasichana yameandaliwa kwa ajili ya Maadhimisho ya Sherehe ya Miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar yanayotarajiwa kufanyika mwezi ujao mwakani.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto aliyevaa kofia) akiyapokea Maandamano ya timu 38 za Mashindano ya Nage Mapinduzi Cup katika Viwanja vya Matumbaku, Wilaya ya Mjini, Unguja, Zanzibar. Mashindano hayo yanawahusisha wasichana kutoka majimbo mbalimbali ya mjini humo yameandaliwa kwa ajili ya Maadhimisho ya Sherehe ya Miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar yanayotarajiwa kufanyika mwezi ujao mwakani.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na wanachama wa Chama cha Kuweka na Kukopa cha Vicoba-Together (hawapo pichani) kabla ya kuzindua kikundi hicho katika sherehe iliyofanyika Skuli ya Chekechea, Miembeni, Zanzibar. Kushoto ni Katibu wa Vicoba Together, Mwashum Mohammed Mustafa. Kulia ni Katibu wa Jimbo la Kikwajuni, Kassim Ally Juma.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni akizikagua timu ya Kikwajuni na Baa kutoka Jimbo la Mtoni kabla ya kuanza Mashindano ya Nage Mapinduzi Cup katika Viwanja vya Matumbaku, Wilaya ya Mjini, Unguja, Zanzibar. Mashindano hayo yanawahusisha wasichana kutoka majimbo mbalimbali ya mjini humo yameandaliwa kwa ajili ya Maadhimisho ya Sherehe ya Miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar yanayotarajiwa kufanyika mwezi ujao mwakani.
 Mchezaji wa Timu ya Kikwajuni, mjini Unguja, Zanzibar akijaza chupa mchanga wakati wa Mashindano ya Nage Mapinduzi Cup katika Viwanja vya Matumbaku, Wilaya ya Mjini, Unguja, Zanzibar. Mashindano hayo yanawahusisha wasichana kutoka majimbo mbalimbali ya mjini humo yameandaliwa kwa ajili ya Maadhimisho ya Sherehe ya Miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar yanayotarajiwa kufanyika mwezi ujao mwakani. Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni alizindua Mashindano hayo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wanachama  wa Chama cha Kuweka na Kukopa cha Vicoba Together. Masauni alikichangia chama hicho shilingi milioni tatu. Picha zote na Felix Mwagara

TASWIRA KATIKA MABANDA YA MAONESHO YA VIWANDA VYA NDANI KATIKA VIWANJA VYA SABASABA JIJINI DAR

December 10, 2016
Kaimu Meneja huduma kwa wateja na Elimu kwa Umma Ndugu Jemes Ndege( kulia)akitoa elimu kwa wananchi waliofika katika banda la TFDA katika maonesho ya viwanda yanayoendelea katika viwanja Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Gaudensia Simwanza (kulia) akitoa maelezo kwa wateja wa waliofika katika banda la TFDA katika maonesho ya viwanda yanayoendelea katika viwanja Sabasaba jijini Dar es Salaam. 
Mwalimu wa Umeme VETA Kipawa, Athuman Ubaya akitoa maelezo kwa wananchi waliofika katika banda la TFDA katika maonesho ya viwanda yanayoendelea katika viwanja Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Mshauri wa Habari PPR, Paschal Mayara akitoa huduma katika maonesho ya Viwanda yanayoendelea katika viwanja Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Wananchi wakipata maelezo katika banda la Dar Ropes katika Maonesho ya viwanda yanayoendelea katika viwanja Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Uchumi na Biashara wa Nchini, Ukraine, Nataliya Mykolska akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Masoko na Mauzo wa Azam, Omary Kuwe walipotembelea banda la Azam katika Maonesho ya Viwanda yanayoendelea katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Wananchi wakipata huduma katika banda MeTL katika maonesho ya viwanda yanayoendelea katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.

RAIS DKT. MAGUFULI AWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI PIA AKUTANA NA MMILIKI WA KIWANDA CHA SARUJI CHA DANGOTE KILICHOPO MTWARA ALHAJI ALIKO DANGOTE IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

December 10, 2016


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Christopher Olonyokie Ole -Sendeka kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mhandisi Mathew Mtigumwe kuwa Katibu Mkuu katika Wizara ya Kilimo Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Maria Sasabo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano), Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Aloyce Kashindye Nzuki kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha  Balozi Grace Alfred Martin kuwa Mkuu wa Itifaki kutoka Wizara ya mambo ya Nje Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Viongozi walioapishwa wakila kiapo cha Maadili mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam. Wakwanza kutoka kushoto ni Mkuu wa Itifaki Balozi Grace Alfred Martin, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Aloyce Kashindye Nzuki, Katibu Mkuu Mawasiliano Dkt. Maria Sasabo, Katibu Mkuu Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe pamoja na Mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Olonyokie Ole-Sendeka.
 Viongozi walioapishwa waki weka saini katika viapo vya maadili Ikulu jijini Dar es Salaam. Wakwanza kutoka kushoto ni Mkuu wa Itifaki Balozi Grace Alfred Martin, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mali asili na utalii Dkt. Aloyce Kashindye Nzuki, Katibu Mkuu Mawasiliano Dkt. Maria Sasabo, Katibu Mkuu Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe pamoja na Mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Olonyokie Ole Sendeka.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi pamoja na viongozi walioapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam. Wakwanza kutoka kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Aloyce Kashindye Nzuki, Katibu Mkuu Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe, Mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Olonyokie Ole Sendeka, Wakwanza kutoka kulia ni Mkuu wa Itifaki Balozi Grace Alfred Martin pamoja na Katibu Mkuu wa Mawasiliano Dkt. Maria Sasabo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika kikao cha pamoja na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika kikao cha pamoja na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote mara baada ya kumaliza kwa kikao chao Ikulu jijini Dar es Salaam.

 Mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote akizungumza mara baada ya kumaliza mazungumzo yake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam. Wakwanza kushoto ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza mara baada ya kumaliza kikao chake na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza mara baada ya kumaliza kikao chake na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote Ikulu jijini Dar es Salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza mara baada ya kumaliza kikao chake na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote Ikulu jijini Dar es Salaam.

 Mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU