Yanga na Mgambo Shooting ngoma droo.

Yanga na Mgambo Shooting ngoma droo.

April 17, 2013
Na Mwandishi Wetu,Tanga.
TIMU za soka Mgambo Shooting na Yanga leo zimeshindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya kufungana bao 1-1,ikiwa ni mechi ya Ligi kuu Tanzania bara.

Mchezo huo ambao ulikuwa na upinzani mkubwa kutokana na timu zote kushambuliana kwa zamu na kuonyesha andanda nzuri na la kuvutia.

Si Yanga wala Mgambo ambayo itashindwa kujilaumu kutokana na nafasi za wazi ambazo waliweza kuzipata na ushindwa kuzitendea haki kutokana na wachezaji wao kushindwa kuzitumia vema.

Mgambo ndio ilikuwa ya kwanza kuweza kupata bao lao kupitia Issa Kanduru katika dakika ya 42 baada ya kumalizia krosi ya Salum Mlima na hatimaye kuweza kukwamisha wavuni bao hilo.

Bao hilo lilidumu mpaka timu zote zinakwenda mapumziko ambapo kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo Yanga waliingia uwanjani hapo na hari na nguvu mpya baada ya kufanya mabadiliko kwenye kikosi chao.

Wakionekana kujipanga na kucheza kwa umakini mkubwa Yanga waliweza kupata bao lao la kusawadhisha kwenye dakika ya 86 kupitia Saimon Msuva.

Mwisho.

Picha za matukio mbalimbali za mechi ya Yanga na Mgambo Shooting kwenye uwanja wa Mkwakwani.

April 17, 2013
 
 
 
 

Vikosi vya Mgambo na Yanga vikiingia uwanja wa Mkwakwani kwenye mechi ya Ligi kuu Tanzania bara

April 17, 2013
 
 
 

Nieleze mikakati yako katika kundi lenu la Majuto Units.

April 17, 2013
Mtayarishaji wa Filamu ya "Kitu Bomba"ambayo itaangia sokono hivi karibuni ambaye pia ni mtoto wa nne wa mzee Majuto na Msemaji wa familia yao Hamza Majuto akizungumza na mmiliki wa blog hii Oscar Assenga kwenye ofisi za Kampuni ya New Habari Cooperation jijini Tanga jana,Picha na Mwandishi wetu,Tanga.
Habari za Michezo leo Tanga

Habari za Michezo leo Tanga

April 17, 2013
COPA Coca Cola wilaya ya Tanga kuanza April 25 mwaka huu.
Na Oscar Assenga, Tanga.

MICHUANO ya Copa Coca Cola ngazi ya wilaya ya Tanga inatarajiwa kuanza kutimua vumbi April 25 hadi Mei 31 mwaka huu katika viwanja ambavyo vitapendekezwa na itashirikisha timu zenye wachezaji chini ya umri wa miaka 15.

Akizungumza blogi hii,Katibu Msaidizi wa Chama cha Soka wilaya ya Tanga,Salim Carlos alisema mashindano hayo yatakuwa tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma ambayo ilikuwa ikishirikisha vijana wenye umri chini ya umri wa miaka 17 toka kwenye klabu zilizokuwa na usajili wa kudumu na kituo.

Carlos alisema kutokana na utaratibu mpya wa mashindano hayo yataitwa FIFA Copa Coca Cola under 15 na yatashirikisha timu za shule za sekondari na vituo vya kukuzia vipaji vilivyo sajiliwa kwa mujibu wa sheria zilizopo za soka.

Aliongeza kuwa timu itakayokuwa mshindi katika michuano hiyo ndio itakuwa bingwa wa wilaya ya mashindano hayo ambapo jumla ya shule za sekondari 10 zinatarajiwa kushiriki katika mashindano hayo.

Katibu huyo alizitaja timu ambazo mpaka sasa zimethibitisha kushiriki kwa kujitokeza kuchukua fomu ni mbili tu ambazo ni Mikanjuni sekondari na Hotel sekondari ambapo fomu za ushiriki zilianza kutoka tangia April 15 mwaka huu.

Aidha aliongeza kuwa wachezaji ambao wataruhusiwa kushiriki mashindano hayo ni wenye umri chini ya miaka 15 pamoja na kuwa na fomu za usajili ambapo watatakiwa kuambatanisha na vyeti halisi vya kuzaliwa.

Alieleza kuwa fomu ambazo zitaweza kupokelewa ni zile ambazo zimekamilika zikiwa na TSM.9 au nakala iliyochukuliwa na mamlaka husika na usajili wake ulianza Machi 19 mwaka huu na utamalizika April 22 mwaka huu.

Mwisho.

“Majuto Units kuachia “Kitu Bomba”

Na Oscar Assenga, Tanga.
KUNDI la Filamu la Majuto Units lenye makazi yake jijini Tanga linatarajiwa kutoa filamu yao ya inayokwenda kwa jina la Kitu Bomba ambayo ilikuwa ni filamu ya mwisho kati ya Msanii Sharomillionea na Mzee Majuto.

Akizungumza na blog hii, Hamza Majuto ambaye ni msemaji wa familia hiyo alisema filamu hiyo ilianza kuachiwa mwezi uliopita iliweza kuvunja rekodi ya mauzo yake baada ya kuuza nakala zaidi ya 10,000 sokoni kutokana na kupokewa vema na mshabiki wao.

Hamza alisema filamu hiyo ilikuwa imebeba mandhari ya ukimwi jinsi unavyohatarisha maisha ya watu kutokana na maambukizo wanayokuwa wakiyapata.

Akizungumzia soko la filamu lilivyo hapa nchini tofauti na miaka ya nyuma, Hamza alisema zamani wasanii wa filamu wakiwa wakicheza kazi zao kutokana na hobi lakini hivi sasa imejeuka kuwa ajira ambayo inaweza kuwainua watu kutoka katika maisha duni na kuelekea kwenye maisha mazuri na yenye kipato kizuri.

Akizungumzia mtu ambaye alikuwa akimvutia katika tasnia hiyo ya filamu kabla ya kuanza kuingia rasmi alisema miongoni mwa wasanii ambao walikuwa wakimvutia sana ni marehemu Steven Kanumba tokea akiwa chuo kikuu jijini Dar es Salaam UDSM.

Aidha alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dokta Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuwasaidia wasanii  hapa nchini ambapo alisema juhudi za kiongozi huyo zinapaswa kuigwa na viongozi waliopo chini yake ili wasanii waweze kuona matunda yao nao na sio kumtakisha tama.

Mwisho.

Na Oscar Assenga, Tanga.

CHAMA cha Mpira wa Wavu Tanzania (TAVA) kinatarajiwa kufanya mkutano mkuu wa uchaguzi Mei 18 mwaka huu katika ukumbi wa Hotel ya Mkonge jijini Tanga ambapo nafasi mbalimbali zinatarajiwa kugombewa katika uchaguzi huo.

Akizungumza na Blogii hii,Mwenyekiti wa Chama hicho,Augustino Agapa alisema maandalizi ya uchaguzi huo yanaendelea vizuri na kila kitu kimekamilika kwa asilimia kubwa ambapo wajumbe watakuwa ni makatibu wa vyama vya mikoa vilivyojishirikisha na TAVA na kamati ya utendaji wanaomaliza muda wao.

Agapa alizitaja nafasi ambazo zinatarajiwa kugombewa katika nafasi hiyo kuwa Mwenyekiti wa chama hichoi,Makamu wa kwanza mwenyekiti wa mipango na maendeleo,makamu wa pili wa mwenyekiti wa fedha na utawala,Katibu Mkuu,Naibu Katibu Mkuu

Aidha alizitaja nafasi nyengine zinazogombewa kuwa ni Mwenyekiti wa kamati ya ufundi,Mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya shule na vyuo,Mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya mikoa,mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya waamuzi na Mwenyekiti wa Kamati ya maendeleo ya makocha.

Nafasi nyengine zitakazogombewa kuwa ni Mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya mpira wa ufukweni, Mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya wanawake,Mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya watoto                                   

Mwenyekiti huyo alisema uchaguzi wa TAVA utasimamiwa na Baraza la michezo la Taifa kwa mujibu wa katiba ya TAVA na Utaratibu wa fomu za wagombea utatolewa muda mfupi ujao.

Mwisho.