RAIS KIKWETE USO KWA USO NA PINTO MWENYEKITI WA TASWA

April 28, 2014

Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), ambaye pia ni mmiliki wa magazeti ya Jambo Leo na Staa Spoti, Juma Pinto wakati wa hafla ya maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Ikulu, Dar es Salaam juzi..PICHA NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG

TBL YAPATA TUZO YA MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA NCHINI

April 28, 2014

 Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid (kulia) akimkabidhi Meneja Vipaji wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Lillian Makau cheti cha shukurani cha kutambua ushiriki wa kampuni hiyo katika mapambano dhidi ya Malaria nchini, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Malaria Duniani, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Katikati ni Balozi wa Malaria Tanzania, Leodegar Tenga.
Katibu wa Afya wa TBL (katikati), akitoa maelezo jinsi kampuni yake ilivyojidhatiti kutoa elimu na tiba ya malaria kwa wafanyakazi pamoja na wananchi.
Katibu wa Afya wa TBL (katikati), akitoa maelezo jinsi kampuni yake ilivyojidhatiti kutoa elimu na tiba ya malaria kwa wafanyakazi pamoja na wananchi.
Wananchi wakiwa katikasherehe za maadhimisho ya hayo kwenye Hoteli ya Kilimanjaro, Dar es Salaam.
Makau akielezea mikakati ya TBL ya kuisaidia jamii na wafanyakazi katika mapambano  dhidi ya Malaria.
 Wageni waalikwa wakiwa katika maadhimisho ya Siku ya Malaria Duniani
 Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid , akimkabidhi Meneja Vipaji wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Lillian Makau (kulia) jinsi kampuni hiyo inavyoshiriki katika mapambano dhidi ya malaria kwa kuisaidia jamii na wafanyakazi wake, alipotembelea banda la TBL wakati wa maadhimisho ya Siku ya Malaria Duniani, Dar es Salaam jana. Katikati ni Katibu wa Afya wa TBL, James Lyimo. Wa pili kulia ni Meneja Uhusiano wa TBL, Editha Mushi.
 Katibu wa Afya wa TBL, James (kushoto0 akijadiliana jambo na Meneja Uhusiano wa TBL, Editha Mushi wakati wa maadhimisho hayo.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa taasisi mbalimbali zinazoshirikiana na serikali katika mapambano dhidi ya Malaria nchini.Mstari wa mbele kutoka kulia ni Athuman Mfutakamba, Waziri Dk. Rashid  Balozi wa Malaria nchini, Leodgar Tenga.PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG

*MAKAMU WA RAIS MGENI RASMI MAADHIMISHO YA SIKU YA USALAMA NA AFYA DUNIANI,KATIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA DAR

April 28, 2014

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na viongozi mbalimbali alipowasili kwenye viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam leo April 28-2014, kwa ajili ya kuhutubia wananchi kwenye maadhimisho ya siku ya usalama na Afya Duniani.
 Afisa mkuu mwandamizi wa mazingira katika mamlaka ya Bandari Thobias Sonda akimpa maelezo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, juu ya utumiaji wa vifaa vya kupimia hewa, wakati alipotembelea Banda la maabara ya mkemia mkuu wa Serikali kwenye Maonesho ya maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya  Duniani yaliyoadhimishwa leo April 28-2014, Viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es salaam.  
 Mtaalam wa uchunguzi wa vyakula katika maabara ya mkemia mkuu wa Serikali Edith Wilbald akimpa maelezo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipotembelea Banda la maabara ya uchunguzi wa vyakula kwenye Maonesho ya maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya  Duniani.
 Mtaalam wa uchimbaji wa madini katika mgodi wa Noth Mara Gold Mine Paul Kagodi akimuonesha Makamu wa Rais vifaa vinavyotumika katika kazi ya uchimbaji wa madini wakati alipotembelea mabanda ya Maonesho kwenye maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya  Duniani yaliyoadhimishwa leo.
 Watumishi wa taasisi mbalimbali wakiwa kwenye maandamano ya maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya Duniani yaliyoadhimishwa leo April 28-2014 kwenye viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam.
 Watumishi wa taasisi mbalimbali wakiwa kwenye maandamano ya maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya Duniani yaliyoadhimishwa leo April 28-2014 kwenye viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam.
 Watumishi wa taasisi mbalimbali wakiwa kwenye maandamano ya maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya Duniani yaliyoadhimishwa leo April 28-2014 kwenye viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea maandamano kwenye maaadhimisho ya siku ya Usalama na Afya yaliyoadhimishwa leo April 28-2014  katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam.
 Wanamuziki wa bendi ya 'OUT Jaz Band' wakitumbuiza kwenye maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya Mahali pa kazi Duniani  yaliyoadhimishwa leo.
 Katibu Mkuu wa Shirikisho la Wafanyakazi Nicolas Mgaya akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya Mahali pa kazi Duniani  yaliyoadhimishwa leo April 28-2014  katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabizi zawadi K. Lwakatare mkuu wa usalama na mazingira Vodacom kwenye maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya yaliyoadhimishwa leo April 28-2014  katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabizi zawadi maalum Naibu Waziri wa Kazi na Ajira Mhe. Makongoro Mahanga wakati wa  maaadhimisho ya siku ya Usalama na Afya Mahali pa kazi Duniani yaliyoadhimishwa leo April 28-2014  katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam.
 Makamu wa Rais, Dkt. Bilal, akihutubia kwenye hafla hiyo.
 Picha ya pamoja...
 Picha ya pamoja....

BLACK BURN MABINGWA WAPYA WA NSSF CUP PANGANI

April 28, 2014
NAHODHA WA TIMU YA BLACK BURN AMBAO NI MABINGWA WAPYA WA KOMBE LA NSSF CUP PANGANI AKIPOKEA KOMBE TOKA KWA MKURUGENZI UENDESHAJI NSSF,C,Cresentias Magori .
NA OSCAR ASSENGA,PANGANI
Timu ya Soka Black Burn  FC ya mjini hapa,imetwaa ubingwa wa
kombe la NSSF mwaka 2014 baada ya kuichapa Ushongo FC bao 2-1 katika mchezo wa fainali uliofanyika uwanja wa kijiji cha Mwera.
 
BAADA YA KUKABIDHIWA KOMBE WAKAPIGA PICHA YA PAMOJA.

Mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa kutokana na timu hizo mbili kuwa na upinzani wa jadi ulishuhudiwa na mamia ya mashabiki walioongozwa na Naibu Mkurugenzi wa NSSF,Cresentias Magori .
Black Burn ndiyo iliyokuwa ya kwanza kuliona lango la wapinzani wao Ushongo FC baada ya Farid Nassoro kufunga bao dakika ya 49
lililotokana na shuti lililopita katikati ya walinzi na kumchanganya
mlinda mlango wa Ushongo,Sebastian Charles .


Dakika ya 60 uwanja huo ulilipuka kwa kushangiliwa baada ya
mshambuliaji,Amour Janja kuipatia timu yake ya Usongo FC ambayo ilikuwa ikichezea katika uwanja wake wa nyumbani kupachika wavuni bao la kusawazisha.
MENEJA WA NSSF MKOA WA TANGA,FRANK MADUGA  kulia akipiga picha na mwamuzi bora mara baada ya kukabidhiwa zawadi yake ya mpira jana


Hata hivyo bao hilo halikudumu muda mrefu kwani dakika ya 77 Black Burn iliongeza bao la ushindi kupitia kwa Jumaa Soud ambapo hadi dakika 90 zinamalizika timu hiyo ikatoka kifua mbele kwa bao 2-1.
Kwa ushindi huo,Black burn ilikabidhiwa na Magori kombe,seti ya sare na pesa taslimu sh 200,000 na Usongo ikatwaa seti ya sare n ash 100,000 huku msindi wa tatu Mwera City ikitwaa seti moja ya sare.
Ligi hiyo ya NSSF ilianza Machi 15 mwaka huu kwa kushirikisha timu 14 ambazo zilizoingia nusu fainali ni Ushongo iliyocheza na Urafiki na kuifunga baoa 2-1 huku Blackburn FC  nayo ikiifunga Mwera City bao 2-1.
                             

SHIRIKA LA HIFADHI YA JAMII NCHINI (NSSF) WAFUNGUA TAWI JIPYA KATA YA MWERA WILAYANI PANGANI.

April 28, 2014
MKUU WA WILAYA YA PANGANI,HAFSA MTASIWA KATIKATI AKIKATA UTEPE KUASHIRIKIA UFUNGUZI WA OFGISI YA NSSF TAWI LA MWERA WILAYANI PANGANI  MWISHONI MWA WIKI KUSHOTO NI MKURUGENZI WA UENDESHAJI NSSF AMBAYE ALIMUAWAKILISHA MKURUGENZI MKUU WA NSSF KULIA WA MWISHO NI MENEJA WA NSSE MKOA WA TANGA,FRANK MADUGA

BAADA YA KUKATA UTEPE WA OFISI HIYO HAPA DC MTASIWA AKISAINI KITABU CHA WAGENI KUSHOTO NI MKURUGENZI WA UENDESHAJI NSSF CRESCENTIUS MAGORI


KABLA YA UFUNGUZI WA OFISI HIYO ALIWEZA KUSALIMIANA NA VIONGOZI MBALIMBALI WA SHIRIKA HILO

KUSHOTO NI MENEJA WA NSSF MKOA WA TANGA,FRANK MADUGA AKIMUONGOZA MKUU WA WILAYA YA PANGANI,HAFSA MTASIWA MARA BAADA YA KUMPOKEA KWA AJILI YA UFUNGUZI WA TAWI HILO


MENEJA WA NSSF MKOA WA TANGA,FRANK MADUGA AKIZUNGUMZA KATIKA HAFLA HIYO KABLA YA KUMKARIBISHA MKURUGENZI UENDESHAJI WA NSSF CRESCENTIUS MAGOTI




Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),  Crescentius Magori akizungumza jambo kwenye hafla hiyo kabla ya kumkaribisha mkuu wa wilaya ya Pangani,Hafsa Mtasiwa

MKUU WA WILAYA YA PANGANI,HAFSA MTASIWA AKIZUNGUMZA KWENYE HAFLA HIYO YA UFUNGUZI WA OFISI YA NSSF TAWI MWERA WILAYANI HUMIO
MAKAMU MWENYEKITI WA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA TANGA,SUZANI UHINGA AKIZUNGUMZA JAMBO KWENYE HAFLA HIYO



MKUU WA WILAYA YA PANGANI,HAFSA MTASIWA AKIWA KWENYE PICHA YA PAMOJA NA WAANDISHI WA HABARI WA MKOA WA TANGA MARA BAADA YA KUMALIZIKA KWA UFUNGUZI WA OFISI HIYO.

Balozi Seif Akutana na Balozi Ndogo wa China Mjini Dodoma.

April 28, 2014

 Balozi Mdogo wa Jamuhuri ya Watu wa China aliyepo Zanzibar Bwana Xie Yunliang akiwasilisha agizo la Serikali yake kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi la kuridhia na kukubali kusaidia Ujenzi wa  uwanja wa Michezo wa Mau Tse Tung uliopo Mtaa wa Mpirani - Kikwajuni Mjini Zanzibar.
 Balozi Mdogo wa China aliyepo Zanzibar Xie Yunliang akibadilishana mawazo na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Ofisini kwake ndani ya Jengo la Pius Msekwa Bungeni Mjini Dodoma.Pembeni yao upande wa kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibarf Mh. Mohamed Aboud Mohamed.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiishukuru Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa China kupitia Balozi Wake Mdogo aliyepo Zanziobar Bw. Xie Yunliang kwa kukubali wazo la SMZ la kuiomba China  kusaidia ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Mao Tse Tung Jina linalotokana na Muasisi wa Taifa hilo la China.(Picha na Hassan Issa wa – OMPR) 



Na Othman Khamis OMPR.
Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa China imeridhia na kukubali kugharamia ujenzi wa Kiwanja cha michezo kilichopewa jina na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar la Mau Tse Tung kilichopo miperani Kikwajuni Mjini Zanzibar.

Kauli hiyo imetolewa na Balozi Mdogo wa Jamuhuri ya Watu wa China aliyepo Zanzibar Bw. Xie Yunliang wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo katika Ofisi yake iliyomo ndani ya Jengo la Msekwa  Bungeni Mjini Dodoma.

Balozi Xie Junliang alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba Timu ya wataalamu wa China inatarajiwa kukifanyia utafiti na uchunguzi kiwanja hicho baadaye mwaka huu sambamba na utiwaji saini Makubaliano ya ujenzi wa kiwanja hicho unaotarajiwa kufanyika mapema mwaka ujao.

Alisema ujenzi wa uwanja huo uliopewa heshima ya Jina la Kiongozi muasisi wa Taifa la China Marehemu Mao Tse Tung utajumuisha kiwanja cha mchezo wa soka pamoja na michezo mengine ya ndani mfano mchezo wa Table Tennis.

“ Tunatarajia ujeni wa kiwanja cha Mao utakapokamilika utakuwa na uwezo wa kuhudumia wanamichezo wa michezo tofauti ukiwemo ule unaopendwa zaidi wa soka “. Alisema Bwana Xie Junliang.

Balozi Mdogo wa China aliyepo Zanzibar alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba uhusiano wa kidugu uliopo kati ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla pamoja na China unastahiki kuenziwa zaidi.

Alimuhakikishia Balozi Seif kwamba Jamuhuri ya Watu wa China itaendelea kuiunga mkono Zanzibar na Tanzania kwa ujumla katika harakati zake za kujikwamua kiuchumi.

Alisema matengenezo makubwa ya ujenzi wa Hospitali ya Abdulla Mzee iliyopo Mkoani Kisiwani Pemba, ujenzi wa maegesho ya ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar pamoja na matayarisho wa matengenezo ya chumba cha wagonjwa mahututi  { ICU } mwezi Juni mwaka huu katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja ni miongoni mwa uthibitisho wa uhusiano wa pande hizo mbili.

 Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameipongeza Jamuhuri ya Watu wa China kwa moyo wake wa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar na Tanzania kwa ujumla katika miradi ya Kiuchumi na Maendeleo.

Balozi Seif alisema mchango wa Serikali ya China kwa Zanzibar umesaidia kuiwawezesha asilimia kubwa ya Jamii Zanzibar kustawika Kijamii na hata kiuchumi kupitia miundo mbinu iliyowekwa na Serikali kwa msaada wa Nchi hiyo rafiki.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alitolea mfano msaada mkubwa uliotolewa na China katika ujenzi wa skuli za Wilaya za Sekondari katika Wilaya zote za Unguja na Pemba.

Alisema mradi huo mkubwa wa sekta ya Elimu umekuja kufuatia ongezeko kubwa la idadi wa wanafunzi wanaofanikiwa kujiunga na masomo ya Sekondari katika maeneo tofauti ya Zanzibar.

“ Kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi hasa eneo la Wilaya ya Magharibi katika Kisiwa cha Unguja tumelishuhudia hivi karibuni katika skuli ya Kijitoupele na Serikali kupitia Wizara ya Elimu tunaliangalia tatizo hilo kwa mtazamo wa kujenga skuli mpya katika Mtaa wa Pangawe “. Alisema Balozi Seif.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliipongeza China kupitia Balozi wake huyo kwa mchango wake mkubwa katika Nyanja ya Elimu mchango ambao tayari watoto wa Zanzibar wanaendelea kufaidika nao.
MASHAMBA YA BALAL KUGAWANYWA KWA WANANCHI WILAYA YA KILOMBERO.

MASHAMBA YA BALAL KUGAWANYWA KWA WANANCHI WILAYA YA KILOMBERO.

April 28, 2014
Aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), marehemu Daudi Balali.


KILOMBERO. 
Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero imeamua kufuta miliki ya mashamba yote makubwa yasiyoendelezwa na taratibu mpya zinafanyika ili kuyamilikisha kwa wananchi.
Kati ya mashamba hayo, matatu ni ya aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), marehemu Daudi Balali na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Klabu ya Simba, Marehemu Priva Mtema yaliyoko katika vijiji vya Lungungole na Merera ambayo wananchi wameshayavamia na kuendeleza shughuli za kilimo.
Akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Kilombero juzi, Mwenyekiti wake, David Ligazio alisema taratibu za kuomba hatimiliki za mashamba hayo zifutwe zinaendelea.
Ligazio alisema wamiliki wa mashamba hayo wameshapewa notisi na orodha yao imeshawasilishwa kwa Kamishna wa Ardhi ili aridhie kufutwa kwa hati za mashamba hayo.
Alisema uamuzi wa kuyataifisha umekuja baada ya halmashauri kubaini kuwa yamekuwa hayaendelezwi na hivyo kusababisha maeneo hayo kuwa misitu wakati wananchi wanahitaji maeneo ya kulima.
Alisema ukaguzi wa kumbukumbu umeonyesha kuwa idadi kubwa ya wamiliki hao hawapo wilayani Kilombero na maeneo hayo yanamilikiwa kwa hati za muda mrefu bila kufuata taratibu.
Alisema utaratibu unaofanyika sasa ni kuwaagiza watendaji na wenyeviti wa vijiji, kuanisha ukubwa halisi wa mashamba hayo ili kurahisisha kazi ya kuyagawa kwa wananchi katika siku zijazo.
Akizungumzia hatua hiyo, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka alisema taarifa hiyo haijafika ofisini kwake, lakini akabainisha kuwa kuna watu wengi wanaomiliki ardhi kubwa mkoani Morogoro bila kuwa na hatimiliki wala kufuata taratibu huku wakiwa wanawatisha wananchi.
Aliwataka wananchi hao kujisimamia, waondoe unyonge na kuzingatia taratibu za ardhi, kwamba inatakiwa kugawiwa kupitia mkutano mkuu wa kijiji, vinginevyo wana haki ya kujitwalia maeneo hayo na kufanya maendeleo mengine.
“Kuna matukio unakuta mtu anakaa na mwenyekiti wa kijiji na kujifungia, wanajadili wenyewe na kugawiana maeneo ya kijiji bila kuwashirikisha wananchi, hawa wananchi wanatakiwa kukataa hali hiyo,” alisema.
Maeneo yanayogawiwa
Mwenyekiti wa halmashauri aliyataja maeneo mashamba yanayotakiwa kugawanywa kwa wananchi na ukubwa wake katika mabano kuwa ni Lungongole (ekari 375) na Merea (ekari 373). 

Pia kuna shamba lenye ukubwa wa hekta 887 linalomilikiwa na Balali, ekari 491 zinazomilikiwa na George Teni katika Kijiji cha Kisegese na ekari 500 zinazomilikiwa na Aloyce Lyenga katika Kijiji cha Idete.MWANANCHI

JK AWAVISHA NISHANI ZA MUUNGANO MIAKA 50 IKULU DAR

April 28, 2014


 Makamanda wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa tanzania (JWTZ), wakiwa katika viwanaja vya Ikulu wakisubili kuanza kwa dhifa ya kutunuku nishani za muungano wa miaka 50



 Dk. Mwele Malecela, akisubili kukabishiwa nishani ya baba yake Samuel Malecela, ambaye yeye hakuwepo
Waalikwa wakiwa katika dhifa hiyo
Mkuu wa Pili wa Majeshi Nchini Jenerali Mstaafu David Musuguri, akiwasalimia makamanda baada ya kuwasili katika dhifa hiyo.
 Mzee david Msuya, akisubili kukabidhiwa
 M\zee Joseph Sinde Warioba au mze wa Serikali tatu, akisubili naye kukabidhi nishani

 Mzee Jenerali david Musuguri akiwa amekaa sambamba na Mkuu wa kwanza wa majeshi Jenerali Mirisho Sarakikya
 Tajiri namba tatu nchini Reginald Mengi, akisubili naye kukabidhiwa nishani kwa Utu wake wa  kuwajari watanzania wenzake

mama Fatma Karume, akisalimiana na Mwele na kulia ni mama maria Nyerere

Mama Salma Kikwete (katikati), akiwa katika dhifa hiyo
 Wapambe wa viongozi wakiwa katika dhifa hiyo
 Rais Mstaafu wa zanzibar Dk, Salimin Amour, akiwasili katika dhifa hiyo
 Viongozi wakiimba  wimbo wa Taifa kabla ya dhifa kuanza
 Rais Jakaya Kikwete naye akiimba wimbo wa taifa

 Viongozi wakifuatilia majina ya watunukiwa
 mama maria Nyerere, akitunukiwa


Mama Fatma karume, akitunukuwa

 Mtoto wa Rais Mstaaf Ali Hassan Mwinyi akitunukiwa  kwa niaba ya baba yake
Mzee William Makapa, akitunukiwa


 Mwele akikabidhiwa
Mzee David Msuya, akitunukiwa

Mzee Warioba, akienda kutunukiwa


 Rais Mstaafu wa Zanzibar, Aman Abeid karume, akitunukiwa


 Mtoto wa Marehemu Edward Moringe Sokoine, akitunukiwa kwa niaba ya baba yake
 Mzee Salim Ahemed Salim, akitunukiwa

 Waziri Kiongozi Mstaafu wa Zanzizibar, akitunukiwa
 Shamsi Vuai nahodha, akitunukiwa




 Rais akipumzika kidogo







 Mtoto wa marehemu paul Bomani, akikabidhiwa tuzo kwa niaba ya baba yake





 Geroge Kahama, akikabidhiwa
 Mzee Job Lusinde, akikabidhiwa