*RAIS KIKWETE AONGOZA MAMIA KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MAREHEMU MEJA JENERALI KEVIN MSEMWA LEO
Amiri
Jeshi Mkuu Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe mama Salma Kikwete
wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Kamishna wa Utafiti na
maendeleo ya Jeshi katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
marehemu Meja Jenerali Kevin Gerald Msemwa wakati wa hafla ya kuaga
mwili wake iliyofanyika katika uwanja wa makao makuu ya Jeshi la Ulinzi
la Wananchi Upanga jijini Dar es salaam leo April 6, 2014. Meja Jenerali
Msemwa alifariki April 3, 2014 katika hospitali ya Jeshi ya Lugalo
jijini Dar es salam.
Amiri
Jeshi Mkuu Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe mama Salma Kikwete
wakitoa mkono wa pole kwa wanafamilia baada ya kutoa heshima za mwisho
kwa aliyekuwa Kamishna wa Utafiti na maendeleo ya Jeshi katika Wizara ya
Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa marehemu Kevin Gerald Msemwa wakati
wa hafla ya kuaga mwili wake iliyofanyika katika uwanja wa makao makuu
ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi Upanga jijini Dar es salaam leo April 6,
2014. Meja Jenerali Msemwa alifariki April 3, 2014 katika hospitali ya Jeshi ya Lugalo jijini Dar es salam.
*MATUKIO YA ZOEZI LA UPIGAJI KURA JIMBO LA CHALINZE LEO, RAIS JAKAYA NA MAMA SALMA WAPIGA KURA
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya mrisho Kikwete akisoma
karatasi ya kupigia kura kabla ya kupia kura kumchagua Mbunge wa Jimbo
la Chalinze kwenye kituo cha kupigia kura cha Zahanati Msoga.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiwa kwenye chumba cha kupigia kura wakati wa
kupiga kura za kumchagua Mbunge mpya wa Jimbo la Chalinze.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga kura yake ya kumchagua Mbunge mpya wa Jimbo la Chalinze.
YANGA YAIBANJUA JKT RUVU MABAO 5-1 UWANJA WA TAIFA
Mshambuliaji
wa Yanga, Simon Msuva, akiruka kukwepa kwanja la beki wa JKT Ruvu,
wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, uliomalizika hivi punde
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo Yanga
imeibuka na ushindi mnono wa mabao 5-1. Mabao matatu yalifungwa na
Mrisho Ngassa, katika dakika ya 7, Dakika ya 15 na Dakika ya 48.
KMKM BINGWA MPYA LIGI KUU ZANZIBAR
Na Abdi Suleiman, Pemba
KMKM imeweza kutetea taji la ubingwa wa soka Zanzibar, baada ya leo jioni kuikong’ota Chipukizi mabao 3-2 katika mchezo wa mwisho wa ligi kuu ya Grand Malt Zanzibar 2013/2014 uliopigwa uwanja wa Gombani Pemba.
KMKM imeweza kutetea taji la ubingwa wa soka Zanzibar, baada ya leo jioni kuikong’ota Chipukizi mabao 3-2 katika mchezo wa mwisho wa ligi kuu ya Grand Malt Zanzibar 2013/2014 uliopigwa uwanja wa Gombani Pemba.
Mabaharia hao wanapaswa kuishukuru pia timu ya Jamhuri ambayo iliilaza Polisi bao 1-0 katika uwanjawa Amani, na kuwasafishia njia washika magendo hao kulipeleka tena kombe la ubingwa makao makuu yao mtaa wa Kibweni.
Subscribe to:
Posts (Atom)