HUSSEIN MSOPA: Sharifu majini aliyejikita kuwaombea wenye matatizo

September 19, 2016
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
“IKIWA hujawahi kupata tatizo huwezi jua kama wapo binadamu wenzetu wanaotabika kusaka dawa au vitu vinavyoweza kuwaondoshea maswahibu yao yanayoendelea kuwapa wakati mgumu katika maisha yao bila kuangalia wanaishi kwa mtindo gani,”. Ndivyo alivyoanza kusema Sheikhe Hussein Msopa maarufu kama Sharifu Majini.
Chifu Hussein Msoma maarufu kama Sheikhe Sharifu Majini akiwa katika majukumu yake ya kawaida kama anavyoonekana pichani.
Ndio, sheikhe huyo mwenye maskani yake Mabibo Mwisho, jijini Dar es Salaam, unaweza kushangazwa na idadi kubwa ya watu wanaotembelea katika ofisi ya sheikhe hiyo, huku kila mmoja wake akiwa na shida yake inayohitaji utatuzi. Kwa wale ambao hawajui lolote kuhusu sheikhe Sharifu majini, pindi wanapopita katika mtaa huo, wanaweza kudhani labda kuna harusi, msiba ayu shughuli yoyote ya kijamii kutokana na ingia tokay a watu katika nyumba ya sheikhe huyo inayotoa huduma mbalimbali za kuombea watu, kuwapatia dawa zikiwamo zinazohusiana na mambo ya majini.
Sheikhe Sharifu Majini pichani.
Watu wanaweza kushangaa au kujiuliza. Je, ni kweli mtu mwenye tatizo anaweza kupata ufumbuzi wa shida yake atakapomuona sheikhe huyo? Katika mazungumzo na mtandao huu yaliyofanyika wiki iliyopita, sheikhe Sharifu anasema kwamba amedhamiria kuwakomboa wale wenye mahitaji na matatizo yanayohusu majini, ukosefu wa uzazi kwa njia za ushirikiana, kusumbuliwa na majini pamoja na kuzitafsiri ndoto mbalimbali zinazohusiana na mifumo ya maisha ya mwanadamu. Sheikhe huyo anasema kwamba uamuzi wake wa kuamua kujihusisha na masuala hayo umetokana na kufahamu adha kubwa inayowakumba binadamu, jambo linalowafanya waishi kwa mashaka katika kipindi chote cha maisha yao.
“Mtu anaweza kwenda hospitali kufanya uchunguzi wa afya ya matatizo ya uzazi na kukuta hana tatizo lolote. Lakini kila anavyojitahidi ili ashike mimba kwa ajili ya kufurahisha nafsi au ndoa yake anajikuta anashindwa kufanikiwa.

MWENGE WA UHURU WAPITA KATIKA MIRADI 9 WILAYANI IKUNGI

September 19, 2016


Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe Geofrey Mwambe akimkabidhi Mwenge wa uhuru  mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu (Kulia).
 Wananchi wakifatilia kwa karibu makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru kutoka Wilayani manyoni kuhamia Wilayani Ikungi
Mkimbiza Mwenge Kitaifa Lucia vitalis Kamafa kutoka Manyara akiuhifadhi mwenge huo kwenye sehemu yake ya kuhifadhiwa

JESHI LA POLISI KILIMANJARO LAWATUNUKU ZAWADI ASAKARI WAKE 34

September 19, 2016
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadiq akipokea salamu za heshima kutoka kwa askari wakati wa gwaride maalum lililoandaliwa wakati wa hafla fupi ya kutunuku zawadi kwa askari 34 wa vyeo mbalimbali waliotekeleza vyema majukumu yao.kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro ,Wilbroad Mutafungwa.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Saidiq akikagua gwaride la heshima baada ya kuwasili katika viwanja vya kikosi cha kutuliza ghasia mjini Moshi kwa ajili ya hafla ya kuwapongeza na kutunuku zawadi kwa asakari 34 waliotekeleza vyema majukumu yao.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Saidiq akihitimisha ukaguzi wakati wa gwaride maalumu lililoandaliwa kwa ajili ya kuwapongeza asakari walitekeleza vyema majukumu yao.
Gwaride likitoka kwa mwendo wa haraka mara baada ya kumalizika kwa ukaguzi.
Ofisa Mnadhimu wa jeshi la Polisi  mkoa wa Kilimanjaro,Koka Moita akizungumza wakati wa hafla ya kuwapongeza na kutunuku zawadi kwa asakari 34 wa jeshi hilo waliotekeleza vyema majukumu yao.
Baadhi ya maofisa wa jeshi la Polisi wakifuatilia matukio katika hafla hiyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutafungwa akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi kwa askari 34  waliotekeleza vyema majukumu yao.
Baadhi ya wageni waalikwa katika hafla hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Said Mecky Sadiq akizungumza wakati wa hafla ya kuwapongeza na kutunuku zawadi kwa asakari 34 waliotekeleza vyema majukumu yao.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutafungwa akimuoneesha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadiq baadhi ya silaha zilizokamatwa hivi karibuni zikidaiwa kutumika katika vitendo vya uharifu.
Mkuu wa Kitengo cha dawa za kulevya cha jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Mkaguzi wa Polisi,Ezekiel Midala akimuonesha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro sehemu ya dawa za kulevya zilizokamatwa na jeshi hilo.
Baadhi ya askari waliotunukuwa zawadi kwa utendaji kazi mzuri wakisonga mbele kwa ajili ya kutunukiwa zawadi.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadiq akitunuku zawadi kwa baadhi ya askari waliofanya vizuri katika kutekeleza majukumu yao.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Utalii ya Asante Tours ,Cuthbert Swai akizungumza wakati wa hafla ya kuwapongeza na kutoa zawadi kwa asakari waliofanya vizuri wakati wa kutekeleza majukumu yao.
Pikipiki mbili aina ya Fekon zilizotolewa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Utalii ya Asante Tours ,Cuthbert Swai kusaidia jeshi la Polisi katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadiq akiwa ameketi juu ya pikipiki na kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Kamishana Mwandamizi Msaidizi wa Polisi,Wilbroad Mutafungwa wakati wa hafla ya kuwapongeza na kutoa zawadi kwa askari  34 wa jeshi hilo mjini Moshi.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadiq akitoa cheti kwa Mkurugenzi wa kampuni ya Ibraline ,Ibrahim Shayo akitambua mchango wa wadau kwa jeshi la Polisi. 

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.
VPL: AFRICAN LYON, TOTO AFRICAN KESHO

VPL: AFRICAN LYON, TOTO AFRICAN KESHO

September 19, 2016

Mzunguko wa tano wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania (VPL) utafungwa kesho Jumanne Septemba 20, 2016 kwa mchezo kati ya African Lyon ya Dar es Salaam na Toto African ya Mwanza kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. African Lyon inaingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu nzuri ya kuilaza Mbao FC mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam wakati Toto African ilitoka kufungwa 1-0 na Tanzania Prisons ya Mbeya.

Raundi ya sita utapigwa Septemba 24, 2016 na Septemba 25, 2016 kwa michezo mitano siku ya Jumamosi na mitatu siku ya Jumapili. Siku ya Jumamosi JKT Ruvu itaikaribisha Mbeya City kwenye Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani wakati Simba itakuwa mwenyeji wa Majimaji ya Songea kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Azam FC itasafiri hadi Mtwara kwenda kucheza na Ndanda kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona wakati Mwadui ya Shinyanga itakuwa mgeni wa Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya na Mtibwa Sugar itakuwa mwenyeji wa Mbao FC ya Mwanza kwenye Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro.
Siku ya Jumapili, Septemba 25, mwaka huu Ruvu Shooting inatarajiwa kuikaribisha Toto African kwenye Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani huku Stand United ikiwa mwenyeji wa Young Africans katika dimba la CCM Kambarage wakati Kagera Sugar itakuwa jijini Dar es Salaam kwenye Uwanja wa Uhuru ikicheza na African Lyon.

RAIS DKT. MAGUFULI AMJULIA HALI SPIKA MSTAAFU SAMUEL SITTA PIA ATEMBELEA KWA KUSHTUKIZA OFISI ZA MAGAZETI YA UHURU NA MZALENDO JIJINI DAR ES SALAAM

September 19, 2016


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samuel Sitta anayeendelea kupata matibabu jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Mke wa Mzee Sitta, Mama Margaret Sitta. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na  Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samuel Sitta mara baada ya kumjulia hali jijini Dar es Salaam.
 Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samuel Sitta akiongoza Sala mara baada ya kujuliwa hali na Rais Dkt. John Pombe Magufuli.kushoto ni Mke wa Mzee Sitta, Mama Margaret Sitta.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana wakati akitoka katika Ofisi Ndogo za CCM Lumumba jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana wakielekea kwenye Ofisi za Magazeti ya Uhuru na Mzalendo zilizopo katika mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akiwasikiliza wafanyakazi wa Magazeti ya Uhuru na Mzalendo mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika ofisi za Magazeti hayo zilizopo Lumumba jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo wakati akizungumza na Wafanyakazi hao wa Magazeti ya Uhuru na Mzalendo mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana wakwaza (kulia) pamoja na Kaimu Mhariri Mtendaji wa Magazeti hayo Ramadhani Mkoma wakwanza (kushoto) wakiomba dua mara baada ya kumaliza kuzungumza na wafanyakazi hao jijini Dar es Salaam
 . Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameshikana mikono na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kushoto pamoja na Msemaji wa  CCM Christopher Ole Sendeka mara baada ya kuzungumza na wafanyakazi wa Magazeti ya Uhuru na Mzalendo jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwashukuru wakaazi mbalimbali wa jijini Dar es Salaam waliokuwa wakimsubiri nje mara baada ya kuskia kuwa amefanya ziara ya kushtukiza katika ofisi za Magazeti ya Uhuru na Mzalendo jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU
DIAMOND TRUST BANK YADHAMINI LIGI KUU YA VODACOM

DIAMOND TRUST BANK YADHAMINI LIGI KUU YA VODACOM

September 19, 2016
Benki ya Diamond Trust (DTB) leo imesaini kuingia mkataba na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kudhamini Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (VPL) kwa msimu wa mwaka 2016/2017.
DTB inaungana na mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) pamoja na wadhamini wengine katika kudhamini ligi hiyo maarufu kama Ligi Kuu ya Vodacom.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye hafla ya utiaji saini huo iliyofanyika Hoteli ya Serena, Mkuu wa Kitengo cha Fedha wa Benki hiyo, Joseph Mabusi amesema:  “Udhamini huu utasaidia zaidi maendeleo ya soka nchini kwa kuziwezesha timu timu shiriki pamoja na jitihada zingine za TFF. Soka inaunganisha Watanzania wa matabaka mbalimbali ambao ni wateja wetu na si kama benki tungependa kuwa karibu nao zaidi kupitia mchezo huu.”
Mabusi aliongeza kwa kusema:  “Tunafurahi na kujivunia kuwa sehemu ya ligi kuu na tunaamini udhamini huu utazidisha ari ya kuwahudumia Watanzania wote.
Benki ya Diamond Trust imekuwa ikiipa kipaumbele michezo mbalimbali ikiwemo soka, ambapo timu rasmi ya soka inayoundwa na Wafanyakazi imefanikiwa kushinda vikombe na mataji mbalimbali ya soka likiwemo taji la ligi ya mabenki nchini inayojulikana kama BRAZUKA KIBENKI mwaka 2015 pamoja na ngao ya hisani ya ligi hiyo mwaka 2016.
Benki pia inadhamini timu ya soka ya Agathon iliyopo Mbagala inayoshiriki ligi soka daraja la tatu. Zaidi ya hayo benki pia inajivunia kuwa moja kati ya wadhamini wa michuano ya CECAFA Kagame Cup mwaka 2015.
Ligi hiyo inajumuisha timu 16 kutoka Tanzania bara zinazocheza kwa mfumo wa mechi za nyumbani na ugenini ambazo ni Young Africans, Simba Sports Club, Azam FC, Mtibwa Sugar, Kagera Sugar, Mbeya City, Majimaji, MbaoFC, African Lyon, JKT Ruvu, Ruvu Shooting, Tanzania Prisons, Stand United, mwadui FC, Ndanda FC na Toto Africans.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa Shirikisho la Soka Tanznaia –TFF wakiongozwa na Rais wao Ndugu Jamal Malinzi, Wafanyakazi wa Benki ya DTB, wawakilishi kutoka Vodacom, wadau mbalimbali wa soka pamoja na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini.
Malinzi ameshukuru na kuupongeza udhamini huo uliotolewa na benki hiyo na pia ameziomba taasisi nyingine kuiga mfano huo ili kukuza soka nchini. “Kwa heshima ana furaha kubwa nawakaribisha DTB Tanzania kwenye ligi kuu na familia ya TFF kwa ujumla.”
Benki ya Diamond Trust ina matawi 25 nchini, ikiwa na matawi kumi na moja (11) jijini Dar es Salaam (Mtaawa Jamaat, Masaki, Morocco, Magomeni, Mbezi, Mbagala, barabara ya Nyerere, Msimbazi - Kariakoo, barabara ya Nelson Mandela, Upanga katika barabara ya umoja wa mataifa na katika makutano ya barabara ya Mirambo na mtaa wa Samora).
Vile vile ina matawi katika miji ya Arusha (2), Mwanza (2) na katika miji ya Dodoma, Kahama, Mbeya, Morogoro, Moshi, Mtwara, Mwanza, Tabora ,Tanga na Zanzibar.
DTB Tanzania ni mshirika wa mtandao wa maendeleo ya kiuchumi wa Aga Khan - Aga Khan Fund for Economic Development (AKFED) ambao ni sehemu ya mtandao wa maendeleowa Aga Khan Development Network).
DTB Kenya ni miongoni mwa wanahisa muhimu wa DTB Tanzania.

DTB Tanzania pia ni sehemu ya mtandao wa mabenki ya DTB Group yenye matawi zaidi ya 120 Afrika Mashariki na kati.

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA AFANYA ZIARA MKOANI MWANZA NA KUAHIDI KUTATUA CHANGAMOTO ZA ASKARI NCHINI.

September 19, 2016
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe.Mwigulu Nchemba, alipofanya ziara kwenye makazi ya askari ya kigoto yalipopo Kata ya kirumba Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza hii leo.
Na George Binagi-GB Pazzo @BMG

WAZIRI MBARAWA AMEMTEUA DKT. MUSA MGWATU KUWA MTENDAJI MKUU WA TEMESA.

September 19, 2016

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchuzi na Mawasiliano (Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame M. Mbarawa(Mb), amemteua Dkt. Musa Mgwatu kuwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA). 

Dkt. Mgwatu amechukua nafasi ya Mhandisi Marcellin Magesa  ambaye amepangiwa majukumu mengine  Wizarani.

Kabla ya Uteuzi huo Dkt. Mgwatu alikuwa  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika Hodhi la Rasilimali za Reli (RAHCO).

Katika hatua nyingine Profesa Mbarawa amemteua Bw. Masanja Kadogosa ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRL) Kukaimu nafasi ya Mtendaji Mkuu wa RAHCO.
Uteuzi huo unaanza mara moja.
Imetolewa na
Eng. Joseph M. Nyamhanga
Katibu Mkuu (Ujenzi)
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

DK. MAGUFULI ATINGA OFISINI KWAKE LEO, AKUTANA NA WAFANYAKAZI WA UHURU

September 19, 2016
index

Mwenyekiti wa CCM, Ras Dk. John Magufuli akiwapungia mkono wananachi waliokuwa na shauku ya kumuona wakati akitoka katika ofisi yake, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam, leo, Septemba 19, 2016.  Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana. (Picha na Bashir Nkoromo).
bn647192

Mwenyekiti wa  CCM Rais Dk. John Magufuli akiwasalimia wananchi waliojitokeza katika Mtaa wa Lumumba, Dar es Salaam, wakati akitoka Ofisini kwake, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, katika Mtaa huo, kwenda Ofisi za Kampuni ya Uhuru Publications Limited, Wachapishaji wa Magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani  leo. Dk. Magufuli alifika katika ofisi yake leo kufanya kazi zake za kichama kwa nafasi yake ya Mwenyekiti wa CCM.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli akifuatana na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipowasili katika Ofisi za Uhuru Publications Limited mtaa wa Lumumba, Da es Salaam, ambako baada ya kutembelea baadhi ya ofusi za kampuni hiyo alizungumza na wafanyakazi ambapo ameahidi kutatua kero zinazowakabili kwa muavuli wake wa uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli akifuatana na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipowasili katika Ofisi za Uhuru Publications Limited mtaa wa Lumumba, Da es Salaam, ambako baada ya kutembelea baadhi ya ofusi za kampuni hiyo alizungumza na wafanyakazi ambapo ameahidi kutatua kero zinazowakabili kwa muavuli wake wa uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli akiwasilikiliza  wafanyakazi wa UPL alipowasili katika ofisi hizo leo. Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana
Mkuu wa Kitengo cha  kompyuta, wa UPL, Moses Makambi akimpatia maelezo Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli, alipoingia chumba cha Usanifu wa kurasa,   
Mkuu wa Kitengo cha  kompyuta, wa UPL, Moses Makambi akimpatia maelezo Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli, alipoingia chumba cha Usanifu wa kurasa,   
Mkuu wa Kitengo cha  kompyuta, wa UPL, Moses Makambi akimpatia maelezo Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli, alipoingia chumba cha Usanifu wa kurasa,   Kushoto ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana
Kaimu Mharuri Mtendaji wa UPL. Ramadhani Mkoma akiongoza  Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli kuingia katika chumba cha habari kuzungumza na wafanyakazi
Mwenyekiti wa CCM, Rais John  Magufuli akiingia katika chumba cha Habari cha Uhuru Publications kuzungumza na wafanyakazi
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpatia maelezo ya utangulizi, Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli. Kushoto ni Kaimu Mhariri Mtendaji, wa UPL Ramadhani Mkoma
Wafanyakazi wakiwa ukumbini
Wafanyakazi wakifuatilia kwa makini  mazungumzo yao na Rais Dk. Magufuli
Mwenyekiti wa CCM, Dk. John Magufuliu akiandika wakati Kaimu Mhariri Mtendaji wa UPL Ramadhani Mkoma akieleza changamoto zinazowakabili wafanyakazi katika utendaji kazi wao wa kila siku
Baadhi ya wafanyakazi wakishangilia baada ya Mwenyekiti wa CCM, Dk. John Magufuli kuahidi kushughulikia kero zao kwa nafasi yake ya Ueneyekiti wa CCm
Mwenyekiti wa CCM Rais Dk. Magufuli akimsikiliza Kaimu Mhasibu Mkuu wa UPL huku akinukuu dondoo muhimu
Mwenyekiti wa Chama Cha Wafayakazi wa UPL cha RAAWU, Moses Makambi akieleza changamoto kwa Dk. Magufuli
Ukumbi wakati wa mkutano wa wafanyakazi wa UPL na Mwenyekiti wa CCM, Dk. Magufuli
Katibu Mkuu wa CCM, akimfafanulia jambo Dk. Magufuli