Picha za Matukio ya Mechi ya Jana kati ya Coastal Union na JKT Ruvu ya Mlandizi mkoani Pwani.

April 16, 2013

 



Coastal Union na JKT Ruvu hakuna mbabe watoka suluhu pacha.

April 16, 2013
Picha wachezaji wakiwa kwenye uwanja wa mkwakwani wakati wa mechi hiyo iliyochezwa jana kwenye uwanja wa Mkwakwani.

Wazee wa kazi wakiwa katika pozi

April 16, 2013
Viogozi wa chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Tanga waliokutwa na mpiga picha wa blog hii wakibadilishana mawazo,kutoka kulia ni Katibu wa Wazazi mkoa wa Tanga,katikati ni Katibu Itikadi na Uenezi chama hichi wilaya ya Tanga,Ndugu Kapange,Picha na Mwanmdishi wetu
TAARIFA ZA LEO KUTOKA TFF.

TAARIFA ZA LEO KUTOKA TFF.

April 16, 2013
Habari zote na Boniface Wambura,Dar es Salaam.
RAMBIRAMBI MSIBA WA MEJA JENERALI MAKAME RASHID

Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko za kifo cha Mkuu wa zamani wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Makame Rashid kilichotokea juzi (Aprili 14 mwaka huu) kutokana na maradhi jijini Dar es Salaam.

 Rais wa TFF, Leodegar Tenga amesema msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kutokana na mchango aliotoa Meja Jenerali Makame Rashid ikiwemo kuwa mlezi wa timu ya Ruvu Stars wakati huo akiwa Kamanda (CO) wa Kikosi cha Ruvu JKT.

Pia aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Mdhamini (Trustee) wa TFF wakati huo ikiitwa Chama cha Mpira wa Miguu Tanzania (FAT) na wakati akiwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya katika miaka ya themanini alikuwa sehemu ya mafanikio kwa timu ya Tukuyu Stars ya Mbeya iliyotwaa ubingwa wa Tanzania Bara mwaka 1987 ikiwa ndiyo kwanza imepanda kucheza Ligi Kuu wakati huo ikiitwa Ligi Daraja la Kwanza.

TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Meja Jenerali Makame Rashid, Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

 Maziko yanatarajiwa kufanyika leo (Aprili 16 mwaka huu) nyumbani kwao mkoani Mtwara. Mungu aiweke roho ya marehemu Sembwana mahali pema peponi. Amina

 MWISHO

VPL KUTIMUA VUMBI VIWANJA VITATU

Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaendelea kesho (Aprili 17 mwaka huu) kwenye viwanja vitatu huku vinara wa ligi hiyo Yanga wakifukuzia ubingwa huo jijini Tanga.

 Yanga inayoongoza ligi ikiwa na pointi 52 itakuwa mgeni wa Mgambo Shooting katika mechi itakayochezeshwa na mwamuzi Athuman Lazi kutoka Morogoro kwenye Uwanja wa Mkwakwani. Waamuzi wasaidizi wa mechi hiyo ni Michael Mkongwa wa Iringa na Godfrey Kihwili wa Arusha wakati Kamishna wa mechi hiyo ni Godbless Kimaro kutoka Moshi.

Kagera Sugar na Toto Africans zitaumana kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba katika mechi namba 164 itakayokuwa chini ya mwamuzi Martin Saanya wa Morogoro.

 Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro, na wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 4,000 utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Mtibwa Sugar yenye pointi 33 na Oljoro JKT yenye pointi 28.

Israel Nkongo kutoka Dar es Salaam ndiye atakayechezesha mechi hiyo akisaidiwa na Hamis Chang’walu (Dar es Salaam) na John Kanyenye (Mbeya). Kamishna wa mechi hiyo ni Ramadhan Mahano kutoka Iringa.

 MWISHO

AS FAR KUWASILI KESHO KUIKABILI AZAM

Wapinzani wa Azam katika michuano ya Kombe la Shirikisho, AS FAR Rabat ya Morocco wanatarajiwa kutua nchini kesho (Aprili 17 mwaka huu) saa 7 mchana kwa ndege ya Emirates.

Msafara wa timu hiyo wenye watu 28 utafikia hoteli ya Sapphire iliyoko maeneo ya Kariakoo, Dar es Salaam tayari kwa mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili itakayochezwa Jumamosi (Aprili 20 mwaka huu) saa 10 kamili jioni Uwanja wa Taifa.

MWISHO.

Wazee wa Uturuki wakifanya mazoezi leo kujiandaa na mechi yao na Mgambo Shooting kesho.

April 16, 2013

Hapa ni mazoezi tu.

April 16, 2013
Kocha Mkuu wa timu ya Yanga,Ernest Brandty akiwa anasimamia mazoezi ya timu hiyo leo kwenye uwanja wa Mkwakwani ambapo timu hiyo kesho inatarajiwa kucheza na Mgambo Shooting kwenye uwanja huo.Picha na Mwandishi wetu.

Picha za Yanga Mazoezini Mkwakwani

April 16, 2013
KLABU ya Yanga wakimsikiliza kocha mkuu wa timu hiyo,Ernest Brandty jana kabla ya kuanza mazoezi leo kwenye uwanja wa Mkwakwani ambapo mazoezi hayo yalianza saa nne kamili asubuhi,Picha na Mwandishi Wetu.