WAZIRI WA MAMBO YA NJE,BALOZI AUGUSTINE MAHIGA ATEMBELEA KITUO CHA MIKUTANO CHA KIMATAIFA NA LAKI LAKI ARUSHA.

December 20, 2015
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Kanda na Kimataifa,Balozi Augustine Mahiga(kulia)akiwasili kwenye  kituo cha mikutano cha  kimataifa cha Arusha International Conference Center(AICC) ambacho ni sehemu ya Wizara hiyo,kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa AICC,Elishilia Kaaya.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Kanda na Kimataifa,Balozi Augustine Mahiga akisaini kitabu cha wageni.

Mkurugenzi Mtendaji wa  Arusha International Conference Center(AICC)Elishilia Kaaya(kulia) akifafanua jambo mbele Waziri Mahiga(kushoto)katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru,Wilson Kambaku

Mkurugenzi Mtendaji wa  Arusha International Conference Center(AICC)Elishilia Kaaya akifafanua jambo mbele Waziri Mahiga(wa pili kulia)wengine ni  Mkuu wa Wilaya ya Arumeru,Wilson Kambaku(kulia)Mwenyekiti wa Bodi ya AICC,Balozi Christopher Lihundi(aliyevaa tai) na Mkuu wa mawasiliano serikalini,Mindi Kasiga.

Mwenyekiti wa Bodi ya AICC,Balozi Christopher Lihundi akizungumza jambo mbele Waziri Augustine Mahiga aliyefika katika kituo hicho tangu ateuliwe kushika wadhifa huo.

Baadhi ya watumishi wa AICC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Kanda na Kimataifa,Balozi Augustine Mahiga akizungumza na wajumbe wa  Bodi ya AICC na watumishi wa kituo hicho ,kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya AICC,Balozi Christopher Lihundi na kulia ni Mkuu wa wilaya ya Arumeru,Wilson Kambaku

Mkuu wa mawasiliano serikalini,Mindi Kasiga akiongoza kipindi cha maswali kwa waandishi wa habari.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiriano wa Afrika Mashariki,Kanda na Kimataifa ,Balozi Augstine Mahiga amesema eneo la Laki Laki lililopo wilaya ya Arumeru mkoani Arusha lililotengwa kwaajili ya ujenzi wa taasisi za kimataifa utaifanya Tanzania kung'ara duniani.

Balozi Mahiga alisema hayo Desemba 19 baada ya kufanya ziara kwenye eneo hilo na Kituo cha mikutano cha kimataifa cha AICC .

Eneo hilo litajengwa Mahakama ya Kimataifa ya Kimbari(MICT)Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu(AfCHPR) na taasisi zingine na kusema ameridhishwa na hatua iliyofikiwa.

Akiwa kwenye kituo cha AICC alipokea taarifa za mradi wa ujenzi wa kituo cha mikutano cha kimataifa cha Kilimanjaro International Convention Center kitachovuta dunia Tanzania.

Pia Waziri alizungumzia hali ya kisiasa nchini  Burundi kuwa inaigusa  Tanzania na kuwa atawasiliana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC)Dk Richard Sezibera kuandaa kuandaa mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje.

HOSPITALI ZAAGIZWA KUTENGENEZA MFUMO WA MALIPO WA KIELEKTRONIKI

HOSPITALI ZAAGIZWA KUTENGENEZA MFUMO WA MALIPO WA KIELEKTRONIKI

December 20, 2015
IMG_9410
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla akifurahi jambo na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Sokoine ya Mkoa wa Lindi, Dkt. Evaristo Kasanga (kulia) wakati wa ziara ya kushtukiza aliyofanya mwishoni mwa juma mkoa wa Lindi.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
Na Mwandishi wetu, Mtwara
NAIBU Waziri katika Wizari wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamisi Kigwangalla ameagiza kubadilishwa kwa mifumo ya utawala, malipo na uendeshaji katika katika hospitali nchini ili kuleta ufanisi na tija.
Akizungumza katika ziara yake ya kujifunza kuona katika hali ya kawaida huwa zinatolewaje katika hospitali za wilaya na mikoa alisema kukosekana kwa mifumo bora ya malipo na motisha kumedumaza utumishi.
Ziara yake hiyo ambayo aliifanya katika hospitali ya mkoa wa Lindi ya Sokoine na Ile ya Mtwara ya Ligula ililenga kuona masuala mbalimbali yanayohusiana na utoaji huduma ili kuwa na nafasi ya kutengeneza hali bora zaidi kimkakati.
Alisema tatizo la upungufu wa dawa na hata raslimali watu linasababishwa na kukosekana kwa mfumo waukusanyaji mapato ulio sahihi na wenye salama ambao utawezesha pia kutoa motisha mbalimbali kwa watumishi ili kuwavutia kufanyakazi katika mikoa ya pembezoni.
Aidha alisema malipo yanayofanyika katika hospitali hizo yanatakiwa kuwa ya kielektroniki kwa kuwa imethibitishwa kila kunapokuwapo na mfumo wa malipo kielektroniki unaboresha mapato na hatimaye kuboresha ufanisi katika uendeshaji wa hospitali pamoja na kuwapo kwa huduma bora za dawa.
Pia ameagiza kuharakishwa kwa mfumo wa malipo kielektroniki kwa wateja wa Bima ili mchango wao usaidie kwa haraka utoaji wa huduma ndani ya hospitali.
Hata hivyo Naibu Waziri huyo alisema aliridhishwa na utendaji katika hospitali ya Sokoine na Ligula na kusema ufanisi wao unatokana na kuwapo kwa mipango inayowezesha kazi kufanywa.
Alisema hospitali ya Sokoine imeanzisha utaratibu wa mawasiliano ambao unawezesha daktari mahali popote pale kuitwa huku kila mmoja akijua kwamba daktari ameitwa eneo Fulani.
Alitaka hospitali nyingine nchini hasa za rufaa kuangalia mfumo wa mawasiliano ya ndani wa Hospitali ya Sokoine ili kuleta ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.
Pia alipongeza utendaji wa hospitali ya Ligula na kusema kwamba kutokana na ufanisi wao na huduma nzuri ndio maana hata wananchi wa nchi jirani wanafika katika hospitali hiyo kupata huduma.
Alisema kama kusingelikuwa na huduma bora wananchi hao wasingelivuka kuja kutafuta huduma Ligula.
Hata hivyo Naibu Waziri huyo alitaka kuwapo na utaratibu wa kudhibiti hali hiyo na kusema kwamba ni matumaini yake kuwa wataalamu wataketi pamoja na kutafuta namna ya kufanya katika mazingira hayo ya pia kuhudumia raia wa nchi jirani.
Naye Mganga Mkuu wa Hospitali ya Ligula ya mkoa wa Mtwara, Dkt. Shaibu Maarifa, alisema kwamba pamoja na huduma wanazotoa wanakabiliwa na changamoto kadha hasa wodi ya wanawake na wajawazito.
Alisema kutokana na ongezeko la watu katika mji wa Mtwara kutokana na kuwapo kwa fursa kubwa za uchumi wa gesi na kiwanda cha saruji cha Dangote, wafanyakazi wamekuwa wakifika na familia zao na hivyo kwa sasa wodi hiyo haitoshi.
Hata hivyo alisema hali ingekuwa mbaya zaidi kama kituo cha afya cha Lipombe kisingesaidiana na hospitali hiyo.
Alisema wodi ya watoto kwa sasa inafanyiwa ukarabati na benki ya Eco na wana mkakati mwingine wa kuomba msaada wa kuondoa ufinyu wa wodi ya wanawake.
Alisema anashukuru Katibu Tawala wa mkoa wa Mtwara, Alfred Luwanda na Mkuu wa mkoa wameshafika katika hospitali hiyo na wameahidi kufanya kila linalowezekana kuhakikisha kwamba matatizo yake yanatatuliwa na kukidhi hospitali ya rufaa.
Kuhusu upatikanaji wa dawa alisema kwamba hospitali hiyo wa sasa ina akiba ya kutosha baada ya serikali kuipelekea sh milioni 80 na tayari wameshazilipa kwa Bohari ya Dawa (MSD).
Aidha alisema dawa za bima afya zipo na kwamba hawatarajii tatizo kwa kuwa wamekubaliana na mamlaka husika kukitokea upungufu watatumia hata fedha za bima kwa ajili ya kupunguza upungufu wa dawa.
Hata hivyo alisema kwamba wanakabiliwa na uhaba wa madaktari bingwa kwani kwa sasa wana dakatri bingwa wa mifupa na wanawake.
IMG_9338
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla akipewa maelezo na Kaimu Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Sokoine ya Mkoa wa Lindi, Damasiana Msalla alipotembelea wodi ya wazazi na kuridhishwa na huduma za hospitalini hiyo wakati wa ziara ya kushtukiza aliyoifanya mwishoni mwa juma mkoani Lindi.
IMG_9435
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Sokoine ya Mkoa wa Lindi, Dkt. Evaristo Kasanga akizungumza jambo na Eleuteri Mangi, Afisa kutoka Idara ya Habari -MAELEZO jijini Dar es Salaam.
IMG_9423
Hospitali ya Sokoine ya Mkoa wa Lindi imetwaa kombe la mshindi wa pili kwa utoaji wa huduma bora Tanzania kwa mwaka 2015.
18
Jedwali linaloonesha baadhi ya gharama za matibabu katika huduma zinazotolewa hospitali ya Sokoine ya Mkoa wa Lindi.
IMG_9349
Ujumbe wa watoa huduma kwa wateja wanaofika kupata huduma hospitali ya Sokoine ya Mkoa wa Lindi.
IMG_9572
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla (katikati) akiongozana na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Ligula ya mkoa wa Mtwara, Dkt. Shaibu Maarifa (kushoto) pamoja na Daktari wa zamu kitengo cha dharura hospitalini hapo, Dkt. Ester Tumwanga kuelekea wodi za wagonjwa wakati wa ziara ya kushtukiza aliyofanya mwishoni mwa juma mkoani humo.
IMG_9525
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiwa kwenye chumba cha dharura katika Hospitali ya Ligula ya mkoa wa Mtwara. Kushoto ni Daktari wa zamu kitengo cha dharura hospitalini hapo, Dkt. Ester Tumwanga.
IMG_9606
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla akitoka kwenye wodi ya wazazi Hospitali ya Ligula ya mkoa wa Mtwara wakati wa ziara ya kushtukiza aliyofanya mwishoni mwa juma mkoani humo. Aliefuatana nae ni Mganga Mkuu wa Hospitali ya Ligula ya mkoa wa Mtwara, Dkt. Shaibu Maarifa.
WASHINDI KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI PANGANI WAPATA ZAWADI

WASHINDI KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI PANGANI WAPATA ZAWADI

December 20, 2015
ø;
Meza kuu,wa kwanza kulia ni Meneja wa redio PANGANI FM Maimuna Msangi, wa pili kutoka kulia ni Mkurugenzi wa shirika la UZIKWASA ambalo limeratibu tamasha hilo VERA PIEROTH,wa tatu ni Kaimu mgeni Rasmi ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya PANGANI Bi Patricia, na wanne ni Mratibu wa masuala ya UKIMWI wilaya ya PANGANI.
ø;
Mkurugenzi wa shirika la UZIKWASA, VERA PIEROTH akizungumza jambo wakati wa kuwakaribisha wananchi wa PANGANI katika tamasha hilo.
Na Mwandishi wetu
Shirika lisilo la kiserikali Wilayani Pangani la UZIKWASA linalojishughulisha na kuziwezesha kamati za kudhibiti Ukimwi, VMACK limezawadia kamati bora za kudhibiti ukimwi Wilayani humo.
Sherehe hizo zimefanyika sanjari na kuwazawadia kijana bora mfano wa kuigwa na mama bora mfano wa kuigwa.
Katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Jaira,K ata ya Madanga wilayani Pangani na kuhudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo wananchi na viongozi kutoka halmashauri ya Wilaya ya Pangani mgeni rasmi alikuwa Kaimu Afisa Maendeleo Wilaya ya Pangani, Bi.Patricia Kinyange.
Akizungumza katika hadhara hiyo Bi. Kinyange amelipongeza shirika hilo kwa kuzijengea uwezo kamati hizo ambazo zinafanya kazi kubwa kwa jamii.
“Kwa kweli shirika la UZIKWASA nawapongeza sana, mnafanya kazi kubwa kwenye jamii ya Pangani na kwakweli watu wa Pangani wanapaswa kujivunia uwepo wenu. Nimeshangaa kuona mambo makubwa yanayofanywa na kamati kutokana na elimu mnayowapatia,mnastahili pongezi kubwa”alisema Bi.Kinyange.
“Mfano mzuri mimi ARUSHA nilipokua nafanya kazi, kamati zipo lakini kwakweli wamelala,unakuta kamati inakutana mara mbili kwa mwaka mzima,lakini huku ni zaidi ya mara kumi,kwakweli nimeshangaa sana,nyinyi ni shirika ambalo linafaa kuigwa,lakini wanakamati niwaombee mzidishe juhudi msiwaangushe wanauzikwasa na sisi kama halmashauri tutajitahidi kushirikiana kwa karibu kabisha na UZIKWASA ili kuendeleza juhudi hizi.”
Katika hatua nyingine mgeni huyo rasmi amempongeza kijana aliyeibuka mshindi katika shindano la kijana bora mfano wa kuigwa na kumtaka kuendeleza juhudi zake na kwamba Halmashauri watamtumia kama darasa kwa ajili ya vijana wengine kujifunza kutoka kwake.
Kwa upande wao kamati iliyoibuka mshindi kwa mwaka wa tatu mfululizo kutoka katika kijiji cha Mseko wamesema umoja na mshikamano ndio nguzo pekee ya ushindi wao,na kwamba shukrani pekee zinapaswa kwenda kwa UZIKWASA kwa mafunzo na ufuatiliaji wao kwani ndio vilivyowafanya kutekeleza mipango waliojiwekea kama wanakamati hadi kuibuka washindi.
‘Naweza kusema kamati yetu imejitoa sana,wanakamati wanatumia muda wao mwingi wa ziada katika kuhakikisha tunatekeleza mipango tuliojiwekea,lakini pia msukumo mkubwa ni kutoka UZIKWASA kwakweli tunawashukuru sana”Alisema Afisa mtendaji mseko.
Kwa upande wake Mratibu wa shughuli hizo kutoka shirika la UZIKWASA ambaye pia ni Afisa wa mradi wa jinsia na uongozi wenye mabadiliko, Bi.Salvata Kalanga amesema haikuwa kazi rahisi kuzipata kamati bora 8,kutokana na ushindani mkubwa uliokuwepo kwa washiriki 15,lakini wanashukuru kumpata mshindi ambaye wanaamini anastahili kutokana na kazi waliyoifanya.
Katika sherehe hizo,mshindi wa kwanza amepata zawadi ya ngao,pamoja na fedha taslimu shilingi laki sita,mshindi wa pili alipata laki 4 na nusu,na mshindi wa tatu alipata shilingi laki 4.
Sherehe ya kuzizawadia kamati bora za kudhibiti UKIMWI hufanyika kila mwaka chini ya shirika la UZIKWASA,lengo ni kuzipa motisha kamati hizo ili zifanye vizuri zaidi.
Mashindano haya na tamasha hili husimamiwa na kuwezeshwa na Asasi ya UZIKWASA Pangani kwa lengo na Kuamsha hamasa, kuchochea, kutafakari na kujifunza na kujenga uwajibikaji miongoni mwa vijana, akinamama na Kamati za Kudhibiti UKIMWI jinsia na uongozi za vijiji.
Mashindano haya huanza baada ya UZIKWASA kuwezesha kamati hizi kwa kuzijengea uwezo na baadae maafisa wa UZIKWASA kuzitembelea kamati hizo na makundi yaliyotajwa na kupima utekelezaji wake kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa na kukubaliwa na wadau hao.
Kamati, vijana, na akina mama walioanishwa kufanya vizuri hutembelewa na kamati nyingine kuweza kujifunza kwa pamoja na kujirudhisha kwa utekelezaji wa kamati hizo. Pia kwa vijana na wakinamama hutembeleana na kupeana taarifa za utekelezaji na kujifunza kwa pamoja. Kamatai hizo na hao vijana na akinamama huchujwa na kubaki wachache ambao wanatekeleza vizuri zaidi.
Baada ya zoezi hilo la kutembeleana walioanishwa huitwa Pangani na kukutanishwa na waamuzi ambao huwasikiliza na kuchambua washindi.
Mwaka 2015 kamati 12 zilichaguliwa kuingia kwenye ushindani huo ambazo ni Mseko, Mwembeni, mkwajuni, mbulizaga, Bweni, mzambarauni, Mtonga, Mikocheni, Langoni,Tungamaa, Sange na Jaira.
Akina mama bora waliongia sita bora kati ya 33 ni kutoka Masaika, Kwa kibuyu, Stahabu, Mwembeni, Mtonga na Langoni. (watatu watazawadiwa)
Vijana bora waliongia sita bora kati ya 33 ni kutoka Msaraza, Kimanga, Mikocheni, Mseko, Boza na Mivumoni.(watatu watazawadiwa).
Mashindano haya yalianzishwa mwaka 2010 ili kuleta msukumo, ushindani na chachu ya utekelezaji wa mipango ya vijiji ya ukimwi na maendeleo ya kijiji kwa ujumla na kuotesha mbegu ya uwajibikaji.
Mwaka 2010 Kamati ya Sanga iliibuka mshindi, mwaka 2011 kamati ya Langoni, iliibuka mshindi, mwaka 2012 kamati ya Langoni iliibuka mshindi tena. Mwaka 2013 kamati ya Mseko iliibuka mshindi na mwaka 2014 Mseko iliibuka mshindi tena.
Mwaka huu wa 2015 mchuano ulikuwa mkubwa na kamati zimejituma na kuwajibika katika utekelezaji wa mipango yao ya maendeleo pamoja na kuyasaidia makundi mbalimbali yenye uhitaji.
Kamati kumi 15 zimetekeleza vizuri. Kamati 12 zimetekeleza wastani. kamati 6 ikiwepo, Ushongo, Kipumbwi, Masaika, Kigurusimba, kimang,a na Mivumoni zinahitaji msukumo wa ziada kwa Kukosa uwajibikaji.
Mashindano haya yameleta msukumo katika shughuli zote za kiuongozi na maendeleo ya vijiji. Palipo na uongozi mzuri na utekelezaji mzuri unakuwepo pia.
UZIKWASA itaendelea kuwajengea uwezo viongozi wangazi zote na wanajamii kuweza kujitathmini, kuzama na kujichunguza na kuweza kufanyia kazi changamoto za kiuongoza na kuwezesha maendeleo katika jamii. Suala la kupinga unyanyasaji wa wanawake na watoto wa kike litapewa kipaumbele.
ø;
Kaimu mgeni rasmi ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii Bi.Patricia akizungumza na wananchi waliohudhuria katika tamasha hilo.
ø;
Burudani ya ngoma ilikua sehemu ya tamasha hilo.
ø;
Washehereshaji wa tamasha hilio, Pili Mlindwa na Shabani Kizamba wakiwajibika.
ø;
Mkurugenzi wa shirika la Uzikwasa na Meneja wa Pangani FM.
ø;
Wanakamati wa kijiji cha Mseko katika picha ya pamoja baada ya kutangazwa washindi, na wameibuka washindi kwa mwaka wa 3 mfululizo.
ø;
Mmoja wa wanakamati ya VMACK ya kijiji cha mseko akicheza kwa furaha mbele ya meza kuu baada ya kutangazwa washindi,
ø;
Kaimu Mgeni rasmi Bi.Patricia akiwa ameshika ngao ambayo ni zawadi ya washindi wa VMACK kwa mwaka 2015.
ø;
Katibu wa kamati hiyo akipokea zawadi, Ngao na Hundi ya shilingi laki sita.
ø;
Vijana bora wa mfano wa kuigwa walioingia katika hatua ya 3 bora, na aliyeibuka mshindi ni kijana aliyevaa tshirt rangi ya njano.
ø;
Wamama walioingia katika tatu bora mama mfano wa kuigwa, na aliyeibuka mshindi ni mama ambaye ameshikilia pochi, ambaye anajulikana kwa jina maaarufu kuti kavu.
ø;
Hapa akipokea zawadi ya hundi ya shilingi laki 1 kwa kua mama/mwanamke bora mfano wa kuigwa kwa mwaka 2015.
ø;
Mwenyekiti wa kijiji cha Jaira akigawa zawadi ya sare za shule kwa viongozi wa vijiji vyote vya Wilaya ya PANGANI kwa niaba ya Aliyekua kijana bora mfano wa kuigwa mwaka 2013-2014,ambayo aliahidi kwa watoto yatima alipochaguliwa.
ø;
Wamama wakifurahia jambo.
ø;
Sehemu/baadhi ya wananchi waliohudhuria katika tamasha la kuzizawadia kamati bora za kudhibiti UKIMWI, kijana bora na mama bora wa mfano wa kuigwa kwa mwaka 2015 zilizofanyika katika kijiji cha JAIRA kata ya MADANGA Wilayani PANGANI.
ø;
Waandishi wa habari kutoka redio PANGANI FM, iliyochini ya shirika la UZIKWASA wakifuatilia kwa makini tamasha hilo (waliovaa tshirt za PANGANI FM).
ø;
Wananchi wa Pangani waliofika katika kijiji cha Jaira wakifuatilia kwa ukaribu tamasha hilo.
WAZIRI UMMY MWALIMU AVAMIA HOSPITALI YA RUFAA YA BOMBO MKOANI TANGA, KUKAGUA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA LEO

WAZIRI UMMY MWALIMU AVAMIA HOSPITALI YA RUFAA YA BOMBO MKOANI TANGA, KUKAGUA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA LEO

December 20, 2015
IMG-20151220-WA0011
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na mmoja wa wahudumu wa afya (jina lake halikuweza kupatikana kiurahisi) wa dirisha la dawa katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Tanga alipofanya ziara ya kushtukiza mchana wa leo Disemba 20, 2015.
-Atoa wiki mbili wawe wamefunga mashine ya kukusanya mapato kwa njia ya Kielektroniki ili kudhitibiti upotevu wa mapato yanayotokana na wananchi kuchangia huduma za afya.
IMG-20151220-WA0012
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na mmoja wa wakina mama anayemhudumia mwanae katika wodi ya watoto Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Tanga alipofanya ziara ya kushtukiza leo mchana Disemba 20, 2015.
IMG-20151220-WA0019
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akimsikiliza mmoja wa akina mama aliyelazwa kwenye wodi ya wazazi wakati wa ziara ya kushtikiza aliyoifanya mchana wa leo Desemba 20, 2015 katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Tanga.
IMG-20151220-WA0020
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga (RMO), Dkt. Clement Marceli akimwelezea changamoto wanazokabiliana nazo katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Tanga Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu (hayupo pichani).
IMG-20151220-WA0017
Daktari aliyekuwa kwenye mafunzo, Dkt. Zuberi (Medical Intern) akitoa maelezo ya namna wanavyohudumia wananchi wanaofika hospitalini hapo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu (kulia) aliyefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani Tanga mchana wa leo Desemba 20, 2015 ambapo Waziri huyo alikutana na changamoto utoro wa madktari wa zamu kutokuwepo kwenye kituo chao cha kazi katika Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani Tanga.
IMG-20151220-WA0016
IMG-20151220-WA0019
Mratibu wa Hospitali ya Rufaa ya Bombo, mkoani Tanga kutoka Idara ya Tiba, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Ibrahimu Maduhu (mwenye tai) akitoa maelezo kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu namna wanavyokabiliana na changamoto ya kuzuia vifo vya mama na mtoto katika hospitali hiyo wakati wa ziara ya kushtukiza iliyofanywa na Mh. Ummy Mwalimu katika wodi ya wazazi leo mchana Disemba 20, 2015.
IMG-20151220-WA0014
Baadhi ya madaktari waliokuwa mafunzoni wakizungumza na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu aliyefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo, mkoani Tanga mchana wa leo Disemba 20, 2015.
IMG-20151220-WA0023
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akipitia orodha ya mahudhurio ya zamu za Madaktari na Wauguzi ambao wengi hawakuwepo kazini wakati wa ziara yake ya kushtukiza katika Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani Tanga aliyoifanya leo mchana Disemba 20, 2015.