MAADHIMISHO YA WIKI YA MLAJI YAFUNGULIWA TANGA NA KATIBU TAWALA MKOA.

March 14, 2014
KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA,SALUM CHIMA ALIYEKAA HAPO AKIPOKEA MAELEZO JANA WAKATI ALIPOTEMBELEA MABANDA YALIKUWEPO ENEO LA TROPICANA JIJINI TANGA

SIMBA SC ITAFANYA MKUTANO WAKE WA WANACHAMA JUMAPILI WIKI HII

March 14, 2014
Klabu ya Simba itafanya mkutano wa wanachama wake Jumapili (Machi 16 mwaka huu) kwa ajili ya kuifanyia marekebisho Katiba yao.

Nachukua fursa hii kuwatakia kila la kheri katika mkutano huo ambao ni muhimu katika kuhakikisha klabu yao inapiga hatua katika maendeleo ya mpira wa miguu na ustawi wake kwa ujumla.
March 14, 2014
TAARIFA KUTOKA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI TFF LEO
SEMINA YA WAAMUZI YAANZA DAR
Semina ya siku mbili kwa waamuzi wenye beji za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na wale wa ngazi ya juu nchini (elite) kwa robo ya kwanza ya mwaka huu inaanza kesho (Machi 15 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

March 14, 2014

BREAKIN NEWZZZ:- RAIS AWAAPISHA RASMI VIONGOZI WA BUNGE LA KATIBA SASA HIVI LIVE!!


Katibu wa Bunge Maalum la Katiba Bw, Yahya Khamis Hamad akiapa mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete Leo Mjini Dodoma.
Katibu wa Bunge Maalum la Katiba Bw. Yahya Khamis Hamad akisaini Kiapo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete Leo Mjini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akisaini kiapo baada ya kumuapisha Katibu bunge Bw. Yahya Khamis Hamad (mbele aliyesimama)

UHURU WA KUPENDA NA KUPENDWA UNAVYOATHIRI PENDO HURIA

March 14, 2014
Uhuru wa kupenda au kupendwa ni moja ya haki binadamu ambayo kama zilivyo haki yoyote ile inatakiwa iheshimiwe kwa sababu kila mmoja ana haki ya kuoensha hisia zake katika kile ambacho moyo wake unaouhusudu.

Uhuru huu wakati mwengine hutafsiriwa kutokana na Dini, kabila au utamaduni wa jamii kwa mujibu wa sheria za nchi au eneo husika.
March 14, 2014

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOANI IRINGA LEO

Kamanda wa polisi mkoani Iringa Kamishina Msaidizi Ramadhan Mungi akitoa taarifa kwa waandishi wa habari asubuhi hii mjini Iringa wakati alipozungumza nao katika ofisi zake zilizopo jengo la mkuu wa mkoa huo. IMG_4471 
……………………………………………………………………………
Ndugu waandishi wa habari , kwa niaba ya askari Polisi wa Mkoa wa Iringa, nitumie fursa hii kuwakaribisha hapa ofisini kwetu.
                Ndugu zangu tumeitana hapa asubuhi hii ili niweze kuwapa taarifa ya usalama katika Mkoa wetu wa Iringa hususani katika Jimbo la Kalenga katika kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi wa Jimbo la Kalenga na usalama wa siku ya uchaguzi wenyewe.Ili iwe rahisi kueleweka taarifa hii nitaitoa kwa kifupi sana kwa kuigawa katika maeneo matatu.
March 14, 2014

HELKOPTA MARUFUKU KWENYE ANGA LA KALENGA SIKU YA UCHAGUZI, WALIOTUMWA KUFANYA FUJO KUKIONA

Kamanda Mungi akizungumza leo
Na Bashir Nkoromo, Iringa JESHI la Polisi, limepiga marufuku chama chochote kurusha helkopta kwenye anga la jimbo la Kalenga, na limeahidi kushughulikia kikamilifu kundi au yeyote atakayejaribu kusababisha au kufanya vujo wakati wa uchaguzi na matokeo ya uchaguzi huo.
Onyo hilo limetolewa asubuhi hii na Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi, wakati akieleza Polisi ilivyojiandaa kuhakikisha uchaguzi mdogo jimbo la Kalenga, Iringa Vijijini, unafanyika kwa amani na utulivu, Jumapili hii, ya Marchi 16, 2014.
March 14, 2014

Wafanyabiashara na wachimbaji Tanzania walifikia soko la madini Kimataifa

1 (7)Wafanybiashara na Wachimbaji waliowakilisha wenzao katika Maonesho ya 53 ya Bangkok Gems and Jewelry Fair’ wakiwasikiliza wageni waliotembelea banda la Tanzania kuona aina mbali mbali za madini ya Vito na Usonara yaliyowasilishwa katika maonesho hayo.
2 (5)Mthamini wa madini kutoka idara ya Uthamini wa madini ya Almas (TANSORT) Bw. Edward Rweymamu (katikati), akiwaeleza jambo wageni waliotembelea banda la Tanzania katika maonesho hayo. Wanaoshuhudia wa kwanza kushoto ni Mratibu kutoka Kituo cha ‘Tanzania Geomological Center’ (TGC), Bw. Musa Shanyangi na wa kwanza kulia ni Mthamini wa Madini kutoka Idara ya  uthamini madini ya almsi  (TANSORT), Wizara ya Nishati na Madini Bibi. Teddy Goliama.
3 (4)Mwandishi wa habari hii (Kushoto) Asteria Muhozya, akifanya mahojiano na wafanyabiashara wa madini walioshiriki maonesho ya Vito na Usonara ili kutaka kujua namna walivyofaidika na ushiriki wao katika maonesho hayo. Anayeongea ni Bw. Jeremiah Simioni Mfanyabiashara kutoka Kampuni ya Tom Gems na katikati ni Mfanyabiashara Mhe. Dorah Mushi kutoka Kampuni ya H.B Mining Company.
…………………………………………………………………..
Na Asteria Muhozya, Bangkok
Wafanyabiashara na wachimbaji wa madini Tanzania wameelezea kufurahishwa na ushiriki wao katika maonesho ya 53 ya madini ya vito na usonara, Bangkok, kutokana na kupata fursa ya kulifikia soko la madini kimataifa.