Kikapu.

May 28, 2013
WACHEZAJI wa mchezo wa kikapu wakijiandaa na bonanza la mchezo huo ambalo litafanyika mwishoni mwa mwezi huu katika uwanja wa Harbours Jijini Tanga.
Uhamiaji waanza kuwaandikisha walowezi wa Malawi na Msumbiji.

Uhamiaji waanza kuwaandikisha walowezi wa Malawi na Msumbiji.

May 28, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.
IDARA ya Uhamiaji Mkoa wa Tanga imeanza kuwaandikisha walowezi wa Malawi na Msumbiji waliokuja mkoani hapa katika kipindi cha miaka ya nyuma ambao walikuwa wakifanya kazi kwenye mashamba ya mkonge na kazi za majumbani.

Akizungumza na blog hii, Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Tanga, Sixtus Nyaki alisema uandikishwaji watu hao unafanyika baada ya kuzungumza nao katika mkutano wa kuwaelimisha kwa kushirikiana na wenyeviti wa mitaa, vitongoji na maafisa watendaji wa kata  na vijiji.

Nyaki alisema wakati wakiwa wanaendesha zoezi hilo wanakumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo baada yao kutokukubali kuandikishwa kwa kuona kama wanafukuzwa hapa nchini hali ambayo inapelekea kuwa na ugumu kiasi.

Alisema katika kupambana na wimbi la uhamiaji haramu mkoani hapa idara hiyo imefungua ofisi ya uhamiaji wilayani Korogwe lengo likiwa ni kuzibiti ongezeko la wahamiaji wanaoingia mkoani hapa kutoka nchi mbalimbali duniani.

Ofisa huyo alisema ofisi hiyo itakuwa na kazi ya kuwahudumia wilaya ya Korogwe na wilaya ya Lushoto wakati idara hiyo ikiendelea kujipanga kwa ajili ya kufungua ofisi nyengine wilayani humo ikiwa ni mkakati wa kupambana na wahamiaji haramu.

Aidha alisema tayari wameshapata ofisi hiyo na ukarabati wake unaendelea ambapo unatarajiwa kukamilika muda sio mrefu ili iweza kufanya kazi zake ambapo aliongeza kuwa idara hiyo pia imeweka vizuizi katika barabara za Tanga-Horohoro, Tanga-Arusha na Tanga-Dar.

Hata hivyo aliogeza kuwa wataendelea kutoa elimu ya uhamiaji shirikishi kwa wananchi katika maeneo mbalimbali lengo likiwa ni kupunguza wimbi la wahamiaji haramu mkoani hapa pamoja na kuweza mikakati ya kupunguza uwepo wapo.

   Mwisho.

KLABU ZA ENGLAND ZIARANI ASIA

KLABU ZA ENGLAND ZIARANI ASIA

May 28, 2013

MAN UNITED, CHELSEA, ARSENAL, CITY, SPURS, LIVERPOOL, SUNDERLAND NDANI YA NYUMBA!!

FERGIE_APOKEWA_CHINAKABLA MSIMU MPYA wa 2013/14 kuanza Klabu kubwa za England zitatirirka Barani Asia kwa Ziara zao za matayarisho lakini pia lengo ni kuteka Soko kubwa huko kwa Klabu zao kwa kujitangaza kwa kishindo.
Arsenal wataanza Ziara yao huko Asia kwa kucheza Jakarta Indonesia Julai 14 na Siku 3 baadae wataenda Vietnam na kumalizia Ziara huko Japan, hii ikiwa Ziara yao ya kwanza Nchini Japan tangu Mwaka 1968.
Huko Japan, Arsenal watacheza na Nagoya Grampus 8, ambayo ni Klabu iliyofundishwa na Meneja wao Arsene Wenger kabla hajatua Arsenal Mwaka 1997, na Mechi hiyo itakuwa Julai 22.
Kisha Arsenal watacheza na Urawa Reds kugombania Saitama City Cup hapo Julai 26 na baada ya hapo kurudi London.
Nao Chelsea, hapo Julai 17 watakuwa huko Bangkok, Thailand kucheza na Kombaini ya Thailand na Tarehe 21 Julai watacheza huko Kuala Lumpur, Malaysia na Julai 25 kucheza Jakarta, Indonesia.
Liverpool watakuwa Australia kucheza na Melbourne Victory na baada ya hapo watapitia Bangkok, Thailand kucheza Mechi moja hapo Julai 28.
Hong Kong itashuhudia Mashindano ya Klabu za Ligi Kuu England kugombea Asia Cup na safari hii washiriki ni Manchester City, Tottenham Hotspur na Sunderland ambao watacheza Mechi zao za Kombe hilo Julai 24 na 27.
Mabingwa wa England, Manchester United, wao watakuwa na Ziara ya Wiki mbili itakayoanza Julai 13 huko Bangkok, Thailand na kisha kuruka kwenda Sydney, Australia na Japan, kucheza na Yokohama F. Marinos na Cerezo Osaka, Timu aliyotoka Shinji Kagawa, na kumalizia Ziara yao huko Hong Kong kucheza na Klabu ya hapo Julai 29.