ABDULRAHMAN KINANA AMPA MWAKYEMBE MWEZI MMOJA KUTOA MAJIBU

December 01, 2014

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa mjini Mtwara katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye  viwanja vya Mashujaa mjini humo akihitimisha ziara yake ya siku 16 aliyoifanya katika mikoa ya Lindi na Mtwara akikagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na serikali kwa kushirikiana na wananchi wenyewe na kuhimiza uhai wa chama cha Mapinduzi CCM, Katika ziara hiyo Katibu mkuu huyo aliongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi, Katika kutano huo Kinana amempa wiki mbili Waziri wa Uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe kutoa maelezo kwanini bidhaa mbalimbali hazisafirishwi kwenda nje
kupitia bandari ya Mtwara, Lakini pia Kinana amewaagiza Waziri wa Nishati na Madini kutoa maelezo ni kwanini wawekezaji wenye kampuni zinazofanya shughuli zao mtwara wanalipia kodi zao jijini Dar es salaam badala ya kulipia mkoani Mtwara ambako wanafanya shughuli zao, Pia waziri wa Ofisi ya Mkamu wa Rais Mazingira amepewa mwezi mmoja kuhakikisha dampo la taka za sumu zinazotupwa na wachimbaji wa gesi na viwanda kuacha mara moja kwa sababu zinahatarisha maisha ya wakazi wa Mtwara, Mwisho akaagiza Ofisi ya Waziri Mkuu kutoa kibali cha kugawa viwanja katika manispaa ya Mtwara kwani viwanja vimeshapimwa, Fedha za kulipa fidia zipo ila kibali kutoka ofisi ya Waziri mkuu ndiyo kimkwama kwa muda wa mwaka mmoja sasa.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MTWARA)
EMERSON ASAINI YANGA

EMERSON ASAINI YANGA

December 01, 2014


Kiungo mbrazil Emerson De Oliviera Neves Roque (kushoto) akisaini mkataba leo wa kuitumikia klabu ya Young Africans, kulia ni Afisa Habari wa klabu Baraka Kizuguto

Kiungo Emerson De Oliveira Neves Roque leo amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia klabu ya Young Africans baada ya benchi la ufundi kuridhika na uwezo wake,na mchezaji mwenyewe kufikia makubaliano hayo ya kuwatumikia watoto wa Jangwani.
Baada ya kufanya mazoezi kwa siku nne mfululizo chini ya makocha Marcio Maximo, Leonardo Neiva na makocha wazawa Salavatory Edward, Shadrack Nsajigwa kwa pamoja wameridhiswa na uwezo wake na kuomba apewe kandarasi la kuitumikia klabu ya Young Africans.
Emerson aliyekua akichezea katika timu ya Bonsucesso iliyopo daraja la pili kwenye jimbo la Rio de Janeiro anachukua nafasi ya mshambuliaji Geilson Santos "Jaja" ambaye ameshindwa kureje nchini kutokana na matatizo ya kifamilia na kuomba klabu ya Young Africans imuache.
Kocha wa Young Africans Marcio Maximo amesema wamerizishwa na uwezo na kiungo mkabaji Emerson na kusema ataisaidia timu katika michuano mbali mbali ya Ligi na Kimataifa.
Ujio wa Emerson unafanya klabu ya Young Africans kufikisha jumla ya wachezaji watano wa kimataifa, wengine wakiwa ni Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima, Hamis Kizza na Andrey Coutinho.

RAIS - UTEUZI WA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI (CAG)

December 01, 2014

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Profesa Mussa Juma Assad kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Taarifa iliyotolewa leo, Jumatatu, Desemba Mosi, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, inasema kuwa uteuzi wa Bwana Assad ulianza Novemba 5, mwaka huu, 2014.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa Bwana Assad ataapishwa kesho, Jumanne, Desemba 2, saa nne asubuhi, Ikulu, Dar es Salaam.
Kabla ya uteuzi wake, Bwana Assad alikuwa Profesa Mshiriki, Idara ya Uhasibu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na anachukua nafasi ya Bwana Ludovick Utouh ambaye amestaafu kwa mujibu wa Sheria za Utumishi wa Umma.
Profesa Assad ni msomi, mwenye weledi, ujuzi na uzoefu mkubwa wa uhasibu na udhibiti wa fedha ambaye ana Shahada ya Uzamivu wa Uhasibu (PHD in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Southampton, Uingereza mwaka 2001 na Shahada ya Uzamivu katika Udhibiti wa Fedha (MA in Financial Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City, Jamhuri ya Ireland mwaka 1991.
Profesa Assad pia ana Stashahada ya Kitaaluma ya Uhasibu (Professional Diploma in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City mwaka 1990 na Shahada ya Biashara (Bachelor of Commerce) ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam mwaka 1988.
Pamoja na uzoefu wa kitaaluma, Profesa Assad anao uzoefu mkubwa katika eneo la uhasibu na ukaguzi. Alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) kwa miaka saba (2007 - 2014); ni Rais na Mjumbe wa Chama cha Wahasibu Afrika (Pan African Federation of Accountants) tangu mwaka 2012; na ni mjumbe wa Bodi kadhaa za Wakurugenzi nchini Tanzania.

Katika kumteua Profesa Mussa Juma ASSAD kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Rais anayo imani kubwa kuwa elimu, weledi, ujuzi na uzoefu ambao Profesa Assad anao utamwezesha kutekeleza vema majukumu ya nafasi hiyo muhimu sana katika utawala bora wa nchi yetu.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
1 Desemba,2014

BUNGE LA VIJANA LAANZA VIKAO VYAKE KATIKA UKUMBI WA MSEKWA BUNGENI DODOMA

December 01, 2014

 Washiriki wa Bunge la Vijana wakifuatilia Mijadala ya Bunge hilo kwa Makini.
 Washiriki wa Bunge la Vijana wakifuatilia Mijadala ya Bunge hilo kwa Makini.
 Washiriki wa Bunge la Vijana wakifuatilia Mijadala ya Bunge hilo kwa Makini.
 Kiongozi wa Shughuli za Serikali katika Bunge la Vijana ndg. Zacharia Magige  kutoka chuo kikuu cha Mzumbe akiwashukuru wabunge wenzie baada ya jina lake kuthibitishwa rasmi na Bunge hilo kuwa Waziri Mkuu katika Bunge la Vijana jana.
 Spika wa Bunge la Vijana Ndg. Edgar Israel akimuapisha aliyechaguliwa kuwa Naibu Spika wa Bunge hilo Ndg. Mussa Yusufu kutoka chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kushika nyadhifa hiyo Bungeni jana.
  kiongozi wa kambi ya Upinzani katika Bunge la Vijana Ndg. Alpha Mazengo akiuliza swali kwa Spika wa Bunge hilo wakati Bunge hilo lilipoketi katika vikao vyake jana
 Spika wa Bunge la Vijana Ndg. Edgar Israel kutoka chuo cha St. John cha Dodoma akiingia Bungeni tayari kwa kuanza kwa Bunge hilo
 Mpambe wa Bunge akiweka siwa mezani tayari kwa kuanza vikao vya Bunge la Vijana
 Spika wa Bunge la Vijana Ndg. Edgar Israel kutoka chuo cha St. John cha Dodoma akisoma dua kabla ya kuanza kwa Bunge hilo mjini Dodoma. Waliosimama mbele yake ni Makatibu Mezani
 Washiriki wa Bunge la Vijana wakisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa maafisa wa Bunge kabla ya kuanza vikao vya Bunge hilo
 Washiriki wa Bunge la Vijana wakisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa maafisa wa Bunge kabla ya kuanza vikao vya Bunge hilo
 Mshauri Msaidizi wa Maswala ya Sheria wa Bunge Ndg. Matamus Fungo akifafanua namna Muswada wa Sheria unavyopitia katika hatua mbalimbali Bungeni.
 Mkurugenzi msaidizi kutoka Kamati za Bunge Ndg. Athuman Hussein akifafanua jambo wakati wa semina ya Maalum kwa Wabunge wa Bunge la Vijana kabla ya kuanza kwa Bunge hilo Jana
 Afisa wa Bunge Ndg. Patson Sobha akielezea baadhi ya taratibu za kibunge wakati wa semina kwa Wabunge wa Bunge la Vijana kabla ya kuanza kwa Bunge hilo jana

AJALI ZA BARABARANI ZAONGEZEKA TABORA ZAUWA IDADI KUBWA YA WATU!

December 01, 2014

Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Ludovick Mwananzila akipata maelezo kutoka kwa Dr.Anna Kichambati wa Redcross Tabora wakati wa sherehe za wiki ya usalama barabarani mkoani Tabora
Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Mwananzila akisalimiana na Afisa mfawidhi wa Sumatra mkoa wa Tabora Bw.Joseph Michael wakati wa wiki ya usalama barabarani mkoa wa Tabora
Mmoja kati ya maafisa wa polisi kikosi cha usalama barabarani Tabora mjini akimuonesha mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Ludovick Mwananzila kifaa maalumu kinachotumika kupima kiwango cha ulevi kwa madereva wazembe.(P.T)
Kikosi cha zimamoto mkoa wa Tabora kikionesha vifaa vinavyotumika wakati wa uokoaji ajali zinapojitokeza.
Sherehe za wiki ya usalama barabarani mkoa wa Tabora zilianza kwa maandamano yaliyopita mitaa mbalimbali hadi viwanja vya mazoezi ya Jeshi la Polisi Tabora ambapo wananchi walishiriki maandamano hayo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora kikosi cha usalama barabarani SSP Peter Mnyandwa akitoa taarifa ya ongezeko la  ajali za barabarani mkoani Tabora ambapo zaidi ya watu 150 wamefariki dunia katika ajali 399 huku watu 520 wamejeruhiwa katika ajali 185.

Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Ludovick Mwananzila akihutubia katika sherehe hizo za wiki ya nenda kwa usalama barabarani ambapo mbali ya kusikitishwa na taarifa ya ajali hizo lakini alisema kuwa asilimia 75 ya ajali hizo zinatokana na makosa ya kibinadamu na hivyo kuzitaka mamlaka husika kuchukua hatua ya kudhibiti kupunguza ajali hizo ikiwa ni pamoja na kutotoa leseni kwa madereva ambao hawajapata mafunzo ya udereva darasani.
Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Mwananzila akimpatia cheti cha pongezi Mwenyekiti mstaafu wa Kamati ya Usalama barabarani mkoa wa Tabora Bw.Moshi Abrahamu maarufu Nkonkota.
Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Ludovick Mwananzila akikabidhi cheti cha pongezi kwa mmiliki wa kampuni ya mabasi ya NBS kwa usafirishaji salama bila kusababisha ajali kwa muda wa zaidi ya mwaka mmoja.
 Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji yafanya Mahafali ya Sita

Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji yafanya Mahafali ya Sita

December 01, 2014

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (mwenye miwani) akiangalia na kupata maelezo kutoka kwa wahusika alipotembelea labaratori ya mitambo ya maji katika Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI) kabla ya kuudhuria maafali ya sita ya Taasisi hiyo hivi karibuni. unnamed1 
Baadhi ya wahitimu kutoka Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI) wakiwa katika maandamano ya kitaaluma wakati wa Maafali ya sita cha Taasisi hiyo hivi karibuni.
unnamed3 
Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI) Dkt. Shija Kazumba (kushoto) akimkaribisha Mgeni rasmi katika maafali ya sita ya Taasisi hiyo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel ambaye pia ni mgeni rasmi wa mahafali hayo.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akiwahutubia wahitimu (hawapo pichani) wakati wa mahafali ya sita ya Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI). Kushoto ni Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI) Dkt. Shija Kazumba na kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi hiyo Prof. Gabriel Roderick Kassenga. unnamed5 
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akipokea risala ya wahitimu iliyosomwa na kuwasilishwa kwa mgeni rasmi na Bw. Magembe Maduhu.
unnamed6 
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akimpa tuzo mhitimu aliyeongoza katika kundi la wanawake na aliyekua na ufaulu mkukwa kuliko wahitimu wote Bi. Fatma Ngano, kulia ni Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI) Dkt. Shija na ushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi hiyo Prof. Gabriel Roderick Kassenga.
unnamed7 
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo ambaye pia ni mgeni rasmi katika mahafali ya sita ya Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI) Prof. Elisante Ole Gabriel (mwenye miwani) katika picha ya pamoja na wakufunzi na wahitimu wa Taasisi hiyo.
unnamed8 
Kikundi cha ngoma kutoka Jeshi la Wananchi Tanzania Mwenge wakitumbuiza wakati wa mahafali ya sita ya Taasisi ya Maendeleo na Usimamizi wa Maji (WDMI) yaliyofanyika hivi karibuni.
 Picha na: Genofeva Matemu – Maelezo
BANDARI YA KASANGA KUANZA KUBORESHWA

BANDARI YA KASANGA KUANZA KUBORESHWA

December 01, 2014


Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Watatu kushoto) akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kulia) mara walipowasili katika bandari hiyo kujionea shughuli mbalimbali za maendeleo bandari hapo. SONY DSC 
Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kushoto) akiwaongoza wakaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango kujionea moja ya meli za kigeni zinazotia nanga katika bandari hiyo. Meli hiyo ni MV Rwegura kutoka nchini Burundi. SONY DSC 
Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kulia) akitoa ufafanuzi juu ya namna bandari yake inavyohudumia meli kutoka nchi jirani. Wanaomsikiliza ni Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ikiongozwa na Bibi Florence Mwanri (Kushoto aliyevaa fulana nyeusi). SONY DSC 
Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ikiwa katika picha ya pamoja katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) zilizopo kwenye Bandari ya Kasanga. SONY DSC 
Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kushoto) akimfafanualia jambo Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kulia) wakati akimkabidhi taarifa ya maendeleo ya bandari hiyo.
…………………………………………………………………….
Na Saidi Mkabakuli, Sumbawanga
Serikali imeazimia kuanza kuiboresha bandari ya kimkakati ya Kasanga inayohudumia nchi za Burundi, Rwanda na Kongo iliyopo katika Ziwa Tanganyika, mkoani Rukwa.
Ahadi hiyo imetolewa na Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri wakati walipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya miundombinu katika Bandari ya Kasanga.
Bibi Mwanri alisema kuwa serikali kupitia Mamlaka ya Bandari Tanzania imepanga kuboresha bandari zote ili kuwa malango kuu la biashara kwa soko la ndani na kwa nchi jirani ili kuongeza uwezo wa kuhudumia shehena kwa ufanisi.
“Tumedhamiria kuendelea kuboresha miundombinu ya bandari hususan miradi iliyoibuliwa katika Programu ya Matokeo Makubwa Sasa ikiwemo Bandari ya Kasanga ili kuweza kukidhi mahitaji ya utoaji wa huduma katika eneo hili,” alisema.
Bibi Mwanri aliongeza kuwa serikali pia imejipanga kuendelea kuboresha miundombinu na ununuzi wa vifaa mbalimbali vya kuhudumia shehena katika bandari za Dar es Salaam, Tanga, Mtwara, Kasanga na Kigoma na kukamilisha maandalizi ya ujenzi wa bandari mpya za Mwambani (Tanga), Mbegani (Bagamoyo) na Bandari Kavu ya Kisarawe.
Akizungumza na ugeni huo, Msimamizi Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa alisema kuwa Bandari hiyo ina fursa nyingi katika kuhudumia shehena na abiria wanaopitia bandarini hapo.
“Bandari yetu ina fursa kubwa za kibiashara kwani tuna wateja wengi kutoka ndani na nje ya nchi wanaotumia bandari yetu kupitishia bidhaa zao, pamoja na abiria wanaosafiri kwenda nje na ndani ya Tanzania,” alisema.
Kwa mujibu wa Mpango wa Maendeleo kwa mwaka ujao wa fedha Serikali imedhamiria kuboresha mazingira yatakayowezesha sekta binafsi kuwekeza katika kujenga miuondombinu na kuboresha usafirishaji wa mizigo katika bandari zote nchini.
Pia, Mpango huo unaweka bayana kuendeleza na ukarabati na ununuzi wa vyombo vya usafiri na usafirishaji katika maziwa.
TAIFA STARS MABORESHO YAINGIA KAMBINI

TAIFA STARS MABORESHO YAINGIA KAMBINI

December 01, 2014

index
Kikosi cha Taifa Stars Maboresho kimeingia kambini leo (Desemba 1 mwaka huu) Bulyanhulu mkoani Shinyanga kujiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Burundi itakayochezwa Desemba 9 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Ikiwa chini ya Kocha Mart Nooij, Stars Maboresho itapiga kambi mkoani humo hadi Desemba 6 mwaka huu ambapo itarejea jijini Dar es Salaam tayari kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Uwanja wa Taifa.
Wachezaji walioingia kambini ni Abubakar Ally (Coastal Union), Abubakar Ally Mohamed (White Bird), Aishi Manula (Azam), Andrew Vicent (Mtibwa Sugar), Atupele Green (Kagera Sugar), Edward Charles (Yanga) na Emmanuel Semwanda (African Lyon).
Gadiel Michael (Azam), Hashim Magoma (Stand United), Hassan Banda (Simba), Hassan Mwasapili (Mbeya City), Joram Mgeveke (Simba), Kassim Mohamed Simbaulanga (African Lyon), Kelvin Friday (Azam) na Makarani Ally (Mtibwa Sugar).
Miraji Adam (Simba), Mohamed Hussein (Simba), Muzamir Ally (Mtibwa Sugar), Omari Nyenje (Ndanda), Pato Ngonyani (Yanga), Rashid Mandawa (Kagera Sugar), Said Hamisi (Simba), Salim Hassan Mbonde (Mtibwa Sugar) na Shiza Ramadhan (Mtibwa Sugar).
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linaishukuru kampuni ya kuchimba madini ya Acacia Mining PLC (zamani African Barrick Gold PLC) kwa kufadhili kambi ya Stars kupitia mgodi wa Bulyanhulu.