WASIFU WA RAIS DKT. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI, MGOMBEA NAFASI YA MWENYEKITI WA CCM TAIFA

July 22, 2016

1.0.  MAISHA YAKE

Ndugu John Pombe Joseph Magufuli alizaliwa Oktoba 29, mwaka 1959 katika kijiji cha Chato, Wilayani Biharamulo katika Mkoa wa Kagera. Hivi sasa Chato ni Wilaya katika Mkoa wa Geita. Ndugu Magufuli ni Daktari wa Falsafa (PhD) ya Kemia. Ana mke  na watoto saba.  Alichaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwezi Oktoba, 2015 kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (C.C.M). Aliapishwa na kuanza rasmi majukumu yake ya kuiongoza Tanzania tarehe 5 Novemba, 2015.

Tangu ameingia madarakani, Rais Dkt. Magufuli, ameonesha kuwa ana sifa zote muhimu za uongozi. Ana dira, maono na malengo kuhusu anakotaka Taifa liende. Ana mikakati ya kutekeleza dira na maono yake. Haogopi kufanya maamuzi makini. Ana kiu ya kuona Taifa linapata maendeleo. Amejipambanua kuwa yeye ni mtetezi wa wanyonge na dhamira yake kubwa ni kuona wananchi wanapata huduma bora  za jamii na kero zao zinaondoka.

2.0.  ELIMU NA MAFUNZO

Rais Dkt. Magufuli alianza elimu ya msingi katika Shule ya msingi Chato mwaka 1967 na kumaliza mwaka 1974. Mwaka 1975 alianza masomo ya sekondari katika Shule ya Seminari ya Katoke Mkoani Kagera.  Mwaka 1977 alihamia shule ya sekondari ya Lake iliyopo Mkoani Mwanza  na kuhitimu kidato cha Nne mwaka 1978. Kuanzia mwaka 1979 hadi 1981 alifanya masomo ya kidato cha Tano na  Sita katika shule ya Sekondari ya Mkwawa Mkoa wa Iringa  .

Mwaka 1981 hadi 1982 alisoma Chuo cha Ualimu Mkwawa na kuhitimu Stashahada ya Ualimu ya Masomo ya Kemia na Hisabati.  Mwezi Julai hadi Disemba mwaka 1983, Dkt. Magufuli alipata mafunzo ya kijeshi  katika Jeshi la  kujenga Taifa kikosi cha Makutupora mkoa wa Dodoma. Mwezi Januari hadi Machi 1984 alihamishiwa kikosi cha mafunzo Jeshi la Kujenga Taifa Makuyuni, Arusha.  Mwezi huo wa Machi alihamia kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa Mpwapwa Dodoma na kumaliza mafunzo mwezi Juni 1984.

Mwaka 1985 alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salaam kusoma Shahada ya kwanza ya Sayansi na Ualimu akijikita katika masomo ya Kemia na Hisabati. Alitunukiwa Shahada hiyo mwaka 1988.  Mwaka 1991 hadi 1994 alisoma na kutunukiwa Shahada ya Uzamili katika fani ya Kemia iliyotolewa na Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Chuo Kikuu cha Salford cha Uingereza. Mwaka 2006 alijiunga na  Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa ajili ya Shahada ya Uzamivu katika Fani ya Kemia na kufanikiwa kuhitimu mwaka 2009.

3.0.  UZOEFU WA NDANI YA  SERIKALI

Baada ya kuhitimu masomo yake ya Stashahada ya Ualimu, mwaka 1982 hadi 1983 Dkt. Magufuli alikuwa Mwalimu katika shule ya Sekondari ya Sengerema iliyopo Mkoani Mwanza akifundisha masomo ya Kemia na Hisabati.  Mwaka 1989 alijiunga na Chama Cha Ushirika cha Nyanza Mkoani Mwanza, ambapo alifanya kazi kama Mkemia Mkuu  hadi mwaka  1995.

Mwaka 1995 alichaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Mashariki Mkoa wa Kagera.  Baada ya Uchaguzi, Rais wa Awamu ya Tatu, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa alimteua kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi nafasi ambayo aliitumikia  hadi mwaka 2000.  Mwaka 2000 alichaguliwa kwa mara ya pili kuwa Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Mashariki lakini mara hii akipita bila kupingwa.  Mwaka huo huo aliteuliwa kuwa Waziri kamili wa Wizara ya Ujenzi hadi mwaka 2005. 

Mwaka 2005 Rais Dkt. Magufuli alichaguliwa kwa mara ya tatu kuwa mbunge wa jimbo la Biharamulo Mashariki, kwa mara nyingine akipita bila kupingwa.   Baada ya uchaguzi, Rais wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alimteua kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuanzia mwaka 2005 hadi mwaka 2008 ambapo alihamishiwa Wizara ya   Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi hadi hadi mwaka 2010.

Mwaka 2010 Dkt. Magufuli alichaguliwa kwa mara ya nne  kuwa  Mbunge lakini, kufuatia mgawanyo wa majimbo uliofanyika, mara hii katika Jimbo jipya la Chato.  Baada ya uchaguzi, aliteuliwa kuwa Waziri wa Ujenzi kuanzia mwaka 2010 hadi mwaka 2015.

Wakati akiwa Mbunge na Waziri, Dkt. Magufuli amefanya shughuli na kushika nyadhifa kadhaa ndani na nje ya nchi. Mwaka 2014, Dkt. Magufuli alishiriki katika Bunge Maalum la Kutunga Katiba Mpya akiwa  ni Mjumbe wa Bunge hilo. Aidha, wakati akiwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliweza kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti Mwenza (Co-Chair) wa Mkutano wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Makazi (UN-Habitat).

Tarehe 25 Oktoba, 2015 Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alichaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na tarehe 5 Novemba, 2015 aliapishwa kushika rasmi wadhifa huo.

4.0.  UZOEFU WA UONGOZI NDANI YA CHAMA

Rais Dkt. Magufuli alijiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka 1977. Amekuwa Mwanachama mwaminifu na ameshika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya Chama. Nafasi alizowahi kushika ni pamoja na kuwa Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Wilaya, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Mkoa, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Mkoa na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa. 

Sambamba na kushika nafasi mbalimbali za uongozi, Dkt. Magufuli mara zote alijitoa kukitetea Chama na kuhakikisha kinapata ushindi. Alishiriki kikamilifu kuwafanyia kampeni wagombea wa CCM katika Chaguzi Ndogo zilizofayika katika majimbo ya Busanda, Biharamulo Magharibi na Igunga na kupata ushindi.  Katika Mkutano Mkuu wa CCM wa tarehe 11 – 12 Novemba mwaka 2012, Dkt. Magufuli alikuwa miongoni mwa Mawaziri wachache waliopata fursa ya kuelezea mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama ya Mwaka 2010 – 2015. Alielezea mafanikio ya utekelezaji wa Ilani, hususan katika sekta ya miundombinu.

Tarehe 11 mwezi Julai, 2015 Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM ulimchagua na kumteua Dkt. Magufuli kuwa mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  Aliinadi vyema Ilani ya uchaguzi ya CCM (2015) na kukiwezesha Chama kupata ushindi mkubwa. Tarehe 25 Oktoba, 2015 alichaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  Nafasi hiyo imemwezesha kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa.

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII,MHANDISI RAMO MAKANI ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA KISIWA CHA RUBONDO

July 22, 2016
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akiwasili katika Hifadhi ya Taifa ya Rubondo.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akipokelewa na Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku (Msukuma) mara baada ya kuwasili katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na Kaimu Mkuu wa mkoa wa Geita ,Herman Kapufi mara baada ya kuwasili katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha  Rubondo. 
 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Utalii katika Shirika la Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo ,Missana Mwishawa muda mfupi baada ya kuwasili katika hifadhi hiyo.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya kisiwa cha Rubondo.
  Mkurugenzi wa Idara ya Utaliii wa Shirika la Hifadhi za Taifa,(TANAPA) Ibrahimu Musa akiteta jambo na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani kabla ya kuanza kikao na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
Mkurugenzi wa Idara ya Utaliii wa Shirika la Hifadhi za Taifa,(TANAPA) Ibrahimu Musa akizungumza wakati wa kikao cha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
Baadhi ya Madiwani wa mkoa wa Geita wakiwa katika kikao hicho.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo ,Missana Mwishawa akisoma taarifa ya hifadhi hiyo kwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani.
Mkuuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo,Missana Mwishawa akimkabidhi Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani taarifa ya Hifadhi hiyo.
Kaimu Mkuu wa mkoa wa Geita ,Herman Kapufi akizungumza katika mkutano wa Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani (kulia kwake) alipotembelea Hifadhi ya Taifa ya kisiwa cha Rubondo.kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utalii wa Shirika a Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa.
Baadhi ya watumishi katika Hifadhi ya taifa ya kisiwa cha Rubondo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisisitiza jambo wakati wa kikao chake na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo alipofanya ziara ya siku moja katika Hifadhi hiyo.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo pamoja na viongozi wengine wa serikali wa mkoa wa Geita mara baada ya kumalizika kwa kikao na watumishi wa hifadhi hiyo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa wa Geita mara baada ya kumaliza kikao na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo. 

Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog kanda ya Kaskazini.
MWENYEKITI WA CCM DK. JAKAYA KIKWETE: MAFISI YALINGOJA MKONO UDONDOKE LAKINI YALIAMBULIA PATUPU

MWENYEKITI WA CCM DK. JAKAYA KIKWETE: MAFISI YALINGOJA MKONO UDONDOKE LAKINI YALIAMBULIA PATUPU

July 22, 2016

1Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete akiimba wimbo maalum kabla ya kufungua  Mkutano wa Halmashauri  Kuu ya CCM Taifa  (NEC) kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma leo Julai 22, 2016. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mtarajiwa, Rais John Magufuli, Wapili kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM , Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, kuliani ni Makamu Mwenyekiti wa CCM , Bara, Philip Mangula na wapili kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.  Mkutano huo ni kwa ajili ya kupitisha jina la Rais Dk. John Pombe Magufuli kuwa mwenyekiti mpya wa CCM ambapo kesho atathibitishwa na Mkutano Mkuu Maalum kwenye ukumbi wa Dodoma Convention Centre mjini Dodoma
Dk. Jakaya Kikwete akizungumza na wajumbe hao wakati akifungua mkutano huo amesema kikao hicho kilikuwa ni cha mwisho kwake kama mwenyekiti wa CCM , Akawashukuru wajumbe hao kwa kumpa ushirikiano kwa miaka kumi yote akiwa Mwenyekiti na akaongeza kwamba kama Chama cha Mapinduzi hakikupasuka mwaka jana hakiwezi kupasuka tena kitaendelea kudumu na kudumu zaidi.
Amesema Kulikuwa na mafisi yaliyokuwa yakingojea mkono udondoke tu ili yaweze kudaka na kula lakini yaliambulia patupu chama kilisimama kidete na kuendelea na mipango mizuri kwa ajili ya watanzania.
(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-DODOMA)
2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mama Samia Suluhu, Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa na Naibu Katibu Mkuu Bara Ndugu Rajab Luhwavi wakishiriki kuimba wimbo maalum wa CCM kabla ya kufunguliwa kwa mkutano huo.
3Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete akfungua  Mkutano wa Halmashauri  Kuu ya CCM Taifa  (NEC) kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma leo Julai 22, 2016. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mtarajiwa, Rais John Magufuli, Wapili kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM , Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein.
4Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete akifungua  Mkutano wa Halmashauri  Kuu ya CCM Taifa  (NEC) kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma leo Julai 22, 2016. kutoka  kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM , Bara, Mzee Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
5Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete akisisitiza jambo wakati akifungua  Mkutano wa Halmashauri  Kuu ya CCM Taifa  (NEC) kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma leo Julai 22, 2016. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mtarajiwa, Rais John Magufuli, Wapili kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM , Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein.
6
Msemaji wa CCM Ndugu Christopher Ole Sendeka akisalimiana na Mzee Mark Mwandosya  katikati ni Mjumbe wa NEC kutoka mkoa wa Singida Ndugu Mwigulu Nchemba.
7
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa NEC kutoka Zanzibar Ndugu Mohamed Abood akisalimiana na Mjumbe mwenzake kutoka Zanzibar pia Balozi Ali Karume katikati anayecheka ni Katibu Mkuu wa CCM Mstaafu Mzee Wilson Mukama.
8
Baadhi ya Wajembe wa NEC wakiwa kwenye mkutano huo kutoka kulia ni Mark Mwandosya, Profesa Peter Msola na Mzee Steven Waira.
9
Mpiga picha wa Makamu wa Rais Bw. Adam Mzee kulia akiwaelekeza jambo waandishi wenzake kabla ya kuanza kwa mkutano huo kutoka kushoto ni  Emilian Malya kutoka Clouds Digital, Bakari Kimwanga kutoka Mtanzania na Said Mwishehe kutoka Jambo leo.
10
Mjumbe wa NEC Godfrey Zambi akisalimiana na Mjumbe mwenzake Hussein Mwinyi katikati ni Khadija Aboud.
11
Christopher Olesendeka akibadilishana mawazo na wajumbe wenzake.
12
Baadhi ya wajumbe wakiwa tayari kwa mkutano huo
13
Wajumbe kutoka mkoa wa Pwani
14
Mzee Mark Mwandosya akizungumza na mjumbe mwenzake Peter Serukamba kutoka mkoani Kigoma
15
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Bi Zamaradi Kawawa katikati akiwa na mkurugenzi wa Redio Uhuru Angela Akilimali kulia na Mwandishi Mwandamizi wa Gazeti la Uhuru Selina Wilson wakiwa katika mkutano huo.
16
Wajumbe kutoka mkoani Mara wakiwa katika mkutano huo
17
Mwenyekiti wa CCM kutoka Mkoa wa Mwanza Bw. Joseph Kasheku Msukumu katikati akiwasikiliza wajumbe wenzake Januari Makamba kulia na Said Mtanda wakati  walipokuwa wakijadiliana jambo.
18
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza Ndugu Anthony Dialo akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Lindi Mzee Ali Mtopa.
20 
Wajumbe wa NEC kutoka mkoani Kilimanjaro.
TANZANIA NA CHINA ZATILIANA SAINI HATI YA MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO (MoU) UJENZI WA RELI YA KATI KWA KIWANGO CHA KIMATAIFA

TANZANIA NA CHINA ZATILIANA SAINI HATI YA MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO (MoU) UJENZI WA RELI YA KATI KWA KIWANGO CHA KIMATAIFA

July 22, 2016

FED1 
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile (aliyeipa mgongo kamera), akizungumza jambo kabla ya kutia saini Hati ya makubaliano ya ushirikiano wa ujenzi wa miradi mbalimbali ukiwemo ujenzi wa Reli ya Kati katika kiwango cha Kimataifa (Standard gauge) na Benki ya Exim ya China, Jijini Dar es salaam.
FED2 
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile (Kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dkt. Leonard Chamuriho (katikati) kabla ya kutia saini Hati ya makubaliano ya ushirikiano wa ujenzi wa miradi mbalimbali ukiwemo ujenzi wa Reli ya Kati katika kiwango cha Kimataifa (Standard gauge) na Benki ya Exim ya China, Jijini Dar es salaam Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James.
FED3 
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile (Kushoto) akitoa maelezo kwa mmoja wa maafisa wa Benki ya Exim-China,  kabla ya kutia saini Hati ya makubaliano ya ushirikiano wa ujenzi wa miradi mbalimbali ukiwemo ujenzi wa Reli ya Kati katika kiwango cha Kimataifa (Standard gauge), na Benki ya Exim ya China, Jijini Dar es salaam.
FED4 
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile na Naibu Meneja Mkuu (Mikopo Nafuu) wa Benki ya Exim ya China, Zhu Ying, wakitia saini Hati ya Makubaliano ya  Ushirikiano wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ukiwemo ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (Standard gauge), Jijini Dar es salaam.
FED5 
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile akipeana mkono na Naibu Meneja Mkuu (Mikopo Nafuu) wa Benki ya Exim ya China, Zhu Ying, mara baada ya kutia saini Hati ya Makubaliano ya  Ushirikiano wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ukiwemo ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (Standard gauge), Jijini Dar es salaam.
FED6 
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip I. Mpango (Mb) (kushoto), akizungumza na Rais wa Benki ya Exim-China, Liu Liange, katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere jijini Dar es salaam kabla ya Rais huyo aliyekuwepo nchini kwa ziara ya kikazi kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli. Kulia ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa.
FED7 
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip I. Mpango (Mb) (kulia), akipeana mkono na  Rais wa Benki ya Exim-China, Liu Liange, katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere jijini Dar es salaam kabla ya Rais huyo aliyekuwepo nchini kwa ziara ya kikazi kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, kuondoka nchini.
FED8 
Rais wa Benki ya Exim kutoka China, Liu Liange (kulia) akiwa katika Uwanja wa ndege wa  Kimataifa  wa JK Nyerere, muda mfupi kabla ya kuondoka nchini kurejea China baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi nchini ambapo Benki yake imeahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania kutekeleza Miradi Kadhaa ya Maendeleo ukiwemo ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha kimataifa (Standard gauge)
FED9  
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip I. Mpango (Mb) (kulia), akiagana na  Rais wa Benki ya Exim-China, Liu Liange, katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere jijini Dar es salaam kabla ya Rais huyo aliyekuwepo nchini kwa ziara ya kikazi kwa mawaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

TBL YAZINDUA BIA MPYA YA NDOVU RED MALT JIJINI DAR ES SALAAM

July 22, 2016

Meneja wa Bia ya Ndovu Red Malt, Nicolas John (wa kwanza kushoto) akifuatiwa na Mkurugenzi wa Masoko TBL Kushila Thomas pamoja na Meneja Masoko wa vinywaji wa kampuni ya TBL Vimal Vaghmaria (wa kwanza kulia) wakionyesha kinywaji cha Ndovu Red Malt mara baada ya kuzindua kinywaji hicho jana katika mgahawa wa 305 The Boks uliopo Kinondoni jijini Dar e Salaam ambapo wateja zaidi ya 50 walihudhuria katika hafla ya uzinduzi wake. Picha zote na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog. Meneja wa Bia ya Ndovu Red Malt, Nicolas John akiongea wakati wa Uzinduzi wa bia ya Ndovu Red Malt uliofanyika jana katika mgahawa wa 305 The Boks uliopo Kinondoni jijini Dar e Salaam ambapo wateja zaidi ya 50 walihudhuria katika hafla ya uzinduzi wake. Meneja Masoko wa vinywaji wa kampuni ya TBL Vimal Vaghmaria amesema: “Ubunifu wa kila bidhaa yetu unalenga kukidhi matakwa ya watumiaji wake ambao ni wateja wetu ambao wanahitaji kutumia bia zilizo bora na zinazokwenda na wakati katika soko”. Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Damian Soul akitoa burudani katika uzinduzi wa bia ya Ndovu Red Malt uliofanyika jana katika mgahawa wa 305 The Boks uliopo Kinondoni jijini Dar e Salaam. Mkurugenzi wa Masoko TBL, Kushila Thomas (wa kwanza kushoto) akijadiliana jambo na Meneja wa Bia ya Ndovu Red Malt, Nicolas John (katikati) pamoja na mgeni mwaliko aliyefika katika uzinduzi wa bia ya Ndovu Red Malt uliofanyika mgahawa wa 305 The Boks uliopo Kinondoni jijini Dar e Salaam. Wageni waalikwa wakijipatia bia ya Ndovu Red Malt. Wageni waaalikwa wakibadilisha nawazo huku wakijipatia kinywaji cha Ndovu Red Malt. Wageni waliohudhuria uzinduzi wa bia ya Ndovu Red Malt uliofanyika mgahawa wa 305 The Boks uliopo Kinondoni jijini Dar e Salaam. Kinywaji cha Ndovu Red Malt. Meneja wa Bia ya Ndovu Red Malt, Nicolas John(kushoto) akiwa na Msanii wa Kuchora Picha Bwana Lute (katikati) wakionyesha furaha yao mara baada ya uzinduzi wa bia hiyo. Maua yaliyohudumia tukio hilo.
 Katika mkakati wake wa kuendelea kuwaletea wateja wake bidhaa zenye bora wa hali ya juu, kampuni ya Tanzania Breweries Limited (TBL) imezindua bia mpya inayojulikana kama Ndovu Red Malt, bia ambayo imetengenezwa kwa kimea kwa asilimia 100 na ikiwa ni mwendelezo wa ubunifu wenye ubora wa bia ya Ndovu Special Malt inayoongoza kwa ubora na bia pendwa kwa watumiaji wengi wa bia nchini. 

 Bia ya Ndovu Red Malt imegundulika na kutengenezwa hapa nchini Tanzania ili kukidhi ladha ya wanywaji wa bia ikiwa na ubora wa kiwango cha juu na yenye ladha ya pekee kwa kulinganisha na aina nyinginezo za bia zilizopo kwenye soko. Uzinduzi wa bia ya Ndovu Red Malt umefanyika katika mgahawa wa 305 The Boks uliopo Kinondoni jijini Dar e Salaam Julai 20 mwaka huu ambapo wateja zaidi ya 50 walihudhuria katika hafla ya uzinduzi wake. 

 Mbali na kuwa na ladha ya aina yake inayoleta burudani kwa watumiaji wake kutokana na kutengenezwa kwa Shahiri kwa asilimia kubwa pia bia ya Ndovu Red Malt inavutia kwa mwonekano wake wa rangi kuwa na rangi ya uwekundu kwa mbali. Meneja Masoko wa vinywaji wa kampuni ya TBL Vimal Vaghmaria amesema: “Ubunifu wa kila bidhaa yetu unalenga kukidhi matakwa ya watumiaji wake ambao ni wateja wetu ambao wanahitaji kutumia bia zilizo bora na zinazokwenda na wakati katika soko”. 

 Alisema utengenezwaji wa bia ya Ndovu Red Malt kwa kutumia Shahiri kwa asilimia asilimia100 kunaleta upekee wa bia hii kwa kulinganisha na bia zingine kwenye soko na ina ladha tamu na mwonekano wake wa kuvutia ambao unaiongezea thamani. Kwa upande wake, Mpishi Mkuu wa Bia wa Kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Cavin Nkya, alisema kuwa bia hii mpya ya Ndovu Red Malt inazinduliwa ikiwa ni uthibitisho wa uwezo wa kampuni katika kuwapatia watanzania kinywaji chenye kiwango cha kimataifa na chenye ubora wa hali ya juu.

 “Ndovu Red Malt ni bia ya daraja la kwanza inayodhihirisha dhamira yetu ya kuwapatia wateja kinywaji ambacho daima wametamani kukipata kikiwa kimesheheni radha murua nay a kipekee,” alisema Nkya. Nkya alimalizia kwa kusema kwamba matokeo mazuri katika utayarishaji kinywaji hiki ni kutokana na uchanganyaji mahiri na wa umakini wa nafaka bora zinazozalisha hapa nchini ambazo zinazotumika kutengeneza bia Ndovu Red Malt. 

 Bia hii ina kiasi cha kilevi cha asilimia asilimia 4 na inapatikana katika chupa zenye muundo maridhawa zenye ujazo wa mililita 375 ,kama zilivyo aina nyingi za bia zinazozalishwa na kampuni ya TBL zilizopo sokoni. Sasa, bia ya Ndovu Red Malt itaanza kupatikana sehemu zote nchini ambako kampuni inasambaza bidhaa zake kuanzia wiki hii kwa gharama ya shilingi 2,000/ kwa bei ya reja reja.