Katikati ni Mwanachama wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) tokea ulipoanzishwa wilayani humo akimuonyesha kadi zake Meneja wa Mfuko wa Bima ya Afya Mkoa wa Tanga(NHIF) Ally Mwakababu. |
AFRICAN SPORTS YAVUTWA SHATI NA FRIENDS RANGERS WALAZIMISHWA SARE YA KUFUNGANA BAO 1-1,MKWAKWANI LEO
KIKOSI CHA FRIENDS RANGERS LEO. |
NA MWANDISHI WETU, TANGA
TIMU za Soka Friends Rangers ya Dar es Salaam na African
Sports “wanakimanumanu” leo zimeshindwa kutambiana baada ya kulazimishana sare
ya kufungana bao 1-1,ikiwa ni muendelezo wa Michuano ya Ligi daraja la Kwanza inayoendelea kutimua vumbi kwenye maeneo
mbalimbali hapa nchini.
Mechi hiyo ilichezwa leo kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani na
kushuhudiwa na wadau wa soka mkoani hapa kutoka maeneo mbalimbali.
Katika mchezo ambao ulikuwa mkali na wenye upinzani huku
timu zote zikionekana kushambuliana kwa zamu ambapo mpaka timu zote zinakwenda
mapumziko Friends Rangers walikuwa wakiongoza kwa bao 1-0 ambalo lilifungwa na
Iddi Ismaili baada ya kupokea krosi iliyopigwa na Credo Dancan upande wa
magharibi.
Bao hilo liliweza kudumu mpaka timu zote zinakwenda
mapumziko ambapo kipindi cha pili kilianza kwa kasi kutokana na timu kufanya
mabadiliko kwa baadhi wa wachezaji wake hali ambayo ilipelekea kucheza kwa
kujiamini na kucheza kwa umakini ikiwemo mashambulizi ya hapa na pale.
Wakionekana kujipanga vizuri,Friends Rangers waliweza
kutulia na kuanza kufanya mashambulizi ya nguvu langoni mwa African Sports kwa
dakika kadhaa lakini bahati haikuweza kuwa yao baada ya wachezaji wake kupiga mashuti
makali yaliyokuwa yakipaa juu ya lango la wapinzani wao hao.
Hata hiyo timu hiyo iliweza kuendeleza wimbi la mashambulizi
langoni mwa African Sports mithili ya mbogo aliyejeruhiwa na hatimaye kuweza
kupata bao la kusawadhisha katika dakika ya 84 kupitia Maulid Abasi ambaye
alitumia uzembe wa mabeki wa wapinzani wao kupachika wavuni bao hilo.
Akzungumza mara baada ya kumalizika,Kocha wa Friends
Rangers,Ally Yusuph Tigana alisema kuwa wanamshukuru mungu kwa kuweza kupata
pointi moja wakiwa ugenini ambayo itawasogeza kwenye nafasi ya juu kwenye
msimamo wa Ligi hiyo.
“Tunamshukuru
mungu kuweza kupata pointi moja ugenini hii ni muhimu sana kwetu tutakwenda kujipanga ili
kuhakikisha tunapata matokeo mazuri mechi yetu inayofuata “Alisema Tigana.
WATU 13 WATIWA MBARONI KWA MADAI YA KUHUSIKA NA MAUAJI YA KITETO
Polisi mkoani Manyara wanawashikilia zaidi ya watu 13 wanaodaiwa
kuhusika na mauaji ya wakulima na wafugaji yaliyotokea wiki iliyopita
katika Kata za Matui na Kiperesa wilayani hapa.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Manyara, Deusdedit Nsimeki amesema bado wanaendelea
na uchunguzi kabla ya kuchukua hatua ya kuwafikisha mahakamani watu hao.
“Hatuwezi
kutaja idadi kamili wala majina yao ila ni zaidi ya watu 13
tunawashikilia, wanadaiwa kuhusika na tukio hilo la mauaji na baada ya
uchunguzi wetu wahusika tutakaowabaini tutawafikisha mahakamani,”
alisema.
Hata hivyo, jana na juzi hali ilikuwa shwari
katika eneo hilo huku wakazi wilayani humo wakishuhudia helikopta ya
polisi ikiwa na makamishna kutoka Makao Makuu ya Polisi, Dar es Salaam
ikizunguka angani kuendelea na ulinzi.
Naye, Mkuu wa
Mkoa huo, Eraston Mbwilo akizungumza kwenye kikao cha ushauri cha mkoa,
alisema chanzo cha mgogoro wa ardhi na mauaji hayo ya Kiteto
yanasababishwa na baadhi ya watu kuhodhi ekari za ardhi bila ya kuwa na
vibali.
“Hili suala la baadhi ya watu kudai kuwa Kiteto
imegeuka kuwa Somalia siyo kweli, mgogoro wa Emboley Murtangos
unasababishwa na baadhi ya watu kujimilikisha ekari nyingi za ardhi
kiholela,” alisema Mbwilo na kuongeza:
“Unamkuta mtu
anamiliki ekari zaidi ya 500 kiholela, huu ni ukiukwaji wa sheria,
vijiji vina utaratibu wa kugawa maeneo, kwa nini wasiufuate?” alihoji.
Alisema
kwa sasa hali ni shwari katika eneo hilo na wanaendelea kufanya
mazungumzo na viongozi wa jamii ya wakulima na wafugaji ili kuhakikisha
kuwa mauaji na vurugu hizo havitokei tena.
Subscribe to:
Posts (Atom)