DAVID MWAMWAJA: LENGO LETU MSIMU UJAO NI KUIRUDISHA JUU PRISONS

September 04, 2014
Kocha mkuu wa Prisons, David Mwamwaja ( wa kwanza kulia)

Na Baraka Mbolembole, Dar es Salaam,

David Mwamaja hajafanya usajili mkubwa licha ya kikosi chake kupambana hadi dakika ya mwisho msimu uliopita ili kusalia katika ligi kuu.

Baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ashanti United, 24 April, Tanzania Prisons ilifanikiwa kubaki katika ligi kuu Bara. Wengi walitaraji timu hiyo ingefanya usajili mkubwa wakati wa dirisha la usajili kwa kuamini kuwa timu hiyo inahitaji mabadiliko makubwa.

 Haijawa hivyo na Mwamaja ameweza kuhakikisha mchezaji wa timu ya Taifa ya Zanzibar, Amir Omary anatua katika kikosi chake kwa lengo la kuongeza makali katika safu ya mashambulizi ambayo ilibebwa zaidi na mshambulizi, Peter Michael na Richard Peter msimu uliopita.

“ Ligi itakuwa ngumu msimu ujao, lakini tunataka kuirudisha juu Tanzania Prisons kama ilivyokuwa enzi za kina Osward Morris.Nimeongezwa katika timu hii kwa lengo la kusaidiana na wachezaji waliopo ili kuifanya Prisons kuwa timu bora msimu ujao.. Tangu nimefika hapa nimepata vitu vingi vipya ndani na nje ya uwanja. Upendo, ushirikiano na umoja ni mambo yaliyotawala hapa” anasema mshambulizi, Amir Omary ambaye amesajiliwa akitokea klabu iliyoshuka daraja ya JKT Oljoro.

Michael alifunga mabao 12 msimu uliopita, Richard alifunga mabao manne na Amir alifunga mabao sita katika kikosi cha Oljoro msimu uliopita na mchexzaji huyo wa Zanzibar Heroes anaamini kuwa umoja wao utawasumbua walinzi wengi msimu wa 2014/15.

“ Ni safu kali ya mashambulizi, kila timu imejiandaa msimu ujao lakini nachoweza kusema tumejipanga kuhakikisha Prisons inafanya vizuri msimu ujao. Mwalimu yoko poa na kila mmoja kikosini anafahamu ni kitu gani ambacho kinatakiwa”
RAIS KIKWETE AKUTANA NA BIBI YAKE RAIS OBAMA WA MAREKANI,JIJINI NAIROBI LEO

RAIS KIKWETE AKUTANA NA BIBI YAKE RAIS OBAMA WA MAREKANI,JIJINI NAIROBI LEO

September 04, 2014
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Bibi yake Rais wa Marekani,Mh. Barack Obama,Mama Sarah Obama walipokutana Leo kwenye hoteli ya Villa Rosa Kempiski  jijini Nairobi, Kenya, wakati Rais Kikwete akijiandaa kurejea nchini.Mama Sarah Obama anatarajia kuzindua taasisi ya kusaidia elimu kijijini Kogelo nchini Kenya,alikozaliwa Baba yake na Rais Obama wa Marekani itakayofahamika kama (Sarah Obama foundation) ambapo atajenga shule kuanzia za awali mpaka sekondari. Rais kikwete sasa hivi yuko mjini Kondoa kuendelea na ziara yake ya Mkoa wa Dodoma.PICHA NA IKULU
Rais Dk.Shein na Marais mbali mbali katika uzinduzi wa Mpamgo wa WIOCC SAMOA.

Rais Dk.Shein na Marais mbali mbali katika uzinduzi wa Mpamgo wa WIOCC SAMOA.

September 04, 2014

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Waziri wa Mambo ya nje ya nchi wa Seychels Jeun-Paul Adam baada ya Waziri huyo kutoa hotuba yake katika Uzinduzi wa Mpango wa Magharibi ya Bahari ya Hindi ya Changamoto za Ukanda wa Pwani namabadiliko tabianchi jana katika  Orator Hotel,Apia Samoa[Picha na Ramadhan Othman,Samoa.] IMG_3346  
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akitoa hutuba yake katika Uzinduzi wa Mpango wa Magharibi ya Bahari ya Hindi ya Changamoto za Ukanda wa Pwani na mabadiliko tabianchi jana katika  Orator Hotel,Apia Samoa   ambapo Mkutano wa Tatu wa Kimataifa wa  Nchi za Visiwa unaendelea.[Picha na Ramadhan Othman,Samoa.],[Picha na Ramadhan Othman,Samoa.] IMG_3349  
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati) Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Bibi Fatma  Abdulhabib Fereji,pamoja na viongozi wengine wakiwa katika  Uzinduzi wa Mpango wa Magharibi ya Bahari ya Hindi ya Changamoto za Ukanda wa Pwani na mabadiliko tabianchi jana katika  Orator Hotel,Apia Samoa ambapo Mkutano wa Tatu wa Kimataifa wa Nchi za Visiwa unaendelea.[Picha na Ramadhan Othman,Samoa.] IMG_3359 
Baadhi ya washiriki katika uzinduzi wa Mpango wa Magharibi ya Bahari ya Hindi ya Changamoto za Ukanda wa Pwani na mabadiliko tabianchi jana katika  Orator Hotel,Apia Samoa ambapo Mkutano wa Tatu wa Kimataifa wa Nchi za Visiwa unaendelea wakifuatilia kwa makini hutuba mbali mbali zilizotolea na Viongozi kutoka Nchi tofauti,(kushoto) Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimaifa Mahadhi Juma Maalim.[Picha na Ramadhan Othman,Samoa.] IMG_3363  
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati)akiteta na  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Bibi Fatma  Abdulhabib Fereji, katika  Uzinduzi wa Mpango wa Magharibi ya Bahari ya Hindi ya Changamoto za Ukanda wa Pwani na mabadiliko tabianchi jana katika  Orator Hotel,Apia Samoa ambapo Mkutano wa Tatu wa Kimataifa wa Nchi za Visiwa unaendelea katika nchi hiyo.[Picha na Ramadhan Othman,Samoa.]

MKURUGENZI NHC ATEMBELEA ENEO LA MRADI WA NYUMBA ZA WATUMISHI HALMASHAURI YA BUSOKELO MBEYA

September 04, 2014

Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw.Nehemia Kyando Mchechu wa kwanza kulia mbele akitembelea eneo la ujenzi wa nyumba za gharama nafuu zitakazojengwa  katika Halmashauri ya Busekelo Mkoani Mbeya alipotembelea Halmashauri hiyo  Septemba 3 mwaka huu .Picha na Saguya wa NHC.
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw.Nehemia Mchechu akielezea mpango wa shirika wa kujenga nyumba za watumishi wa Halmashauri ya Busekelo alipotembelea Halmashauri hiyo jana .Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Busokelo Bw. Meshack Mwakipunga  na kulia  kwa Mkurugenzi Mkuu wa  NHC ni Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Busekelo Bw Saidi Mderu .
 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Busokelo Bw,Meshack Mwakipunga akiutembeza ujembe wa shirika la Nyumba la Taifa  kwenye eneo la viwanja vitakavyojengwa  nyumba  na NHC hivi karibuni.
Ujumbe wa NHC na Halmashauri ya Busokelo ukiendelea kutambua  viwanja vitakavyojengwa Nyumba na NHC hivi karibuni
 
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw.Nehemia Mchechu akitoa maelezo ya kuridhia eneo walilopewa na Halmashauri ya Busekelo ili kujenga nyumba hivi karibuni.
Ujumbe ukikagua kazi ya kutengeneza matofali kwa ajili ya kujengea nyumba katika Halmashauri ya Busokelo.
Mhandisi wa  miradi ya nyumba wa NHC Kanda ya Mbeya Bw.Mtili akitoa maelezo ya hatua iliyofikiwa ya ufyatuaji wa matofali ya  kujengea nyumba katika Halmashauri hiyo.
 
Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC  ulipata fursa ya kutembelea shamba la mwekezaji wa Kilimo cha Maparachichi baada ya kumaliza ziara yake katika Halmashauri ya Busokelo,ambapo kupitia uwekezaji huo wananchi wa busokelo na maeneo mengine wamepata fursa ya ajira.
Ujembe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC ukipewa maelezo na Meya wa Jiji la Mbeya Bw.Athanas Kapunga yanayohusu fursa za uwekezaji ambazo NHC inaweza kuzitumia kukuza uchumi wa jiji hilo.

Shirika la Nyumba la Taifa lakabidhi mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana Arusha

September 04, 2014
 
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Nyirembe Munasa, Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Bi.Rachel Kassanda  wakiwa tayari kutoa hundi kwa mmoja wa kiongozi wa vikundi vya vijana baada ya kupokea hundi. (Picha zote kwa Hisani ya Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Jamii)
 
Kiongozi wa mbio za mwenge Rachel Kassanda akikagua matofali na nyuma yake ni mkuu wa wilaya ya Arumeru Nyerembe Munasa.
 Maafisa toka NHC Amoni Mazanda na Gibson Mwaigomole wakiangalia baadhi ya mambo yaliyoratibiwa na wenyeji wao H ya Meru
 
Maafisa wa shirika wa mauzo na miliki Amoni Mazanda wakiwa na maafisa maendeleo wa Halmashauri ya wilaya ya Arusha Mwatumu Dossi na wa Halamashauri ya Meru Bwana Mrema
 Jiwe la Msingi
  
Nyumba za gharama nafuu zilizopo Longido kama zinavyoonekana pichani
 Wageni wakiwasili eneo la nyumba za Shirika la Nyumba la Taifa Longido
Mbunge wa Longido Lekule Laizer akiwa na Mkuu wa wilaya ya Longido James Olle Millya wakiangalia jiwe la msingi la mradi wa nyumba za gharama nafuu Longido.
 
Maelezo kwa kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa wakati wa makabidhiano ya mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana

KUANZA MCHUJO WA WAGOMBEA WAKE LEO

September 04, 2014
 Mkurugenzi wa Organizesheni, Mafunzo na Uratibu wa Kanda wa Chama cha demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Singo Kigaila Benson akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati akitamngaza majina ya wagombea mbalimbali katika chaguzi za chama hicho.
 Mkurugenzi wa Organizesheni, Mafunzo na Uratibu wa Kanda wa Chama cha demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Singo Kigaila Benson akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati akitamngaza majina ya wagombea mbalimbali katika chaguzi za chama hicho.Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Habari CHADEMA, Tumaini Makene.

OKWI.BANDA WASAJILIWA TIMU MBILI-TFF

September 04, 2014


Na Fadha Kidevu Blog
SHIRIKISHO la soka Tanzania TFF,limetoa majina ya wachezaji waliosajiliwa na timu 14 ambazo zinashiriki Ligi Kuu ya Tanzania bara huku majina ya wachezaji Emmanuel Okwi na Abdi Banda yakitokea kwenye timu mbili.

Jina la Okwi linatokea kwenye usajili wa timu za Simba na Yanga ilhali jina la beki wa kushoto Banda,limetokea kwenye usajili wa Coastal Union na Simba .

Fadha Kidevu ilijaribu kuwatafuta viongozi wa TFF,wanaoshuhulika na maswala ya usajili ili kutaka kujua sakata hilo na vipi litaamuliwa lakini viongozi hao hawakuweza kupatikana.

Suala hilo linatarajiwa kutolewa uwamuzi baada ya kumalizika kipindi cha mapingamizi ambayo itakuwa ni Septemba 6 kabla ya Kamati ya Maadili na hadhi za wachezaji itakapokutana na kutoa suluhisho la tatizo hilo.