Ufunguzi wa baraza la wafanyakazi jijini Dar

April 29, 2014


Katibu Mkuu,Ofisi ya Makamu wa Rais Bw.Sazi Salula (katikati) akifungua rasmi kikao cha Baraza la wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais kilichofanyika Karimjee jijini Dar es Salaam leo hii kulia ni Naibu katibu Mkuu  Eng. Angerina Madete, na wa kwanza kushoto Katibu wa Baraza Bw. Isaya Kisiri.
 Sehemu ya wajumbe wa baraza la wafanyakazi toka Ofisi ya Makamu wa Rais wakimsikiliza Katibu Mkuu Bw. Sazi Salula wakati wa ufunguzi wa Baraza la wafanyakazi kikao hicho kimefanyika leo katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.

KAMPUNI YA SIMU YA VODACOM YAWAUNGANISHA BUHIGWE KWENYE MTANDAO WA SIMU ZA MIKONONI

April 29, 2014


Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Charles Gishuli akiuzindua rasmi mnara wa Vodacom kuashiria kuanza kupatikana huduma za kampuni hiyo ya simu nchini katika kijiji cha Bukuba kilichopo Buhigwe mkoani Kigoma. Pembeni yake ni Meneja wa Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim. Wengine ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya hiyo Malcelina Mbehoma na Mwenyekiti wa Halmashauri Abel Kabona. Vodacom inaendeleza mkakati wake wa kuwaunganisha watanzania wa vijijini na huduma za mawasiliano ya simu za mkononi ili kuwawezesha kuboresha maisha yao.
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma Charles Gishuli (mwenye koti) akitumia simu yake ya mkononi kutuma fedha kupitia huduma ya M-pesa mara tu baada ya kuzindua huduma za Vodacom katika kijiji cha Bukuba mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Abel Kabona. Vodacom inaendeleza mkakati wake wa kuwaunganisha watanzania wa vijijini na huduma za mawasiliano ya simu za mkononi ili kuwawezesha kuboresha maisha yao.
Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim akimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Charles Gishuli jinsi ambavyo wakazi wa kijiji cha Bukuba Mkoani Kigoma wanavyoweza kupata huduma za Intaneti kupitia mtandao wa Vodacom mara baada ya Mkuu huyo wa Wilaya kuzindua rasmi huduma za Vodacom kijijini hapo mwishoni mwa wiki. Kushoto (mwenye kofia nyekundu) ni Mhandisi wa Vodacom Mkoa wa Kigoma Adam Nyamgali.
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Charles Gishuli akiongea na wakazi wa kijiji cha Bukuba na vijiji jirani waliofika kushuhudia uzinduzi wa mnara wa mtandao wa Vodacom kijijini hapo mwishoni mwa wiki. Kulia ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim. Wengine kutoka kuhsoto ni Mhandisi wa Vodacom Adam Nyamgali, Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya Renatus Mkasa na Kaimu Mkurgenzi Mtendaji wa Wilaya Malcelina Mbehoma. Kupatikana kwa huduma za Vodacom kijijini hapo kunatarajiwa kufungua ukurusa mpya wa maendeleo ya kiuchumi an kijamii kijijini hapo.
Mhandisi wa Vodacom Mkoani Kigoma Adam Nyamgali akimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma jenereta inayozalisha umeme wa kuendeshea mnara wa mawasiliano wa kampuni hiyo. Mkuu huyo wa Wiayaa aliuzindua mnara huo uliopo kijiji cha Bukuba mwishoni mwa wiki. Vodacom inaendeleza mkakati wake wa kuwaunganisha watanzania wa vijijini na huduma za mawasiliano ya simu za mkononi ili kuwawezesha kuboresha maisha yao.

BASI LA HOOD LATEKETEA KWA MOTO ,ABIRIA WANUSURIKA

April 29, 2014


Zaidi ya Abiria 55 waliokuwa ndani ya Basi la kampuni ya Hood, wakisafiri kutoka Mbeya kwenda Arusha walinusurika kufa baada ya Basi hilo kushika moto na kuteketea kabisa katika kijiji cha Kilolele-Chalinze Mkoani Pwani.

*WANANCHI WAASWA KUZINGATIA USAFI WA MAZINGIRA

April 29, 2014


 Afisa Mazingira wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke Bw.Ernest Mamuya akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)kuhusu hatua zinazochukuliwa na Manispaa hiyo katika kuhakikisha  kuwa kanuni na taratibu za usafi wa mazingira zinazingatiwa na wananchi wote kwa kuyaweka mazingira yao katika hali  ya usafi ili kujikinga na magonjwa ya milipuko.
Pix.Afisa Afya wa Manispaa ya Temeke Bw.Willium Muhemu akifafanua kwa waandishi wa habari mafanikio yaliyofikiwa na Manispaa hiyo katika kuwaondoa wafanyabiashara wanaofanya biashara katika maeneo yasiyo rasmi pamoja na watu wote wanaochafua mazingira,Kulia ni Afisa Uhusiano wa Manispa hiyo Bi. Joyce Nsumba. Picha zote na FRANK MVUNGI-maelezo
****************************************
Na Hassan Silayo-MAELEZO
Wananchi wameaswa kuzingatia usafi wa mazingira kwa kuwa jukumu la kila mwananchi kulinda na kutunza na kuzingatia kanuni za usafi wa mazingira.
Hayo yamesemwa na Afisa Afya wa Manispaa ya Temeke Bw. Willium Muhemu wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Bw. Muhemu alisema manispaa hiyo imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha kuwa kanuni za usafi, taratibu na sheria za usafi wa mazingira zinazingatiwa na wadau wote wa mazingira ili kuepusha mlipuko wa magonjwa.
“Moja ya mikakati iliyowekwa na manispaa ya Temeke ni kuhakikisha kwamba hakuna mtu anayefanya biashara katika maeneo yasiyo rasmi ili kuzuia uchafuzi wa mazingira na yeyote atakaye kiuka utaratibu huo atachukuliwa uchafuzi wa mazingira” Alisema  Bw. Muhemu
Naye Afisa Mazingira wa Manispaa hiyo Bw. Ernest Mamuya alisema kuwa ili kuhakikisha kuwa manispaa hiyo inakuwa katika hali ya usafi wakati wote wanao mpango mpango wa kuongeza magari ya kubeba taka , kuwa na dampo la kudumu la kuhifadhia taka na kuhakikisha taka zinazolewa kwa wakati.
Akitoa wito kwa wananchi Bw. Mamuya alisema kuwa wananchi wanapaswa kuzingatia kanuni za usafi katika ngazi za familia ili kuunga mkono mpango wa manispaa katika utunzani wa mazingira.
Maafisa afya wa kata wanaendesha zoezi la ukaguzi wa nyumba kwa nyumba kwa kushirikiana na wajumbe wa kamati za afya za mitaa husika ili kuhakikisha kuwa wananchi wanazingatia kanuni za usafi.

*MAMA SALMA AZINDUA CHANJO YA KUZUIA MAAMBUKIZO YA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI KWA WASICHANA WENYE UMRI WA MIAKA 9-16

April 29, 2014

 Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Ndugu Leonidas Gama akimpokea Mke wa Rais Mama Salma Kikwete kwenye Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tarehe 28.4.2014. Mama Salma alikwenda Moshi kuzindua rasmi chanjo ya kuzuia maambukizi ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana wa umri wa miaka 9 hadi 16.
 Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mwakilishi wa Shirika la kuhudumia watoto, UNICEF, hapa nchini Dkt. Sudha Sharma, mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Mandela uliopo katika eneo la Pasua katika Manispaa ya Moshi kwa kulikofanyika uzinduzi rasmi ya chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana.
Maandamano ya vikundi mbalimbali kutoka katika Mkoa wa Kilimanjaro wakipita mbale ya mgeni rasmi Mama Salma Kikwete wakati wa sherehe ya uzinduzi wa chanjo kwenye uwanja wa Mandela huko Pasua mjini Moshi tarehe 28.4.2014.

Maandamano ya vikundi mbalimbali kutoka katika Mkoa wa Kilimanjaro wakipita mbale ya mgeni rasmi Mama Salma Kikwete wakati wa sherehe ya uzinduzi wa chanjo kwenye uwanja wa Mandela huko Pasua mjini Moshi tarehe 28.4.2014.
  Mamia ya watu waliohudhuria sharehe za uzinduzi wa chanjo ya kuzuia maambukizi ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni rasmi, Mama Salma Kikwete katika sherehe hiyo.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia mamia ya wananchi na wanafunzi waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa chanjo ya kuzuia saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana wenye umri wa miaka 9 hadi 16 huko Pasua, Moshi tarehe 28.4.2014.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa chanjo ya kuzuia maambukizi ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana kwenye sherehe iliyofanyika huko Pasua, Moshi Mjini tarehe 28.4.2014. Wengine katika picha (kushoto kwenda kulia) ni Ndugu Leonidas Gama, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dkt. Rufaro Chatora, Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani hapa nchini, Dkt Kebwe Stephen Kebwe, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Neema Rusibamayila, Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya, Mama Salma na wa Kwanza kulia ni Mwakilishin wa Shirika la Kuhudumia watoto (UNICEF) hapa nchini  Dkt. Sudha Sharma.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizungumza naza mtoto Salma Abillah mara baada ya kupata chanjo ya kuzuia saratani ya shingo ya kizazi na baadaye kumkabidhi kadi yake ambayo anatakiwa kurudi tarehe 28.10.2014 kwa ajili ya kupata chanjo ya pili.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete anaonekana akitoa chanjo ya matone kuzuia ugonjwa wa polio kwa mtoto Ahmad, miezi 10, aliyefika kwenye sherehe ya uzinduzi wa chanjo ya kuzuia maambukizi ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana huko Pasua, Moshi tarehe 28.4.2014.