CRDB Bank Marathon Congo yakusanya Dola 50,000 kusaidia wodi ya watoto Hospitali ya Jason Sendwe DRC

August 04, 2024

 

Gavana wa Jimbo la Haut-Katanga, Jacques Kyabula (katikati) akimkabaizi mfano wa hundi yenye thamani ya Dola za Marekani 50,000 Waziri wa Afya, Joseph Nsambi Bulanda wa Haut-Katanga (watatu kulia), zilizokusanywa katika CRDB Bank Marathon Congo iliyofanyika leo Agosti 4 2024 katika jiji la Lubumbashi DRC. Wengine pichani ni Balozi wa Tanzania nchini DRC, Said Mshana (wapili kulia), Mwenyekiti wa Bodi ya Kundi la Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay (watatu kushoto), Mwenyekiti wa Bodi wa CRDB Bank DRC, Dkt. Fred Msemwa (wapili kushoto), Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Benki ya CRDB, Bruce Mwile (wakwanza kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank DRC, Jessica Nyachiro.
Lubumbashi – CRDB Bank Marathon imefanyika leo kwa mara ya kwanza nje ya mipaka ya Tanzania katika jiji la Lubumbashi ambapo zaidi ya wakimbiaji 1,000 wameshirikina kufanikisha lengo la kukusanya USD 50,000 kwa ajili ya kusaidia wodi ya watoto katikaHospitali ya Jason Sendwe.

Mgeni rasmi katika mbio hizo ambazo zimewekahistoria katika marathon ambazo zimewahikufanyika katika jiji la Lubumbashi alikuwa ni Gavana wa Jimbo la Haut-Katanga Mhe. Jacques Kyabula ambaye aliambatana na mawaziri 10 wa Jimbo hilo wakiongozwa na Waziri wa Michezo, pamoja na Waziri wa Afya.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mbiohizo za hisani zilizobeba kaulimbiu isemayo‘Tabasamu Limevuka Mipaka’ Gavana Kyabulaameipongeza Benki ya CRDB kwa kuwaletapamoja WaCongo pamoja na washiriki kutoka mataifa ya jirani kuja kuchangia kuboreshahuduma za afya kwa watoto na kukuza ustawi wa jamii.

"Tunaishukuru CRDB Bank Marathon kwa kusaidia jitihada za Serikali kuboresha huduma za afya kwa wananchi. Serikali yetu inatoakipaumbele kikubwa katika afya, na tunafurahishwa na jitihada zinazofanywa na Benki ya CRDB katika kusaidia kuboresha afyaya watoto," alisema Gavana Kyabula.
Kwa upande wake Balozi wa Tanzania nchiniDRC, Balozi Said Mshana aliipongeza Benki ya CRDB kwa juhudi zake za kukuza mahusianoya kimataifa na kuimarisha umoja na mshikamano katika jamii. Balozi Mshanaalisema mbio hizo zilizozaliwa Tanzania zinaonyesha ubunifu ambao taasisi za kitanzania zinaweza kupeleka nje ya nchi katikakusaidia kukuza ustawi wa jamii.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB Bank DRC, Dkt. Fred Msemwa alieleza kuwa marathon hiyoni sehemu ya mkakati wa Benki kusaidia juhudiza serikali katika kukuza ustawi wa watu wa Congo. "Marathon hii si tu inahamasishamichezo, bali pia inajenga utamaduni wa kujitolea kwa jamii.

Benki yetu inaamini kwa kuwaleta watu pamoja tunaweza kuyafikiamakundi mengi kwa urahisi na hivyo kukuza ustawi wa jamii kupitia programu bunifu kama CRDB Bank Marathon, lakini pia kupitia huduma na bidhaa zetu bunifu tutaweza kusaidia jitihadaza kukuza ujumuishi wa kifedha na kiuchumi," alisema.
Akitangaza matokeo ya mbio hizo, MkurugenziMtendaji wa CRDB Bank Congo, Jessica Nyachiro, aliwashukuru washirika wa mbio hizoAfricell, Orange, Ogowe Cleaning, Kin Marche, Policlynique Delta, Shalina, Vinmart Foundation, SUNU Insurance, na Dukan. “Pamoja na kuwahuu ni mwaka wa kwanza kwa mbio hizi lakinimwitikio umekuwa mkubwa sana. Tunawashukuru sana washirika wetu na wakimbiaji wote mlioungana nasi kusambazatabasamu kwa watoto.”

Marathon iliyofanyika leo Lubumbashi ni ya kwanza kati ya tatu ambazo zimepangwakufanyika mwaka huu nchini DRC, Burundi, na Tanzania. Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation ambao ndio waandaji wa mbio hizo, Tully Esther Mwambapa ameeleza furaha yakebaada ya mbio hizo zilivyopokelewa vizuri sana nchini DRC.

Tully amewashukuru Watanzania ambaowamejitokeza kwa wingi kushiriki mbio hizo za DRC ikiwamo kuwashukuru washirika wakuu wa mbio hizo Sanlam, CRDB Insurance Company, na Clouds Media. "Nitumie nafasi hiikuwakaribisha watu wote kuendelea kujisajilikwa mbio za Burundi tarehe 11 Agosti na Tanzania tarehe 18 Agosti," aliongezea.

Papy Kayombo, mshindi wa mbio za Kilometa21 katika CRDB Bank Marathon Congo, ameeleza furaha yake ya kushiriki katika mbiohizo na kusema ushindi wake ni sehemu ya kusambaza tabasamu kwa watoto ambaowatapata matibabu katika hospitali ya Jason Sendwe.

Kayombo alisema, "Katika jiji la Lubumbashi utamaduni huu ni mpya na ninaonautasaidia sana kujenga mshikamano katikajamii. Naipongeza sana Benki hii yetu ya CRDB, imeonyesha upendo mkubwa sana kwa watotowetu na sisi tunaahidi kuiunga mkono."

Viongozi hao pia waliambatana na Balozi wa Tanzania nchini DRC, Balozi Said Mshana, Balozi wa Burundi nchini DRC, pamoja viongozimbalimbali wa Benki ya CRDB wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay, na Kaimu MkurugenziMtendaji wa Benki ya CRDB, Bruce Mwile.




PROFESA ASSAD ATAKA USHIRIKIANO UJENZI WA HOSPITALI YA KIISLAMU TANGA

August 04, 2024

 










Na Oscar Assenga, TANGA

MDHIBITI  na Mkaguzi  Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mstaafu Profesa Mussa Assad amesema ni umuhimu kuwepo kwa ushirikiano wa pamoja ili kuhakikisha ujenzi wa Hospitali ya Kiislamu Mkoani Tanga unakamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma.

Profesa Assad aliyasema hayo mwishoni mwa wiki Jijini Tanga wakati aliposhiriki kwenye Kongamano la tathimini ujenzi wa Hospitali ya Kiislamu Mkoa wa Tanga lililokwenda sambamba na kufanyika kwa harambee ya kuchangia ujenzi wake huku akieleza ni ushirikiano ni lazima wawe wamoja katika kufanikisha hilo.

Harambee hiyo ilikwenda sambamba na uliokwenda sambamba na kukagua eneo la Ujenzi wa Hospitali hiyo lililopo Kata ya Masiwani, Kupanda miti ya Matunda pamoja na kuweka jiwe la Msingi.

Alisema kwa sababu jambo ambalo linafanyika ni la kuokoa maisha na ukiokoa maisha ya mtu mmoja utakuwa umeokoa maisha ya watu wote kwani hata vitabu vitakatifu vya Mungu (Quran) vimeandikwa hilo.

“Hata vitabu vitakatifu vya Mwenyezi Mungu vinaeleza kumtibu mtu mmoja na kuyaokoa maisha yake ni sawa utakuwa umeuokoa umma nzima lakini tatizo ambalo analiona ni ajizi kwamba wanafikiria hawawezi leo kufanya jambo hilo labda wasubiri kesho itawezakena na mwisho miaka inapita anzeni sasa”Alisema.

“Hilo ni tatizo kubwa la ajizi hivyo tuondoe ajizi tulifanye kazi hi kwa ushirikiano mkubwa ili kuweza kutimiza malengo tuliojiwekea ya kuhakikisha ujenzi wa eneo hilo unaendelea “Alisema

“Leo nimefurahi kwa sababu kuna kazi kubwa imefanywa na amesikitika hatua zake zimekwenda taratibu mno na nimekuwa nikipita sana kwenye eneo hilo kila mwezi kwenda Tongoni na wala sijasikia kuwepo wa shughuli hizi pia kinachomsikitisha zaidi ni kumetolewa nondo 72 katika ujenzi huu”Alisema

Aidha alisema maana yake hawajali vitu vyao wenyewe hivyo ni wajibu wao kuhakikisha wakifanya vitu hapo vilindwa ili kuepusha kuibiwa na wezi jambo ambalo litapelekea kuepukana na vitendo hivyo.

“Lakini niwasihi katika jambo hilo tuwe pamoja na kuongeza mshikamano ili kulifanikisha jambo hilo na mwakani mungu akipenda kutakuwa wamepandisha jengo pia tutaendelea kuona namna wadau mbalimbali wanaweza kuchangia kwenye ujenzi huu”Alisema

Kwa makadirio ya Fedha za ujenzi wa Hosptali hiyo unakadiriwa kuwa ni zaidi ya Sh.Bilioni 2.4 sio fedha ndogo hivyo ni lazima waone namna ya wao wenyewe wajipange wafanya juhudi kubwa za kuanza kazi hiyo na wao waanze wenyewe na wao watakaoona hivyo wanaweza kuona namna ya wadau wengine kuwaunga mkono.

“Lakini niwaambie kwamba Mwenyezi Mungu akijalia nikirudi Dar nitahamasisha wenzangu kuona namna nzuri ya kuliendelea jengo hlo lianze haraka sana kutokana na umuhimu mkubwa lilikokuwa nalo”Alisema

Alisema kwamba Mwenyezi Mungu amewajalia neema nyingi waislamu hivyo ni vema wajiulize wameifanyia nini hiyo neema ya umri wamekaa miaka miwili jengo hilo hivyo maana yake wamefanya ajizi na hawakufanya hima ya kutekeleza kazi hiyo.

“Jambo la muhimu ni kujikumbusha kwamba tumepewa neema ya umri siku zinavyokwenda tujipime namna gani tumefanya kazi hizo inshallah Mwenyezi Mungu ajalie tukae pamoja juhudi hizi ziendelezwe ili mwakani tusiwe na msingi tuwe tumepanda kama sio ghorofa moja itakuwa ghorofa mbili na hilo tutaliweza kama tutakuwa wamoja”Alisema

Awali akizungumza kuhusu mradi huo wa Ujenzi wa Hospitali inayozingatia maadili ya Kiislamu Mjumbe wa Halmashauri Kuu wa Baraza la Waislamu Taifa (Bakwata) Sheikh Khamis Mataka alisema kwamba MwenyeziMungu atalipa nguvu jambo hilo ili litimie na uwezo huo wanao.

Alisema kwamba uwezo wa kulitimiza jambo hilo upo ndani yao wao wenyewe wakiondokana na matatizo na changamoto walizojiwekea wao wenyewe wataona namna suala hilo litakavyopata mafanikio.

Naye kwa upande wake Dkt Ally Fungo alisema kwamba mradi huo wa kimkakati umedhamiria kutatua tatizo la kimkakati kama halitatatuliwa litaadhidhiri dhamira ya jamii ya kiislamu kwa kwa maana hapo watakuwa na kituo cha afya cha kutoka tiba kinachzingtia maadili ya kiislamu ambayo ni ya kibinadamu.

Alisema kwamba hospitali hiyo haitakuwa ya waislamu pekee bali wote lakini haiwezekani wakina mama wakatibiwa na daktari mwanaume hiyo ni hospitali ya kimkakati kutatua kimkakati hospitali ya waislamu wenyewe kwa fedha zao wenyewe.

“Hospitali hii itakuwa na majengo sana kuanzia Jengo la Utawala ,Jengo la Madaktari,Wodi za Wakina Mama,Kina Baba ,Maabara,Mochwari ,na nyenginezo na gharama zake kwa awali tungetumia Bilioni 1.5 lakini kipindi kimepita miaka mitatu iliyopita”Alisema

Hata hivyo alisema kutokana na uchumi duniani kuadhirika hivyo sasa wamefanya ufuatiliaji vitu vimebadilika na bei ya vitu imeongezeka na hivyo watalazimika watumie bilioni 2.4 hilo sio jambo dogo ni kubwa hivyo watashirikiana na wadau wote kufanikisha hilo.

TBS YAENDELEA KUTOA ELIMU YA VIWANGO NANENANE LINDI

August 04, 2024

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limewashauri wajasiriamali kuzingatia matakwa ya kisheria katika masuala ya afya,usalama na mazingira kwenye usindikizaji wa bidhaa mbalimbali kwa lengo la kuzalisha bidhaa bora na salama.