TAARIFA KUTOKA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI TANZANIA (TFF) LEO

August 15, 2017
UCHAGUZI KAMATI YA UONGOZI TPLB

Uchaguzi wa Kamati ya Uongozi (Management Committee) ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara utafanyika Jumapili Oktoba 15, 2017 jijini Dar es Salaam.

Fomu kwa ajili ya wagombea zitaanza kutolewa Agosti 17, 2017 kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu kwa wagombea ni saa 10.00 jioni Agosti 23, mwaka huu.

Nafasi zitakazowaniwa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Wajumbe watatu kuwakilisha klabu za Ligi (PL), Wajumbe wawili wa kuwakilisha klabu za Ligi Daraja la Kwanza (FDL), na Mjumbe mmoja wa kuwakilisha klabu za Ligi Daraja la Pili (SDL).

Ada ya fomu kwa nafasi za Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti ni Sh 200,000 (Shilingi lakini mbili) wakati nafasi nyingine zilizobaki ni Sh 100,000 (Shilingi laki moja).

Uchaguzi utaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za Uchaguzi za TFF toleo la 2013.

Wagombea kwa mujibu wa kanuni za uendeshaji wa Bodi ya Ligi Kuu ni marais au wenyeviti wa klabu husika.

Wagombea wanatakiwa kuwa wenyeviti au Marais wa klabu husika.

Nafasi ya Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania inagombewa na klabu za Ligi Kuu pekee.

MALALAMIKO YA KLABU KATIKA USAJILI

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limepokea malalamiko kutoka baadhi ya timu na vituo vya kuibua na kukuza vipaji vya soka zikidai fidia baada ya wachezaji wao kusajiliwa na klabu nyingine msimu wa 2017/18.

Jana Agosti 14, 2017 ilikuwa siku ya mwisho kwa timu na vituo vya kuibua na kukuza vipaji kuwasilisha malalamiko yao TFF kuhusu fidia za mafunzo; ada ya usajili; ada za maendeleo na kuvunjwa kwa mikataba kutoka katika timu walizochezea hadi msimu uliopita.

TFF imepokea malalamiko ya Kagera Sugar ya Kagera dhidi ya Azam FC ya Dar es Salaam kuhusu mchezaji Mbaraka Yussuf wakati Majimaji ya Songea pia imelalamika Azam kuhusu mchezaji Idd Kipangwile.

Alliance ya Mwanza imelalamikia Pamba pia ya Mwanza kuhusu mchezaji Juma Nyangi ambako madai hayo yamekwenda mbali zaidi yakisema kuwa mchezaji husika amebadili jina kwa lengo la kudanganya.

Kwa upande wake, African Lyon imeondokewa na wachezaji 19 na inadai fidia katika timu, wachezaji kwenye mabano za Majimaji (Saleh Malande); Lipuli (Hamad Manzi, Lambele Reuben na Mussa Nampoka); Young Africans (Rostand Youthe Jehu); Tusker FC (Abdul Hilal) na Ndanda kwa wachezaji Hamad Tajiri na Baraka Majogoo.

Madai mengine ni dhidi ya Coastal Union kwa wachezaji Baraka Jaffary, Omary Salum, Raizen Hafidh na Fred Lewis huku madai mengine ni kwa Kagera Sugar kwa wachezaji Omar Abdallah, Abdallah Mguhi na Vicent Ludovic na Alhaji Zege .

RAIS DKT. MAGUFULI AAGANA NA MGENI WAKE RAIS WA MISRI PIA AKUTANA NA WAZIRI WA ZAMANI WA MAMBO YA NJE WA JAPAN

August 15, 2017

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama pamoja na mgeni wake Rais wa Misri Abdel Fattah Al Sisi wakati wa nyimbo za mataifa mawili zikipigwa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere(JNIA). Rais huyo wa Misri ameondoka mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili hapa nchini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsindikiza mgeni wake Rais wa Misri Abdel Fattah Al Sisi wakati akielekea kupanda ndege mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili hapa nchini
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais wa Misri Abdel Fattah Al Sisi mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili nchini.

Culture of secrecy still embedded in public officials

August 15, 2017
The culture of secrecy is still embedded in public officials especially in the central government as opposed to Local Government despite improvement in service delivery and access to information, a recent study has revealed.
A study which was conducted by the Media Institute of Southern Africa (MISA) Tanzania Chapter with support from the Collaboration on International ICT Policy for East and Southern Africa (CIPESA) aimed at looking at Access to Information in Local Government Authorities (LGAs) and Central Government offices in Tanzania. The LGAs were represented by the City and Municipal Councils and the Central Government was represented by the Regional Commissioners’ Offices.
This study wished to find out how central government and local government authorities are transparent and accountable to citizens. The study also strived to find out how the general public do/can access information in public offices.
Practical experience from Journalists who conducted the study shows that there is an improvement in service delivery and access to information in some of the public offices especially in Local Government as opposed to Central Government.
However, they say laxity among public servants is still a big problem in public service. “If you received someone’s documents, while would you say you can’t see them just a week later?” questions Haika Kimaro, Mwananchi Correspondent in Mtwara. 
Similar sentiments were echoed by George Binagi, a Radio Journalist in Mwanza. “I submitted my questions in writing to the Regional Commissioner’s Office. I went back 10 days after and yet I did not get the answers , they looked for my letter and they never saw it” .
“At Kigoma Ujiji Municipal Council they received the letter but they did not reply and even after going there for follow up, the Secretary claimed to have misplaced the letter”, says Rhoda Ezekiel, Uhuru Newspaper Correspondent in Kigoma Region.
Jacquline Jones, Mass Communication graduate and intern at MISA Tanzania offices says she went to the Dar es Salaam Regional Commissioner’s office posing as a student researcher. But because she didn’t have the letter from her university they refused to offer her the information she requested, saying their work procedures don’t allow them to do so regardless of the information she wanted.
“Their customer service is awful and the people at the registry department they were quite harsh and rude. One of them actually shouted at me for insisting on getting my answers in a written form”, says Ms Jones.
She also submitted a similar request (but with different questions) to the Dar es Salaam City Council, which, according to the Information Officer it needed at least four different Heads of Sections, who gladly availed to her all the information she wanted.
One of the questions that were asked to those who did the study was, “Did you experience good customer care among those who receive visitors/respond to telephone calls?”  According to Zulfa Musa, Mwananchi Newspaper Correspondent in Arusha, there are telephones in the City Council’s offices which are received by their assistants, but the Director and his secretary have private phones that they both receive and call personally. She says that while at the office she witnessed different people receiving good service and direction and if the person in charge was not around, they were told that the person will be informed when she/he gets back.
As previously said, the study used journalists as researchers. According to the findings, it was very interesting to see how people who usually seek information from these public offices are treated in some offices. The question that researchers ask themselves is how ordinary citizens would be treated in some of these very same offices if people with proper identification like them face those challenges.
In its concluding remarks, the study tells that it is hard to deny the fact that free and easier access to government-held information is key to development of any democracy. It is an important aspect in promoting transparency and accountability.
According to Information experts, access to quality and timely information by everyone, and most importantly to rural population, is crucial in facilitating informed dialogue, monitoring and evaluation of development issues at the local level and to enhance governance and accountability for improved delivery of service and implementation of projects.
“There was an Access to Information Act that was passed in 2016. The only challenge I see for now is that both public servants and the general public are unaware of this Law. There is a need for sensitization of the law among public servants. It is in public offices where most of the information is generated. It is important they know what the law entails”, says Sengiyumva Gasirigwa, Information and Research Officer at MISA Tanzania.
He adds that there is a need for specialized trainings/seminars/workshops for public officials on Freedom of Information (FOI) issues and the public’s Right to Know (Access to public-held information) vis-à-vis its importance to country’s development.
Geofrey Adroph BLOGGER P.O.BOX 24793, Mob: +255 755 274953 /+255 713 363965, Email: pamojapure@gmail.com. Blog: http://www.pamoja.co.tz/ DAR ES SALAAM, TANZANIA

DKT. KALEMANI AENDELEA KUZINDUA MIRADI YA UMEMEMVIJIJINI AWAMU YA TATU (REA PHASE III MIKOA YA KUSINI NA RUKWA

August 15, 2017
                   Na Henry Kilasila - Rukwa

Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Dkt Medard Kalemani ameendelea na ziara za uzinduzi wa Miradi ya Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA PHASE III) ambapo Agosti 14, 2017 alikuwa Mikoani Rukwa katika Kijiji cha Kabwe Wilaya ya Nkasi.

Dkt. Kalemani alisema jumla ya Shilingi Bilioni 42.5 zitatumika kupeleka umeme katika Mkoa huo na kuongeza Mradi huo utatekelezwa katika vipindi viwili tofauti ambapo sehemu ya kwanza itahusisha upelekaji umeme katika vijiji 111.

"Sehemu ya pili itahusisha vijiji 145 ambapo itaanza baada ya kukamilika kwa sehemu ya kwanza. Kufikia mwaka 2021 vijiji vyote vya Mkoa wa Rukwa vitakuwa vimepatiwa umeme".Alisema Dk. Kalemani.

Aidha, Dkt. Kalemani alimtambulisha Mkandarasi atakayejenga Mradi wa REA Mikoani humo Kampuni ya Kitanzania ya Nakuroi Investment Company Limited.

Alimwagiza Mkandarasi kuhakikisha anapeleka umeme Kijiji kwa Kijiji na Kitongoji kwa Kitongoji bila kuruka na sehemu zinazotoa huduma za Kijamii kama Mashule, Zahanati, Magereza, Visima vya maji, Nyumba za Ibada na sehemu mbalimbali.

Pia alitoa maagizo kwa TANESCO kupeleka Ofisi katika Kijiji cha Kabwe na katika maeneo yote yenye Wateja wengi lakini wapo mbali na Huduma za TANESCO.

Aliongeza kwa kuwataka Mameneja na Watalaamu wa TANESCO kutokukaa Ofisini bali wawafuate Wateja.Awali, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji TANESCo, Dkt. Tito E. Mwinuka aliwaomba Wananchi hao wa Kabwe kuwa waaminifu na kutoa ushirikiano kwa Watendaji wa TANESCO kabla na hata baada ya Mradi kukamilika.

"Muitunze miundombinu ya umeme, msiihujum wala kuichoma moto". Alisema Dkt. Mwinuka.Alisema TANESCO imejipanga kuhakikisha Wananchi hao wanapata huduma ya umeme iliyobora na ya uhakika.

Mbunge wa Nkasi, Ali Kessy aliwaeleza Wananchi kuwa mradi huo wa usambazaji umeme vijijini hauna malipo ya fidia hivyo watoe ushirikiano kwa wakandarasi hao wakati wanatekeleza mradi huo.

Mkuu wa Wilaya ya Nkansi Mheshimiwa Saidi Mtanda aliushukuru Uongozi wa TANESCO kwa kwani umekuwa ukitoa ushirikiano pale unapohitajika.
"Mheshimiwa Mgeni Rasmi katika Kijiji cha Nyamare kwenye chanzo cha maji tulileta Mkandarasi akatukadilia bei ya Transifoma milioni 60, tuliwasiliana na uongozi wa TANESCO wametufungia Transfoma kwa pesa zao milioni 24". Alisema Mheshimiwa Mtanda.

Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Dkt Medard Kalemani alimalizia uzinduzi Mkoani Rukwa kwa kuwakabidhi Wazee kumi zawadi ya kifaa cha UMETA.
Naibu waziri Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Dkt Medard Kalemani akifurahia baada ya kuzindua mradi wa REA RUKWA
Naibu Waziri Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani akiwasili eneo la uzinduzi Mkoani Rukwa, akiwa amepokelewa na mwenyeji wake Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mheshimiwa Saidi Mtanda.
Kutoka kushoto Mkurugenzi Mkuu REA, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Dkt. TITO E. Mwinuka katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Kampuni ya Nakuro Investment Company Limited inayojenga Mradi huo wa umeme Mkoani humo. 

FAIDA YA SERIKALI KUGHARAMIA ELIMU BURE NI WANAFUNZI KUFAULU–PROFESA NDALICHAKO

August 15, 2017

Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii

SERIKALI inatoa sh. bilioni 18.77 kwa ajili ya kugharamia elimu bure ili kila mtanzania apate elimu bora na faida yake kwa serikali hiyo ni kuona wanafunzi wanafaulu darasa la Saba na Kidato cha Nne na kuendelea na elimu ya kidato cha tano na hadi chuo kikuu.

Hayo ameyasema leo Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako wakati wa uzinduzi mabweni katika shule ya sekondari Nasibugani ambayo ujenzi wake uko katika hatua ya mwisho pamoja na Shule ya Sekondari Mwinyi ambayo ujenzi umekamilika kwa kuingia wanafunzi katika mabweni hayo wilayani Mkuranga mkoani Pwani .

Profesa Ndalichako amesema serikali ya awamu ya tano imeondoa imeondoa gharama katika shule ya msingi na sekondari ili kuondosha mzigo kwa wazazi wengine ambao walikuwa wanashindwa kugharamia elimu hiyo.

Amesema mabweni katika shule ya sekondari Nasibugani na Mwinyi zenye Kidato cha Kwanza hadi Sita ni kuongeza sehemu ya kumwezesha mwanafunzi kusoma kwa muda mrefu na kuweza kondokana na vishawishi vinavyopatikana mtaani.

Aidha amesema kuwa serikali itaendelea kuboresha shule mbalimbali ikiwemo pamoja na makazi ya walimu yaliyo bora pamoja na huduma zingine ikwemo umeme katika shule ya Sekondari Nasibugani.

Amesema kuwa Mkuranga iko nyuma kielimu ni ukweli usiofichika hivyo walimu pamoja na watendaji kuhimiza suala la elimu ili viwanda vilivyopo na wanamkuranga wanufaike na sekta hiyo.

Waziri Profesa Ndalichako amempongeza Mbunge wa Mkuranga Abdallah Ulega kuanzisha Program kwa wanafunzi wa sekondari kuwa Hakuna Kufeli.

Amesema Program hiyo ifanywe kwa vitendo kwa wanafunzi kujitoa zaidi kusoma kwani mtihani uko karibu lakini wakitumia program hiyo watafanya vizuri na kuondoa sifuri katika shule zao na kuanza daraja la kwanza hadi la tatu.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga amesema kuwa wanaomba chuo cha Ufundi katika wilaya hiyo ili vijana waweze kujiunga na kuweza kutumika katika sekta ya viwanda vilivyojengwa Mkuranga.

Amesema kuwa zaidi ya vijana 900 hawana ajira hivyo chuo cha ufundi ni sehemu sahihi kwa vijana na wataendelea kuongeza mwaka hadi mwaka kadiri wnavyohitimu.

Mbunge wa Mkuranga Abdallah Ulega amesema kuwa jitihada mbalimbali katika kuboresha miundombinu ya shule pamoja na serikali kuongeza walimu.Amesema kuwa wanafunzi wanavyofanya vizuri ni furaha na kuweza kuwa nguvu ya uandaji wa vijana katika mapinduzi ya elimu.

 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia , Profesa Joyce Ndalichako akizindua mabweni mawili katika Shule ya Sekondari Nasibugani  iliyopo Wilaya ya Mkuranga.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia , Profesa Joyce Ndalichako akipanda mti katika shule ya Sekondari Nasibugani.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia , Profesa Joyce Ndalichako akizindua mabweni mawili yaliyokamilika katika shule sekondari Mwinyi iliyopo Wilaya ya Mkuranga.
 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga  akizungumza wananchi na wanafunzi katika shule ya Sekondari Nasibugani.

SHAKA AINGIA PEMBA KWA KISHINDO

August 15, 2017
Na Mathias Canal, Pemba

Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 amewasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.

Ambapo hii Leo atakuwa katika Wilaya ya Chakechake, katika Ziara hiyo Katibu Mkuu UVCCM Taifa atakagua utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya CCM katika kipindi hiki Cha Miaka mitano 2015-2020

Aidha, Shaka atashiriki shughuli Mbalimbali za kijamii sambamba na kuzungumza na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 akisalimiana na Wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM na Jumuiya zake mara baada ya kuwasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 akisalimiana na Wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM na Jumuiya zake mara baada ya kuwasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 akisalimiana na Wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM na Jumuiya zake mara baada ya kuwasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 akisalimiana na Wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM na Jumuiya zake mara baada ya kuwasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka leo Agosti 15, 2017 akisalimiana na Wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM na Jumuiya zake mara baada ya kuwasili Visiwani Pemba-Zanzibar kwa Ziara ya kikazi.

Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi's visit to Tanzania in pictures

August 15, 2017
 The plane carrying Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   touches down at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam in Tanzania ahead of his two-day official visit set to open a new chapter for more enhanced bilateral cooperation between the two countries.
  Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   arrives at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam in Tanzania ahead of his two-day official visit
 President Dr. John Pombe Magufuli receives Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   arrives at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 President Dr. John Pombe Magufuli walks with his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   arrives at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
  President Dr. John Pombe Magufuli walks with his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   arrives at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 

  President Dr. John Pombe Magufuli walks with his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   stand for the two countries' National Anthems  at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
  President Dr. John Pombe Magufuli walks with his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   stand for the two countries' National Anthems  at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 The Vice President Hon. Samia Suluhu Hassan, Prime Minister Kassim Majaliwa and other top government officials ready to receive Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi    at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 Government officials receive Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi    at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   inspects the guard of honour at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 President Dr. John Pombe Magufuli introduces Vice President Hon. Samia Suluhu Hassan to the Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi     at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 President Dr. John Pombe Magufuli is introduced to Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi's delegation    at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 The Vice President Hon. Samia Suluhu Hassan, President of Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein, Prime Minister Kassim Majaliwa brave the afternoon drizzle to  receive Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi    at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
  Ululation as Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi    arrives at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
  Traditional dances welcome to Tanzania Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi    at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
  Mount Usambara Brass band welcome to Tanzania Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi    at the Julius Nyerere International Airport (JNIA) in Dar es Salaam 
 President Dr. John Pombe Magufuli walks welcomes to the state House his  guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  
 President Dr. John Pombe Magufuli offers a giant Makonde carving to his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  
 President Dr. John Pombe Magufuli shakes hands with  his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  
 President Dr. John Pombe Magufuli offers a painting  to his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  
 President Dr. John Pombe Magufuli receives a traditional bowl from his  guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  
 President Dr. John Pombe Magufuli shakes hands with  Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  before their tete-a-tete at the State House in Dar es salaam 
  President Dr. John Pombe Magufuli in a tete-a-tete with his guest Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi   at the State House in Dar es salaam 
  President Dr. John Pombe Magufuli walks Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  to the conference room for official talks at the State House in Dar es salaam 
 Traditional dances entertain
  President Dr. John Pombe Magufuli in bilateral talks with  Egyptian President Abdel Fattah El-Sisi  at the State House in Dar es salaam 
 Some Tanzanian Cabinet Minister chat moments before the two leaders make their addresses