MHE BITEKO ASIFU UTENDAJI WA RC SHINYANGA KUKABILIANA NA MIGOGORO YA MADINI

February 02, 2018
 Naibu Waziri wa madini Mhe Doto Mashaka Biteko akisitiza jambo wakati akizungumza kwenye kikao cha kazi Mara baada ya kutembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga akiwa katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani humo, leo 2 Februari 2018. Picha Zote Na Mathias Canal
 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi Zainab R. Telick akitoa taarifa ya sekta ya madini katika Mkoa huo mbele ya Naibu Waziri wa madini Mhe Doto Mashaka, leo 2 Februari 2018.
Naibu Waziri wa madini Mhe Doto Mashaka Biteko akisalimiana na watumishi mbalimbali katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga mara baada ya kutembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga akiwa katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani humo, leo 2 Februari 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi Zainab R. Telick akitoa taarifa ya sekta ya madini katika Mkoa huo mbele ya Naibu Waziri wa madini Mhe Doto Mashaka, leo 2 Februari 2018.

Na Mathias Canal, Shinyanga

Naibu Waziri wa madini Mhe Doto Mashaka Biteko amesifu juhudi zinazofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe Zainab R. Telack za kukabiliana na migogoro mbalimbali inayojitokeza jambo ambalo linarahisisha na kuboresha utendaji wa Wizara ya madini nchini.

Naibu Waziri huyo ametoa pongezi hizo leo 2 Februari 2018 wakati akizungumza kwenye kikao cha kazi Mara baada ya kutembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo wakati wa ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Shinyanga.

Katika ziara hiyo iliyoanza Leo 2 Februari 2018 na kumalizika kesho 3 Februari 2018 katika Mkoa wa Shinyanga Naibu Waziri huyo wa wizara ya madini atatembelea na kuzungumza na wachimbaji wadogo katika eneo la Mwazimba na Wachimbaji wadogo wa kikundi cha Kasi Mpya.

Mhe Biteko amemweleza Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kuongeza msisitizo zaidi katika usimamizi madhubuti wa sheria, Kanuni na taratibu za nchi pamoja na kuwa na majukumu ya sekta zote lakini sekta ya madini aongeze juhudi pia ili kuinua mpango wa Wizara ya madini kuongeza nguvu katika mchango kwenye pato la Taifa kufikia asilimia 10% kutoka asilimia 4% ya sasa.

Naibu Waziri huyo amesema serikali ngazi ya wilaya na Mkoa ni vema wakaendelea kuwalea wachimbaji wadogo, wakati na wakubwa katika utekelezaji wa sheria ya madini na kanuni zake.

Aliongeza kuwa Mkuu wa Mkoa na watendaji wote wa sekta ya madini hawapaswi kuogopa migogoro katika sekta hiyo kwani ili kuwasaidia wachimbaji wadogo ni lazima kukabiliana na migogoro mbalimbali inayojitokeza baina ya wachimbaji wenyewe na wawekezaji sambamba na sintofahamu baina yao na baadhi ya watendaji wa serikali.

Aidha, amekitaka chama cha wachimbaji wadogo nchini kuisaidia serikali kufichua uovu unaofanywa na baadhi ya wachimbaji Wasio waaminifu ikiwa ni pamoja na utoroshwaji wa madini mbalimbali jambo ambalo ni kuwaibia watanzania na kinyume na Sheria ya madini sambamba na usafirishaji wa madini.

Mhe Biteko aliongeza kuwa wachimbaji wadogo na wakubwa kote nchini wanapaswa kujibainisha katika ulipaji kodi kwani kufanya hivyo kutaimairisha utendaji wa Wizara katika mchango wa pato la Taifa ikiwa ni pamoja na serikali kuwatambua na kuongeza ufanisi wa kuwahudumia.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa alimweleza Mhe. Biteko serikali ya Mkoa wa Shinyanga imejipanga kusimamia vema sekta hiyo kwani ni nguzo kubwa ya uchumia wa Mkoa huo na akaiomba Wizara ya madini kuendeleza ushirikiano na ofisi yake ili kuongeza tija katika usimamizi wa sekta ya madini.

UJENZI RASMI BOMBA LA MAFUTA KUANZA MEI

February 02, 2018
Na Veronica Simba – Dodoma
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Nishati na Kampuni ya Total wamekubaliana kuharakisha hatua zote za awali katika Mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Uganda hadi Hoima Tanga ili shughuli za ujenzi rasmi zianze mwezi Mei mwaka huu.
Makubaliano hayo yalifikiwa Alhamisi, Februari 1, wakati Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani alipokutana na uongozi wa juu wa kampuni hiyo wizarani Dodoma.
Aidha, makubaliano mengine yaliyofikiwa katika kikao hicho ni kuwa kazi za awali za maandalizi ya ujenzi ziwe zimekamilika ifikapo mwezi Machi mwaka huu.
“Ni lazima tuharakishe mchakato huu kama Mheshimiwa Rais Magufuli alivyoagiza. Hivyo, tumekubaliana kwamba shughuli zote za maandalizi ziwe zimekamilika ifikapo Machi mwaka huu ili kuwezesha shughuli rasmi za ujenzi wa Bomba kuanza mwezi Mei,” alifafanua Waziri Kalemani.
Vilevile, katika kikao hicho, Rais wa Kampuni ya Total sehemu ya Afrika, Guy Maurice ambaye alikuwa kiongozi wa Ujumbe huo, alibainisha nia ya kampuni yake kuwekeza katika shughuli nyingine mbalimbali zinazohusiana na Mradi wa Bomba jambo ambalo alisema litainufaisha zaidi Tanzania. 
Mbali na makubaliano yote yaliyofikiwa, Waziri Kalemani pia alisisitiza kuwa ni muhimu kampuni ya Total iwasilishe Mpango-Kazi wake wizarani mapema iwezekanavyo ili utumike kama mwongozo-rejea katika kutathmini utekelezaji wa Mradi huo mkubwa.
Kampuni ya Total ndiyo mwekezaji katika utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa Bomba la Mafuta kutoka Uganda hadi Hoima, Tanga.
Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. Hamisi Mwinyimvua, Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Wizara Lusius Mwenda, Mkurugenzi wa Sera na Mipango Haji Janabi na maafisa wengine waandamizi kutoka wizarani.
 Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (katikati), akiongoza kikao baina ya viongozi na wataalam wa Wizara (kulia) na Ujumbe kutoka Kampuni ya Total (kushoto). Kikao hicho kilifanyika Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, Februari Mosi, mwaka huu.
 Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, akisalimiana na Ujumbe kutoka Kampuni ya Total kabla ya kuanza kwa kikao baina yao kujadili utekelezaji wa Mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Uganda hadi Hoima-Tanga. Kikao hicho kilifanyika Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, Februari Mosi, mwaka huu.
 Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (kushoto), akimsikiliza Rais wa Kampuni ya Total sehemu ya Afrika, Guy Maurice (kulia) wakati wa kikao baina yao kujadili utekelezaji wa Mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Uganda hadi Hoima-Tanga. Kikao hicho kilifanyika Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, Februari Mosi, mwaka huu.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. Hamisi Mwinyimvua, akisalimiana na Ujumbe kutoka Kampuni ya Total kabla ya kuanza kwa kikao baina ya Wizara na Ujumbe kutoka Kampuni hiyo kujadili utekelezaji wa Mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Uganda hadi Hoima-Tanga. Kikao hicho kilifanyika Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, Februari Mosi, mwaka huu na kiliongozwa na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani.
 Viongozi na wataalam wa Wizara ya Nishati, wakiwa katika kikao baina ya Wizara na Ujumbe kutoka Kampuni ya Total kujadili utekelezaji wa Mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Uganda hadi Hoima-Tanga. Kikao hicho kilifanyika Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, Februari Mosi, mwaka huu na kiliongozwa na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (hayupo pichani).
Ujumbe kutoka Kampuni ya Total wakiwa katika kikao baina yao na Viongozi na wataalam wa Wizara ya Nishati kujadili utekelezaji wa Mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Uganda hadi Hoima-Tanga. Kikao hicho kilifanyika Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, Februari Mosi, mwaka huu na kiliongozwa na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (hayupo pichani).

DC SHINYANGA AKABIDHI HUNDI ZA MIKOPO MIL 25 KWA VIKUNDI VYA VIJANA NA WANAWAKE HALMASHAURI YA SHINYANGA

February 02, 2018

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amekabidhi hundi za mikopo shilingi milioni 25 kwa vikundi vitatu vya vijana na kimoja cha wanawake zilizotolewa na halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
MTULIA:MNIKOPESHE KURA ZENU,NITAWALIPA MAENDELEO

MTULIA:MNIKOPESHE KURA ZENU,NITAWALIPA MAENDELEO

February 02, 2018

Mgombea Ubunge jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya CCM, Ndugu Maulid Said Mtulia akinadi sera zake jukwaani eneo la Msufini kata ya Mwananyamala.
IMG_20180201_173351.jpg
Katibu wa Itikadi na uenezi CCM Taifa Humphrey Polepole akimkabidhi ilani ya uchaguzi ya CCM 2015 - 2020 Mgombea Ubunge jimbo la Kinondoni, Ndugu Said Maulid Mtulia
IMG_20180201_175138.jpg
IMG_20180201_175959.jpg
Maelfu ya Watu walijitokeza kwenye mkutano wa CCM katika viwanja vya Msufini kata ya Mwananyamala.
***********
*YALIYOSEMWA NA MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KINONDONI KWA TIKETI YA CCM, NDUGU MAULID SAID MTULIA KWENYE MKUTANO WA KAMPENI ENEO LA MSUFINI, KATA YA MWANANYAMALA LEO ALHAMIS FEBRUARI 01, 2018*

"Nimejiunga kwenye chama chenye dola na chenye ilani ya uchaguzi, tatizo lipo wapi? - Mtulia

"Kama mimi Msaliti mbona wao wameshindwa kuungana kwa pamoja kupambana nami msaliti? Uko wapi umoja wao wa Ukawa? Nani msaliti hapo? - Mtulia

"Nyote ni mashahidi namna ambavyo nimekuwa nikitoa pesa zangu mfukoni kunyonya maji wakati wa mafuriko" - Mtulia

"Mtulia mimi nilienda Mahakamani kuzuia bomobomoa nyote mlishuhudia ubomoaji ule ulizuiwa mpaka kesho" - Mtulia

"Chama hiki ndicho kilichotoa pesa kujenga soko la Msisiri, kujenga madaraja na kujenga madarasa. Nipo kwenye chama sahihi chenye kuleta maendeleo kwa jamii." - Mtulia

"Nimekabidhiwa ilani na Polepole na nikishinda nitaanza na agizo la kuhakikisha pesa za Vijana na Wanawake toka Manispaa zinatolewa mapema iwezekanavyo" - Mtulia

"Mkimchagua Mtulia matatizo ya maji, mifereji na kuchimba mitaro, kujenga barabara na matatizo mengineyo yatakwisha kabisa" - Mtulia

"Nimejitoa mhanga ya kujiuzulu ili kuwaokoa Wana Kinondoni" - Mtulia

"Pasipo kushirikiana na Serikali mimi Mbunge ningepata wapi hela za kujenga barabara, kujenga mifereji, kujenga maghorofa? Ukiwa Kiongozi mpinzani ni ngumu kuleta maendeleo kwa Wananchi, nawaambia ukweli." Mtulia

"Nikiwa Mbunge kupitia tiketi ya CCM kutanipa urahisi wa kuwaletea maendeleo wana Kinondoni" - Mtulia
"Mkinikopesha kura zenu, nitawalipa maendeleo ya kweli wana Kinondoni. Naomba kura zenu wana Kinondoni." - Mtulia